Uzalendo kwa Taifa letu - Tanzania

Shayu

Platinum Member
May 24, 2011
608
1,653
Ndugu zangu, dada na kaka zangu. Naandika nakala hii kutokana na dhamira yangu ya kizalendo juu ya taifa langu na watu wake kwa ujumla.

Nikiwa mzalendo na raia wa taifa hili. Nina wajibu wa kutoa maoni yangu kuhusu mwelekeo na mustakabali wa taifa letu.

Mimi sio maarufu miongoni mwa watu wa taifa hili. Lakini naamini mawazo yangu yanaweza kuleta mchango mkubwa kwa taifa hili au kuonya kuhusu mwelekeo ambao tunaelekea kama taifa. Taifa lolote lile hujengwa na watu kutokana na jitihada zao za pamoja katika kujiletea maendeleo yao wenyewe, wakitumia fikra zao katika kujikomboa na kutawala mazingira.

Hatuwezi kuendelea kama hatutalipenda taifa hili na kujitolea kwa dhati kabisa katika kuliendeleza kwa faida ya vizazi vyetu. Ni ukweli usiopingika binadamu hawezi kufanikiwa katika jambo lolote lile isipokuwa kwanza kutia juhudi na kupenda jambo analolifanya. Ni ukweli usiopingika kabisa kiini cha watu kuishi katika taifa ni umoja bila umoja hakuna taifa. Lazima tuwe tumekusanywa na lengo ambalo sisi kama taifa lazima tulifanikishe. Ikiwa kila mmoja wetu akitia juhudi katika kufanya kazi na katika kufikiri kwa ajili ya manufaa ya taifa tutapiga hatua. Taifa hata siku moja haliwezi kujengwa katika misingi ya ubinafsi ni kinyume na uasilia wa watu kuishi kama taifa na ni kiashiria cha kuporomoka kwa utaifa na madhara yake ni vita na uharibifu.

Ni Aibu kwa viongozi wetu kusaka uongozi hadi kwa waganga wa kienyeji. Mtu kama huyu hafai kuongoza wananchi, ni mbinafsi na mroho, anataka uongozi kwa faida zake binafsi na anasa.Kiongozi wa kweli ni yule anaye organize watu kutumikia taifa lao wenyewe, sio yule anayetumia nafasi hiyo kujinufaisha na kuishi maisha ya anasa wakati watu wake wakiteseka.

Tumekuwa taifa lisilokuwa na mwelekeo, wananchi hawajui wanapoelekea, ni nini mission ya taifa? tumekuwa watu wa binafsi na wenye choyo.

Ubinafsi huondoa mantiki ya watu kuishi katika taifa, kama taifa ni lazima tujue, nini kimetuunganisha na wapi tunataka kuelekea, Kujumuika kwetu kwa pamoja ni ili tuwe na maisha mazuri kuliko haya tuliyo nayo, ili tuishi kwa amani, undugu na upendo, ili kulinda taifa letu dhidi ya maadui wa kigeni.

Haki za kila mmoja wetu ni muhimu ili kujenga taifa lenye umoja. Tuna taifa ambalo watu wake hawajui wajibu wao kwa nchi yao wenyewe , hii ni hali ya hatari sana. Ni lazima tujenge taifa ambalo vijana watajua wajibu wao kwa taifa, hili ni jambo muhimu sana.

Taifa huvunjika na kusambaratika kabisa, Tusifikiri kwamba Tutataishi milelele katika nchi hii kama hatukujenga misingi ya umoja na mshikamano wetu. Ni lazima tufikirie upya juu ya ujenzi wa taifa letu na mustakabali wetu kama taifa. Ufisadi hutugawa lakini haki utuleta pamoja, ni ukweli pia taifa lisilo kuwa na malengo ya pamoja watu wake ufikiria ubinafsi, sio utaifa na mwelekeo wa taifa. Ni muhimu kwetu kuamini katika taifa hili, Jukumu la kiongozi yeyote yule makini katika hali tuliyonayo sasa ni kuziondoa akili za watu katika ubinafsi na kuzileta katika utaifa. Watu lazima wajue taifa lao linapoelekea na wanaamini nini kama taifa.

