Wito: "wanaoua Albino na wenyewe muwaue!" - Pinda

Ilibidi ieleweke raisi wetu alikuwa katika ziara hiyo kichama au kiserikali
kama ni chama basi chama chake kupitia msemaji wake wangetoa maelezo ya
ziada kutokana na kauli hizo za raisi na kama ni serikali basi tujue ule
ndio msimamo wa serikali na iwekwe kwa njia ya maandishi kwamba serikali ya
jamhuri ya muungano wa tanzania msimamo wake ni huo


inatia uchungu sana unapoona viongozi wetu wakuu wanavyokuwa na kauli za
ajabu ajabu kama hizi na ambazo vyama vyao wala serikali haijutii kauli hizi
wala kuja mbele ya vyombo vya habari kutolea maelezo ya ziada


mimi naona kiongozi anapokuwa katika shuguli za kiserikali kama ilivyokuwa
kwa yeye kikwete asiruhusiwe kabisa kujihusisha na vijembe au kufanya
shuguli za kichama pale ameenda kutumikia wananchi wa jamhuri ya muugano wa
tanzania ambao serikali yao haina dini wala kabila .


Kama wataendelea na kauli hizi basi wawe na wasemaji wao ambao ndio kazi yao
hiyo


--

...mmhh...vipi tena mkuu........hapa anazungumziwa Mizengo Pinda - Waziri Mkuu.....au?
 
people are wrong to assume that he didn't say what he is said to have said.. and are also wrong to assume that he didn't mean what he said.
 
Magobe....well said,

i couldn't agree with you more than what you wrote above,........however, experience ya watu wengi hapa kuhusu waandishi inatufanya tuangukie mitego ya ku-undermine taaluma hii ya uandishi wa habari........wakati mwingine tukisoma taarifa kutoka magazetini tunaogopa ku-comment.....simply bse facts ni ndogo kuliko "rhetorics" in a way.........

vinginevyo......nakubaliana na wewe......pple don't underestimate hii fani ya uandishi wa habari.........

Ogah, asante kwa mchango wako. Unajua watu wengi hawajui uandishi wa habari ni kitu gani na hivyo wanadhani wasipoelewa kitu ni lazima walaumu taaluma yenyewe na kudhani waandishi siyo wasomi - hawajaenda shule na siyo watu makni.

Ila inabidi na sisi tuwe na uelewa na tuwe tunajiuliza maswali. Kuna mfano ninataka niutumie kuonyesha namna mojawapo waandishi wa habari wanavyoweza kuandika kitu sahihi lakini wasomaji wakaona wamepotoshwa. Ukisoma habari iliyoandikwa hivi (soma hapa chini), utasemaje waandishi ni waongo?


Juma alikuwa akiendesha gari lenye abiria 30. Mara alipata ajali saa 7 mchana na abiria 3 walikufa papo kwa hapo, 20 walikimbizwa hospitali na abiria wengine 7 walikuwa wazima.

Tuchukue kuwa habari zimewafikia waandishi wa habari kutoka vyombo vya habari 3 (X,Y, Z) na kila mmoja akatuma mwandishi mmoja.

Mwandishi kutoka chombo cha habari X alifika sehemu ya ajali saa 7:10 mchana kabla maiti au majeruhi hawajapelekwa hospitali; mwingine kutoka chombo cha habari Y alifika sehemu ya ajali saa 8:30 na kukuta vijana wakisaidia kuinua gari na hivyo akaonelea aende kuuliza hospitali kujua idadi kamili ya waliokufa na majeruhi na wa mwisho kutoka chombo cha habari Z alipigiwa simu kuwa maiti 3 na majeruhi 10 wamepelekwa hospitali. Kesho yake unafikiri habari zitakazoandikwa kwenye vyombo vya habari 3 zitakuwa sawa?

Obviously, mwandishi wa habari kutoka X aliyefika saa 7:10 mchana atasema 'Ajali ya gari mchana imeua 3, imejeruhi 20 na 7 ni wazima'.

Mwandishi wa habari aliyefika saa 8:30 anaweza akaripoti karibu sawa na X kwa vile atakuta tu eye-witnesses na pengine kwa vile alifika pia hospitali anaweza kukuta majeruhi wengine 2 wamekufa. Hivyo yeye atasema, 'Ajali iliyotokea saa 7:10 imeua 5, kujeruhi 17 na 7 ni wazima'.

Mwandishi kutoka Z ataweza kwanza kufika sehemu ya ajali, kisha kwenda hospitali na baadaye kuonana na wale wazima 7. Akifika hospitali anaweza kukuta idadi ya waliokufa imeongezeka na majeruhi imepungua na pia anaweza kukuta wawili kati ya wale waliosema ni wazima wamegundua tatizo baadaye walipofika nyumbani na hivyo wakaonelea waende hospitali (kwa nia ya kulazwa kama itabidi). Kwa hiyo yeye habari yake itasomeka 'Ajali iliyotokea jana mchana, iliua watu 7, majeruhi 8 na 5 ni wazima'.

