NAMBA MOJA AJAYE NCHINI
JF-Expert Member
- Oct 29, 2019
- 8,520
- 17,426
Wananchi wa wa kata ya Loya jimbo la Igalula wanataka majibu ya ahadi zako kuhusu mambo yafuatayo:-
1.Ukarabati makini wa Barabara ya Mabeshi - Loya hasa baada ya mafuriko ya mwaka huu! Hadi sasa wananchi wanapata adha ya nauli kubwa kutoka Loya hadi Tabora mjini kwa Basi la Mama's One wanateswa na nauli kubwa ya 12000/= na bei kubwa ya mizigo hadi 50000/= kwa mizigo midogo tu. Fanya hima wapiga kura wako wanateseka!!
2. Juzi ulifanya kikao Loya Secondari wananchi wa Loya hawakusikia chochote kuhusu maabara zao za shule zilizotelekezwa na fedha zake kuliwa na viongozi wakiwemo madiwani, watendaji kata na vijiji, mkuu wa shule na mwenyekiti wa chama cha CCM Loya! Wote wamekula fedha bila kumsahau mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Uyui. Maabara za Loya zimebaki Magofu na makazi ya popo. Umefumbia macho maabara hz ukabaki unatoa hongo za 20000/= kwa wajumbe wakati wa kupiga picha na laki moja kwa mkuu wa kituo cha polisi Loya eti hela ya betri ya Gari.
3. Kwenye kikao hicho hicho umefumbia swala la nyumba za walimu ambazo hazijakamilika hadi sasa!! Kitendo kinachofanya mwalimu mmoja kuishi darasani kwa kukosa nyumba ya kuishi. Alipokuomba kuhusu ukarabati wa nyumba ulitoa majibu mepesi yasiyo na mashiko!
4. Pia Daraja la Ng'wala ambalo uliahidi wananchi wa Loya hadi leo hakuna hata dalili wananchi wa Loya kila mwaka wanazika wapendwa wao kwa ajali ya maji ya mto huu. Juzi hukuzungumzia kuhusu daraja hili. Porojo za kuwananga washindani na kuwatisha wajumbe na mtendaji kata kua wapo timu venance hazina mashiko kwetu wanaloya!!!
5. Ndugu Ntimizi rudi kwenye kutekeleza ahadi zako Usiwatishe wajumbe kwa umafia na uchawi. Acha kugawa posho za kahawa na hongo hayo haya wasaidii wana loya.
6.Kuhusu Umeme kumbuka ni mpango wa serekali wa umeme vijijini na sio juhudi zako!!!Maana nasikia kila unautaja taja wakati tunajua huo ni mpango wa serekali kuu na sio juhudi zako!Usiwadanganye wanachi eti umeleta Umeme!!!
Natumai utajikita kwenye maendeleo na sio siasa chafu
tulizoziona na kuzisikia!
7.Naona ujenzi wa maabara moja umekamilika lakini hii Maabara hii wanajina lao wameiita multipurpose laboratory eti itumike kea masomo yote kinyume na utaratibu wa kawaida!!Mamlaka husika toeni fedha ili magofu mengine mawili yamaliziwe wanafunzi wapate Maabara za kutosha kuliko huu usanii wa neno multipurpose laboratory kwani maabara ya Biology na physics hazifanani wala ya kemia!!!Nadhani nimeeleweka!!tulipata wasaa kutembelea maabara hiyo tukaona haitoshelezi mahitaji ya wanafunzi!!FANYA hima wadau wa elimu Wilaya ya Uyui!!!
8.Naona Basi la Mamaz wakati mwingine linapaki pale Lutona badala ya kwenda stendi ya loya pale senta kama kawaida take kutokana na usanii wa Tanroads Uyui kwa kukarabati Bara bara chini ya kiwango AMBAYO huharibika wakati wa masika kama nilivyoona juzi kwenye ziara yangu fupi!!kumbe Tanroads Uyui wanapiga fedha za Barabara na kukarabati chini ya kiwango kama nilivyoona nitakuja tena mwakani 2023 kuangalia pia kama Daraja la mto ng'wala kama limekamilika!kwasababu nimeona wanunuzi wakibanika samaki zao lakini hawana usafiri wa uhakika Hadi Sasa na serikali kukosa mapato ya ushuru na mzunguko wa fedha wa mauzo ya samaki nchini!!Tanroads Uyui wanaichezea serikali na kuikosesha mapato naomba ile serikali makini isiyoonekana ufanye kazi take hii inayoonekana inalea upigaji na wizi kwa ujumla!!!Maeneo ya uzalishaji na ya kimkakati kama haya Sio ya kuchezea chezea kama Tanroads wanavochezea fedha za serikali!!mwakani nikija nikakuta upumbavu kama huu nitawepeleka mahakamani Tanroads!!
