Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,442
- 113,451
Wanabodi,
Hii ni Nipashe ya Leo
Kwa Maslahi ya Taifa" ya leo inajikita kwenye Ibara ya 18 ya Katiba kuhusu moja ya haki muhimu sana ndani ya katiba, yetu ya JMT ya mwaka 1977, kuanzia Ibara ya 18 – 24, katiba yetu imetoa haki zifuatazo: 18. Uhuru wa Maoni. 19. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo. 20. Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine. 21. Uhuru wa kushiriki shughuli za umma. 22. Haki ya kufanya kazi. 23. Haki ya kupata ujira wa haki. 24. Haki ya kumiliki mali.
Haki hizi sio hisani sio huruma, sio option, kusema zinaweza kutolewa au laa!, haki hizi ni stahili, zinapaswa kutolewa na kuheshimiwe na Watanzania wote ikiwemo serikali na viongozi, na taasisi zote. Kwa leo nitajikita zaidi kwenye Ibara ya 18, inasema
18: Uhuru wa Maoni Sheria Na. 15 ya 1984 ib. 6"
(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa kutoingiliwa kati mawasiliano yake.
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.
Haki hizi na uhuru huu wa kutoa maoni, unakwenda sambamba na mipaka ya kawaida ya uhuru, yaani hakuna uhuru usio na mipaka, mwisho wa uhuru wako ni pale uhuru wa mtu mwingine unapoishia. Huu uhuru wa kutoa mawazo yako, unapaswa kuheshimiwa na wote, hata kama hukubaliani na mawazo hayo, na wewe pia unapaswa kuheshimu uhuru, maoni na mawazo yaw engine, hata kama hukubaliani nayo
Leo nimejikita kwenye ibara hii, kufuatia juzi kati hapa, kuna mtu ametoa mawazo yake kuhusu jambo fulani, mtu huyo ameshambuliwa kila kona kwa kushukiwa kama mwewe anavyotaka kunyakua kifaranga cha kuku, wengine wakimbeza, wengine wamdhihaki na wengine hata kufikia kiwango cha kumtukana na kumdhalilisha!
Kilichopelekea mtu huyo kushambuliwa, ni kwa sababu tuu amekosoa jambo fulani!. Kutokana na kutoa nawazo yake ya ukosoaji, naona kuna watu wanataka kuingilia haki hii muhimu na kujimilikisha wao kwa kuingilia uhuru wa maoni wa watu wengine na hata kuwapangia ni maoni gani watoe!. Yaani wenye haki ni wanaosifu tuu na kupongeza, lakini ukikosoa, inakuwa nongwa
Toka enzi za Rais Mwinyi, Rais Mkapa, Rais Kikwete na Rais Magufuli, wote walisifiwa na walikosolewa!. Ile haki ya kusifu na kupongeza, inapaswa kwenda sambamba na haki ya kukosoa!. Hivyo kuna watu wanataka haki iwe na haki ya kusifu tuu na kupongeza tuu, lakini kukosolewa iwe nongwa, ni kosa, ni dhambi!.
Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia katika mkutano wa 47 wa wanasheria Afrika Mashariki uliofanyika mkoani Arusha, amesema haya kuhusu kushirikisha watu/taasisi ambazo ziko dhidi yake
Kwa mfano Tanzania, miaka minne mitano iliyopita tulikuwa na Tanganyika Law Society ambayo frankly speaking ilikuwa siyo chama cha Wanasheria, kilikuwa chama cha Wanaharakati na mapambano yao yalikuwa ni dhidi ya Serikali.
Sasa mimi nikijua wewe ni dhidi yangu nitakushirikishaje? Siwezi kukushirikisha, si ndiyo! Mpaka unioneshe kwamba am here to support you, I'm here to serve a country, I'm here kuonesha ujuzi wangu kwa nchi yangu.
Nikikuona una sura hiyo nitakushirikisha, nikikuona una sura ya uadui nami sitaweza kukushirikisha. Utatumia Sheria zote za Kimataifa, zoooote na mimi nitatumia zangu za ndani ya nchi kuku-bar usishiriki kwangu.
Kukosoa serikali, sio kosa, wala ukosoaji, sio uadui, sio chuki, na sio dhidi ya serikali, ukosoaji wa serikali ni differing opinion ambao pia ni haki ns
na unalindwa na katiba, amlimradi ukosoaji huo uwe ni ukosoaji unaofanywa kwa nia njema ya kuisaidia kujenga nchi, kuisaidia serikali na kuwasaidia viongozi, ambao unaitwa constructive cricism, ukosoaji wenye nia ya kujenga na kusaidia, ambao huendana na ushauri wa njia bora ya kufanya hilo jambo unalokosoa. Ukosoaji mbaya ni ule wa kubagaza, kuzodoa, kutumia lugha za kuudhi, kutukana na kudhalilisha.
