Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,738
- 155,424
Wizara itoe taarifa sahihi kwamba kirusi hiki kipya kinaua hata kama ulichanjwa.Wizara ya Afya imesema hivi karibuni kumekuwa na tishio la kutokea Wimbi la Nne kutokana na taarifa za ongezeko la visa vipya na kuwepo kwa wasafiri wengi ndani na nje ya Nchi katika kipindi cha sikukuu za mwisho wa mwaka
Kutokana na kuibuka aina mpya ya Kirusi cha Corona kiitwacho Omicron, kinachosemekana kuwa na uwezo wa kusambaa haraka, Serikali imesisitiza Wananchi kuendelea kujitokeza kupata chanjo
Pia, imehimiza uvaaji barakoa, unawaji mikono kwa maji tiririka na sabuni au kutumia vipukusi, kufanya mazoezi na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima
Serikali semeni ukweli