Tukio moja reporters 3 na stories 3 tofauti - lakini zote zinazungumzia tukio lilelile ila muda wa reporters kufika kwenye tukio ni tofauti na kwa vile muda ni tofauti, obviously baadhi ya details za tukio zitakuwa tofauti pia.

Wasomaji wakisoma hizi stories 3, kwa vyovyote watalaani waandishi wa habari wakidhani wamewapotosha. But in the actual sense, kila mwandishi aliripoti kitu sahihi kabisa kadiri ya ama alivyoshuhudia au kupata habari ya ajali ilivyotokea.

Mara ngapi tunasikia hoja za namna hii lakini ni nani alisha'take time' kutafakari kwa nini tukio moja linaweza kuripotiwa na watu 3 na kila mmoja akawa na details tofauti? Hivyo, tujitahidi kuilewa hii taaluma. Ni 'technical' na siyo lazima details zikiwa tofauti au habari ikiwa haijitoshelezi basi waandishi hawajui, NO. Wakati mwingine it is done purposely ili wahusika waliojaribu kuficha habari fulani watoe habari hizo wao wenyewe kwa umma.

Mfano, mwandishi akienda polisi kupata habari na akinyimwa ushirikiano ataandika bila details lakini atasema: 'Polisi alipoulizwa kuhusu habari hii alikataa kutoa ushirikiano na polisi mwenyewe atakapokabwa na wakubwa wake atasema 'Mwandishi wa habari ameni'quote' vibaya'. Kwa hiyo, inabidi tujifunze intricacies za journalism na siyo kulaumu tu bila kujua namna gani habari zinapatikana. Siyo rahisi kupata habari kwa vile watu wengi hawana ushirikiano. Kwa upande mwingine baadhi ya waandishi wa habari wana mapungufu. Lakini tusiidharau taaluma hii; inatufundisha na kutuhabarisha mengi kuliko hao wanaodhani ni wasomi kuliko waandishi wa habari wanavyotufundisha/tuhabarisha.
 
Last edited:
Hata Mwakyembe jana ame vindicate ninacho ki-guess kila siku humu kwamba waandishi ni watoto wa shule. Mwakyembe kasema mwandishi wa MwanaHALISI aliyemnukuu juzi ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza Nyegezi. !

Kuhani, kama mwakyembe amesema maneno hayo basi Mwakyembe basi inabidi nihoji umakini wake wa kusoma na kufikiri. Mwandishi wa Mwanahalisi(tena si wa habari, ni wa makala) hakumnukuu Mwakyembe, alinukuu alichonukuliwa Mwakyembe na mwandishi wa Mwananchi Januari 14 kutokana na mkutano wake wa Kyela maneno ambayo Mwakyembe hakuyakanusha siku zote. (Same as Pinda, kama amenukuliwa vibaya alipaswa akanushe au ofisi yake ikanushe na kusema bayana alichokisema hasa ni nini).

Kwa hiyo:

1. Aliyeandika maneno ya Mwakyembe na kumnukuu kwenye habari ni mwandishi wa Mwananchi, ambaye si mtoto wa shule.

2. Kilichoandikwa na Mwanahalisi ni Makala ya uchambuzi ambayo ilinukuu habari ya Mwananchi, sasa badala ya kulaumu makala ya Mwanahalisi; Mwakyembe alipaswa kuihukumu habari ya Mwananchi(kama iliandika kitu ambacho hakusema) na kuhoji umakini wa Mwananchi badala ya kuhoji uhuru wa Mwanahalisi kuchapa makala ya uchambuzi.

Its crummy press or crummy politicians?

.........ndiyohiyo.
 
Kuhani, kama mwakyembe amesema maneno hayo basi Mwakyembe basi inabidi nihoji umakini wake wa kusoma na kufikiri. Mwandishi wa Mwanahalisi(tena si wa habari, ni wa makala) hakumnukuu Mwakyembe, alinukuu alichonukuliwa Mwakyembe na mwandishi wa Mwananchi Januari 14 kutokana na mkutano wake wa Kyela maneno ambayo Mwakyembe hakuyakanusha siku zote. (Same as Pinda, kama amenukuliwa vibaya alipaswa akanushe au ofisi yake ikanushe na kusema bayana alichokisema hasa ni nini).