Kwenye Freedom of expression ni haki kwa wote,wenye kusifu na kupongeza, wana haki ya kusifu na kumpongeza kwa kuupiga mwingi, na wenye kukosoa wana haki ya kukosoa, hivyo haki ya kusifu inakwenda sambamba na haki ya kukosoa, ibara ya 18 ya katiba inataka haki ya kusifu iheshimiwe na haki ya kukosoa pia iheshimiwe.
Tukawasisitiza watu humu kuwa Rais Samia na yeye ni binadamu, sio malaika!, Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda
Hivyo kama ilivyo kwenye haki ya kupiga kura, inakwenda sambamba na haki ya kupigiwa kura, vivyo hivyo kwenye haki ya kusifu na kumpongeza rais Samia, haki hiyo ya kumpongeza, inakwenda sambamba na haki ya kumkosoa rais Samia, mkosoaji asishambuliwe yeye, ishambuliwe hoja yake!.
Hitimisho
Wanaosifu wasifu kwa hoja, ni haki yao kusifu, lakini pia, wanao kosoa, wakosoe kwa hoja kwa kutumia ukosoaji wa contructive criticism, ukosoaji wenye nia njema ya kujenga, kwa kutumia lugha ya staha na amini usiamini, unaweza kukuta, wanaomkosoa Rais Mama Samia, ndio wanao msaidia zaidi kuliko wanaomsifu kwa kuupiga mwingi!, huku tukiwaomba viongozi wetu, wazidishe kungumusha (kuzifanya ngozi zao kuwa ngumu), ngozi zao kwa kufuata msemo wa kizungu wa “take the bitter with the sweet”, kama wanavyofurahia kidonge kitamu kwenye matamu na mazuri, pia wawe tayari kupokea vidoge vichungu kwenye machungu, ila pia utafiti wa dawa, umethibitisha vidoge vichungu ndio vinatibu homa, ili upone lazima ukubali kumeza kidonge kichungu. Viongozi wetu wawe na ngozi ngumu, kumeza vidonge vyote vitamu na vichungu!, upinzani sio uadui, kusifia sio kosa, sio dhambi na sio kupenda, na kukosoa sio kuchukia, sio uadui sio dhambi!, kuna wanaompenda sana Mama na wanamkosoa kwa mapenzi mema ili asishindwe!.
Wasalaam
Paskali
Hii ni Nipashe ya Leo
Kwa Maslahi ya Taifa" ya leo inajikita kwenye Ibara ya 18 ya Katiba kuhusu moja ya haki muhimu sana ndani ya katiba, yetu ya JMT ya mwaka 1977, kuanzia Ibara ya 18 – 24, katiba yetu imetoa haki zifuatazo: 18. Uhuru wa Maoni. 19. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo. 20. Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine. 21. Uhuru wa kushiriki shughuli za umma. 22. Haki ya kufanya kazi. 23. Haki ya kupata ujira wa haki. 24. Haki ya kumiliki mali.
Haki hizi sio hisani sio huruma, sio option, kusema zinaweza kutolewa au laa!, haki hizi ni stahili, zinapaswa kutolewa na kuheshimiwe na Watanzania wote ikiwemo serikali na viongozi, na taasisi zote. Kwa leo nitajikita zaidi kwenye Ibara ya 18, inasema
18: Uhuru wa Maoni Sheria Na. 15 ya 1984 ib. 6"
(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa kutoingiliwa kati mawasiliano yake.
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.
Haki hizi na uhuru huu wa kutoa maoni, unakwenda sambamba na mipaka ya kawaida ya uhuru, yaani hakuna uhuru usio na mipaka, mwisho wa uhuru wako ni pale uhuru wa mtu mwingine unapoishia. Huu uhuru wa kutoa mawazo yako, unapaswa kuheshimiwa na wote, hata kama hukubaliani na mawazo hayo, na wewe pia unapaswa kuheshimu uhuru, maoni na mawazo yaw engine, hata kama hukubaliani nayo
Leo nimejikita kwenye ibara hii, kufuatia juzi kati hapa, kuna mtu ametoa mawazo yake kuhusu jambo fulani, mtu huyo ameshambuliwa kila kona kwa kushukiwa kama mwewe anavyotaka kunyakua kifaranga cha kuku, wengine wakimbeza, wengine wamdhihaki na wengine hata kufikia kiwango cha kumtukana na kumdhalilisha!
