mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,855
- 8,251
mbona hujasema tususie misikiti,fwedha ,tende,mazulia yatokayo huko yakheWITO TUGOMEE KUPANDA NDEGE ZA EMIRATES NA QATAR AIRWAYSQATAR NA UAE KULIPA GHARAMA ZOTE ZA MAUAJI YANAYOFANYWA NA CRUSADERS WA MAREKANI , UINGEREZA NA UFARANZA.KISA WANAMCHUKIA GHADDAFI KWASABABU ALIKUA AKIWAMBIA UKWELI KWAMBA WAO NI PUPPETS WA WESTERN POWER.Taarifa za uhakikaa ni kwamba serikali za kifalme za UAE na QATAR ambazo zenyewe sio za kidemokrasia ndizo zitabeba gharama zote za vita dhidi ya serikali halali ya Libya.Pia nchi hizo ndio pekee katika Arab league ,Jumuia ya Madikteta ya waarabu(ambayo Gadhafi alijitoa kuachana na unafiki wao lakini wakamlamba miguu kwani ingepoteza sifa ya kuwepo kwake)ambazo zimepeleka ndege za kivita kwa ajili ya kushiriki mauaji dhidi ya waislamu wenzao wa Libya.
Tangu mauaji hayo yaanze mamia ya watu ,wakiwemo wanawake na watoto wameuliwa.Idadi inayopita ya raia waliokufa kabla ya mashambulizi ya Crusaders hayajaanza.Sababu zilizotolewa na QATAR na UAE ati ni kuzuia mauaji yanayofanywa na majeshi ya serikali ya Libya.lakini cha kujiuliza Serikali ya Libya kweli inapambana na waandamanaji raia? Au inapambana na uasi uliobuniwa na Sarcorzy rais wa Ufaranza??
Jee waasi wa Bhengazi ni haki kupambana kwa niaba ya miji mengine ya Libya? Waasi hao pia wana bendera yao tofauti na bendera ya serikali ya Libya? Bendera wanayotumia wao ni kifalme aliyepinduliwa na jeshi la Libya wakiongozwa na Gadhafi …kwa hiyo QATAR NA UAE wanaona haya kwao ni sawa?
Mfalme huyu Idrissa aliyepinduliwa aliruhusu nchi yake iwe kibaraka wa Magharibi..wakati wa vita vya SUEZ Ufaransa na Uingereza waliruhusiwa kutumia base zao zilizokuwepo Libya kuipiga EYGPT….haya ndiyo yaliyosababisha wanajeshi wa Libya kumuondowa Kibaraka Mfalme pamoja na Bendera yake…..leo hawa waasi bila ya aibu wanabeba bendera ya puppet huyu na inajulikana kwamba Mfalme Idris alitoka Bhenghazi sasa kuna wachache waliokua wakifaidi kwa sababu waliokua wakifaidi kama zilivo falme za QATAR NA UAE ni familia zao na watoto wao kama hujawa AL MAKHTOUM AU BIN HAMAD AU NAHAYAN BASI HUWEZI KUPATA UWAZIRI , UBALOZI AU HATA MKUU WA TRAFIC.
Leo QATAR NA UAE wapo mbele kuwatetea wasi hawa wana peleka ndege zinaua raia wa Libya, nchi hizi zina kibri cha mali…na leo waasi wa Bhengazi wanawakamata na kuwaua raia WEUSI wa Libya….kwani hapo zamani mfalme wao aliwabagua na kuwatenga .Libya ni nchi yenye raia weusi karibu 45% .
Lakini serikali ya Libya imejitahid kuwaweka raia wote kuwa ni sawa.
Kuna kila dalili ndugu zetu weusi watabagulia na serikali inayotakiwa na QATAR NA UAE…
Hakuna nchi itayokaa kimya kuona waasi wanateka kambi za jeshi wanasaidiwa na maadui na MACRUSADERS basi ikakaa kimya …..ina wajibu wa kulinda usalama wa mipaka ya nchi na raia wake….kama inavofanya serikali ya Libya…
Kabla ya waasi hawajateka kambi za jeshi Ghaddafi hakutumia ndege kuwapiga wandamanaji..alitumia mabomu yamachozi kama police wa London walivofanya juzi….lakini walipo chukua silaha tena nzito kuharibu miji na mali za serikali Nayo serikali ilibidi itumie silaha kuweka hali ya usalama, QATAR NA UAE nao wangefanya kama alivofanya Ghaddafi…
Kwa vile wanatumiwa dhidi ya waislam wenzao na kwa vile Libya ilikua ni afrika zaidi kuliko Uarabu…..Waafrika na Watanzania tuoneshe kuchukizwa kwa nchi hizi mbili kutumiwa dhidi ya walibya kwa maslahi ya nchi za Magharibi….
Kwa kuanzia tusipande ndege zao na tujizuie kwenda UAE kwa ajili ya biashara…kma ni bishara nendeni China..
TUSUSIE KUPANDA NDEGE ZA UAE NA QATAR KUANZIA SASA HII ..KILA MTU AMWAMBIE MWENZAKE ..MISIKITINI…KOTE ..KWENYE FACEBOOK…..HAWA JAMAA HAWATUSAIDII CHOCHOTE …AFADHALI GHADDAFI……TUONESHE KWAMBA WANACHOFANYA SIO SAHIHI WANATIA AIBU UTU WAO…
TUSUSIE