Taifa imara hujengwa katika umoja na mshikamano wa watu wake na sisi watu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, tulioamua kuwa taifa, tutambue hilo, uwepo wa taifa hili unategemea sana maamuzi yetu tunayoyafanya. Kwahiyo umakini mkubwa unahitajika tunapoongelea masuala yanayohusu taifa letu. Taifa ni kitu ambacho kinavunjika na kusambaratika ili tuendelee kuwa pamoja inabidi umakini mkubwa. Nchi haijiendeshi yenyewe bali huendeshwa na busara za watu wake na viongozi wao. Aina ya taifa hutegemea sana aina ya viongozi tulionao, Ubora au ubovu wa taifa lolote hutegemea busara na akili za viongozi wa taifa hilo. Uchu na tamaa zitatugawa, ni sawa sawa na kukata tawi ulio kalia, tutalisambaratisha taifa hili alafu tuanze kulaumiana. kila mtu anajua hali ilivyo tete ya taifa letu, Watu wachache wanatikisa nchi kwaajili ya ubinafsi wao na kutishia amani shauri ya ufisadi.


Ninachoona sasa katika taifa letu ni mgawanyiko, wa dhahiri kabisa unaotukana na ubinafsi, ufisadi, utafutaji umaarufu wa kijinga, uwekaji pesa mbele kuliko maslahi ya taifa hasa katika yale mambo ya msingi yanayo tuleta pamoja. tumekuwa wabomoaji wa taifa na sio wajenzi, Vyombo vya habari ambavyo vingetumika kama tool ya kujenga utaifa vimekuwa vyombo vya kisiasa vinavotumiwa kufanya propaganda kwa maslahi ya magenge, Kumekuwa na uhuni mkubwa unaendelea katika taifa letu, Waliopewa dhamana wanaacha kufuatilia mambo ya msingi na kufuata starehe na anasa.

Kuanguka na kunyanyuka kwa tawala yeyote ile kunategemea sana misingi ya kimaadili na kinidhamu ya taifa hilo, pasipo nidhamu taifa lolote halitoweza kupiga hatua ya kimaendeleo.

Taifa lisilokuwa na nidhamu ni kama mbegu zilizomwagwa shambani bila mpangilio. haliwezi kuzalisha chochote, mimea itaota na kufa. Utakuwa na watu upande mmoja wanajenga taifa na upande mwingine wanaiba kile tunachokijenga. utakuwa na viongozi wasiowajibika na wafanyakazi wanaofika kazini saa tatu, utakuwa na wabunge wanaochaguliwa vijijini na kuja mjini kustarehe badala ya kuishi na wananchi na kujua matatizo yao na kuyatatua kwa pamoja. Tutakuwa na taifa lisilokuwa na mpangilio wala heshima.


Hatutaweza kujenga taifa la watu wanaojitolea kwa dhati kwaajili ya ujenzi wa taifa lao wenyewe. Tutazaa watu wabinafsi na mantiki yote ya sisi kuishi kama taifa itafutika, kutokana na huu ufisadi na ubinafsi utatupelekea tupigane vita na taifa tulilolijenga litafutika kabisa. Ni lazima kila mmoja wetu katika taifa hili ajue ana jukumu la dhati kabisa katika ujenzi wa taifa hili, kwasababu majaliwa ya taifa hili ni majaliwa ya kila mmoja.

