Will a weakened America emerge victorious against communist China?

Bahati nzuri miaka ya juzi kati nimevutiwa kusomasoma kuhusu China hivyo nilipata mawili matatu. Hiki kitabu kimoja kilikuwa kinazungumzia mapinduzi ya AI, AI ndiko dunia inakoelekea. Unapozungumzia mapinduzi ya nne ya viwanda unazungumzia AI. Atakaye tawala AI ataishika dunia. Kwenye hii sekta US ndiyo alikuwa pioneer lakini China amecatch up na kuna uwezekano mkubwa wa kumpita US. Ili AI ifanye kazi inahitaji mabilioni ya data wanasema China kwa idadi yake ya watu na sheria zake kuhusu usiri wa data hiki ni kitu rahisi sana kwake. Kwa hiyo AI ya china ndiyo iko kwenye mazingira bora ya kustawi.

Hiki kitabu kingine (China disruptors)kinazungumzia makampuni ya China. Makampuni binafsi ndiyo huendesha uchumi wa nchi zilizoendelea. Ukiulizwa leo kati ya China na Marekani ni wapi makampuni yanapata ushindani mkubwa wa kibiashara kutoka makampuni mengine ya ndani unaweza sema US. Haiko hivyo, China kwa kila kampuni moja linalosimama kuna makampuni maelfu kadhaa yanakuwa yamekufa. China hakuna copyrights law au tuseme hazisimamiwi kihiivyo, sasa ukigundua kitu leo kesho mwenzako ameiga. Mara kakampuni kameanzishwa kameiga. Makampuni yamebuni mbinu mbalimbali, app kama we chat imebidi iwe app ya kila kitu ili kusurvive. Hizi biashara za mitandaoni, Makampuni ya China yanawekeza mtandaoni na yanajenga store(duka), yanafanya kila mbinu. Ni mazingira magumu sana kusurvive. Hilo linamaanisha nini? Linamaanisha kampuni inayoweza survive China ikitoka huku duniani hakuna wa kusimama nayo. Pia Kampuni zao zina njaa balaa, zinanunua kampuni za Marekani kama zina kichaa vile. Kitu kingine ni quality ya bidhaa, wamejifunza sana kwenye hii sekta.

Military, kwanza wanasema China hana tabia ya ubeberu(emperialism) hivyo hana haja ya kuweka mabase ya mbali na kushika sehemu za mbali. Changamoto kubwa ya kijeshi kwa China ni South China Sea na Taiwan. Hii south China Sea anagombania na mataifa mengi sana lakini wanasema kwa jinsi nchi hizi na hata Taiwan yenyewe zinavyoitegemea China kwa uchumi wao hakuna atakayethubutu kupigana au kuleta fyokofyoko japo wananunua mandege, manyambizi na kubluff. China anahakikisha wanamtegemea zaidi kiuchumi(Sun tzu anasema kumpiga adui bila kupigana ndiyo hekima kuu)

China imeendelea mpaka hapo kwa sababu ya kubadili sera zake na kuruhusu zaidi sekta binafsi kuingia kwenye uchumi. Lakini mageuzi hayo hayatoshi bado na kila siku yanafanyika ili kufanya shughuli fulani za kiuchumi zifanyike. Waandishi wanasema China bado inahitaji kufanya mapinduzi makubwa zaidi ili izidi kusonga mbele vinginevyo maajabu ya kiuchumi iliyoyapata miaka ya karibuni hayataweza kusogea mbele tena. Isipofanya mabadiliko makubwa kwenye sera zake na namna inavyoendesha mambo isahau kuipita US.

Mi nimeona nizungumzie upande wa China, ila mambo ya kuifanya Marekani ishinde au ishindwe siyaelewi vizuri, imekuwa nchi isiyotabirika, si ajabu ikatumia advantage yake(jeshi).
 
China overtook America as the largest exporter of merchandise since 2009,
Trump was just the last straw that broke the camel's back.

hata wa china wameaanza kuamini.

 

Marekani haitatamalaki katika utukufu tena
 

Marekani haitatamalaki katika utukufu tena
Wangekuwa na mapenzi nayo ya huba wangezuia DT asiporwe presidency na machokoraa ya JB
 
Hoja kubwa ya Graham T Allison, Kishore Mahbubani na Joseph Nye siyo The Decline of America kama wakina Huntington wanavyosema kwenye The Clash of Civilization, but rather The Relative Decline of America. Marekani anaweza kuwa na uchumi huu-huu ambao anao sasa lakini Uchina akiendelea kukua kwa kasi hii basi atakuwa na uchumi mkubwa mara mbili ya Marekani hadi kufika 2070. Suala zima la Relative Decline halikuguswa kabisa na Huntington wala Hoffman, kama kuna sehemu wamelizungumzia tuoneshane.

Ahsante sana.
Hiyo hoja unayoisema kuhusu "Relative Decline of America" si hoja ngeni. Hoja hiyo imekuwa ikizungumzwa nchini Marekani tangu miaka ya 50. Kama nilivyosema hapo awali, mijadala hii imekuwa ikijirudia kila baada ya wakati fulani. Si mijadala mipya!

Unazungumzia tasnifu (thesis) ya Huntington ya The Clash of Civilization ambayo ni ya miaka ya 90. Lakini, rejea machapisho ya Huntington ya miaka ya 80 kurudi nyuma; amezungumza sana kuhusiana na hoja hiyo. Jaribu kutafuta chapisho lake mojawapo linalofahamika kama The U.S. - Decline or Renewal?

Pia, kuna machapisho ya wanazuoni wengine kuhusiana na suala hilo, si hao wawili pekee. Wapo kina Robert Keohane waliozungumzia pia hoja hiyo miaka ya 80. Kuna machapisho kama vile After Hegemony na mengineyo. Hiki kinachozungumzwa kipindi hiki na Graham Allison na wenzake ni muendelezo tu wa yale yaliyokuwa yakisemwa na kina Huntington na wenzake [zamani zile] karne iliyopita.
 
Hiyo hoja unayoisema kuhusu "Relative Decline of America" si hoja ngeni. Hoja hiyo imekuwa ikizungumzwa nchini Marekani tangu miaka ya 50. Kama nilivyosema hapo awali, mijadala hii imekuwa ikijirudia kila baada ya wakati fulani. Si mijadala mipya!

Unazungumzia tasnifu (thesis) ya Huntington ya The Clash of Civilization ambayo ni ya miaka ya 90. Lakini, rejea machapisho ya Huntington ya miaka ya 80 kurudi nyuma; amezungumza sana kuhusiana na hoja hiyo. Jaribu kutafuta chapisho lake mojawapo linalofahamika kama The U.S. - Decline or Renewal?

Pia, kuna machapisho ya wanazuoni wengine kuhusiana na suala hilo, si hao wawili pekee. Wapo kina Robert Keohane waliozungumza pia hoja hiyo miaka ya 80. Kuna machapisho kama vile After Hegemony na mengineyo. Hiki kinachozungumzwa kipindi hiki na Graham Allison na wenzake ni muendelezo tu wa yale yaliyokuwa yakisemwa na kina Huntington na wenzake [zamani zile] karne iliyopita.
Amerikkkkka has been on a decline from the very moment she acquired an international hyperpower status.
 
Mkuu, huo msemo unanikumbusha kauli ya msomi mmoja [Profesa] kutoka nchi Urusi aliyewahi kutabiri miaka ya 90 mwishoni kuwa itakapofika mwaka 2010, Marekani itagawanyika vipande sita na kimojawapo (Alaska) kitarejea Urusi.
Sasa hivi US imegawanyika vipande 538 :) So, Mrusi wako alikuwa muungwana sana (so generous) katika kutabiri kwake. Unaelewa hilo Engineer!??? :)
 
Ewaaah, wewe umeongea vitu muhimu sana na kuonesha mifano hai kabisa: Marekani iko mbele sana japo kitaalamu wanasema iko kwenye Relative Decline Phase. Sasa kwenye hoja yako nimeona mambo mengi ambayo ntayaweka kwenye makundi matatu, ili kuweza kuyachambua vizuri.

Mosi, The Western Institutional Advantage: Hapa tunazungumzia ushawishi wa taasisi kubwa za kimataifa ambazo aidha zilianzishwa kwa mchango au ushawishi wa Marekani. Mfano UN, IMF, WB, UE, WTO, NATO, TPP ambazo Marekani huzitumia kuendesha na kufanikisha mambo yake. Mbali na hapo, taasisi hizi zinaaminika sana na nchi mbalimbali za duniani kwasababu ya uwazi na mchango ambao zimetoa kwa nchi nyingi.

Pili, The Service Market: Uchina amemshinda Marekani kwenye uuzaji wa bidhaa (merchandise) na siyo huduma. Linapokuja suala la huduma, nadhani Marekani na Canada ndiyo wako mbele kuliko nchi zote duniani. Kila taasisi kubwa ambayo inatoa huduma aidha itakuwa ni ya Marekani, ina hisa za Marekani au inatumia Platform za kimarekani. Kama ulivyosema huduma za kimtandao (Google, Microsoft, Facebook, Instagram, Twitter), huduma za kielimu (Harvard, Stanford, Yale), burudani (Hollywood), usafirishaji (uber). Ikumbukwe haya makampuni kama Google yanatoa huduma dunia nzima bila kulipa kodi hivyo kumtajirisha sana Marekani.

Tatu, Military and Alliance Network: Marekani ana jeshi kubwa sana lenye nguvu japo sidhani kama yeye peke yake anaweza kumfanya Uchina jambo lolote kipindi hiki. Kinachombeba Marekani ni kwamba mpaka leo hii ana mikataba zaidi ya 60 ya ulinzi na mataifa mbalimbali duniani. Mikataba mikubwa ndiyo kama ile ya NATO, ANZUS, US-JAPAN na US-KOREA hivyo ana mkono mrefu kuliko Uchina.

Sasa suala la teknolojia mpya kama (Nano-Tech, AI)naomba niliweke hivi: Bado hizi teknolojia hazijaingia sokoni rasmi hata tufahamu mshindi ni nani. Hebu angalia mfano huu, wanasema teknolojia ya 5G ni ya kimapinduzi sana na muhimu sana katika kufanya tafiti za AI. Dunia ilitegemea Marekani angekuwa wa kwanza lakini bahati mbaya sana Uchina ndiyo anayeongoza mpaka sasa.

Kuhusu Huawei vikwazo vyote bado havijazuia kampuni kusonga mbele, na haimaanishi kwamba Uchina alikuwa hawezi kutengeneza Conductors. La hasha, yeye naye anaokoa gharama kubwa zitokanazo na tafiti na uzalishaji (Comparative Advantage). Lakini kubwa la kuliangalia ni kwamba Uchina ya leo imefika mahala pakubwa kiteknolojia kiasi kwamba hata baada ya mlipuko wa CORONA wao walikuwa moja kati ya nchi za kwanza kabisa duniani kufanikiwa kudhibiti ugonjwa na kutengeneza chanjo.

Mwisho kabisa, navyosema Relative Decline namaanisha nini: Kwamba wewe mkuu T14 Armata unaweza ukawa ndiyo mtu mrefu sana Tanzania mwenye futi 8. Lakini akatokea MALCOM LUMUMBA akawa ana futi 9, hili halimaanishi wewe ni mfupi bali wewe ni mfupi kuliko MALCOM LUMUMBA. Hivyo Marekani ni taifa lenye nguvu na mifumo yake ni imara sana lakini ukweli mchungu ni kwamba kuna sehemu nyingi ambazo ameanza kuachwa na Uchina kutokana na ukuaji wa kasi wa Uchina.

NB: Masuala ya nishati hasahasa Fracking (The Shale Revolution) are undisputed, America has energy security.
Lakini suala la Ukubwa wa PPP kuchangiwa pekee na wingi wa watu nadhani halijakaa sawa sana hivyo lipitie upya.
Kwenye hoja ya pili, service market ndio ukomavu wa biashara na uzalishaji. Ndio maana kina Apple wanauza devices ila bado wanawekeza kwenye huduma kama Apple Tv na iOS za kuendeshea hizo products. China bado inazalisha tu ila kwa kasi sana inakuja. Marekani ina patents nyingi sana zinazotumika duniani na inaendelea kusajiri nyingine. Uzalishaji wa China hata Vietnam na India wanaweza jaribu kuweka mazingira rafiki wakavuta kiasi kidogo cha uwekezaji, US ana biashara ambazo huzikuti kwingineko kirahisi. Hatujaona China ikija na conglomerates kama CocaCola, Pepsi, Microsoft, McDonald's, Nike, Ford au Boeing.