1.Ukarabati makini wa Barabara ya Mabeshi - Loya hasa baada ya mafuriko ya mwaka huu! Hadi sasa wananchi wanapata adha ya nauli kubwa kutoka Loya hadi Tabora mjini kwa Basi la Mama's One wanateswa na nauli kubwa ya 12000/= na bei kubwa ya mizigo hadi 50000/= kwa mizigo midogo tu. Fanya hima wapiga kura wako wanateseka!!
2. Juzi ulifanya kikao Loya Secondari wananchi wa Loya hawakusikia chochote kuhusu maabara zao za shule zilizotelekezwa na fedha zake kuliwa na viongozi wakiwemo madiwani, watendaji kata na vijiji, mkuu wa shule na mwenyekiti wa chama cha CCM Loya! Wote wamekula fedha bila kumsahau mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Uyui. Maabara za Loya zimebaki Magofu na makazi ya popo. Umefumbia macho maabara hz ukabaki unatoa hongo za 20000/= kwa wajumbe wakati wa kupiga picha na laki moja kwa mkuu wa kituo cha polisi Loya eti hela ya betri ya Gari.
3. Kwenye kikao hicho hicho umefumbia swala la nyumba za walimu ambazo hazijakamilika hadi sasa!! Kitendo kinachofanya mwalimu mmoja kuishi darasani kwa kukosa nyumba ya kuishi. Alipokuomba kuhusu ukarabati wa nyumba ulitoa majibu mepesi yasiyo na mashiko!
4. Pia Daraja la Ng'wala ambalo uliahidi wananchi wa Loya hadi leo hakuna hata dalili wananchi wa Loya kila mwaka wanazika wapendwa wao kwa ajali ya maji ya mto huu. Juzi hukuzungumzia kuhusu daraja hili. Porojo za kuwananga washindani na kuwatisha wajumbe na mtendaji kata kua wapo timu venance hazina mashiko kwetu wanaloya!!!
5. Ndugu Ntimizi rudi kwenye kutekeleza ahadi zako Usiwatishe wajumbe kwa umafia na uchawi. Acha kugawa posho za kahawa na hongo hayo haya wasaidii wana loya.
6.Kuhusu Umeme kumbuka ni mpango wa serekali wa umeme vijijini na sio juhudi zako!!!Maana nasikia kila unautaja taja wakati tunajua huo ni mpango wa serekali kuu na sio juhudi zako!Usiwadanganye wanachi eti umeleta Umeme!!!
Natumai utajikita kwenye maendeleo na sio siasa chafu
tulizoziona na kuzisikia!
7.Naona ujenzi wa maabara moja umekamilika lakini hii Maabara hii wanajina lao wameiita multipurpose laboratory eti itumike kea masomo yote kinyume na utaratibu wa kawaida!!Mamlaka husika toeni fedha ili magofu mengine mawili yamaliziwe wanafunzi wapate Maabara za kutosha kuliko huu usanii wa neno multipurpose laboratory kwani maabara ya Biology na physics hazifanani wala ya kemia!!!Nadhani nimeeleweka!!tulipata wasaa kutembelea maabara hiyo tukaona haitoshelezi mahitaji ya wanafunzi!!FANYA hima wadau wa elimu Wilaya ya Uyui!!!
8.Naona Basi la Mamaz wakati mwingine linapaki pale Lutona badala ya kwenda stendi ya loya pale senta kama kawaida take kutokana na usanii wa Tanroads Uyui kwa kukarabati Bara bara chini ya kiwango AMBAYO huharibika wakati wa masika kama nilivyoona juzi kwenye ziara yangu fupi!!kumbe Tanroads Uyui wanapiga fedha za Barabara na kukarabati chini ya kiwango kama nilivyoona nitakuja tena mwakani 2023 kuangalia pia kama Daraja la mto ng'wala kama limekamilika!kwasababu nimeona wanunuzi wakibanika samaki zao lakini hawana usafiri wa uhakika Hadi Sasa na serikali kukosa mapato ya ushuru na mzunguko wa fedha wa mauzo ya samaki nchini!!Tanroads Uyui wanaichezea serikali na kuikosesha mapato naomba ile serikali makini isiyoonekana ufanye kazi take hii inayoonekana inalea upigaji na wizi kwa ujumla!!!Maeneo ya uzalishaji na ya kimkakati kama haya Sio ya kuchezea chezea kama Tanroads wanavochezea fedha za serikali!!mwakani nikija nikakuta upumbavu kama huu nitawepeleka mahakamani Tanroads!!