William Malecela: Watoto wa viongozi na uongozi wa taifa letu!

Apr 27, 2006
26,588
10,375
by William Malecela on Saturday, May 14, 2011

Ni lazima tukubaliane kwanza kwamba watoto wa viongozi wa Tanzania ambao wengi wameanza kuingia kwenye siasa na kushika nafasi mbalimbali wana haki kabisa ya kushika nafasi yoyote ya uongozi wa taifa kama Watanzania wengine. Haki yao ya Kikatiba kuchaguliwa au kushiriki nafasi yoyote ya kisiasa kwa mujibu wa taratibu na sheria zilizopo haifutwi au kuondolewa kwa sababu ya nafasi za baba zao kwa taifa letu, sasa au huko nyuma.

-Tatizo kubwa ambalo lipo au niseme mawili ni kwamba kuna hisia kuwa watoto hao wanapewa nafasi hizo si kwa sababu ya kustahili wao wenyewe bali kwa sababu ya kubebwa au kutengenezewa mazingira ya kushika nafasi mbali mbali kwa sababu ya wazazi wao. Hili tumejionea likitokea kwa vyama vyote vya siasa nchini, yaani watoto na ndugu wa viongozi wakishiriki kwenye uongozi pia!

- Na pili, endapo wanashika nafasi ambazo zinahusiana na masuala ya utawala na sheria itakuwa vigumu sana kwa watoto hao kutengua au kuchukua hatu ambazo zitawaonesha kuwa wanafumua mambo yaliyoyofanywa na wazazi wao au hata kushindwa kuchukua hatua mbalimbali kwa sababu ya wazazi wao.

- Hivyo, hisia za haya mawili zinawafanya wananchi wengi kuona kuwa katika nafasi kadha wa kadha hasa za kisiasa ni vigumu sana kwa watoto kuwawajibisha wazazi wao - aidha kwa kusahihisha makosa yao au kuwachukulia hatua kama inapasa. Jambo la msingi ni kuweka msingi na utaratibu kuwa kila Mtanzania anapata nafasi ya kulitumikia taifa lake kwa kustahili kwake yeye mwenyewe na si upendeleo (uwe wa kidugu, kidini, kikabila, rangi au ushawishi).

- Na pale inapotokea kuwepo ushahidi wa upendeleo kutokana na nafasi za baba zao basi wananchi tujitokeze na kusema wazi palipopindishwa sheria, lakini sio kulalama tu bila sababu za msingi na hasa wivu, maana ni haki yao pia kushiriki taifa bila kuvunja sheria.

Ahsanteni.

William Malecela.
 
Nimekupata mkuu... hatuwezi kuwahukumu watoto wa viongozi wote kwa makosa ya wazazi wao au kuwasifia kwa matendo ya wazazi wao. Wote wahukumiwe na kusifiwa kwa matendo na mambo yao wenyewe.

Jambo kubwa la muhimu ni kutambua tofauti ya watoto ambao wanatumia migongo ya wazazi wao kupata nafasi mbalimbali na wale ambao wamejithibitisha kuwa haijalishi kama wazazi wao walikuwa nani bado wangeweza kufanya vizuri na hata kufikia nafasi walizonazo.
 
Binafsi ni muumini wa fair play kwenye fair ground, hata hivyo hili jambo ni ndoto katika nchi inayoitwa Tanzania.

Mtoa mada akitaka kujua kama kweli watoto wa wakubwa wanaogelea wenyewe au wanabebwa kwa mbeleko hana shida ya kupata uthibitisho huo. Hawa watu tumekua nao na wengine tumesoma nao kabla nchi haipatwa na wazima na kuanza kurusha watoto wa wakubwa wakasome Ulaya, Marekani na Afrika kusini. Uwezo wao darasani na kwenye mambo mengine tumeuona na tunaujua vizuri sana. Unaweza kuangalia vyeti vyao vya kuanzia form 4 hadi GPA zao za vyuo. Pia unaweza kuangalia rekodi zao za kushiriki uongozi toka utotoni.... Haya na mengine mengi yatakuonesha wale ambao kweli wamekuwa na vipaji vya uongozi au mapandikizi ya kulinda maslahi ya wazazi wao!

