Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,942
- 4,413
Mkazi wa Vingunguti Sokoine Mtunda, ameuawa na wananchi wenye hasira kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, Faustine Shilogile, amesema tukio hilo limetokea majira ya saa 3:00 usiku huko Vingunguti kwa wachinja nyama.
Akielezea sababu ya kifo hicho, Kamanda Shilogile amesema, mtu huyo ambaye pia ni mchinjaji wa wanyama katika eneo hilo, anadaiwa kuwa usiku alirejea nyumbani toka mzigoni na kumkuta mkewe, Bi. Muta Mazengo, 25, akiwa na doti mbili za khanga mpya ambazo hazifahamu.
Alisema kutokana na hilo, Bw. Mtunda alimhoji mkewe alikozitoa khanga hizo kwa sababu anafahamu wazi kuwa mkewe hana uwezo wa kuzipata khanga hizo bila ya kununuliwa.
Amesema kutokana na kubanwa na maswali ya mumewe, mkewe alimtaja kijana aliyetambulika kwa jina la Bw. Hossen kuwa ndiye aliyempa khanga hizo.
Akasema kwa hasira mumewe alimbeba mkewe hadi kwa kijana huyo usiku ili kwenda kujua kulikoni hadi akampa mkewe kanga hizo.
Alisema Hussein alikanusha kuwa si yeye aliyempa kanga hizo, ndipo alipomuitia mwizi Bw. Mtunda,ambapo wananchi wenye hasira walijitokeza na kuanza kumshambulia kwa fimbo na vitu mbalimbali hadi kumuua.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, Faustine Shilogile, amesema tukio hilo limetokea majira ya saa 3:00 usiku huko Vingunguti kwa wachinja nyama.
Akielezea sababu ya kifo hicho, Kamanda Shilogile amesema, mtu huyo ambaye pia ni mchinjaji wa wanyama katika eneo hilo, anadaiwa kuwa usiku alirejea nyumbani toka mzigoni na kumkuta mkewe, Bi. Muta Mazengo, 25, akiwa na doti mbili za khanga mpya ambazo hazifahamu.
Alisema kutokana na hilo, Bw. Mtunda alimhoji mkewe alikozitoa khanga hizo kwa sababu anafahamu wazi kuwa mkewe hana uwezo wa kuzipata khanga hizo bila ya kununuliwa.
Amesema kutokana na kubanwa na maswali ya mumewe, mkewe alimtaja kijana aliyetambulika kwa jina la Bw. Hossen kuwa ndiye aliyempa khanga hizo.
Akasema kwa hasira mumewe alimbeba mkewe hadi kwa kijana huyo usiku ili kwenda kujua kulikoni hadi akampa mkewe kanga hizo.
Alisema Hussein alikanusha kuwa si yeye aliyempa kanga hizo, ndipo alipomuitia mwizi Bw. Mtunda,ambapo wananchi wenye hasira walijitokeza na kuanza kumshambulia kwa fimbo na vitu mbalimbali hadi kumuua.