Kwa hiyo:

1. Aliyeandika maneno ya Mwakyembe na kumnukuu kwenye habari ni mwandishi wa Mwananchi, ambaye si mtoto wa shule.

2. Kilichoandikwa na Mwanahalisi ni Makala ya uchambuzi ambayo ilinukuu habari ya Mwananchi, sasa badala ya kulaumu makala ya Mwanahalisi; Mwakyembe alipaswa kuihukumu habari ya Mwananchi(kama iliandika kitu ambacho hakusema) na kuhoji umakini wa Mwananchi badala ya kuhoji uhuru wa Mwanahalisi kuchapa makala ya uchambuzi.

Its crummy press or crummy politicians?

.........ndiyohiyo.


Kuhani:

Ushahidi huu hapa chini;

Aliyemnukuu Mwakyembe ni Mwandishi wa Mwananchi Richard Kilumbo ambaye si mtoto wa shule. Kama Mwakyembe aliona kauli hii ni ya uongo kwamba hakusema maneno hayo, angekanusha. Badala ya kumlaumu Mwanachuo Kikuu Isango Josephat(ambaye umemuita mtoto wa shule) kwa kuandika Makala ya Uchambuzi kwenye Mwanahalisi kuchambua madhara ya kauli ya Mwakyembe kama ilivyonukuliwa na Mwananchi.

Hapa ni kama Pinda, badala ya kulaumu Mwananchi na Tanzania Daima, Pinda aeleze ni ni hasa alisema sio nini alimaanisha. Akanushe hizo kauli alizonukuliwa na hayo magezeti kama hawawezi kukanusha basi wote Pinda na Mwakyembe waache umma uzijadili hizo kauli zao.


Dk. Mwakyembe awakatalia wapiga kura kuondoka CCM
Richard Kilumbo,Kyela

MBUNGE wa Jimbo la Kyela Dk Harrison Mwakyembe,amesema hana mpango na wala hafikirii kukiacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kujiunga vyama vya upinzani nchini.

DK. Mwakyembe alisema hakuna Chama chochote cha upinzani kinachoweza kufananishwa kwa ubora , umakini, uzuri wa sera na hata uwingi wa wanachama na CCM.

Kauli hiyo aliitoa juzi kwenye mkutano wake na wananchi wa jimbo lake uliofanyika viwanja vya Siasa mjini hapa ambapo baadhi ya wananchi walimtaka kuihama CCM ili afanye kazi ya kufichua mafisadi kupitia kambi ya upinzani.

Mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Erick Satta mkazi wa mjini hapa alisema wananchi wa jimbo lake wanamwamini mbunge huyo kwa kiwango kikubwa, lakini wanaingiwa na shaka na mahali aliko (CCM)ambako alisema wananchi wanaamini, mbunge wao anabanwa, na hawezi kusema lolote linalopingana na sera na itikadi ya Chama.

Satta alisema ili aweze kufanikisha azma ya kuwakomboa wananchi wa Tanzania mbunge huyo hana budi kubadilika na kujiunga na mageuzi ambako ataungwa mkono kutoka kwa wananchi na viongozi wenzake wa vyama vya upinzani.

Alimtaka mbunge huyo kukubaliana na matakwa ya wananchi wengi wanaomshinikiza kuihama CCM kwa madai kimejaa mafisadi wasiowezwa kushughulikiwa na kiongozi wa ndani ya Chama hicho.

" Tunakupenda,tuko nawe na tutakuchagua mwaka 2010, ukiwa ndani ya Chama kingine, cha Siasa na siyo CCM" alisema Satta.

Akijibu hoja kwa kupinga msimamo huo, Dk. Mwakyembe aliwabeza wale wote wanaomshinikiza kuihama CCM na kusisitiza kwamba, hapa nchini hakuna Chama cha siasa kilicho makini na chenye sera safi zinazotekelezeka na chenye wanachama wengi kuliko CCM.

Dk. Mwakyembe alisema, mtu yeyote anayetaka kupambana na maovu yanayofanywa na baadhi ya watu walio na nia mbaya na Taifa lao hana budi kuendelea kubaki ndani ya CCM.

"Ukitaka kufanya mambo yako vizuri,na unataka usikilizwe, uishi maisha marefu ni bora, ubaki CCM kuliko ukawa kwenye upinzani na kupayuka mambo bila ushahidi wa kutosha.

Alisema utetezi na uchungu wa mtu yoyote hauwezi kusikika, na kufanyiwa kazi kwa kina, kama utafanywa na wapinzani walio nje ya CCM.

Akitetea msimamo wake alisema ni lazima watu washindane na kubezana kwa hoja kuliko kuleta ubishi usio na manufaa.

"Fikiria ujasiri unaofanywa na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete , ni mkubwa mno, lakini wapo watu wanaobeza jambo ambalo hata CCM ingefanya nini, wapo watu ambao wataendelea kubeza tuu.

