William Shao nimemkubali

Yo Yo

JF-Expert Member
May 31, 2008
11,217
1,702
Jalada.jpg

Jana kupitia channel 10 kwenye kipindi cha tutafika? mwandishi william Shao alikuwepo akichambua kitabu chake hicho,mwandishi kweli ana point za kutosha niliona mpaka Dr Lwaitama alikuwa kimya akisikiliza point zake.
 
Unamkubali kasemaje?
Eleza hoja ieleweke si wote tuliangalia channel 10.
 
Kuna kazi za mwandishi mmarekani anaitwa Moore, tizama Truth Hollywood Speak Out ya 2011, ukishamaliza kuzisoma na kutizama then njoo na anachokiongea bwana Shao, hata hivyo ni mwandishi mzuri
 
Mimi nimesoma hicho kitabu, na nimekuwa nikisoma hata makala zake alizokuwa akiliandikia gazeti la Rai. Kwa kweli hoja alizotoa katika kitabu hicho ni nzito, tena nzito sana. Pia hicho kipindi cha Channel Ten nilikiangalia, nikatamani kitudiwe. Hata Makwaia aliyekuwa akimhoji Shao alipigwa na bumbuwazi kwa data alizokuwa akimwaga, na yule daktari wa UDSM Doctor Lwaitama naye alikaa kimya akimsikiliza. Pembeni yake alikuweko mwandishi wa siku nyingi anayeitwa Tagalile. Aliyoyasema katika Channel ten mbona madogo? Uianza kusoma kitabu hicho hutakiweka chini. Hata mimi namkubali, tena namkubali sana.
 
Nilisikia aliacha uhariri DARLEO na sasa gazeti hilolimekufa. Nilisikia Business Times nayo iko matatano. wafanyakazi wake hawajalipwa kwa miezi mitano mfululizo, na wengine wanakimbia. Anayejua zaidi atujushe.
 
labda utaje kampuni ya Business Times. Ukitaja dar leo..ah.. Magazeti ya jioni hayalipi. Abdiel M. aliona mapema akafunga Alasiri
 
Kwahiyo jamaa bado anaishi, sasa si aseme Kama yu hai dunia nzima tujue USA waongo
 
Kwahiyo jamaa bado anaishi, sasa si aseme Kama yu hai dunia nzima tujue USA waongo
 
Watanzania ndio kawaida yetu

Kuibua hoja ambayo ilishaibuliwa

This is Lack of bright people
Kabisa mkuu kachukua hoja zilizo shaibuliwa muda kazitoa kwenye kingereza kaziandika kwa kiswahili, basi watanzania wamemuona ni mtu bright na makini sana.
Any way akili ni nywele ukitaka kula na kipofu usimshike mikono..
 
Kabisa mkuu kachukua hoja zilizo shaibuliwa muda kazitoa kwenye kingereza kaziandika kwa kiswahili, basi watanzania wamemuona ni mtu bright na makini sana.
Any way akili ni nywele ukitaka kula na kipofu usimshike mikono.
Ulishasoma kitabu hicho? Kama umekisoma sawa, lakini kama hujakisoma umejuaje hoja alizotoa zimeshaibuliwa na wengine? Au ni ule wivu wa maendeleo ya wengine?????
 
Zamani alikuwa akaiandika kuhusu fremason kwenye rai ghafla akapotea ikabidini mpigie ili kujua muendelezo wa makala akanambia wenye gazeti wamegoma asiendelee. Akahamia gazeti la tazama. yuko vizuri. Anajitahidi kutufanya tufikirie tusiamini kila kitu toka kwa mokoloni
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom