Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 13,495
- 51,090
Hivi hii serikali ya CCM iko madarakani kwa Uhalali upi?
Miaka 60 ya Uhuru imepiga marktime na kufanya mambo mengi yasiyo ya maana na kuacha mengi ya maana.
1. Hivi Wakati Serikali ya CCM inavumilia ufisadi wa EPA , Rada Meremeta, Kagoda, Richmondi Ndege ya Rais, hizo pesa zisingeweza kusaidia kuondoa kero ya maji kwa wananchi?
2. Hivi ma V8, Mamisafara makubwa, maposho manene wanayolipana yasingeweza kisaidia kuondoa shida ya maji kwa wananchi?
3. Wanakimbiza Mwenge, Wanalipa wastaafu hadi asilimia 80% ya mishahara ya viongozi walioko madarakani, hizo pesa zisingeweza kuondoa kero ya maji ya wananchi?
4. Tumezunguukwa na maziwa makubwa, tuna mito mikubwa, tuna bahari. Hizi serikali za CCM toka mwaka 1961 zimeshindwaje kutatua kero ya maji kwa wananchi?
5. Wanafanya mamiradi makubwa kabla ya kusolve matatizo ya maji, wanajenga uwanja wa ndege Chato, Daraja la kupita baharini Dar, Wakati wananchi hawana maji
6. Wanawalipa Syimbion, shilingi bilioni 300 kwa mkataba wa kihuni ulioingiwa tena kiujanjaujanja wakati mkataba wa awali ulikuwa umeshaisha!
7. Walihonga watu waunge mkono juhudi, ili majimbo yao yawe wazi kisha zitumike pesa za umma kurudia tena chaguzi. Mapesa haya ya wananchi yangesaidia kuondoa kero ya maji
8. Wanatumia mabilioni kulipa wabunge hewa, waliobungeni kinyume cha katiba. Hizo pesa zingesaidia kuondoa kero ya maji
Kwa hakika Watanzania tumechoka na Ujinga, Ukosefu wa maono, Ubinafsi na kukosewa heshima na serikali hii ya CCM.
Wametufikisha katika hatua sasa ya kutufanya tuamke, tusimame, tupambane nayo kwa hali na mali, kwa jasho na machozi kwa kuwa sasa imegeuka kuwa serikali dhalimu, isiyotosheleza haja zetu!
Sasa tunatangaza kuanza maandamano yasiyo na kikomo, kuitaka serikali hii ilete maji, kama haitoleta maji tutayafuata kwa Mawaziri, wao hawakosi maji
Kama haitoleta maji tutayafuata Ikulu, huko nasikia yako mengi hayakatiki.
Haiwezekani tukaendekeza upumbavu huu
Kama hamuwezi kutatua shida ya maji ondokeni, Tokeni madarakani. Hamna legitimacy tena ya kuitwa serikali au viongozi.
Serikali gani nyinyi, hamuwezi chochote. Nyambaafu!
Failure wakubwa nyinyi!.
Miaka 60 ya Uhuru imepiga marktime na kufanya mambo mengi yasiyo ya maana na kuacha mengi ya maana.
1. Hivi Wakati Serikali ya CCM inavumilia ufisadi wa EPA , Rada Meremeta, Kagoda, Richmondi Ndege ya Rais, hizo pesa zisingeweza kusaidia kuondoa kero ya maji kwa wananchi?
2. Hivi ma V8, Mamisafara makubwa, maposho manene wanayolipana yasingeweza kisaidia kuondoa shida ya maji kwa wananchi?
3. Wanakimbiza Mwenge, Wanalipa wastaafu hadi asilimia 80% ya mishahara ya viongozi walioko madarakani, hizo pesa zisingeweza kuondoa kero ya maji ya wananchi?
4. Tumezunguukwa na maziwa makubwa, tuna mito mikubwa, tuna bahari. Hizi serikali za CCM toka mwaka 1961 zimeshindwaje kutatua kero ya maji kwa wananchi?
5. Wanafanya mamiradi makubwa kabla ya kusolve matatizo ya maji, wanajenga uwanja wa ndege Chato, Daraja la kupita baharini Dar, Wakati wananchi hawana maji
6. Wanawalipa Syimbion, shilingi bilioni 300 kwa mkataba wa kihuni ulioingiwa tena kiujanjaujanja wakati mkataba wa awali ulikuwa umeshaisha!
7. Walihonga watu waunge mkono juhudi, ili majimbo yao yawe wazi kisha zitumike pesa za umma kurudia tena chaguzi. Mapesa haya ya wananchi yangesaidia kuondoa kero ya maji
8. Wanatumia mabilioni kulipa wabunge hewa, waliobungeni kinyume cha katiba. Hizo pesa zingesaidia kuondoa kero ya maji
Kwa hakika Watanzania tumechoka na Ujinga, Ukosefu wa maono, Ubinafsi na kukosewa heshima na serikali hii ya CCM.
Wametufikisha katika hatua sasa ya kutufanya tuamke, tusimame, tupambane nayo kwa hali na mali, kwa jasho na machozi kwa kuwa sasa imegeuka kuwa serikali dhalimu, isiyotosheleza haja zetu!
Sasa tunatangaza kuanza maandamano yasiyo na kikomo, kuitaka serikali hii ilete maji, kama haitoleta maji tutayafuata kwa Mawaziri, wao hawakosi maji
Kama haitoleta maji tutayafuata Ikulu, huko nasikia yako mengi hayakatiki.
Haiwezekani tukaendekeza upumbavu huu
Kama hamuwezi kutatua shida ya maji ondokeni, Tokeni madarakani. Hamna legitimacy tena ya kuitwa serikali au viongozi.
Serikali gani nyinyi, hamuwezi chochote. Nyambaafu!
Failure wakubwa nyinyi!.