Elimu na sheria vina nafasi kubwa sana katika kujenga maadili ya jamii, katika mwelekeo tunaoutaka na katika kubadilisha tabia za watu. ili kujenga raia wema na kuunda taswira ya taifa tunalolihitaji, kulinda utaratibu na muundo mzima wa taifa. Pasipo sheria hatuwezi kuwa na kitu kinachoitwa taifa. ni kama yai na gamba lake.Taifa lisilotii utawala wa sheria kunauwezekano mkubwa taifa hilo likasambaratika. sheria ndizo zinazolinda taifa. Ni jukumu la kila raia kuzitii, Kwani tumejiwekea sisi wenyewe kama mwongozo wetu, zinalinda haki za kila mmoja wetu na mahusiano yetu kama binadamu. Tumeunda mahakama, bunge, polisi nk Lengo letu ni kujenga jamii bora yenye nidhamu na utaratibu, amani yetu itakuwepo ikiwa vyombo hivi vitafanya kazi yake kikamilifu na kwa uaminifu na kwa mashirikiano bila kuangalia vyama bali vikisukumwa na uzalendo na hamu ya kuona taifa hili likiendelea, lazima tutambue sisi ni watu wamoja na lazima tuwe na malengo kama taifa.

Ni jukumu letu kila mtanzania mzalendo kuamua na kujenga roho ya uzalendo ndani yake na kujifunza kutokana na utumwa waliopitia mababu zetu. Lazima tujiulize ni nini tunajivunia kama taifa? ni kitu gani tunachoweza kusema mbele ya mataifa mengine na kujivunia ? wakati umefika kwa taifa hili kuacha kuendelea kuishi bila malengo, lazima tujitoleee nafsi zetu na maisha yetu kwa ajili ya ukombozi wa taifa hili. Mimi kila wakati naamini kama tutahangaika kwa pamoja, kama tutakuwa wazalendo kwa kulipenda taifa letu na kulitumikia tutafanikiwa, sijaona popote duniani watu walipokuwa na lugha moja na nia moja walifeli katika harakati zao.

Ni lazima tufanye harakati za ukombozi wa taifa hili. Lazima tutangaze vita, vita ya kulinyanyua taifa hili dhidi ya maadui aliosema mwalimu nyerere, kufikiria uvumbuzi na kuacha kuwa watu wa mizaha na kufuata mambo ya kijinga tuwe wamoja na tujenge taifa letu kwa nguvu moja. Udhaifu wetu unatokana na kutokuwa wamoja kwetu, Umoja katika malengo ndio njia na mkombozi sahihi wa taifa letu. Umaskini wetu unatokana na udhaifu wa viongozi wetu, Ufisadi, ujinga na kutokjitolea kwetu kwa dhati kwaajili ya taifa letu.Naandika leo hii kwenu kama wito wa uzalendo na uhuru. wenye lengo la kuleta mapinduzi. Mapinduzi sio kutoa serikali moja na kuiweka nyingine, mapinduzi ni kuondoa mfumo mzima na kuuweka mwingine. Mfumo wa ufisadi, fitna, ubinafsi choyo na kila takataka. Tujenge nchi yetu katika umoja , uzalendo na kujitolea ili kujenga taifa imara na tishio.


Tuna wito sasa hivi, wito wa kizalendo utakaopelekea taifa letu kujitegemea. Tunatukanwa kwasababu hatutaka kujitegemea na hili liwe fundisho kwetu tuwe na machungu ya kujitegemea kama taifa ili tuwe na uhuru, ili tuheshimiwe, Hakuna mtu atakaye kuheshimu kama wewe ni ombaomba tutatoka kwa donor mmoja hadi mwingine lakini hakuna hatakaye tuheshimu. Vijana wa taifa hili natumia wakati wangu kuamsha hisia zenu ndani yenu za kizalendo ili mpate mwanga na kulipenda taifa hili nakulitumikia ili kuleta heshima, naongea na nyinyi kwasababu nyinyi ndio wenye nguvu, nyinyi ndio mtakaoleta mapinduzi ya kweli katika taifa letu. Serikali yeyote isiyokuwa na malengo ya kujitegemea kwa taifa letu, isiyokuwa na malengo ya kuleta watu pamoja, isiyokuwa na malengo ya kutumikia wananchi haina budi kutoka madarakani, ili tulete heshima kwa taifa letu. Watu wazalendo wenye hamu ya kuleta maendeleo kwa taifa hili wapo na wenye uchu wa dhati kabisa kwa maendeleo ya taifa. Lazima tujue mwelekeo wa taifa hili na baadae yetu.

