Wito: Posho za nyumba, umeme, maji na simu kwa mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa zifutwe

Lukusi

Member
Dec 23, 2016
13
55
Kuetekeleza Agizo la Mh Waziri Mkuu kwa vitendo kama mwananchi wa kawaida namuomba Waziri na Katibu Mkuu mwenye mamlaka azifutilie mbali posho za Nyumba, Umeme, Simu na Maji kwa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Idara katika Wizara, Mikoa na Halmashauri.

Kwa ufupi Posho hizi zilizobatizwa jina la Utility zinaweka tabaka baina ya watumishi wa Umma, inasikitisha na Kushangaza Wakuu wa Idara na Viongozi mbalimbali wa Kisiasa ambao wengi wao mishahara yao inaanzia 3,700,000/= hadi 5,500,000/= kulipwa tena posho za nyumba, umeme, maji na simu ilihali mishahara yao ni mikubwa na inajitosheleza.

Posho ambazo viongozi hawa hupata kila mwezi kwa ajili ya nyumba, umeme, maji na simu ni Tsh 975,000/= ambapo posho tu wanayopokea inazidi mshahara wa afisa wa kawaida mwenye degree anayelipwa TSH 710,000/= kwa mwezi hapo hujaweka makato ya kodi, bima ya afya na mifuko ya jamii.

Mh Waziri Mkuu kama tunataka kuleta usawa katika watumishi wa umma anza nahii posho ya 975,000/= ambayo hata Mh Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ndugu hapi analamba kila mwezi nje ya mshahara wake.
 
Ila kupanga ni kuchagua sisi walimu tunapewa mia tatu take home baada ya kila kato wanalojisikia kutukata mara kodi sijui heslb (15%) mara nssf cjui cwt n.k. Mbona hatuna posho hata ya chakula tu ambayo manjagu tena wengine wana fails nyingi (F) kuliko pass (D) kwenye vyeti vyao vya o-level ukilinganisha na wale wanaosomea ualimu?
Wanalipwa posho mara za chakula uniform sijui duka mara genge mara vinjwaji as few to mention. Hizi nchi zisizoendelea bhana hawadhamini mwalimu wala elimu. Shule zinafunguliwa unaingia class unakutana na vilaza wa kitanzania zaidi ya 80 kwenye darasa moja hao unatakiwa ukomae nae mpaka waweze KKK ila maslai sasa hamna. Ngoja tuwaze kwa nguvu la kufanya huu sio utaratibu wengine maposho lukuki na posho lake moja tu ni zaidi ya salary ya mwalimu
 
Hii kitu nimewahi kuhoji mara kibao, iweje mtu unalipwa mshahara mkubwa ila wanapata huduma nyingine bure? Halafu unakuta anayelipwa kidogo ndio anajigharamia vitu vyote
 
Kuetekeleza Agizo la Mh Waziri Mkuu kwa vitendo kama mwananchi wa kawaida namuomba Waziri na Katibu Mkuu mwenye mamlaka azifutilie mbali posho za Nyumba, Umeme, Simu na Maji kwa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Idara katika Wizara, Mikoa na Halmashauri.

Kwa ufupi Posho hizi zilizobatizwa jina la Utility zinaweka tabaka baina ya watumishi wa Umma, inasikitisha na Kushangaza Wakuu wa Idara na Viongozi mbalimbali wa Kisiasa ambao wengi wao mishahara yao inaanzia 3,700,000/= hadi 5,500,000/= kulipwa tena posho za nyumba, umeme, maji na simu ilihali mishahara yao ni mikubwa na inajitosheleza.

Posho ambazo viongozi hawa hupata kila mwezi kwa ajili ya nyumba, umeme, maji na simu ni Tsh 975,000/= ambapo posho tu wanayopokea inazidi mshahara wa afisa wa kawaida mwenye degree anayelipwa TSH 710,000/= kwa mwezi hapo hujaweka makato ya kodi, bima ya afya na mifuko ya jamii.

Mh Waziri Mkuu kama tunataka kuleta usawa katika watumishi wa umma anza nahii posho ya 975,000/= ambayo hata Mh Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ndugu hapi analamba kila mwezi nje ya mshahara wake.