Alisema, Rais Kikwete amefanya mambo mengi na yenye ushujaa kwa kuweza kuwafikisha viongozi waandamizi aliowahi kufanya nao kazi katika awamu mbalimbali akiwa Waziri , lakini amefanikisha kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola wakituhumiwa kuitia hasara Serikali ya awamu ya tatu kwa kuruhusu msamaha wa kodi ya Sh 11 bilioni.

"Hivi, ni nani kati yenu, anayeweza kuruhusu rafiki yake wa karibu akamatwe, hata kama amekosea?, na ni Kiongozi gani katika awamu zote tatu zilizopita aliyeweza kuwa jasiri akaruhusu marafiki na viongozi wenzake wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya dola kama si Rais Kikwete"aliwauliza wananchi Dk.Mwakyembe.

Hata hivyo, pamoja na kusifia mafanikio mbalimbali yaliyoletwa na Serikali ya awamu ya nne, Dk Mwakyembe alizungumzia pia kazi nzuri iliyofanywa na Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, ambaye alisema aliimarisha na kuinua Uchumi wa nchi.

Kuhusu sakata la kukatika katika kwa umeme wilayani Kyela , mbunge huyo alisema atayapeleka mawazo ya wananchi waliomtaka mbunge wao ayafikishe mambo hayo kwa Waziri wa Nishati na Madini William Ngereja ya kuruhusu wananchi wa Kyela wautumie umeme unaozalishwa na Kiwira Coal Mine ili kuepuka na kero hiyo.

Chanzo: Mwananchi


Na Isango Josephat Ng'imba

HUYU ndiye Dk. Harrison Mwakyembe au vyombo vya habari vimetudanganya? Soma kauli aliyonukuliwa akitoa na kukaririwa na gazeti la Mwananchi toleo la 14 Januari 2009:

"Ukitaka kufanya mambo yako vizuri, na unataka usikilizwe, uishi maisha marefu, bora ubaki CCM kuliko ukawa kwenye upinzani na kupayuka mambo bila ya ushahidi wa kutosha.”

Tumesoma kuwa Mwakyembe alitoa kauli hiyo kwenye mkutano na wananchi wa jimbo lake uliofanyika viwanja vya Siasa, mjini Kyela ambako baadhi ya wananchi walimtaka kuhama CCM ili afanye kazi ya kufichua mafisadi kupitia kambi ya upinzani.

Akijibu hoja za wananchi hao, Dk. Mwakyembe alitumia maneno niliyonukuu hapo juu ambayo ndio chanzo cha hofu yetu kuhusu “mpiganaji huyu.” Kauli hii inalenga kutuambia nini?

Hii ina maana hakuna usawa? Kwamba katika CCM utasikilizwa lakini katika upinzani utapuuzwa? Kumbe madai ya upinzani kuwa utawala huu hauna usawa ni sahihi?

Kwamba “maisha marefu” yanapatikana CCM peke yake? Kwamba walioko upinzani maisha yao mafupi kwa kuwa hawaungi mkono CCM? Hii ni kwa kuwa ni masikini, hawana chakula au ni maadui na hivyo watauawa na CCM?

Nadhani Mwakyembe alisema haya bila kujua kutakuwa na mwandishi wa habari kunukuu kauli yake. Vinginevyo anajua uwezo mkubwa wa wabunge wa upinzani na umma mkuu ulioko nje ya bunge na nje ya vyama.

Mikataba ya ovyo kama ule wa Buzwagi; kashfa ya Richmond iliyomwangusha Edward Lowassa katika uwaziri mkuu; wizi mkubwa Benki Kuu na mengine, yameibuliwa na wabunge hawa. Kwanza yalibezwa, baadaye yakakumbatiwa; CCM ikayadandia kutafuta umaarufu.

Mwakyembe anataka kusema nini kwa wananchi wa jimbo la Kyela wasiokuwa CCM? Je, yeye alichaguliwa na wana-CCM peke yao? Je, maadili ya kujua mema na mabaya yanatofautishwa kwa kutumia misingi ya uanachama wa vyama vya siasa?

Kama ni lazima kuwa CCM au kubaki humo ili ufanikiwe, ina maana wasio wanachama wa chama hicho ni watu wa kulaaniwa? Mwakyembe anatufundisha nini sisi tuliomwona mzalendo, aliyesimama bila kutetereka kutetea maslahi ya nchi katika sakata la Richmond?

Kama alivyonukuliwa ndivyo alivyo; kwa maana kwamba amekuwa akificha sura yake halisi, na kwamba anaona kuwa maisha nje ya CCM hayawezekani, basi amejipunguzia sana heshima tuliyowahi kumpa.