Hatuoni dunia ikikimbilia kuwekeza kwenye soko la hisa la China, Wachina wenyewe makampuni yao makubwa wanayasajiri kwenye soko la Kimarekani. Hatuoni cream za dunia zikikimbilia China, Wachina wanaenda kusoma na kufanya kazi Marekani na sio kinyume chake.

Hatuoni fedha ya China ikifanya manunuzi, hata China yenyewe haijiamini ina-devaluate Yuan yao ili kuzuia matumizi yake kwenye exchange duniani. USD inazunguka dunia nzima bila kuathiri uchumi wa US.

Hapo namba tatu kwenye jeshi. Marekani ina jeshi kubwa mno na lenye nguvu. Dunia haijalishuhudia jeshi la US likiitetea mipaka yake, huwa tunaona vita za kujitakia ambazo wakishindwa simply wanaondoka. China haina silaha za aina yoyote kutishia Marekani, ukiachana na makombora kama DF-41 vita ya China vs US hakuna Mchina atakanyaga kwenye shores za mainland US. China doctrine zake ni kuizuia US isifike Southern China sea, hata ikitaka kufikisha majeshi yake eneo kama Maryland itaanzaje? Tangu WW2 tunajua madhara ya kupigia vita kwako yalivyo, US kaingia vita zote za karne ya 20 na 21 bila kupigana nyumbani.

Hizi Norinco na Shenyang haziwezi tengeneza silaha za kuzishinda Raytheon, General Dynamics, Boeing, Lockheed Martin, Huntington Ingalls, Northrop Grumman na nyingine nyingi za US.

China hakuna derivative ya DARPA yenye miradi mikubwa ya kimapinduzi kwenye ulinzi. Elimu ya China nayo sio supportive sana kwenye ulinzi kama US. Hata uuzaji wa silaha US anaongoza kuwauzia superpowers ila China bado ananunua silaha muhimu kwa Russia. China anauza silaha kwa kina Nigeria, Pakistan, Sri Lanka ambao wanakwepa masharti na kutafuta bei nafuu ila hawana budget ya kuchukua kwa wingi.

Bila hata allies US vs China lazima China isiishinde US kimapigano. US inaweza shinda au kutoka suruhu ila sio kushindwa. Kwanza experience aliyonayo US ni kubwa mno na yuko kila mahala duniani.

Kwenye ujasusi, cyber warfare na cyber security bado US anamzidi China. Hapa China hajaifikia Israel au Russia.

Tukiachana na ulinzi ambao ni muhimu kuhakikisha usalama wa biashara zote za nchi na ustawi wa sera zake. Maendeleo yajayo tumekubaliana yanatokana na nani anafanya nini na anamiliki nini kwa sasa katika teknolojia.

China ina kina Huawei, ZTE na CSMC ambao hawajazishinda Intel, AMD au Apple.

Kampuni kubwa za magari duniani haziko China. Hata kampuni za EV zinazoibuka US inaongoza ila China iko karibu sana.
5G China anaongoza ila wapo kina Ericsson na Nokia walikuwa wanakuja (hawana fedha). Ikumbukwe Nokia na Ericsson waliitoa 4G, Japan walishatoa 3G kupitia Docomo. Leo hii wako wapi?
Tutakuja kupata 6G wakitokea watu ambitious kama Elon Musk.

Artificial Intelligence na robotics wapo US, Japan na Russia wanakuja vizuri. Tumeona baadhi ya demo za robots kutoka US na Russia ila hatujaona demo za China. AI iko integrated sana kwenye teknolojia za magari kama Tesla na kwenye smartphone. Kwenye AI kompyuta na robots zitafidia watu na uzalishaji utapungua gharama uku kasi ikiwa ileils hakuna likizo wala kuchoka. China sioni kama anaongoza hapa, atategemea idadi yake ya watu na gharama zake ndogo za uzalishaji.

Nilitazama production site ya F-35, wanatumia laser beam kuelekeza mfanyakazi wapi pa kufunga nati, wapi pa kuchomeka hiki. China hana precision hii kwenye uzalishaji na hivo faults kwenye systems muhimu kama kompyuta hazikwepeki wakati huo speed ya kuzalisha hana ila atategemea wingi wa watu.