Ukweli unabaki pale pale kwamba kuna watoto wengi wa wakubwa siku hizi wanasukumizwa kwenye siasa hata kama wengine hawajui hata ABC ya siana ila kwa sababu ni muhimu kilinda mali za wazazi wao na kuendeleza utawala wa kiukoo. Mbona kwenye awamu ya kwanza watoto wa wakubwa hawakuwa wengi kwenye siasa kama sasa??

Inakera sana...ial yana mwisho!!
 
Nepotism!
Tatizo kiafrika hao watoto wa vigogo wengi kuna ushahidi wanafika walipo kwa kubebwa mno,kuna nidhamu ya uoga huyu ni mtoto wa fulani na mara nyingi vigogo kuweka mikono yao, jiulize kwanini ridhiwani now anaibuka na issue kibao?

Anyway ni mtoto wa magogoni lakini kwanini hasa ya kisiasa? Lazima tuzuie huu ujinga na watoto wa viongozi wataopewa nafasi hata wananchi wakiri huyu kichwa na atalisaidia taifa kweli na sio kujaza watu viazi kisa mgongo wa baba zao. Najua kwanini ume-raise hii issue but watu kama wewe ebu simama penye ukweli kwa nia njema bila kuogopa mtu na hasa chama ili tujue kweli una malengo mema.

Mfano: Umekuwa ukitetea maovu ya CCM kipropaganda hata pasipostahili, maana yake akili yako imefungwa kupita alipopita mzee wako. Kama kweli ni kijana na una uchungu na nchi hii kwanini usiwe mkweli na kwa uwazi kunusuru nchi na si chama?
 
Tatizo ni matayarisho extra wanayopewa kusomeshwa vyuo vya nje vyenye sifa za kimataifa, huku sisi wenzenu tukipata mafunzo kwenye shule za kata zilinazozoofishwa na ufisadi wa baba zenu!

Halafu hizi nafasi za wakuu wa wilaya wanazozawadiwa kuwajengea CV na kuwatajirisha ni matumizi mabaya ya madaraka. Katiba tunayoitaka ni kuondoa ubaguzi huu, itupe haki sawa na fursa sawa. Sio wengine walipiwe mabilioni kusoma Oxford na sisi hata madawati hakuna na tunasoma Eckenford! Hatuna ugomvi na mwl. JK Nyerere kwa kuwa watoto wake walipewa fursa sawa!

Je yupi mtoto wa hawa mafisadi waliosomeshwa kwa fedha za mafisadi anaweza kujiunga CDM na kupinga ufisadi kwa nguvu zote! Angalau Makongoro alifanya hivyo kwa kuwa alijua hakula cha kifisadi! Mpaka baba yake alipofariki mafisadi wakamrubuni!

Nadhani Nyerere angelikua hai Makongoro asingelirubuniwa na Mkapa!
 
Tatizo kiafrika hao watoto wa vigogo wengi kuna ushahidi wanafika walipo kwa kubebwa mno,kuna nidhamu ya uoga huyu ni mtoto wa fulani na mara nyingi vigogo kuweka mikono yao, jiulize kwanini ridhiwani now anaibuka na issue kibao?

Anyway ni mtoto wa magogoni lakini kwanini hasa ya kisiasa? Lazima tuzuie huu ujinga na watoto wa viongozi wataopewa nafasi hata wananchi wakiri huyu kichwa na atalisaidia taifa kweli na sio kujaza watu viazi kisa mgongo wa baba zao. Najua kwanini ume-raise hii issue but watu kama wewe ebu simama penye ukweli kwa nia njema bila kuogopa mtu na hasa chama ili tujue kweli una malengo mema.

Mfano: Umekuwa ukitetea maovu ya CCM kipropaganda hata pasipostahili, maana yake akili yako imefungwa kupita alipopita mzee wako. Kama kweli ni kijana na una uchungu na nchi hii kwanini usiwe mkweli na kwa uwazi kunusuru nchi na si chama?

Kweli mkuu,

Napata shida kuwabaini watoto wa vigogo ambao wana independent minds...Kwani walio wengi wameishia kujificha nyuma ya miavuli ya wazazi wao na kwa hiyo chama (CCM). Ina maana hakuna mtoto wa Rais msaatafu au aliyeko madarakani, ex-PM au wengine ambao hawakubaliani na sera za CCM? Kama wapo litakuwa jambo jema ila kama hawapo basi hoja zetu kwamba hawana ujasiri wa kukaa upande tofauti na wazazi wetu unakuwa na nguvu zisizopingika!
 
