Wimbi la viongozi na wanachama kukimbia vyama vyao vya siasa: Ni uoga, sifa au kutafuta maslahi?

hippocratessocrates

JF-Expert Member
Jul 1, 2012
3,598
1,539
Salaam.

Hivi karibuni tumeshuhudia wimbi kubwa la wanachama mbalimbali wakiwemo na na viongozi wa ngazi ya Udiwani hadi Taifa kukimbia vyama vyao kuelekea vingine. Hasa hili liitwalo "mafuriko" la wanachama wengi wa CCM kuhamia CHADEMA/UKAWA.

Ninajiuliza ni nini hasa kilichopelekea 'mbio' hizi?

1. Uoga:
Hofu ya kuona ukihama hali haitakuwa shwari ya usalama binafsi na kwamba kiongozi mmoja akianzisha na akawa 'salama', basi wengine wanaweza kufuata? Kama ndivyo ni aina gani ya viongozi(wasio shupavu tulikuwa/tulio nao), pili ni aina gani ya udikteta wa viongozi ndani ya vyama kuwapa "hofu" wanachama? Tutegemee nini pale Baraza la mawaziri likivunjwa?

2. Sifa:
Nchi hii tumetawaliwa na mihemko, hata kama jambo hatujalitafakari lakini kwa sababu ya ushabiki, wengi wetu tumekuwa katika mkumbo. Kama ndivyo, inatusaidia nini hasa kwa hawa wanaohama?

3. Maslahi:
'Muda wa kufanya/kupiga mahesabu ndiyo huu'
Tumeshuhudia wengi wa walio "katwa" ndiyo walio na wanaoendelea kuhama! Je, ni kweli wangeonyesha nia hiyo hiyo ya kutaka mabadiliko hata ndani ya vyama vyao kama 'wasingekatwa'? Kinachowaleta ni demokrasia au Maslahi? Kama ni demokrasia kwanini wasikubali kushindwa ndani ya vyama vyao?

Ni nini hasa lengo lao na zaidi kama CHADEMA/UKAWA tumejiandaaje/ni mkakati gani 'tulionao' kuhakikisha wanaokuja ni 'safi' na si mamluki au "Makapi"?
 
Salaam.

Hivi karibuni tumeshuhudia wimbi kubwa la wanachama mbalimbali wakiwemo na na viongozi wa ngazi ya Udiwani hadi Taifa kukimbia vyama vyao kuelekea vingine. Hasa hili liitwalo "mafuriko" la wanachama wengi wa CCM kuhamia CHADEMA/UKAWA.

Ninajiuliza ni nini hasa kilichopelekea 'mbio' hizi?

1. Uoga:
Hofu ya kuona ukihama hali haitakuwa shwari ya usalama binafsi na kwamba kiongozi mmoja akianzisha na akawa 'salama', basi wengine wanaweza kufuata? Kama ndivyo ni aina gani ya viongozi(wasio shupavu tulikuwa/tulio nao), pili ni aina gani ya udikteta wa viongozi ndani ya vyama kuwapa "hofu" wanachama? Tutegemee nini pale Baraza la mawaziri likivunjwa?

2. Sifa:
Nchi hii tumetawaliwa na mihemko, hata kama jambo hatujalitafakari lakini kwa sababu ya ushabiki, wengi wetu tumekuwa katika mkumbo. Kama ndivyo, inatusaidia nini hasa kwa hawa wanaohama?

3. Maslahi:
'Muda wa kufanya/kupiga mahesabu ndiyo huu'
Tumeshuhudia wengi wa walio "katwa" ndiyo walio na wanaoendelea kuhama! Je, ni kweli wangeonyesha nia hiyo hiyo ya kutaka mabadiliko hata ndani ya vyama vyao kama 'wasingekatwa'? Kinachowaleta ni demokrasia au Maslahi? Kama ni demokrasia kwanini wasikubali kushindwa ndani ya vyama vyao?

Ni nini hasa lengo lao na zaidi kama CHADEMA/UKAWA tumejiandaaje/ni mkakati gani 'tulionao' kuhakikisha wanaokuja ni 'safi' na si mamluki au "Makapi"?

kwani chadema ni wasafi?? mpaka wawe na uwezo wa kuwazuia hao wachafu?

kinachotakiwa kwa sasa ni mabadiliko! hoja ya usafi au uchafu weka pembeni, hakuna msafi chadema, hakuna msafi CCM! ila muda wa wale wachafu 'confirmed' wa CCM kutoka na kuingia wachafu 'infered' hawa wa ukawa


kumbuka lengo lao wote ni madaraka, usijitie upofu katika hilo
 
kwani chadema ni wasafi?? mpaka wawe na uwezo wa kuwazuia hao wachafu?

kinachotakiwa kwa sasa ni mabadiliko! hoja ya usafi au uchafu weka pembeni, hakuna msafi chadema, hakuna msafi CCM! ila muda wa wale wachafu 'confirmed' wa CCM kutoka na kuingia wachafu 'infered' hawa wa ukawa


kumbuka lengo lao wote ni madaraka, usijitie upofu katika hilo

Hoja ya usafi haiwezi kuwekwa pembeni.

Kama ulivyosema lengo lao wote ni madaraka, kama ndivyo namna madaraka hayo, ustawi na uadilifu kabla ya kuhama chama huusika hapa. Mabadiliko tuyatakayo ni lazima kuambatana na hili. Tusitegemee mabadiliko kwa "mafedhuli" wale wale walioharibu nchi na kutaka kuhamia vyama vingine baada ya kuona mambo ni magumu bila ya wao kukubali uharibifu walioufanya.
 
Back
Top Bottom