Mapambano yangu sio dhidi ya chama chochote au kikundi chochote cha watu, Mapambano yangu dhidi ya mfumo wa uovu wa rushwa na ufisadi unaoangamiza taifa na umoja wetu, Mapambano yangu ni dhidi ya ubinafsi, ili kuleta umoja na mshikamano wa watu wa taifa hili, ili kuleta mwelekeo na dira kwa taifa letu, ili kuunganisha juhudi katika ukombozi, ili kuleta uzalendo na uhuru wa kweli wenye kujitegemea............

Aluta continua!
 
''Aim must be the well being of our country''
 
Uko wapi uzalendo wetu vijana ikiwa mnakubali kuuza nchi kwa kuchumia matumbo yenu!?


Shame on you,shame on you.Unexpected matter amongst unexpected guys where are we leading for?

Nimekuwa mara nyingi nikiumia sana moyo kutokana na tuhuma nyingi zinapo angukia kwa vijana hasa katika suala la kushindwa kiuongozi.Ndiyo maana nimekuwa muumini mzuri kupinga umri wa urais kuwa chini ya miaka 40.

Wakati bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania enzi ya mfumo wa chama kimoja ilikuwa nadra sana kusikia wazee wale(wabunge) kutuhumiwa kula rushwa tofauti na sasa au kwa kuwa tu uwazi hakuwa kama hivi sasa.

Cha ajabu na kweli yanayo jiri leo na yanazidi kukithiri ni kitendo cha wawakilishi wetu(wabunge) kuhusishwa na rushwa ili kuiuza nchi yetu kwa ajili ya kuchumia matumbo yao.Mbaya zaidi watuhumiwa hao wamekuwa vinara wa kujipambanua kuwa watetezi wa wanyonge.

Cha kushangaza miongoni mwao wapo vijana ambao tuliwaamini kutokana na utendaji wao wa kutukuka lakini leo hii wame tuangusha,tunategemea nini.Kwanini vijana wenzetu hampendi kutembea ndani ya maneno yenu.Ikiwa mnakubali kuhongwa kwa ajili ya kuzorotesha maendeleo na kudumaza uchumi wa nchi,je mkipewa nchi si mtatuuza sisi pamoja na mali zetu!

Napozungumzia kudumaza uchumi ni kutokana na kukubali kuhongwa ili kuzidi kuusimika uongozi unaopenda nchi iwe TANZAGIZA kwa strategic za kubumba wakati zinapingana na hali halisi.

Niliwahi kuzungumza huko siku za nyuma kuwa bunge letu linatakiwa livunjwe kutokana na kukosa uzalendo wa kuwa simamia na kuwawakilisha wananchi wake,leo hii yamedhihirika.Pia niliwahi kutuma ujumbe kupitia JF kuitaka kamati ya POAC ya mh.Zitto kufuatilia ufisadi unaofanywa na viongozi ndani ya Tanesco kuhusiana na ununuzi holela wa matairi pamoja na rim zake kuwea hazikidhi hali ya kitanzania,kamati ilikaa kimya kumbe ikijua kuna maslahi ya wajumbe ndani ya Tanesco.

Dr Slaa aliwahi kusema"unapo mnyooshea mwenzako kidole lazima uangalie usafi wako kwanza ndipo unyooshe kidole"Kwa hili la leo ndani ya bunge tunataka ripoti iwe wazi,kwani hata kiti cha Spika kimekuwa kinatumika vibaya katika kufumbia macho ubaya wa wajumbe wake.