William to some extent nimekupata. Ila naomba nitofautiane na wewe pale unapotumia neno 'hisia. Nionavyo mimi si hisia - ni reality ya mambo on the ground. UVCCM kwa mfano imekuwa kama NAVY SEAL. They are shooting from all directions and when you read their names hasa wakati wanafanya Press conferences you are left with one conclusion- DEAL OR ALIVE.

Na kama ujuavyo maisha ya hapa bongo ni ya 'kimjini-mjini' hivyo copy & paste ni mojawapo ya mbinu muhimu za hii style ya kimjini-mjini, na akianza mmoja wengine tunafuatia.
 
Binafsi ni muumini wa fair play kwenye fair ground, hata hivyo hili jambo ni ndoto katika nchi inayoitwa Tanzania.

Mtoa mada akitaka kujua kama kweli watoto wa wakubwa wanaogelea wenyewe au wanabebwa kwa mbeleko hana shida ya kupata uthibitisho huo. Hawa watu tumekua nao na wengine tumesoma nao kabla nchi haipatwa na wazima na kuanza kurusha watoto wa wakubwa wakasome Ulaya, Marekani na Afrika kusini. Uwezo wao darasani na kwenye mambo mengine tumeuona na tunaujua vizuri sana. Unaweza kuangalia vyeti vyao vya kuanzia form 4 hadi GPA zao za vyuo. Pia unaweza kuangalia rekodi zao za kushiriki uongozi toka utotoni.... Haya na mengine mengi yatakuonesha wale ambao kweli wamekuwa na vipaji vya uongozi au mapandikizi ya kulinda maslahi ya wazazi wao!

Ukweli unabaki pale pale kwamba kuna watoto wengi wa wakubwa siku hizi wanasukumizwa kwenye siasa hata kama wengine hawajui hata ABC ya siana ila kwa sababu ni muhimu kilinda mali za wazazi wao na kuendeleza utawala wa kiukoo. Mbona kwenye awamu ya kwanza watoto wa wakubwa hawakuwa wengi kwenye siasa kama sasa??

Inakera sana...ial yana mwisho!!

- Nafikiri mkuu hukunielewa, maana watoto na ndugu wa viongozi wapo pande zote mbili za vyama vya siasa, halafu mfano wa awamu ya kwanza ni batili kwa sababu one can question too mbona kwenye awamu ya kwanza hatukuwa na vayma vingi, halafu unaonekaan kukubali unachokikataa, point ya msingi ni kwamba watoto wa viongozi wana haki ya kushiriki taifa kama wananchi wengine wote, ili mradi hawavunji sheria, Mbowe awe Mwenyekiti wa Chadema na Hussein awe waziri wa jamhuri ni sawa tu, ila wakiharibu wahukumiwe kama wananchi wengine wote bila huruma!

William @ NYC, USA.
 
Nimekupata mkuu... hatuwezi kuwahukumu watoto wa viongozi wote kwa makosa ya wazazi wao au kuwasifia kwa matendo ya wazazi wao. Wote wahukumiwe na kusifiwa kwa matendo na mambo yao wenyewe. Jambo kubwa la muhimu ni kutambua tofauti ya watoto ambao wanatumia migongo ya wazazi wao kupata nafasi mbalimbali na wale ambao wamejithibitisha kuwa haijalishi kama wazazi wao walikuwa nani bado wangeweza kufanya vizuri na hata kufikia nafasi walizonazo.
Nimewahi kuhudhuria mikutano ya makongoro Nyerere kipindi hicho akiwa nccr mageuzi, alitoa mfano wa aina yake na alizungumza mengi mno ya kushtua nafikiri amesahau yote lakini tujiulize ccm ilipofika hata mtoto mdogo anajua lakini hata akina willy bado wanapigana ikibidi waendelee kutawala,huyu willy juzi tu amezungumzia kufungua tawi after ccm kujivua gamba! Lakini hapo nyuma hajawahi kukiri ccm kuna gamba na cha kushangaza tayari kuna hila kwenye huko kujivua gamba lakini bado huyu huyu willy anaongea kipropaganda eti kauli ya mkulu ni ya mwisho bila kukiri tatizo la mgawanyiko! Ndio hawa wanaotegemea majina ya wazazi wao kupita mle mle,hataki kuudhi wakubwa! Tusidanganyane simama kwenye ukweli na ili kweli ikupe uhuru willy!
 
