Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,377
- 217,438
Miongoni mwa mambo ambayo nchi hii itajutia katika maisha yake yote yaliyosalia hapa duniani ni kuruhusu John Magufuli kuwa Rais wake , aliyoyatenda alipokuwa Rais kwa hiyo miaka mitano na Ushee kila mtu ameyaona , hakuna haja ya kuyarudia
Kabla ya kuwa Rais Magufuli alikuwa Waziri , kila mwenye macho aliona mambo aliyoyatenda akiwa Waziri , yalikuwemo Mazuri na Mabaya , huyu aliisababishia serikali hasara kwa kukamata meli ya uvuvi , hakuna aliyesahau hili , alipania kubomoa jengo la Tanesco Ubungo , akakatazwa na Mizengo Pinda , lakini alipotwaa madaraka akalibomoa , wala barabara iliyojengwa haikufika hata ulipokuwa ukuta wa Jengo hilo , hakuwa na sababu yoyote ya kulibomoa zaidi ya ile "UNANIJUA MIMI NI NANI"
Magufuli hakuwahi kuwa muumini wa Demokrasia kuanzia jimboni kwake , mara zote alifanya njama ili apite bila kupingwa , Uongozi ni jambo la Pamoja , yeye aliamini kwenye akili yake tu , haya yote viongozi wake wa chama waliyajua .
Ziara ya Marekani ya Rais Samia imeweka wazi yale yote tuliyokuwa tunayatilia shaka , Ripoti ya CAG imeonyesha wazi kwamba Magufuli hakuwahi kuwa Mlinzi wa rasilimali za Taifa kama tulivyodhani , alitudanganya na Ukuta wa Mererani huku madini yakiibwa !
Kwa kufupisha , Natoa wito kwa Wadau wote wenye uchungu na nchi hii KUWAFUNGULIA MASHITAKA JAKAYA KIKWETE , ABDULRAHMAN KINANA , waliokuwa viongozi wa juu wa ccm na Kamati Kuu ya Chama hicho kwa kuruhusu John Magufuli kugombea Urais wa Tanzania huku wakijua kwamba ana Mapungufu ya kutisha .
Nakala : Peter Kibatala
Kabla ya kuwa Rais Magufuli alikuwa Waziri , kila mwenye macho aliona mambo aliyoyatenda akiwa Waziri , yalikuwemo Mazuri na Mabaya , huyu aliisababishia serikali hasara kwa kukamata meli ya uvuvi , hakuna aliyesahau hili , alipania kubomoa jengo la Tanesco Ubungo , akakatazwa na Mizengo Pinda , lakini alipotwaa madaraka akalibomoa , wala barabara iliyojengwa haikufika hata ulipokuwa ukuta wa Jengo hilo , hakuwa na sababu yoyote ya kulibomoa zaidi ya ile "UNANIJUA MIMI NI NANI"
Magufuli hakuwahi kuwa muumini wa Demokrasia kuanzia jimboni kwake , mara zote alifanya njama ili apite bila kupingwa , Uongozi ni jambo la Pamoja , yeye aliamini kwenye akili yake tu , haya yote viongozi wake wa chama waliyajua .
Ziara ya Marekani ya Rais Samia imeweka wazi yale yote tuliyokuwa tunayatilia shaka , Ripoti ya CAG imeonyesha wazi kwamba Magufuli hakuwahi kuwa Mlinzi wa rasilimali za Taifa kama tulivyodhani , alitudanganya na Ukuta wa Mererani huku madini yakiibwa !
Kwa kufupisha , Natoa wito kwa Wadau wote wenye uchungu na nchi hii KUWAFUNGULIA MASHITAKA JAKAYA KIKWETE , ABDULRAHMAN KINANA , waliokuwa viongozi wa juu wa ccm na Kamati Kuu ya Chama hicho kwa kuruhusu John Magufuli kugombea Urais wa Tanzania huku wakijua kwamba ana Mapungufu ya kutisha .
Nakala : Peter Kibatala