Wimbo wa Sikukuu ya kuzaliwa: Ifike mahali tuwe na wimbo kwa lugha yetu ya kiswahili na Serikali kwa kushirikiana na wadau isimamie jambo hili

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,998
144,329
Tangu nikiwa mtoto mdogo mpaka leo hii nikiwa ni mtu mzima,sijawahi kusikia wimbo ya kusindikiza sikuku ya mtu kuzaliwa(birthday) unaoimbwa kwa lugha ya kiswahili zaidi ya huu tuliouzoea wa kutumia maneno ya kingereza jambo ambalo mimi huwa siku zote naliona haliko sawa japo linaoneekana ni la kawaida tu kwa watu wengi.

Hata katika nchi nyingine za kiafrika,sijui kama nao wana wimbo unaoimbwa kwa kutumia lugha zao za asili au za mataifa yao kusindikiza sikukuu hii na hii inatokana na ukweli kwamba, sikukuu hii ya kuzaliwa haikuwa utamaduni wetu na kama tulikuwa na utamaduni huu,basi wimbo wa kusindikiza sikukuu hii kwa lugha zetu za asili au za mataifa yetu ya kiarika ni jambo ambalo hatukuwahi kuwa nalo(tulikuwa tunasherehekea bila kuimba).

Sasa tujiulize,kwa upande wetu sisi watanzania,je,i ni sahihi mpaka leo kusherekea sikukuu ya kuzaliwa huku tukiimba wimbo huu wenye maneno ya kingereza na wakati huo huo tukijinadi kukuza lugha yetu ya kiswahili?

Labda niulize,hivi wachina,wakorea na hata warusi,nao husherekea sikukuu hii kwa kutumia wimbo huu wenye maneno ya kingereza?

Binafsi nato wito kwa serikali kutangaza donge nono kwa mtu yoyote iwe mtu binafsi,mwanamuziki,bendi ya muziki,n.k atakaeweza kutunga maneno/wimbo mfupi wa kusindikiza siku hii ya kuzaliwa utakaotumia maneno ya kiswahili ili na sisi tuwe na wimbo unaotumia lugha yetu ya Taifa badala ya kuiga kila kitu.

Kama tunaona kutumia kingereza katika mawasiliano yetu ni kutukuza kingereza na kupuuza lugha yetu,basi tujue matumizi ya huu wimbo ni muendeleo ule ule wa kuthamini vya wenzetu na kupuuza vya kwetu.

Labda nimalizie kwa kuuliza, hivi watu mmekaa kama familia alafu kuanzia baba,mama,watoto,ndugu na jamaa mko busy kuimba sijui happy birthday dear nani, hivi huwa hatujishitukii au kuona hili jambo haliko sawa?

In short,hatuoni kuna kasoro katika hili jambo?

Au timu fulani ya wabantu na mashabiki wao kuimba happy birthday pale uwanjani siku ile nako kulikuwa sahihi?
 
Harminize hana wimbo wa siku ya kuzaliwa? Shida lazima uonekane umesoma kwa kuongezea kiingereza kwa mbali.
 
Serikali ndo isimamie?

You gotta be kidding me!

Stupid beyond belief?
Unaelewa maana ya kusema serikali kwa kutumia wadau au umeangali tu ID ya nani kaleta mada ukakurupuka kuchangia?

Wasukumu(baadhi) ni wazi ni watu wa chuki kupitiliza!!
 
Wakati fulani walikuja wageni fulani kutoka Japan hapa kazini. Sasa mmoja wao siku hiyo alikuwa anaadhimisha siku yake ya kuzaliwa. Akatuomba tumuimbie wimbo wa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa kiswahili. Tukaishia kujiuma uma tu.
 
Salary naamini kabisa uko smart kuliko hii hoja yako!nadhan haitatusaidia chchte kile kwenye ustawi mzima wa nchi yetu..haya mwachie Makonda!
Bora tungeanza hata kujadili as Nation wapi tuko vizuri zaidi!maana kila sehem tunafeli tu
 
Salary naamini kabisa uko smart kuliko hii hoja yako!nadhan haitatusaidia chchte kile kwenye ustawi mzima wa nchi yetu..haya mwachie Makonda!
Bora tungeanza hata kujadili as Nation wapi tuko vizuri zaidi!maana kila sehem tunafeli tu
Hii issue huwa ni ya aibu bora hata kuacha kuimba kabisa!!!
 
Wakati fulani walikuja wageni fulani kutoka Japan hapa kazini. Sasa mmoja wao siku hiyo alikuwa anaadhimisha siku yake ya kuzaliwa. Akatuomba tumuimbie wimbo wa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa kiswahili. Tukaishia kujiuma uma tu.
Mkuu,hapa mpaka siku atokee kiongozi aseme jambo kama hili ndio labda watu wataelewa kuwa japo hili ni jambo dogo,ila halipendezi hata kidogo na ni bora kuacha kuimba kabisa.
 
Kuna wajimga wananibeza hapa wakiona hii ni hoja ya kipuuzi kumbe wao ndio wapuuzi.
Lazma uonekane mpumbavu kupita kiasi, si bora ungefanya utafuti juu ya wimbo wa taifa nafikir ungefanya hivo ungeshauri tuimbe wetu kuliko huu wa kukopi.
 
Lazma uonekane mpumbavu kupita kiasi, si bora ungefanya utafuti juu ya wimbo wa taifa nafikir ungefanya hivo ungeshauri tuimbe wetu kuliko huu wa kukopi.

Kwakuwa mmeumbwa kutawaliwa na hamjali thamani ya kuwa na vyenu,ni wazi mtaona sawa tu kukusanyika watu wazima na kuanza kuimba birthday fulani.
 
Naona na wewe umegeuka kuwa nationalist, lugha za mabeberu huzitaki eee????

Ila hivi birthday kwa Kiswahili ni nini?
Haya mambo ya kisasa kuyapeleka kwa Kiswahili ni ngumu sana, sababu sio ya Kiswahili
Kiswahili ukikitumia kwenye ukisasa, ukisasa unakuwa hauna "swag" tena kama umeiga ya wazungu, usipoiga na lugha yake unaonekana hujayaelewa wala huendani nayo

Ni kama kusema tubatize watoto majina yetu ya asili wakati tunafuata dini ambazo sio za asili, mzazi gani atakuelewa umbatize mtoto wake jina la "kishenzi".?
 
Naona na wewe umegeuka kuwa nationalist, lugha za mabeberu huzitaki eee????

Ila hivi birthday kwa Kiswahili ni nini?
Haya mambo ya kisasa kuyapeleka kwa Kiswahili ni ngumu sana, sababu sio ya Kiswahili
Kiswahili ukikitumia kwenye ukisasa, ukisasa unakuwa hauna "swag" tena

Umeiga ya wazungu, iga na lugha yake
Ni lazima wawepo watu au mtu wa kuja na wazo ndio mambo huanza hivyo.
 
Mleta mada yuko sahihi asibezwe ingawaje hoja ni binafsi zaidi siyo jambo la kitaifa
Asante kwa kunielewa, ila uje tu hata Ikulu huu ndio wimbo unaotumika.

Mara nyingi unapokuja na jambo ambalo watu wamelizoea hata kama halifai au lina madhara,ni lazima tu utapingwa tena sana maana wanadamu ndivyo tulivyo.
 
Back
Top Bottom