Mwl Nyerere aliwahi kusema"mke wa Caeser hatakiwi kuwa na doa la ubaya"Kwa falsafa hii ya mwalimu mh.Spika chini ya bunge lake ameshindwa kukidhi hadhi ya kiti hicho na bunge lake kutuhumiwa kuhongwa kuliko mabunge yote yaliyopita.Kwa mantiki hiyo basi naye anatakiwa kujiuzuru kisiasa japokuwa yeye hajahongwa ila bunge lake kupitia kamati ya kudumu ya ya hesabu za serikali(POAC) imehongwa.

Na mwisho natoa wito kwa vijana wenzetu pamoja na wana JF kuwafunda vijana wenzetu ili waweze kuangalia kwanza maslahi ya taifa na njaa baadae.Njaa ni kweli zinauma lakini ukiziendekeza unaewza kuzivalia kibwaya.
 
Well said sammosses,hata sijui hii nchi inakwenda wapi,kama mhimili wa mwisho wa kurekebisha mihimili mingine,bunge,nalo limeoza kwa rushwa,mpaka wabunge wengine wanafikishwa mahakamani,am just lost to be honest
 
Well said sammosses,hata sijui hii nchi inakwenda wapi,kama mhimili wa mwisho wa kurekebisha mihimili mingine,bunge,nalo limeoza kwa rushwa,mpaka wabunge wengine wanafikishwa mahakamani,am just lost to be honest

Nafikiri tujaribu kuangalia kama kuna mtu ana jua sheria ama kanuni ya kutokuwa na imani na bunge atuwekee hapa ili tuweze kufanikisha tunawang'oa wabunge maslahi ili tuweze kuunda bunge kama chombo cha kuwatetea wanyonge
 
Its true that sometimes we fail to understand what our representatives are doing in the parliament.

Its also hard to believe that what we expected from them is quite different from what they are doing now. We believed in them and entrusted all our faith to them to say on behalf of us and present our problems in all aspects ranging from social, political, economic and welfare to the government, but thing are opposite, they are there just for their sake and for the betterment of their Political parties, their families and but enough for their stomach.

Youths are no long the dream and the future of this country. They are doing what we didn't send them to do. Things are really discouraging and there is no more faith on them. we have lost another five years!!!!

From the Government, Parliament and the judiciary, things are not clear and there are claims and blames now and then, where will we say that we have won? In which sector we are capable of saying that we have at least succeeded?

Shame on all Tanzanians who put this kind of GOVERNMENT on POWER!!!! Thing will never change unless we change the whole GOVERNMENT, the ROOTS of the SYSTEMS that have led us into TOTAL POVERTY....this is not possible under CCM.....I'm sure THINGS WILL BE THE SAME UNDER THE SAME PARTY...CCM.....!!!
 
Mimi nadhani issue siyo wazee au vijana na pia sikubaliani na hoja ya vijana kupewa urais napenda tuchague rais bila kujali ni kijana au mzee ili mradi anakidhi vigezo tulivyoweka kigezo namba moja ni kujali maslahi ya nchi yetu tatizo tulilonalo na bado litaendelea kutusumbua ni mmonyoko wa maadili na limekuwa kubwa baada ya kuvunjwa azimiio la arusha tusipotenganisha uongozi na maslahi binafsi tutakuwa watu wa kutafuta sababu mara vijana,wazee,udini,ukabila
 
Rais wetu amekuwa mara nyingi is out of his talks,ana weza sema lazima tutenganishe siasa na biashara but he failed to acknowledge things from his tips of mouth is real his desire.We discouraged with all things going on under an umbrella of system.But the main plan is to eliminate locally party by using ballot paper for the coming election.Hatuwezi kuwa watu wakulalamika kila siku.

