Wito: Vijana na wasomi tuungane kulikomboa taifa 2015 !

Nyami2010

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
227
50
Wasalaam wanaJF

WITO: 2015 tunahitaji kuwa na akina Mhe. Mnyika 15, akina Mhe. Janauary 15, akina Mhe Tundu Lissu 20 ili Tanzania yetu ifikapo 2025 tuwe na uchumi angalau kama ule wa Botswana! Tanzania tuna kila kitu, jamani!

Tutafikaje hapo: Vijana na wasomi, chonde chonde kila mmoja kwa nafasi na wakati wake tuanze harakati na mipango ya kujitokeza kwa wingi ifikapo 2015 ili Taifa hili tusiendelee kuwaachia watu wasio na huruma. Ndugu zangu, siasa ni kila kitu hapa kwetu Tanzania. Uchumi ni siasa, Michezo ni siasa, Afya ni siasa, Kilimo ni siasa, n.k, n.k.

Tunahitaji kuwa na MODEL au njia inayoweza kutuunganisha vijana na wasomi wote nchini na walioko nje ya nchi ili 2015 tuikomboe Tanzania!

Tukiendelea kusema siasa ni mchezo mchafu na haifai, tutaendelea kuwa na watu wabovu wanaofanya maamuzi, wanasinzia bungeni, hawajali na mwisho wa siku maamuzi yao ndiyo mustakabari wa Taifa!

Tujitokeze wote bila kujali tunapitia chama gani, muhimu ni vijana na wasomi tujipange kulikomboa taifa kupitia ballot box 2015!

Ninawasilisha na mbarikiwe sana!
 
Hoja nzuri mkuu, na si lazima kugombea lakini tushirikiane kuwaelimisha jamii ambayo haielewi mbele wala nyuma na sisi tumesomeshwa kwa kodi zao hata kama ni shule za kata, lengo ni kuwa tuwasaidie kisiasa, kiuchumi na kijamii. Tatizo ni kuwa wasomi wanapoingia kwenye nafasi fulani wanasahau kusudi la kusomeshwa kwao na jamii maskini iliyotarajia kunufaika . Wasomi tusipolitafakari hili ni kweli wananchi hawa maskini hawakufanyi kitu, lakini kwa kuwa Mungu anaona na amewasikia hawa watu na alijua kusudi lao kwetu ndugu zangu siku moja kama Mungu yupo tutatoa mahesabu.
 
tatizo ni kuwa hao wasomi unaowaomba waungane, nao wanatafuta mbinu n a njia za kujiingiza kwenye siasa ili wapate ulaji
 
Nadhani tufike mahali mimi na wewe tuumize akili nini kifanyike wasomi wasomi wajitambue na kuwa na moyo wa uzalendo. Pili tufanye nini kwa hawa wananchi ili wafahamu nini matarajio yao kutoka kwa wasomi. Tatu nini kifanyike wasomi wanaposhindwa kukidhi haja wananchi? Tukifanikiwa kutoa maoni sahihi na kupenyeza katiba ya nchi hasa wakati huu wa marekebisho ya katiba na ikaundwa sheria nadhani tutanufaika.
 
Umesomeka mkuu, sasa tunaanzaje mabadiliko hayo? fafanua.

Mimi naamini njia ya kwa ni elimu ya uraia kwa mtu na mtu. Watu wenye elimu (ya kweli) wana uwezo mkubwa wa kushawishi wengine ya hoja zenye mantiki. Tufanye hivyo, jaribu kuwaelimisha watu walio karibu nawe mpaka waelewe umuhimu wa mabadiliko na kuamini kuwa through the ballot box we can make changes.

Watu wengi wanatamani mabadiliko lakini utasikia "sikupiga kura kwa sababu CCM wangeshinda tu". Bila kujua kuwa kwa kutopiga kura ndio hasa unawapa ushindi CCM. Kauli kama "sikuwa na muda" bila kujua kuwa kura yako itakuongoza kwa miaka mitano ijayo.

Tupeane elimu ya uraia na haki zetu halafu umuhimu wa kupiga kura na sio kulalamika tu.
 