Ina maana uchungu wa mwana-CCM kwa nchi hii unatofautina na uchungu wa mwana wa chama kingine? Kwamba tatizo la mwana-CCM ni tatizo zaidi kuliko tatizo la raia mfuasi wa chama kingine? Tunawaweka wapi wale wasio wafuasi wa chama chochote?

Nakaribia kushawishika kwa kauli ya rafiki yangu kuwa raia wa Tanzania si “Watanzania” maana “Watanzania” wana maisha bora kama kauli mbiu ya “maisha bora” inavyosawiri kwao. Sisi tusio na maisha bora si Watanzania.

Nisingejisikia vibaya iwapo Mwakyembe angesema atafanyia kazi ilani ya CCM na kwamba hana mpango wa kuhama chama chake, kuliko kutoa kauli zinazolingana na vitisho.

Nimesadikishwa kuwa kwa mwanafalsafa hakuna tamko la bahati mbaya. Nami naona Mwakyembe alikusudia kusema hayo na ameyasema. Kwa kuwa kila kauli ina gharama, basi kauli ya Mwakyembe imemgharimu heshima.

Mwandishi ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu – ualimu – Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine, SAUT, anayepatikana kwa simu: 0786-426414 na baruapepe: joseisango@yahoo.com

Chanzo: Mwanahalisi
 
Mwanakijiji,

Umeamua kuendeleza jambo lisilo na ukweli wowote.Nilikuonya asubuhi ila unaendelea tena kwa staili mpya,ulitaka kutumia pesa kupata habari ukashindwa..kwa faida ya nani sasa.?tujadili inshu za maana na siyo hili jambo lisilo na manufaa

Kuna tatizo la waandishi wetu tulio nao nyumbani.wanakurupuka wakisikia neno moja tu .

Mhe. Pinda hakusema maneno ya gazeti la Mwananchi

Huyu ni Waziri Mkuu wa nchi anawashauri wananchi wajichukulie sheria mkononi, anawaamuru vijana wa CCM wavunje sheria za nchi, anaonyesha dharau kwa katiba aliyoapa kuiheshimu na kwa mbwembwe na jeuri anatamka hivyo hadharani - halafu Gembe, msomi aliyebobea na anayetumia avatar ya Mwalimu, haoni uzito wala umuhimu wa kuhoji hili. Words fail me !!!
 
Umeua albino, kukata viungo vyake na nakukimbia navyo. Tunakufukuza na kukukamata, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama? Hatutaweza kusubiri, tutakuuwa tu!"

Mizengo Pinda

Umeiba fedha za umma, ukachukua na kupeleka kwenye akaunti yako ama kununua majumba ya kifahari. Tutakuvizia na kukuzunguka, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama kwa ufisadi? Hatutaweza kusubiri, tutakuzomea na kukupiga mawe tu!"

Asha Abdala
 
Umeua albino, kukata viungo vyake na nakukimbia navyo. Tunakufukuza na kukukamata, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama? Hatutaweza kusubiri, tutakuuwa tu!"

Mizengo Pinda

Umeiba fedha za umma, ukachukua na kupeleka kwenye akaunti yako ama kununua majumba ya kifahari. Tutakuvizia na kukuzunguka, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama kwa ufisadi? Hatutaweza kusubiri, tutakuzomea na kukupiga mawe tu!"

Asha Abdala

Asha

kama hizi kauli zinatoka kwa mwanachama mwa chama m-badala aliye mstari wa mbele kwenye strategic plan za kuhakikisha chama m-badala kinaingia chukua madaraka 2010; inaashiria kuwa huko chama m-badala hamjui au mnajua ila hamzingatii utawala wa sheria. Ni masikitiko makubwa kwa nchi yangu kama unayesema unataka kugombea uongozi huko chama mbadala unapigia debe mob justice!

Hakuna pa kukimbilia na chama kilichopo madarakani kitazidi kuitawala hii nchi miaka mingi ijayo.
 
Umeua albino, kukata viungo vyake na nakukimbia navyo. Tunakufukuza na kukukamata, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama? Hatutaweza kusubiri, tutakuuwa tu!"

Mizengo Pinda

Umeiba fedha za umma, ukachukua na kupeleka kwenye akaunti yako ama kununua majumba ya kifahari. Tutakuvizia na kukuzunguka, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama kwa ufisadi? Hatutaweza kusubiri, tutakuzomea na kukupiga mawe tu!"

Asha Abdala

Asha

kama hizi kauli zinatoka kwa mwanachama mwa chama m-badala aliye mstari wa mbele kwenye strategic plan za kuhakikisha chama m-badala kinaingia chukua madaraka 2010; inaashiria kuwa huko chama m-badala hamjui au mnajua ila hamzingatii utawala wa sheria. Ni masikitiko makubwa kwa nchi yangu kama unayesema unataka kugombea uongozi huko chama mbadala unapigia debe mob justice!