Nchi za wajinga ndivyo zilivyo mtanyonywa mpaka muharishe
 
Ndiyo maana wana viburi vya kila siku kutuimbia wimbo kuwa tujiajiri, wakati wenyewe wenye uwezo wa kupata hata mtaji wa m50 hawasubutu kujiajiri!
 
Zifutwe posho zote ad za sim...tena posho izo utakuta wanapewa mkononi sasa kama dc anapewa 975,000/= kwa maongezi gan?yanasaidia nn nchi hii...zifutwe tuu
 
Naunga mkono hoja, lakini umewasahau wanajeshi,polisi, wabunge na magereza.hili likifanyika ndio dhana ya kubana matumizi ingeeleweka.kwani kwa sasa ubanaji umeelekezwa kwa watumishi wa umma tu.,.
 
thubutuuu. labda posho hizo zingelenga tabaka la watumishi wa umma. wanasiasa wote wanafanana kazi yao ni kunyanyasa watumishi hasa wa kada ya chini....
 
Mawazo ya kimasikini yanazidi kushamiri awamu hii, nadhani ni kwa vile rais anaupenda umasikini na kuupigia debe na kudai yeye ni rais wa masikini na anawapenda masikini basi kila mtu anadhani umasikini ni sifa na anataka awe masikini.

Watu masikini wana wivu sana hawataki kuona mtu anafaidi,wao wanataka kila mtu awe kama wao,wakisikia flani anafaidi hivi roho inawauma sana.

Haya ya kutaka sijui nini kuondolewe,itafika hatua mtataka hata rais asiishi ikulu na aaipewe ulinzi maana ni gharama.

Heri uwe masikini lakini uwe na mawazo ya kitajiri kama mimi kuliko kua masikini na mawazo ya kimasikini kama mtoa mada, mawazo ya kimasikini ni mabaya sana.

Hii inatokana na rais kupandikiza mawazo ya kimasikini kwa watu na kuona kila aliefanikiwa ni fisadi au kila anaeishi vizuri ni mwizi. Hii nchi bwana.
 
Mawazo ya kimasikini yanazidi kushamiri awamu hii, nadhani ni kwa vile rais anaupenda umasikini na kuupigia debe na kudai yeye ni rais wa masikini na anawapenda masikini basi kila mtu anadhani umasikini ni sifa na anataka awe masikini.

Watu masikini wana wivu sana hawataki kuona mtu anafaidi,wao wanataka kila mtu awe kama wao,wakisikia flani anafaidi hivi roho inawauma sana.

Haya ya kutaka sijui nini kuondolewe,itafika hatua mtataka hata rais asiishi ikulu na aaipewe ulinzi maana ni gharama.

Heri uwe masikini lakini uwe na mawazo ya kitajiri kama mimi kuliko kua masikini na mawazo ya kimasikini kama mtoa mada, mawazo ya kimasikini ni mabaya sana.

Hii inatokana na rais kupandikiza mawazo ya kimasikini kwa watu na kuona kila aliefanikiwa ni fisadi au kila anaeishi vizuri ni mwizi. Hii nchi bwana.
kiongozi hapa kuna hoja ya msingi, huwezi kusema watu wana mawazo ya kimasikini wakati hao wakubwa wanagharamiwa fedha na hawa hawa masikini ili waishi hayo maisha unayoyaona ni ya kitajiri huu ni unyonyaji. Wangekuwa wanatoa fedha zao mfukoni kujigharamia hakuna ambaye angepiga kelele.
 
Kuetekeleza Agizo la Mh Waziri Mkuu kwa vitendo kama mwananchi wa kawaida namuomba Waziri na Katibu Mkuu mwenye mamlaka azifutilie mbali posho za Nyumba, Umeme, Simu na Maji kwa Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri na Wakuu wa Idara katika Wizara, Mikoa na Halmashauri.