Pia sipendi kuamini vijana ni taifa la kesho,though they were not capable to show their streangth of feelings if they can.Obama alipingia ikulu ya Marekani alisema movement for change,yes we can by cooperation amongst us,lakini kwetu wabunge wetu vijana wameshindwa kuonyesha integrity na kukubali kutumika kama chombo cha kuzidi kuwanufaisha mafisadi,wapi tunakwenda with this dump country.
 
Wapo Wabunge kama wanne vijana zitto yumo na mwenzie December Marope ambao wana ukwasi wa kutisha. Huyo mwingine ambaye hakupewa kura hata moja aana miradi mikubwa sana ndani ya TANESCO ambayo inafahamika. Amewahi kunukuliwa na wafanyakazi wa TANESCO akiomba tenda akiwa mwenyekiti wa kamati fulani la bunge, kwamba angeleta wawekezaji toka India. Wanaokabiliwa na tuhuma nzito ni wale waliochukua uongozi mwezi uliopita.

Wale waliotangulia wako wapi? Waandishi tulijaribu na kupigwa STOP hata kabla ya kuanza. Mtu huyu ana madudu makubwa sana lakini Kila mtu Kimya. Kulikoni?

Sitaji jina kwa sabau thread yangu itaondolewa dakika 20 zijazo, wote mnamjua tu.
 
Wapo Wabunge wabunge kama wanne vijana zitto yumo ambao wana ukwasi wa kutisha. Mwingine ambaye hakupewa kura hata moja, ana miradi mikubwa sana ndani ya TANESCO ambayo inafahamika. Amewahi kunukuliwa na wafanyakazi wa TANESCO akiomba tenda akiwa mwenyekiti wa kamati fulani la bunge, kwamba angeleta wawekezaji toka India. Wanakabiliwa na shutuma nzito ni wale waliochukua uongozi mwezi uliopita. Wale waliotangulia wako wapi?
Waandishi tulijaribu na kupigwa STOP hata kabla ya kuanza. Mtu huyu ana madudu makubwa sana lakini Kila mtu Kimya. Kulikoni?

Nani huyo? Januari Makamba?
 
we mtaje tu mkuu jina lake km ni february marope au december manyuzi watu wajue.
 
Kumbukeni huyu MaRope alichukua dollar million moja za mzungu kupitia kwa dada yake zilizomuwezesha kumuondoa Shellukindo mjengoni; na ahadi aliyotoa kwa yule mzungu ni kuwa angeupata uwaziri wa nishati na madini na hapo angerudisha zile fedha!!!

Hakufaninikiwa kupata uwaziri wa Nishati lakini alifanikiwa kupata uenyekiti wa kamati ya bunge ya Nishati na madini; Je aliitumia kamati ille kujipatia fedha zikiwemo zile za yule mzungu na kama ni hivyo inawezekana baadhi ya fedha hizo zilitoka TANESCO?

Tafakali.
 
Kaaaazi kwelikweli!!!!!

Ina maana hakuna msafi hata mmoja!!!!!!!!!!!!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Ni Bora Tanzania ingeendelea kutawaliwa na Wakoloni kuliko huu Uhuru wa kuibiana huu tunaouona sasa. Kama kila kitu kinaibiwa si bora tungeendelea kutawaliwa! Inatisha sana.
 
Mkuu Escobar umenena vema hata mimi nilikuwa najiuliza sana huu uswaiba wa February ma-rope na nyepesi ulitoka wapi na ulikolezwa na kitu gani?mbona huko nyuma hatukuwahi kuusikia?ghafla tulikuja kuona they are close friend,anyway si hoja lakini hapa kwa taarfia hii nadhani kuna uhusiano wa kifisadi kama mkuu mmoja anavyosema,tena ni mwandishi kwa madai yake kwamba alijaribu kuhoji ukwasi wa february wakapigwa stop,nadhani vijana hawa ni hatari,kwa kweli natamani nitangaze kuwa hawa madogo ni janga la taifa.
 
Back
Top Bottom