- Nafikiri mkuu hukunielewa, maana watoto na ndugu wa viongozi wapo pande zote mbili za vyama vya siasa, halafu mfano wa awamu ya kwanza ni batili kwa sababu one can question too mbona kwenye awamu ya kwanza hatukuwa na vayma vingi, halafu unaonekaan kukubali unachokikataa, point ya msingi ni kwamba watoto wa viongozi wana haki ya kushiriki taifa kama wananchi wengine wote, ili mradi hawavunji sheria, Mbowe awe Mwenyekiti wa Chadema na Hussein awe waziri wa jamhuri ni sawa tu, ila wakiharibu wahukumiwe kama wananchi wengine wote bila huruma!

William @ NYC, USA.

Mkuu sijaribu na siwezi kusema kuwa watoto wa wakubwa hawana haki au wasipewe haki ya kuwa wanasiasa na kwa hiyo kupewa fursa ya kuongoza. Ninalojaribu kusema ni kwamba katika siku za hivi karibuni watoto wa wakubwa wanasukumizwa kwenye siasa na wazazi wao ili kulinda maslahi ya familia. Uongozi umechukuliwa kama kampuni binafsi kwa hiyo wazazi wanakuwa kama Wahindi.

Wanawaandaa watoto mapema kuendesha biashara za familia. Kama wangeachwa wapambane kama tulivyopambana nao enzi za shule, naamini hali hii unayoiona sasa ingekuwa tofauti kabisa!!
 
by William Malecela on Saturday, May 14, 2011 at 1:56pm


@ NEW YORK CITY: Ni lazima tukubaliane kwanza kwamba watoto wa viongozi wa Tanzania ambao wengi wameanza kuingia kwenye siasa na kushika nafasi mbalimbali wana haki kabisa ya kushika nafasi yoyote ya uongozi wa taifa kama Watanzania wengine. Haki yao ya Kikatiba kuchaguliwa au kushiriki nafasi yoyote ya kisiasa kwa mujibu wa taratibu na sheria zilizopo haifutwi au kuondolewa kwa sababu ya nafasi za baba zao kwa taifa letu, sasa au huko nyuma.

-Tatizo kubwa ambalo lipo au niseme mawili ni kwamba kuna hisia kuwa watoto hao wanapewa nafasi hizo si kwa sababu ya kustahili wao wenyewe bali kwa sababu ya kubebwa au kutengenezewa mazingira ya kushika nafasi mbali mbali kwa sababu ya wazazi wao. Hili tumejionea likitokea kwa vyama vyote vya siasa nchini, yaani watoto na ndugu wa viongozi wakishiriki kwenye uongozi pia!

- Na pili, endapo wanashika nafasi ambazo zinahusiana na masuala ya utawala na sheria itakuwa vigumu sana kwa watoto hao kutengua au kuchukua hatu ambazo zitawaonesha kuwa wanafumua mambo yaliyoyofanywa na wazazi wao au hata kushindwa kuchukua hatua mbalimbali kwa sababu ya wazazi wao.

- Hivyo, hisia za haya mawili zinawafanya wananchi wengi kuona kuwa katika nafasi kadha wa kadha hasa za kisiasa ni vigumu sana kwa watoto kuwawajibisha wazazi wao - aidha kwa kusahihisha makosa yao au kuwachukulia hatua kama inapasa. Jambo la msingi ni kuweka msingi na utaratibu kuwa kila Mtanzania anapata nafasi ya kulitumikia taifa lake kwa kustahili kwake yeye mwenyewe na si upendeleo (uwe wa kidugu, kidini, kikabila, rangi au ushawishi).

- Na pale inapotokea kuwepo ushahidi wa upendeleo kutokana na nafasi za baba zao basi wananchi tujitokeze na kusema wazi palipopindishwa sheria, lakini sio kulalama tu bila sababu za msingi na hasa wivu, maana ni haki yao pia kushiriki taifa bila kuvunja sheria.

Ahsanteni.

William Malecela.

William umeleta mada yenye msingi na ambayo tunapaswa kuijadili kwa mapema na marefu, kwanza kabisa nakubalina na wewe ni haki ya kila mtanzania kushika nafasi yoyote ile kulitumikia Taifa lake. Tatizo kubwa liliopo ni mfumo wetu wa kisiasa ndio unaoleta mashaka makubwa pale watoto wa wakubwa wanapopandikizwa kwenye nafasi za uongozi kwa upendeleo, kumbuka Tanzania bado hutujawa na demokrasia ya kweli.

