leonaldo
JF-Expert Member
- Oct 26, 2014
- 2,585
- 3,179
Kwani kuna yeyote aliyerazimishwa kuchanga?Ndugu zangu,
Leo hii ingetokea Bob Marley akafufuka angewacharaza viboko akina Lissu na Chadema kwa kitendo cha kutumia wimbo wake wa "one love" kunyang'anya wananchi hela zao za chakula kwa kisingizio cha kampeni.
Bob Marley alikuwa mwanahatakati aliyetetea maslahi ya wanyonge kupitia muziki bila kuwachangisha.
Kila sehemu wakati wa kampeni wimbo huu wa "one love" unapigwa na ghafla baadhi ya viongozi wa Chadema wanapita na mifuko kushawishi watu watoe walichonacho na kibaya zaidi hakuwa uwazi katika matumizi ya michango hiyo.
Nimalize kwa kuwashauri muwe na huruma waachieni wananchi hela zao za chakula na dawa.