Hakuna pa kukimbilia na chama kilichopo madarakani kitazidi kuitawala hii nchi miaka mingi ijayo.

Hebu soma tena alichoandika ukielewe - hii kansa ya kukurupuka naona inaenea kwa kasi. Please read between the lines !!!
 
Mwandishi wa habari anaweza kuripoti ukweli fulani lakini ukakanushwa kwa makusudi na kwa bahati mbaya ukikanushwa kwa namna hiyo, huyo mwandishi wa habari ataonekana mwongo. Lakini anayekana ukweli ataonekana yuko sahihi.

Mwandishi wa habari anaweza akakatazwa kuripoti tukio fulani kwa vile linagusa maslahi ya watu fulanifulani au hata kama ataripoti owner wa gazeti anamwambia editor wake kuwa stori fulani isitoke kwenye gazeti lake au kama ikitoka anapewa nakala tofauti na ile ya mwandishi wa habari. Haya yanafanyika! Baadhi ya viongozi wana waandishi wao na hawataki mwandishi mwingine yeyote na kabla ya kuripoti kitu wanaambiwa kitu gani waandike.

Na ujue mwandishi wa habari anapoleta stori kwa editor siyo yeye (mwandishi wa habari) tena anayeamua hiyo stori itoke hivyo au ibadilishwe. Je, wewe ungekuwa mwandishi wa habari katika mazingira hayo ungefanya nini - yaani ulichoandika hakitoki vile na kama kikitoka unakuta kimebadilishwa baadhi ya 'contents' zake?

Unakumbuka pia kulitangazwa kuna njaa Singida au Arusha (sikumbuki vizuri pia ni mkoa gani kati ya hiyo 2) miaka michache iliyopita na kwamba mtoto mmoja alifuka kwa kukosa chakula lakini waziri fulani akakanusha na kusema alikufa kwa 'malnutrition' na siyo njaa? Yaani yeye alijidai anajua kilichomwua mtoto kuliko hata mama mzazi aliyekuwa hana chakula nyumbani.

Jounalists ni watu wanaojituma sana na wanafanyakazi kwenye mazingira magumu mno. Lakini sisi Watz tumejazwa tu na 'prejudice' kuhusu hawa watu na kwa bahati mbaya wakiripoti kitu ambacho ni sahihi na baadaye kikikanushwa na wakubwa kwa sababu fulanifulani za kisiaza tunaona wao ndio hawajui - hawana elimu!

However, kunaweza kuwa na 'factual errors' katika reporting, pengine kwa sababu watu waliotakiwa kuthibitisha walificha baadhi ya information. If that happens haina maana kwamba basi hii taaluma ni bure kabisa - 'shoddist of all professions'.


Kama haya ndio yamo kwenye taaluma ya uandishi wa habari, na kama ndugu wewe ni mwandishi wa habari basi umeconfess kuwa press ya Tanzania ni crummy, na shoddy.

Yaani hapa na wewe umeponda huo uandishi vile vile, umegongelea msumari wa moto kwenye kidonda. Hivyo usiseme unatetea. Waeleze ukweli hao waandishi wajue wapi wanateleza, wajifunze na kujirekebisha.
 
Umeiba fedha za umma, ukachukua na kupeleka kwenye akaunti yako ama kununua majumba ya kifahari. Tutakuvizia na kukuzunguka, je tukupeleke polisi tusubili uhukumiwe na mahakama kwa ufisadi? Hatutaweza kusubiri, tutakuzomea na kukupiga mawe tu!"

Asha Abdala

Hebu soma tena alichoandika ukielewe - hii kansa ya kukurupuka naona inaenea kwa kasi. Please read between the lines !!!

haya baba, maneno ya Asha hayo, yeye na wenzie hawataweza kusubiri mafisadi wahukumiwe mahakamani, watawapiga mawe tu.
 
Last edited by a moderator:
haya baba, maneno ya Asha hayo, yeye na wenzie hawataweza kusubiri mafisadi wahukumiwe mahakamani, watawapiga mawe tu.

Soma kauli ya Pinda halafu soma ya kwangu utaona kuwa ni Satire inayotaka kuonyesha ujinga wa Pinda na madhara ya kauli yake kwa mfumo mzima wa utawala wa sheria katika nchi yetu!
 
Kuhani, kama mwakyembe amesema maneno hayo basi Mwakyembe basi inabidi nihoji umakini wake wa kusoma na kufikiri. Mwandishi wa Mwanahalisi(tena si wa habari, ni wa makala) hakumnukuu Mwakyembe, alinukuu alichonukuliwa Mwakyembe na mwandishi wa Mwananchi Januari 14 kutokana na mkutano wake wa Kyela maneno ambayo Mwakyembe hakuyakanusha siku zote. (Same as Pinda, kama amenukuliwa vibaya alipaswa akanushe au ofisi yake ikanushe na kusema bayana alichokisema hasa ni nini).

