BalaaMkuu tunaomba sana usichokijua pia maombi ni mashtaki kwa Mungu kwa unayemuombea asiye na hofu ya Mungu. Aliye na visasi, muuaji, asiyetenda haki etc etc
mnafiki mkubwa wewe, Ben saa nane anaenda mwaka wa pili hajulikani alipo, Tundu Lissu anauguza majeraha, Azory naye alitekwa hajulikani alipo, kuna watu ni wagonjwa mahospitalini hawana msaada, kuna watu wamefungwa bila hatia na husemi tuwaombee, acha kujipendekeza wewe.Nawasalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo
Kwa ndugu zangu Waislamu nanyi pia nawasalimu!
Sote tu familia moja ya JF
Leo tarehe 01/02/2018 nimerejea tena kuwaomba tuzidi kumuombea Rais wetu mpendwa Dkt John Magufuli. Majukumu aliyokabidhiwa ni makubwa na yanahitaji sio tu ujasiri mkubwa ili kuweza kuyatekekeza ipasavyo bali pia yanahitaji mibaraka ya Mungu.
Kama mwana familia ya JF usiku huu tena nawaomba kwa unyenyekevu mkubwa kuwa m zidi kumuombea Kiongozi wetu mpendwa ili afanikishe yale yote aliyokusudia kuyafanya kwa faida ya nchi yetu Tanzania. Mjitahidi kutenga muda wetu kwa kumuombea Kiongozi wetu azidi kupata nguvu za kuwatumikia Watanzania wote.
Natambua yapo mengi mazuri aliyofanya hadi sasa na nyie ni mashuhuda wa hayo lakini kumbukeni kuwa yapo mengi pia anayotakiwa kuyakamilisha. Ukweli yote aliyokusudia kuyafanya yatawezekana tu kwa uwezo wa Mungu unaotokana kupitia maombi yetu. Natambua kuwa safari ni ndefu ikiwa na majaribu mengi lakini kwa neema za Mungu tutafika salama kwenye nchi ya ahadi.
Niwashukuru sana kwa kunielewa na Mungu azidi awabariki sana.
Mungu wetu tunakuomba uzidi kumbariki na kumpa ulinzi Rais wetu yeye pamoja na familia yake.
Shetani hana nafasi tena mbele za Mungu
Usiku mwema wapendwa