Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,606
- 1,956
Nawasalimu katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo
Kwa ndugu zangu Waislamu nanyi pia nawasalimu!
Sote tu familia moja ya JF
Leo tarehe 01/02/2018 nimerejea tena kuwaomba tuzidi kumuombea Rais wetu mpendwa Dkt John Magufuli. Majukumu aliyokabidhiwa ni makubwa na yanahitaji sio tu ujasiri mkubwa ili kuweza kuyatekekeza ipasavyo bali pia yanahitaji mibaraka ya Mungu.
Kama mwana familia ya JF usiku huu tena nawaomba kwa unyenyekevu mkubwa kuwa m zidi kumuombea Kiongozi wetu mpendwa ili afanikishe yale yote aliyokusudia kuyafanya kwa faida ya nchi yetu Tanzania. Mjitahidi kutenga muda wetu kwa kumuombea Kiongozi wetu azidi kupata nguvu za kuwatumikia Watanzania wote.
Natambua yapo mengi mazuri aliyofanya hadi sasa na nyie ni mashuhuda wa hayo lakini kumbukeni kuwa yapo mengi pia anayotakiwa kuyakamilisha. Ukweli yote aliyokusudia kuyafanya yatawezekana tu kwa uwezo wa Mungu unaotokana kupitia maombi yetu. Natambua kuwa safari ni ndefu ikiwa na majaribu mengi lakini kwa neema za Mungu tutafika salama kwenye nchi ya ahadi.
Niwashukuru sana kwa kunielewa na Mungu azidi awabariki sana.
Mungu wetu tunakuomba uzidi kumbariki na kumpa ulinzi Rais wetu yeye pamoja na familia yake.
Shetani hana nafasi tena mbele za Mungu
Usiku mwema wapendwa
UPDATES:
Hivi sasa ni saa 8:51 usiku
Nimeshaamka naendelea na maombi maalumu kumuombea Rais wetu Dkt John Magufuli.
Tafadhali mwana JF amka na utumie angalao dakika tano tu kumuombea Rais wetu.
Ubarikiwe sana
Kwa ndugu zangu Waislamu nanyi pia nawasalimu!
Sote tu familia moja ya JF
Leo tarehe 01/02/2018 nimerejea tena kuwaomba tuzidi kumuombea Rais wetu mpendwa Dkt John Magufuli. Majukumu aliyokabidhiwa ni makubwa na yanahitaji sio tu ujasiri mkubwa ili kuweza kuyatekekeza ipasavyo bali pia yanahitaji mibaraka ya Mungu.
Kama mwana familia ya JF usiku huu tena nawaomba kwa unyenyekevu mkubwa kuwa m zidi kumuombea Kiongozi wetu mpendwa ili afanikishe yale yote aliyokusudia kuyafanya kwa faida ya nchi yetu Tanzania. Mjitahidi kutenga muda wetu kwa kumuombea Kiongozi wetu azidi kupata nguvu za kuwatumikia Watanzania wote.
Natambua yapo mengi mazuri aliyofanya hadi sasa na nyie ni mashuhuda wa hayo lakini kumbukeni kuwa yapo mengi pia anayotakiwa kuyakamilisha. Ukweli yote aliyokusudia kuyafanya yatawezekana tu kwa uwezo wa Mungu unaotokana kupitia maombi yetu. Natambua kuwa safari ni ndefu ikiwa na majaribu mengi lakini kwa neema za Mungu tutafika salama kwenye nchi ya ahadi.
Niwashukuru sana kwa kunielewa na Mungu azidi awabariki sana.
Mungu wetu tunakuomba uzidi kumbariki na kumpa ulinzi Rais wetu yeye pamoja na familia yake.
Shetani hana nafasi tena mbele za Mungu
Usiku mwema wapendwa
UPDATES:
Hivi sasa ni saa 8:51 usiku
Nimeshaamka naendelea na maombi maalumu kumuombea Rais wetu Dkt John Magufuli.
Tafadhali mwana JF amka na utumie angalao dakika tano tu kumuombea Rais wetu.
Ubarikiwe sana