Matatizo mengi yanayojitokeza sasa hivi ni viongozi wengi waliopo serikalini wamewekwa si kwa maslahi ya Taifa bali ni maslahi binafsi, tukirudi nyuma kwenye suala la watoto wa wakubwa kupewa nafasi labda nikuulize swali moja ikiwa leo unapewa nafasi ya uongozi serikalini au ndani chama upo tayari kuhoji makosa ya uongozi aliyoyafanya Mzee Malecela? Tusikatae ukweli hutaweza kufanya hivyo. Hisia za watanzania dhidi ya viongozi wetu ni sahihi kabisa suala la wivu halipo, kila mtoto anamuenzi mzee kwa yale aliyomfanyia hata kama ni madogo lakini kwa uwezo wake.

Jaribu kunipa mfano wa mtoto wa kiongozi ambaye yupo kwenye siasa ambaye hakuwekwa kwa maslahi mtu fulani. Tusikatae ukweli siasa ya Tanzania imetekwa nyara na viongozi walafi, ni jukumu la kila mtanzania kupinga maovu ya viongozi wetu ili nchi irudi kwenye mstari ulionyooka.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Tatizo kiafrika hao watoto wa vigogo wengi kuna ushahidi wanafika walipo kwa kubebwa mno,kuna nidhamu ya uoga huyu ni mtoto wa fulani na mara nyingi vigogo kuweka mikono yao, jiulize kwanini ridhiwani now anaibuka na issue kibao?

Anyway ni mtoto wa magogoni lakini kwanini hasa ya kisiasa? Lazima tuzuie huu ujinga na watoto wa viongozi wataopewa nafasi hata wananchi wakiri huyu kichwa na atalisaidia taifa kweli na sio kujaza watu viazi kisa mgongo wa baba zao. Najua kwanini ume-raise hii issue but watu kama wewe ebu simama penye ukweli kwa nia njema bila kuogopa mtu na hasa chama ili tujue kweli una malengo mema.

Mfano: Umekuwa ukitetea maovu ya CCM kipropaganda hata pasipostahili, maana yake akili yako imefungwa kupita alipopita mzee wako. Kama kweli ni kijana na una uchungu na nchi hii kwanini usiwe mkweli na kwa uwazi kunusuru nchi na si chama?

- Mkuu sijawahi hata mara moja kutetea uozo iwe wa CCM chama changu, au Chadema msimamo wangu uko wazi sana kuanzia hapa na blogs zote ninazoshiriki, ukweli ni ukweli na uongo ni uongo, CCM wakifanya vyema ninasema na wakiharibu ninasema na kule Facebook ninasema wazi bila kuficha on ishus,

- HOWEVER: nisichotaka ni kuwa bendera fuata upepo, hapana shule nimejisomesha sana huku majuu kwa hela zangu mwenyewe, ili nisiwe mjinga wa kufikiriwa na wengine, I like CCM ambako mimi ni member sikatai kwamba kuna mambo mengi ndani ya CCM hayakubaliki, ndio maana ninataka mabadiliko kutokea from within na wengine muyalete form outside, waamuzi ni wananchi. I like Chadema as chama, lakini siwaamini sana baadhi ya viongozi wake! Otherwise wote tupo pamoja na TAIFA KWANZA!

William @ NYC, USA.
 
Katika hili suala la watoto wa wakubwa wanaolazimishwa kuingia kwenye siasa, pia kumezuka kundi la wanasiasa madalali. Hawa kwa maoni yangu ni vijana ambao wana uwezo mkubwa tu wa kujenga hoja ila wanalazimishwa kufanya siasa za maji taka kwa sababu wako kwenye payroll za wenye fweza.

Binafsi naamini kuwa hii nchi inahitaji viongozi ambao watapimwa kwa uwezo wao wa kuwaongoza wananchi na si ukoo au familia zao au uhusiano na vigogo/wafanyabiashara wakubwa. Mbali na hayo tutaendelea kucheza ngoma ya mduara tena wenye kipenyo kidogo sana!!
 