Ukombozi wa Tanzania hautakuja kwa sanduku la kura, hili ndilo jambo ambalo watu wanatakiwa kuanza kulizoea. Ukombozi wa sanduku la kura mara nyingi hutokea kwenye nchi ambazo zina demokrasia angalau ya kiwango kikubwa.
Tanzania inaendeshwa na wahalifu, wauaji, na majambazi ya hali ya juu. Katika mazingira kama haya sanduku la kura halitabadilisha mfumo kwa sababu nguvu ya elimu haiishindi nguvu ya hela, hasa hela chafu kama za hapa nchini.
Hili ni angalizo, msije mkafarijiana kwa mambo yasiyokuwepo na baadaye yakageuka vilio.
 
Ninadhani tunahitaji kuwa na mfumo wa 'Elimu ya Umma kwa Jamii" ambao utawaelimisha na kuwaunganisha vijana wote nchini bila kujali itikadi zao, ili kuanzia sasa hadi ifikapo 2015 wafanye maamuzi juu ya hatma ya nchi. Hii iwe ni kupitia sanduku la kura, na INAWEZEKANA tena sana!

Ni mfumo au njia gani hiyo, kwa kweli sijui....Pengine tuelimishane..
 
Kwa mara ya kwanza najitokeza hapa japo nimekuwa mfuasi wa kusoma tu kwamda mrefu.Nimekongwa na wazo lako mwanJF kwamba vijana wasomi tujiunge pamoja tuelimishe wale ambao hawakubahatika kuupata mwang ili ifikapo 2015 waweze kufanya uhamuzi sahihi. Binafsi nakubaliana na wewe na hapa nataka nipendekeze kwamba tujiorganize kupitia ukuras huu tuwe na na mikutano ya hapa na pale kila moka. Tunaweza kupata waratibu wa kila mkoa na kila Wilaya kupitia hapapa then tuweke mikakati. Ili kuondoa mamluki na wasio na nia njema kusiwepo na aina yoyote ya viburudisho ila commitment za watu. Ki-ukweli jamani tusipojitoa mhanga Taifa linaangamia ili hali lina kila kitu. Haya ndo mawazo yangu janmani. Wito ni kwamba tujadiliane tuone itakuwa vipi.
 
Naona watu wnauliza kwamba tunzeje ili lisitupe shida nikutangaza tu kwamba vijana walio mkoafulani au chuofulani tukutane mahala fulani saa fulani na mada inatengenezwa inakuwa nidiyo mwongozo wa vijana wote watakapo kutana kote nchini. Aidha katika mikutano hiyo tuwaache nje vijana walio katika nafasi za kimokana kitaifa hii ni kuepuka kuwa influenced na mawazo yao katika hatua zaawali. Lakini pia wao tuwaache wendelee na majukumu yao ya Kitaifa, lakini pia tukumbuke wapo vijana toka vyama vyote walio katika nafasi za uongozi kama bungeni, na mabaraza ya vijana lakini hawani focus yoyote juu ya mstakabari wowote wa Taifa hili. TUSINGOPE KUANZA, NIWAPE MFANO WA JONGOO, ALIPONZAA MTOTO WAKE KUTOKANA NA MIGUU YAKE KUWA MINGI MTOTO AKAMUULIZA MAMA " SASA NIANZE NA MGUU GANI KUTEMBEA? MAMA YAKE AKAMJIBU " WE ANAZA NA WOWOTE UTAONA INACHNGANYA TU NA UNASONGA MBELE" Basi nasisi tuchanganye mbele kwa mbele. Maoni yangu haya
 
Watu wakishapata elimu ya uraia akili kupata mabadiliko huwa haifundishwa. Kwani nani aliwafundisha Tunisia na wengine ndani na nje ya Afrika? elimu ni silaha isiyoshindwa kamwe na huwezi kuiangamiza.
 
Naona watu wnauliza kwamba tunzeje ili lisitupe shida nikutangaza tu kwamba vijana walio mkoafulani au chuofulani tukutane mahala fulani saa fulani na mada inatengenezwa inakuwa nidiyo mwongozo wa vijana wote watakapo kutana kote nchini. Aidha katika mikutano hiyo tuwaache nje vijana walio katika nafasi za kimokana kitaifa hii ni kuepuka kuwa influenced na mawazo yao katika hatua zaawali. Lakini pia wao tuwaache wendelee na majukumu yao ya Kitaifa, lakini pia tukumbuke wapo vijana toka vyama vyote walio katika nafasi za uongozi kama bungeni, na mabaraza ya vijana lakini hawani focus yoyote juu ya mstakabari wowote wa Taifa hili. TUSINGOPE KUANZA, NIWAPE MFANO WA JONGOO, ALIPONZAA MTOTO WAKE KUTOKANA NA MIGUU YAKE KUWA MINGI MTOTO AKAMUULIZA MAMA " SASA NIANZE NA MGUU GANI KUTEMBEA? MAMA YAKE AKAMJIBU " WE ANAZA NA WOWOTE UTAONA INACHNGANYA TU NA UNASONGA MBELE" Basi nasisi tuchanganye mbele kwa mbele. Maoni yangu haya

