Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,063
- 22,755
Listi ya mafisadi ilikuwa bado mbichi na serikali ilikuwa bado inatafakari ifanye nini, ikaingia Richmond. Serikali ikachanganyikiwa kwa kuanza kujitokeza kwa dalili za wazi za wananchi kukosa imani na serikali walioiweka wenyewe madarakani. Wakati serikali haijakaa sawa EPA na watoto wake wakawa wanabisha hodi huku JF ikitema cheche kwa data za uhakika kama kawaida. Hofu kuu ikatanda ndani ya CCM na serikali yake na hoja kuu ikawa - hapa tusipocheza kama Pele tumekwisha.
Mbinu zikasukwa kwa mtindo wa zimamoto na hatua ya kwanza ikawa ni kuisafisha Richmond kupitia TAKUKURU. Wakati wanatambua kuwa Tanzania ya leo ni tofauti na ya juzi, maji yakawa yameshamwagika na kitendo hicho kikawa kama vile wamemwaga petroli kwenye moto. Haraka haraka Bunge likaunda tume kwa lengo la kuinusuru serikali. Vibangusilo vikapatikana lakini kwa vile moto ulikuwa unazidi kuwa mkali, ikaamuliwa bangusilo mkuu naye lazima aunganishwe - naye akakubali japo shingo upande.
Badala ya hatua hizi kupoza hasira za wananchi ndio mambo yakazidi kuwa mambo na hatari ya kuumbuana ikawa inapiga hodi. Haraka haraka mweka hazina mkuu naye akatoswa na ikaundwa timu ya wataalamu kufuta nyayo za wahusika na kuhakikisha hakuna nyaraka zote zenye ushahidi zimebaki sehemu husika kwa kile kilichoitwa uchunguzi wa kitaalam. Na sheria ya nyaraka za siri ikaanza kupigiwa kelele ku"preempt" kutolewa kwa nyaraka zaidi - luckily it was too late
Baada ya kujiridhisha kuwa hakuna tena ushahidi zaidi wa kuweza kuwatia hatiani mhusika/wahusika wakuu, mbinu ikasukwa ya kuwafikisha mahakamani waliotupiwa makombo na kuwaacha waliokaa meza kuu wakitanua. Lakini pamoja na hatua zote hizi, kiu ya wazalendo wanaolilia haki haikuweza kuzimwa. Mpiganaji moja akajitokeza live kufunua vizibo vya maji machafu - La haula, taharuki wakajitokeza maruga ruga wakataka kufunika kombe mwanaharamu apite - kumbe la kuvunda halina ubani!!
My take: Ni wapi ulimwenguni ambapo soo kama hii ya kisanii ingewezekana isipokuwa hapa bongo tu. Hivi sasa mafisadi watajitokeza na kuongea kwa kujiamini kuwa wako salama - but could they be in for a rude awakening. Heko wazalendo wote waliouona huu mchezo tokea mapema na wakafanya kile ambacho mwananchi yeyote mwenye uchungu na taifa lake aweza kukifanya - nawapa pongezi nyingi. Nimejaribu kuifupisha hii tetesi kwa sababu bado sina uhakika wake - On the other hand I really hope it is not true.
Mbinu zikasukwa kwa mtindo wa zimamoto na hatua ya kwanza ikawa ni kuisafisha Richmond kupitia TAKUKURU. Wakati wanatambua kuwa Tanzania ya leo ni tofauti na ya juzi, maji yakawa yameshamwagika na kitendo hicho kikawa kama vile wamemwaga petroli kwenye moto. Haraka haraka Bunge likaunda tume kwa lengo la kuinusuru serikali. Vibangusilo vikapatikana lakini kwa vile moto ulikuwa unazidi kuwa mkali, ikaamuliwa bangusilo mkuu naye lazima aunganishwe - naye akakubali japo shingo upande.
Badala ya hatua hizi kupoza hasira za wananchi ndio mambo yakazidi kuwa mambo na hatari ya kuumbuana ikawa inapiga hodi. Haraka haraka mweka hazina mkuu naye akatoswa na ikaundwa timu ya wataalamu kufuta nyayo za wahusika na kuhakikisha hakuna nyaraka zote zenye ushahidi zimebaki sehemu husika kwa kile kilichoitwa uchunguzi wa kitaalam. Na sheria ya nyaraka za siri ikaanza kupigiwa kelele ku"preempt" kutolewa kwa nyaraka zaidi - luckily it was too late
Baada ya kujiridhisha kuwa hakuna tena ushahidi zaidi wa kuweza kuwatia hatiani mhusika/wahusika wakuu, mbinu ikasukwa ya kuwafikisha mahakamani waliotupiwa makombo na kuwaacha waliokaa meza kuu wakitanua. Lakini pamoja na hatua zote hizi, kiu ya wazalendo wanaolilia haki haikuweza kuzimwa. Mpiganaji moja akajitokeza live kufunua vizibo vya maji machafu - La haula, taharuki wakajitokeza maruga ruga wakataka kufunika kombe mwanaharamu apite - kumbe la kuvunda halina ubani!!
My take: Ni wapi ulimwenguni ambapo soo kama hii ya kisanii ingewezekana isipokuwa hapa bongo tu. Hivi sasa mafisadi watajitokeza na kuongea kwa kujiamini kuwa wako salama - but could they be in for a rude awakening. Heko wazalendo wote waliouona huu mchezo tokea mapema na wakafanya kile ambacho mwananchi yeyote mwenye uchungu na taifa lake aweza kukifanya - nawapa pongezi nyingi. Nimejaribu kuifupisha hii tetesi kwa sababu bado sina uhakika wake - On the other hand I really hope it is not true.