Kilichopelekea mtu huyo kushambuliwa, ni kwa sababu tuu amekosoa jambo fulani!. Kutokana na kutoa nawazo yake ya ukosoaji, naona kuna watu wanataka kuingilia haki hii muhimu na kujimilikisha wao kwa kuingilia uhuru wa maoni wa watu wengine na hata kuwapangia ni maoni gani watoe!. Yaani wenye haki ni wanaosifu tuu na kupongeza, lakini ukikosoa, inakuwa nongwa
Toka enzi za Rais Mwinyi, Rais Mkapa, Rais Kikwete na Rais Magufuli, wote walisifiwa na walikosolewa!. Ile haki ya kusifu na kupongeza, inapaswa kwenda sambamba na haki ya kukosoa!. Hivyo kuna watu wanataka haki iwe na haki ya kusifu tuu na kupongeza tuu, lakini kukosolewa iwe nongwa, ni kosa, ni dhambi!.
Rais Samia Suluhu Hassan akihutubia katika mkutano wa 47 wa wanasheria Afrika Mashariki uliofanyika mkoani Arusha, amesema haya kuhusu kushirikisha watu/taasisi ambazo ziko dhidi yake
Kwa mfano Tanzania, miaka minne mitano iliyopita tulikuwa na Tanganyika Law Society ambayo frankly speaking ilikuwa siyo chama cha Wanasheria, kilikuwa chama cha Wanaharakati na mapambano yao yalikuwa ni dhidi ya Serikali.
Sasa mimi nikijua wewe ni dhidi yangu nitakushirikishaje? Siwezi kukushirikisha, si ndiyo! Mpaka unioneshe kwamba am here to support you, I'm here to serve a country, I'm here kuonesha ujuzi wangu kwa nchi yangu.
Nikikuona una sura hiyo nitakushirikisha, nikikuona una sura ya uadui nami sitaweza kukushirikisha. Utatumia Sheria zote za Kimataifa, zoooote na mimi nitatumia zangu za ndani ya nchi kuku-bar usishiriki kwangu.
Kukosoa serikali, sio kosa, wala ukosoaji, sio uadui, sio chuki, na sio dhidi ya serikali, ukosoaji wa serikali ni differing opinion ambao pia ni haki ns
na unalindwa na katiba, amlimradi ukosoaji huo uwe ni ukosoaji unaofanywa kwa nia njema ya kuisaidia kujenga nchi, kuisaidia serikali na kuwasaidia viongozi, ambao unaitwa constructive cricism, ukosoaji wenye nia ya kujenga na kusaidia, ambao huendana na ushauri wa njia bora ya kufanya hilo jambo unalokosoa. Ukosoaji mbaya ni ule wa kubagaza, kuzodoa, kutumia lugha za kuudhi, kutukana na kudhalilisha.
Kwenye Freedom of expression ni haki kwa wote,wenye kusifu na kupongeza, wana haki ya kusifu na kumpongeza kwa kuupiga mwingi, na wenye kukosoa wana haki ya kukosoa, hivyo haki ya kusifu inakwenda sambamba na haki ya kukosoa, ibara ya 18 ya katiba inataka haki ya kusifu iheshimiwe na haki ya kukosoa pia iheshimiwe.
Tukawasisitiza watu humu kuwa Rais Samia na yeye ni binadamu, sio malaika!, Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda
Hivyo kama ilivyo kwenye haki ya kupiga kura, inakwenda sambamba na haki ya kupigiwa kura, vivyo hivyo kwenye haki ya kusifu na kumpongeza rais Samia, haki hiyo ya kumpongeza, inakwenda sambamba na haki ya kumkosoa rais Samia, mkosoaji asishambuliwe yeye, ishambuliwe hoja yake!.
Hitimisho
Wanaosifu wasifu kwa hoja, ni haki yao kusifu, lakini pia, wanao kosoa, wakosoe kwa hoja kwa kutumia ukosoaji wa contructive criticism, ukosoaji wenye nia njema ya kujenga, kwa kutumia lugha ya staha na amini usiamini, unaweza kukuta, wanaomkosoa Rais Mama Samia, ndio wanao msaidia zaidi kuliko wanaomsifu kwa kuupiga mwingi!, huku tukiwaomba viongozi wetu, wazidishe kungumusha (kuzifanya ngozi zao kuwa ngumu), ngozi zao kwa kufuata msemo wa kizungu wa “take the bitter with the sweet”, kama wanavyofurahia kidonge kitamu kwenye matamu na mazuri, pia wawe tayari kupokea vidoge vichungu kwenye machungu, ila pia utafiti wa dawa, umethibitisha vidoge vichungu ndio vinatibu homa, ili upone lazima ukubali kumeza kidonge kichungu. Viongozi wetu wawe na ngozi ngumu, kumeza vidonge vyote vitamu na vichungu!, upinzani sio uadui, kusifia sio kosa, sio dhambi na sio kupenda, na kukosoa sio kuchukia, sio uadui sio dhambi!, kuna wanaompenda sana Mama na wanamkosoa kwa mapenzi mema ili asishindwe!.
Wasalaam
Paskali