Mawazo mazuri, ebu tuanze basi!
 
tatizo ni kuwa hao wasomi unaowaomba waungane, nao wanatafuta mbinu n a njia za kujiingiza kwenye siasa ili wapate ulaji

mwaka 2010 vijana wengi waliomaliza vyuo walienda kugombea udiwani kwenye kata zao ndo maana halmashauri nyingi hazikaliki siku hizi. Ukombozi wa kweli huanzia chini na siyo juu. Ukiwa diwani utakuwa karibu zaidi na wananchi muda mwingi kuliko hao wabunge ambao wanasababisha watu tuzichukie siasa za nchi hii. Wananchi wengi wanapenda mabadiliko ila hawana elimu ya kutosha. Tuache kugombea vyeo kwenye key board na simu, nenda majimboni ukatoe changamoto na mabadiliko. Mimi kila mgonjwa dawa ikikosekana namwambia,hii ni sababu ya serikali mbovu walioichagua. Nikimpa na mfano wa hela zinavyopotea ananielewa.
 
Duniani kote ukombozi wa kweli hufanywa na vijana lakini vijana watanzania munanishangaza sana munakubali kutumika mukipewa simu,vijisenti na vit- shirt basi munatuliza boli nchi hii ni yenu wazee wanahesabu siku warudi walikotoka lakini nyie munaibiwa mbele ya macho yenu mumebweteka,embu badilikeni basi
 
Wasalaam wanaJFWITO: 2015 tunahitaji kuwa na akina Mhe. Mnyika 15, akina Mhe. Janauary 15, akina Mhe Tundu Lissu 20 ili Tanzania yetu ifikapo 2025 tuwe na uchumi angalau kama ule wa Botswana! Tanzania tuna kila kitu, jamani! Tutafikaje hapo: Vijana na wasomi, chonde chonde kila mmoja kwa nafasi na wakati wake tuanze harakati na mipango ya kujitokeza kwa wingi ifikapo 2015 ili Taifa hili tusiendelee kuwaachia watu wasio na huruma. Ndugu zangu, siasa ni kila kitu hapa kwetu Tanzania. Uchumi ni siasa, Michezo ni siasa, Afya ni siasa, Kilimo ni siasa, n.k, n.k. Tunahitaji kuwa na MODEL au njia inayoweza kutuunganisha vijana na wasomi wote nchini na walioko nje ya nchi ili 2015 tuikomboe Tanzania!Tukiendelea kusema siasa ni mchezo mchafu na haifai, tutaendelea kuwa na watu wabovu wanaofanya maamuzi, wanasinzia bungeni, hawajali na mwisho wa siku maamuzi yao ndiyo mustakabari wa Taifa! Tujitokeze wote bila kujali tunapitia chama gani, muhimu ni vijana na wasomi tujipange kulikomboa taifa kupitia ballot box 2015! Ninawasilisha na mbarikiwe sana!
Pamoja sana
 
Approach ni hii, tuteneneze joint venture ngazi ya kata, ninamaana vijana ngazi ya kata mjiunge,, mgawane kazi kulingana na uwezo na taaluma. wasaidieni wazazi, vijana wenzenu kutatua matatizo yao hasa ya ufahamu, muwape elimu ya uraia, mjipange kila kata, hadi jimbo.
 
Tuko pamoja mkuu vijana tupo tumejaa tele! mimi najitokeza siwezi kuvumilia uozo unaoendelea katika utawala uliopo naomba vijana wenzangu na wazee mniunge mkono bado natafakari niingie katika nafasi ipi lakini cha msingi nipate nafasi ya kuwatumikia watanzania wenzangu.
 
kama kweli vijana tunaipenda nchi yetu na tunahitaji mapinduzi makubwa ya kisiasa na kiuchumi basi tujitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura. Sio kukaa mnasema mala huyu hafai huyu anafaa wakati wa kupiga kura ukifika hauna kitamburisho. Huu ni uji.nga. na upu. mbavu. !
 
Back
Top Bottom