Alexander The Great
JF-Expert Member
- Aug 28, 2018
- 4,502
- 23,581
Habari wana Jamii,
Nimekaa na kutafakari kuhusu kesi ya Ugaidi Ya Freeman Mbowe na Wenzake ambayo inakaribia kuanza mwezi ujao. Na ndio nikaamua kuanzisha hii thread maalum ya kuomba kesi hio irushwe "LIVE COVARAGE" kwa kutumia Channel Maalum (Za Bure) kama ilivyofanyika;
I) South Africa - Katika kesi ya Oscar Pistorious (Mkimbiaji Kilema - Mwana Paralympic).
II) Kenya - Katika kesi ya kupinga Uchaguzi Mkuu uliopita.
Kwasababu kuu,
1) Ni Kesi yenye umuhimu na mvuto (attention) mkubwa kitaifa na kimataifa.
2) Kuepusha msongamano wa raia kwenda kuisikiliza Mahakamani kwasababu ya maambukizi ya Covid 19.
3) Raia wa Tanzania walio ndani na nje ya nchi wana haki ya kujua, kuona, kusikiliza mashtaka yalio dhidi ya kiongozi wao wa Chama Kikuu Cha Upinzani.
4) Vyombo visivyo vya Serikali (NGO's, Donners e.t.c) vina mvuto wa kujua na kufuatilia dhidi ya kuendeshwa kwa kesi hio kubwa.
5) Ni haki ya kisheria na katiba kwa kila mtu kujua au kufuatilia kesi mahakamani ambayo ana mahusiani nayo, au yenye maslahi nae.
6) Kuna raia wanaishi mbali na Dar Es Salaam na hawana uwezo wa kwenda kushuhudia kesi ya kiongozi wao.
7) Mahakama Ya Kisutu ni ndogo kuweza kutosheleza watu wote watakao kwenda kushuhudia kesi hio.
8) Usalama kwa washtakiwa. Live coverage itapunguza msongamano wa watu nje ya mahakama kwaajili ya usalama wa washtakiwa. Sio kesho tusikie watu wasiojulikana wamemimina risasi kwenye gari ya washtakiwa na kuwaua au kuwajeruhi. Week hii gari ya kina Freeman Mbowe iliharibika mahakamani, hivi kweli unasafirisha makomandoo na mwenyekiti wa upinzani ambao wana kesi kubwa na yenye public interest kidunia kwenye gari bovu??? Usalama wao huoni unakua mashakani??? Watu wasiojulikana (Kama Serikali inavo waita) wakivamia na silaha za moto na kuwamiminia risasi???
9) Dunia na Taifa kwa ujumla lijiridhishe kwamba watuhumiwa watatendewa haki.
Kwa unyenyekevu mkubwa ningependa kutoa vito (Tuweke Itikadi Za Vyama Pembeni) kwa;
A) Wana Familia Wenzangu Wa JamiiForums Na Wana Mitandao Ya Kijamii - Kupaza Sauti.
B) Wanasheria na Mawakili Wote - Kupeleka Maombi Mahakamani Ya Kutoa Kibali Cha Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
C) Wanasiasa - Kupaza Sauti Serikali/DPP Ikubali Maombi Ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
D) Wana Habari - Kupeleka Maombi Mahakamani na Kupaza Sauti ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
E) NGO's (Human Rights Watch) - Kupeleka Maombi Mahakamani na Kupaza Sauti Ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
#KesiYaUgaidiLIVE.
Zitto
Pascal Mayalla
Mfano wa Kesi Ya Uchaguzi Kenya.
Mfano Wa Kesi Ya Oscar Pistorious Nchini South Africa.
Nimekaa na kutafakari kuhusu kesi ya Ugaidi Ya Freeman Mbowe na Wenzake ambayo inakaribia kuanza mwezi ujao. Na ndio nikaamua kuanzisha hii thread maalum ya kuomba kesi hio irushwe "LIVE COVARAGE" kwa kutumia Channel Maalum (Za Bure) kama ilivyofanyika;
I) South Africa - Katika kesi ya Oscar Pistorious (Mkimbiaji Kilema - Mwana Paralympic).
II) Kenya - Katika kesi ya kupinga Uchaguzi Mkuu uliopita.
Kwasababu kuu,
1) Ni Kesi yenye umuhimu na mvuto (attention) mkubwa kitaifa na kimataifa.
2) Kuepusha msongamano wa raia kwenda kuisikiliza Mahakamani kwasababu ya maambukizi ya Covid 19.
3) Raia wa Tanzania walio ndani na nje ya nchi wana haki ya kujua, kuona, kusikiliza mashtaka yalio dhidi ya kiongozi wao wa Chama Kikuu Cha Upinzani.
4) Vyombo visivyo vya Serikali (NGO's, Donners e.t.c) vina mvuto wa kujua na kufuatilia dhidi ya kuendeshwa kwa kesi hio kubwa.
5) Ni haki ya kisheria na katiba kwa kila mtu kujua au kufuatilia kesi mahakamani ambayo ana mahusiani nayo, au yenye maslahi nae.
6) Kuna raia wanaishi mbali na Dar Es Salaam na hawana uwezo wa kwenda kushuhudia kesi ya kiongozi wao.
7) Mahakama Ya Kisutu ni ndogo kuweza kutosheleza watu wote watakao kwenda kushuhudia kesi hio.
8) Usalama kwa washtakiwa. Live coverage itapunguza msongamano wa watu nje ya mahakama kwaajili ya usalama wa washtakiwa. Sio kesho tusikie watu wasiojulikana wamemimina risasi kwenye gari ya washtakiwa na kuwaua au kuwajeruhi. Week hii gari ya kina Freeman Mbowe iliharibika mahakamani, hivi kweli unasafirisha makomandoo na mwenyekiti wa upinzani ambao wana kesi kubwa na yenye public interest kidunia kwenye gari bovu??? Usalama wao huoni unakua mashakani??? Watu wasiojulikana (Kama Serikali inavo waita) wakivamia na silaha za moto na kuwamiminia risasi???
9) Dunia na Taifa kwa ujumla lijiridhishe kwamba watuhumiwa watatendewa haki.
Kwa unyenyekevu mkubwa ningependa kutoa vito (Tuweke Itikadi Za Vyama Pembeni) kwa;
A) Wana Familia Wenzangu Wa JamiiForums Na Wana Mitandao Ya Kijamii - Kupaza Sauti.
B) Wanasheria na Mawakili Wote - Kupeleka Maombi Mahakamani Ya Kutoa Kibali Cha Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
C) Wanasiasa - Kupaza Sauti Serikali/DPP Ikubali Maombi Ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
D) Wana Habari - Kupeleka Maombi Mahakamani na Kupaza Sauti ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
E) NGO's (Human Rights Watch) - Kupeleka Maombi Mahakamani na Kupaza Sauti Ya Kuoneshwa LIVE COVERAGE.
#KesiYaUgaidiLIVE.
Zitto
Pascal Mayalla
Mfano wa Kesi Ya Uchaguzi Kenya.
Mfano Wa Kesi Ya Oscar Pistorious Nchini South Africa.