Binafsi yangu nilikuwa sifaidiki chochote na uwepo wake hapa jukwaani maana muda mwingi alikuwa ana utumia kwa ajili ya kujisifu na kutetea mambo ya ajabu ajabu yasiyo kuwa na tija kwa mustakabali wa taifa letu!
Kuna mjadala ulisha wekwa kuhusu tabia zake za kuanika picha zake na wadada wakiwa viwanja wakijirusha kwenye blog yake. Nadhani huu ndio muda muafaka wa yeye kwenda kuendeleze blog yake ya madada poa home of great thinkers viatu vimembana!
Sent from BlackBerry 8520 authorized by JamiiForums
ana hoja gani ya maana yule?Nilipata bahati ya kusafiri naye gari moja for long trip toka Dodoma mpaka Dar na tulizungumzia kujitoa kwake, kwa vile sababu zake pia ameisha ziwasilisha rasmi kwa uongozi wa jf, kiukweli, sio za kupuuzwa!. Kwa vile mazungumzo yetu hayakuwa rasmi, kama nilivyoongea na Dr. Slaa, sio busara kuyaleta humu ila hoja za William sio za kupuuzwa.
Katika kipindi cha StarTV Wiliam Malecela amefunguka ya kuwa kujiondoa JF, "KUJIONDOA JF KUNATOKANA NA TOFAUTI ZA KIITIKADI".
Inavyofahamika JF watu wote au washiriki wote wanashiriki katika hoja mbalimbali kwa mstakabali wa kulijenga taifa letu kukosoana, kutoa mawazo n.k bila kujali itikadi, jinsia, kabila, dini n.k.
Kauli ya Mh. William Malecela imethibitisha kitu kimoja sera ya CCM kinyume ya mahubiri yao majukwaani ya kudumisha upendo,mshikamano bila kujali itikadi, jinsia, kabila,dini n.k. Kama umeondoka kwa sababu za kiitikadi hapa alama ya kuuliza ???????.
Na picha ambayo naipata ni kwamba CCM midahalo, kukosoana n.k. HAVITAKIWI ili kupata uongozi wa CCM unapashwa kukaakimya katika kukikosoa chama CCM ama kuyataja maovu yake.
Nafikiri hii ni moja ya masharti ambayo yamekusukuma kutoka JF.
Nilipata bahati ya kusafiri naye gari moja for long trip toka Dodoma mpaka Dar na tulizungumzia kujitoa kwake, kwa vile sababu zake pia ameisha ziwasilisha rasmi kwa uongozi wa jf, kiukweli, sio za kupuuzwa!.
Kwa vile mazungumzo yetu hayakuwa rasmi, kama nilivyoongea na Dr. Slaa, sio busara kuyaleta humu ila hoja za William sio za kupuuzwa.
Kilichomtoa William Malecela JF si hoja hiyo, ninavyofahamu wadau wa JF kufumua nje siri ya aliyekuwa mmiliki wa Ze-Utamu kwamba ni William malecela kwa vile ilielezwa jina la Malecele ndilo lililoainishwa kwamba ni mmiliki wa Zeutamu. William Malecela alikiri hapa kwamba huyo mmoja wapo mtajwa ambaye jina la mwisho ni Malecela ni jamaa yake na anamfahamu.
Tukumbuke kuwa mtandao huo maarufu katika mambo ya ngono haukubakiza kitu hadi kugusa wakuu wa Magogoni kuwadhalilisha kwa kutumia Illustration na hivyo dhamiri zinaweza kumwibua aliyejificha kujiona katika kioo mambo ambayo alikuwa anawafanyia ambao kwa sasa anawachuchumia kupata ulaji.
JF ni Wiki-Leaks ya bongo kama ilivyokuwa Mwanahalisi bana, wakifumua mambo hapa wahusika utaona wanatapatapa na kuhangaika kutafuta njia ya kutokea, maana yake wameshikwa pabaya.
NDEGE MJANJA HUNASWA KWENYE TUNDU BOVU