Kwa hiyo:

1. Aliyeandika maneno ya Mwakyembe na kumnukuu kwenye habari ni mwandishi wa Mwananchi, ambaye si mtoto wa shule.

2. Kilichoandikwa na Mwanahalisi ni Makala ya uchambuzi ambayo ilinukuu habari ya Mwananchi, sasa badala ya kulaumu makala ya Mwanahalisi; Mwakyembe alipaswa kuihukumu habari ya Mwananchi(kama iliandika kitu ambacho hakusema) na kuhoji umakini wa Mwananchi badala ya kuhoji uhuru wa Mwanahalisi kuchapa makala ya uchambuzi.

Its crummy press or crummy politicians?

.........ndiyohiyo.

HabarindioHiyo,

Huyo mwandishi wa MwanaHALISI Mwakyembe amesema ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza Nyegezi. Na akaongeza kwamba huyu mwanafunzi alichukua info zake kutoka MWANANCHI.

Sasa hapo Mwakyembe kakosea nini kuonyesha kwamba katika mlolongo wa waandishi waliosambaza hizi habari kuna vi-rookie rookie vya shule humu! Responsible journalist huwezi kuchukua nukuu iliyoandikwa na wadaku wa MWANANCHI.

Sasa Habarindiohiyo, unatetea hawa ndugu zako waandishi, hebu nambie, kuwa mzalendo dakika moja, huyu mwandishi anaeuliza hapa Pinda hasa alisema nini sio yule yule alieandika taarifa inayosambaa na kusomwa all over the place sasa hivi akidai kwamba Pinda kasema hayo maneno, halafu kumbe hana uhakika, anaenda kuuliza wabunge wa CCM ambao nao hawakuwepo, mara anakuja kuuliza jamvini, mara anatoa zawadi kwa mwenye habari, wakati ameshaandika ripoti ndeeeefu ambayo hajai-retract bado, sasa jama kazi hizo sio upotoshaji huo? No, you tell me, utanambia tuna waandishi kweli hapo?

Kibaya kinachochekesha zaidi ni kwamba habari yenyewe imetoka kwenye mkutano wa wazi halafu mwandishi anasema aliyehutubia ana mpango wa kuficha alichohutubia! Kama kimefichwa mbona ametuhabarisha kwamba kimesemwa, umejuaje?

Wanaoua Albino nao wauawe - Pinda

Written by M. M. Mwanakijiji
Friday, 23 January 2009

KATIKA hali ya isiyo ya kawaida, Waziri Mkuu Mizengo Pinda jana aliwaambia wananchi kuwa wanaoua watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) pamoja vikongwe ni hawana budi kuuawa kwa kuwa wakisubiri mahakama kuwahukumu, watakuwa wanakosea. Waziri Pinda, ambaye ameanza ziara katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yenye lengo la kuhamasisha vita dhidi ya mauaji ya vikongwe na albino, aliutaka Umoja wa Vijana wa CCM kuongoza vita hiyo, akisema lina jeshi zuri.

Mauaji ya albino yamekuwa ni tatizo kubwa nchini na hasa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Pamoja na serikali kutangaza hatua kadhaa za kupambana na wauaji hao, bado matukio ya kuuawa kwa watu hao wenye ulemavu wa ngozi yamekuwa yakiendelea kuripotiwa, lakini Waziri Pinda ameenda mbali zaidi katika kukabiliana na tatizo hilo alipotaka wauaji hao wauawe badala ya kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Kauli ya Pinda, ambayo inaweka maswali katika suala la utawala bora, imekuja wakati ambao wananchi wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi na kuua vikongwe kutokana na imani za uchawi.

Akihutubia wakati wa kufungua mkutano wa 16 wa Shirikisho la Vyama vya Kuweka na Kukopa (SCCULT) kwenye ukumbi wa Chuo cha Utumishi Umma mkoani hapa, Waziri Pinda alisema iwapo wananchi wataendelea kuwahurumia wauaji hao ambao wanatafuta viungo vya albino wakitegemea mahakama itatenda haki huku nao wakiongeza kasi ya mauaji kwa Watanzania, watakuwa wanakosea.

Hivyo alisema kwamba kuanzia sasa mtu yeyote atakayemuona mtu amemkata shingo au mkono mweziwe basi naye auawe papo hapo hii itakuwa ndiyo dawa kwani vingozi wote tumechoka na mauji hayo.

"Mkimuona mtu akamkata mwingine shingo naye muueni kwani sasa viongozi wote tumechoka... no more, I can't tolerate anymore (imetosha, siwezi kuvumilia tena)," alisema Pinda huku akiwaacha watu midomo wazi.