- Mkuu sijawahi hata mara moja kutetea uozo iwe wa CCM chama changu, au Chadema msimamo wangu uko wazi sana kuanzia hapa na blogs zote ninazoshiriki, ukweli ni ukweli na uongo ni uongo, CCM wakifanya vyema ninasema na wakiharibu ninasema na kule Facebook ninasema wazi bila kuficha on ishus,

- HOWEVER: nisichotaka ni kuwa bendera fuata upepo, hapana shule nimejisomesha sana huku majuu kwa hela zangu mwenyewe, ili nisiwe mjinga wa kufikiriwa na wengine, I like CCM ambako mimi ni member sikatai kwamba kuna mambo mengi ndani ya CCM hayakubaliki, ndio maana ninataka mabadiliko kutokea from within na wengine muyalete form outside, waamuzi ni wananchi. I like Chadema as chama, lakini siwaamini sana baadhi ya viongozi wake! Otherwise wote tupo pamoja na TAIFA KWANZA!

William @ NYC, USA.

Hongera mkuu kama uko hapo kwa uamuzi na mapenzi yako ni si kwa maelekezo ya mzee! Pia hongera sana kama uliondoka Tz kwa pesa zako (kama wengine waliofoji bank statement) na kwenda huko majuu kujisomesha kwa kubeba mabox.

Ila wenzio wengi wamebebwa tena bila hata sifa zinazotakiwa. Kwa mfano....Urusi na majirani zake walitoa nafasi nyingi tu karibia 50 za masomo mwaka 1993. Zaidi ya 85% zilichukuliwa na wakubwa wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya juu wa wakati huo na kuwagawia ndugu zao na washirika wao wa karibu! Hali ilikuwa hivyo kwa nafasi nyingine nyingi...

Haya mambo yanaumiza sana...Ila bado naamini yana mwisho!
 
Mtoto wa nyoka ni nyoka, baba akisema anjivua gamba limezeeka, katoto hata hakjui lina vuliwaje nako kanashabikia kwa makosa makosa mwisho kanaharibu hata maana ya kujivua gamba. Hii ni hadithi ya mfano wa watoto wa nyoka magamba, watoto wa vigogo kama alina Willy, Nape, January na Riz1 woote wanashabikia kitu wasichokijuwa. Kuweni na maamuzi yenu binafsi siyo kubaki kwenye chama utadhani nalo ni kabila.

Huwezi kuhama kabila hata kama linashutumia kwa mila na desturi zake, lakini dini na chama, unahama bila wasiwasi. Hawa watoto wa vigogo hatiuwezi kuwashangaa kubaki CCM kwa vile, ufisadi wa wazazi wao ndiyo uliowawezesha kufika hapo walipo. Makongoro aliweza kuthubutu kuhama chama alichokiasisi baba yake tena bado akiwa hai, alifanya vile kwa sababu hajanufaika na CCM kama watoto wa magamba wanavyo nufaika leo na ufisadi wa chama cha magamba.
 
Kaka Willium Salaam,

Kwanza nitangulize kutoa tongotongo lifuatalo....hakuna mtu anaeona WIVU kwa watoto wa viongozi wa Tanzania kisiasa na wao kufuata nyayo za baba zao....wala kusema mtu hastahilio kuwa mwanasiasa kwa kuwa mzazi wake alikuwa mwanasias sio sahihi kwa kuwa unamkosea haki yake ya kikatiba....hivyo binafsi sioni tatizo wewe na watoto wengine wa vigogo nao kuwemo kwenye siasa

But wait here, let's face reality, hebu tuambie ukweli, ungekuwa unetumia "Matonya" mbele ya jina lako ungekuwa hapo? labda ndio lakini sidhani mtu kama Ridhiwani angefika hapo. Vipi yule mtoto wa Ghadaffi, can you tell me angekuwa na uwezo? Je angesikika hata kwenye TV akibwabwaja kumtetea mzazi wake kama angekuwa ni mtoto wa kawaida?

Nasema hivi kwa sababu wengi wa watoto wa wakubwa hawaingii kwenye siasa kwa sababu wanajua kuna jukumu la kufanya bali kwa sababu wanajua kuna "keki ya kula" ambayo wamezoea kuila siku zote na wangependa waendelee kuila....Ni kweli wapo wenye uwezo na nia njema, hawa nafasi wanaistahili ila sio kama yule mtoto wa mkuu wa wilaya fulani niliesoma nae bonge la kilaza lakini alienda nje na leo ni mfanyakazi jiwizara moja eti na yeye anatupangia sera na mipango ya maendeleo...................what a shit...
 
Back
Top Bottom