Kwa ufupi Posho hizi zilizobatizwa jina la Utility zinaweka tabaka baina ya watumishi wa Umma, inasikitisha na Kushangaza Wakuu wa Idara na Viongozi mbalimbali wa Kisiasa ambao wengi wao mishahara yao inaanzia 3,700,000/= hadi 5,500,000/= kulipwa tena posho za nyumba, umeme, maji na simu ilihali mishahara yao ni mikubwa na inajitosheleza.

Posho ambazo viongozi hawa hupata kila mwezi kwa ajili ya nyumba, umeme, maji na simu ni Tsh 975,000/= ambapo posho tu wanayopokea inazidi mshahara wa afisa wa kawaida mwenye degree anayelipwa TSH 710,000/= kwa mwezi hapo hujaweka makato ya kodi, bima ya afya na mifuko ya jamii.

Mh Waziri Mkuu kama tunataka kuleta usawa katika watumishi wa umma anza nahii posho ya 975,000/= ambayo hata Mh Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ndugu hapi analamba kila mwezi nje ya mshahara wake.


Kwa kweli kama Waziri anauchungu na fedha za nchi aanze na posho za wale wanaoanza na mishahara mikubwa kama kuanzia M2.5 sio kuhangaika na hawa wenye vimishahara vidogo.

Makatibu wakuu, mawaziri na wengineo posho zao ziondolewe nao pia ni watumishi wa umma na wana posho kubwa sanaa...
 
Inatakiwa kiongozi awe mfano na sio kuwalazimisha watu wafanye kitu ambacho wewe hupendi kukifanya.
Uongozi ni dhamana na sio unyanyasaji
 
Naunga hoja. Kwa nini wimbo wa Hapa Kazi tu uwe kwa baadhi ya watu na wengine waendelee kuishi vizuri kwa jasho la walala hoi?! Kubana matumizi tuanzie na juuuuuu sio kuwadhulumu wananchi wa kawaida tuuuu!
 
Hizo posho soon zitafutwa maana nchi imefilisika ni swala la muda tu, nasikia kuna harufu ya vikwazo
 
Tumefuta posho kwa viongozi kuanzia ngazi za wilaya tu.
Viongozi wa ngazi za kitaifa,wabunge na majeshi yetu,wataendelea na posho kama kawaida na hii ni kwasababu ya mazingira magumu ya kazi wanayopambana nayo katika majukumu yao ya kila siku.

Ahsanteni sana,
kwa kunisikiliza
 
kiongozi hapa kuna hoja ya msingi, huwezi kusema watu wana mawazo ya kimasikini wakati hao wakubwa wanagharamiwa fedha na hawa hawa masikini ili waishi hayo maisha unayoyaona ni ya kitajiri huu ni unyonyaji. Wangekuwa wanatoa fedha zao mfukoni kujigharamia hakuna ambaye angepiga kelele.
Watu hao hawalipwi hayo kwa hisani, wanalipwa hayo kutokana na kazi na hatari zinazoambatana na hiyo kazi.

Nasema ni mawazo ya kimasikini maana masikini ndio anaona mwenzake anafaidi basi wafanane,huyu alietoa mada anaona hao wakurugenzi na madc sijui nani wanafaidi sana waondolewe hizo huduma wawe sawa na yeye.

Mtu ni katibu mkuu,yeye ndie mtendaji na msimamizi mkuu wa mambo ya wizara kuanzia watumishi,fedha nk,unataka alipwe laki saba bila marupurupu afanane na wewe unaefunsisha huko nyampulukano sec school,haiwezekani.

Lazima muelewe, watu hawalipwi mishahara wao na hawapewi hizo huduma wao, inalipwa huduma wanayoitoa,inalipwa kazi wanayoifanya,usione mbona Mkuu wa wilaya Flani bwana flani analipwa hiki na hiki, hapana, halipwi bwana flani, inalipwa kazi anayoifanya bwana flani.


Haya ni mawazo ya kimasikini. Kama mawazo ya kimasikini hayatatutoka tuna safari ndefu ya maendeleo. Kwa nini usifight kua kama yeye ulipwe hizo badala yake unataka yeye awe kama wewe?
 
18 Reactions
Reply
Back
Top Bottom