Aliviomba vyama vya siasa kushirikiana na wananchi kuhakikisha suala hili la mauji linakwisha kwani wauji "tunaishi nao na ni rahisi kulimaliza iwapo tutakuwa kitu kimoja katika kuondoa kashifa hii ambayo imekuwa mbaya kwa nchi yetu".

Aliuagiza Umoja wa Vijana wa CCM kuhakikisha mauaji hayo yanatokomezwa kabisa, akisema kuwa ni jeshi zuri ambalo likiamua kutokomeza kabisa mauaji ya vikongwe na ndugu zetu maalbino inawezekana.

"Umoja wa vijana mna jeshi zuri ambalo naamini mkiamua mnaweza kutokomeza mauaji ya wazee wetu pmoja na ndugu zetu maalbno na kazi hiyo nawaagiza muanze leo msisubri auawe mwingine tena," alisema waziri mkuu.

Baada ya kumalizika kwa mkutano huo, baadhi ya watu wanaoonekana kuwa ni wa "serikali" waliwafuata baadhi ya waandishi wa habari, akisihi suala hilo lisiripotiwe magazetini kwa madai kuwa kauli hiyo ya Waziri Pinda inaweza kusababisha matatizo.

Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia amekuwa mstari wa mbele kupiga vita mauaji hayo, alitofautiana na Waziri Pinda katika moja ya hotuba zake aliposema kuwa adhabu ya kuua haitofautishi muuaji wa albino na muuaji mwingine na kwamba watakaopatikana na hatia ya kuua albino, atakabiliana na adhabu ya kifo kama ilivyo kwa muuaji mwingine.

Waziri Pinda alionekana kukerwa na mauaji ya albino wakati alipopata taarifa kwamba kuna mama mwingine aliuawa usiku wa kuamkia juzi.

"Nimeambiwa kuwa juzi wilayani Sengerema kuna mama mmoja ambaye ni mlemavu wa ngozi amekatwa mkono na wauaji wakaondoka na mkono huo na tayari mama huyo amekufa," alisema Pinda na kusisitiza kushughulikia wauaji hao.

Akitoa takwimu za mauaji ya vikongwe na malbino alisema mwaka 2003 waliuwawa vikongwe 517, mwaka 2004 waliuawa vikongwe 444, mwaka 2005 (494), 2006 (vikongwe 386), mwaka 2007 (vikongwe 526) na albino sita na mwaka 2008 (vikongwe 526 na albino 28).

Alisema tayari mwaka huu wameuawa albino watatu hivyo kufanya albino na vikongwe waliouawa kufikia kuwa jumla 2,900.

Waziri mkuu ameanza ziara ya siku nne kutembelea mikoa ya Shinyanga, Tabora na Mwanza ili kuhamasisha wananchi watokomeze vitendo vya mauaji ya vikongwe na watu weye ulemavu wa ngozi
.
 
huyu mwandishi anaeuliza hapa Pinda hasa alisema nini sio yule yule alieandika taarifa inayosambaa na kusomwa all over the place sasa hivi akidai kwamba Pinda kasema hayo maneno, halafu kumbe hana uhakika, anaenda kuuliza wabunge wa CCM ambao nao hawakuwepo, mara anakuja kuuliza jamvini, mara anatoa zawadi kwa mwenye habari, wakati ameshaandika ripoti ndeeeefu ambayo hajai-retract bado, sasa jama kazi hizo sio upotoshaji huo? No, you tell me, utanambia tuna waandishi kweli hapo?

hapa ndipo ninaposhangaa; ungekuwa mchambuzi mzuri ungejua kuwa habari iliyokuwa kwenye mwanakijiji.com imetoka Mwananchi na imeandikwa na Victor Kinambile wa Tabora. Tulipoiupload kuna mahali ambapo unaweka jina la mwandishi au gazeti na sehemu nyingine ina default name la m.m. mwanakijiji

Kwa makosa yetu wakati tunaipandisha hatukujaza hiyo sehemu ya kwanza na hivyo inajaza sehemu ya pili. Ni mpaka hapa ninaposoma kwako ndiyo najua kosa lilipotokea na tayari tumesahihisha. Mara nyingi watu wakiona tumesahau kuweka source wanatushtua na hivyo tunasahihisha.

Sasa hiyo habari haikuandikwa na mimi bali na Victor. Natumaini hiyo itasaidia katika uchambuzi wako ujao kwa sababu yawezekana umesoma ukiwa na mawazo "mwandishi ni mwanakijiji" and hence your scathing attacks on Tanzanian journalists which has has become a standard banner for you rightly or wrongly.
 
Back
Top Bottom