Teknolojia nyingine za zamani kidogo kwa US bado China hajazifikia. China hana true stealth technology ambayo US anayo tangu 1980s, hana uwezo wa kutengeneza injini za ndege kama P&W pale US, aircraft carrier ndio anayo moja ya kwake ikiwa diesel powered wakati US anazo zaidi ya kumi nuclear powered, nuclear submarines bado sana. Yani nuclear technology bado hajafikia US, mpaka majuzi hapa China ilikuwa inatumia coal wakati wenzake walishahama muda sana uko.

Katika ustaarabu na kutegemeana kwa mifumo na taasisi China haijaongoza. Benki, mashirika ya bima, mifuko ya uwekezaji popote duniani na taasisi zinazojitegemea viko zaidi wazi na endelevu kwa US. Utasikia FDA imezuia Monsanto kuuza dawa flani, FAA imezi-ground Boeing Max mpaka izichunguze, FBI imechunguza Russiagate na kukuta rais Trump hana hatia. Ingekuwa China ungesikia CPP wamefanya hivi, serikali imefanya kile, serikali ime...
Nchi haina hata mgawanyo wa mamlaka itaanzaje kuongoza ulimwengu.

Naamini ili nchi iipite Marekani lazima kwanza iifikie, hata Britain kabla haijapitwa na Marekani kwanza zililingana kisha Marekani akaipita. Sasa China hajaweza kulingana na Marekani, hayuko mzimamzima kuna vitu yuko mbele vingine nyuma kabisa uko
 
ofcoz China is now a threat to USA, however not possible to suppress USA. Ni kweli China anaspidi Kali ya ku kutaka ku undertake marekani Ila kwa bahati mbaya China hajajua madhaifu ya amerika ,na kwa bahati mbaya amerika anayajua madhaifu ya China,na anajua wakati upi wa kuanza ku deel na madhaifu ya China,na mlango wa Siri wa kutekelezwa anaujua na Alisha ufanyia analysis yakutosha.

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Unazungumzia tasnifu (thesis) ya Huntington ya The Clash of Civilization ambayo ni ya miaka ya 90. Lakini, rejea machapisho ya Huntington ya miaka ya 80 kurudi nyuma; amezungumza sana kuhusiana na hoja hiyo. Jaribu kutafuta chapisho lake mojawapo linalofahamika kama The U.S. - Decline or Renewal?
Nimeliona hilo bandiko la Huntington huko Foreign Policy amezungumzia ukuaji wa nchi kama Japan ukilinganisha na ukuji wa uchumi wa Marekani: Akasema uchumi wa Marekani haujatanuka tena wakati wenzake wanakuwa na kuanza kumfukuzia. Linaloongelewa na Joseph Nye na John Mearsheimer ni kwamba Relative Decline ya Marekani kwasasa ni kwamba hafukuziwi tena na Uchina tena bali ashapitwa tayari kwenye baadhi ya maeneo ya msingi kama Uchumi.

Narudia tena nilichokisema huko juu, Uchina ndiyo taifa pekee ambalo limemshinda Marekani kwenye nguvu ya soko in terms of Purchasing Power Parity (PPP) na Volume of International Trade. Ujerumani Magharibi, Japani na Umoja wa Kisovieti hawakuwahi kumshinda Marekani kwenye soko hata siku moja (Kama wamewahi nioneshe ushahidi), wao walikuwa wajaribu kumfikia Marekani lakini hawakufanikiwa.

Purchasing Power Parity and International Trade ndivyo viliifanya Marekani liwe taifa lenye nguvu kuliko yote duniani hadi kuyashinda mataifa tajiri kama dola la Ujerumani na Uingereza. Tokea mwaka 1872 hadi 2014 Uchina ndiyo taifa pekee lilifanikiwa kumshinda Marekani kwenye PPP kubwa na International Trade (Trade in Merchandise).
 
Bahati nzuri miaka ya juzi kati nimevutiwa kusomasoma kuhusu China hivyo nilipata mawili matatu. Hiki kitabu kimoja kilikuwa kinazungumzia mapinduzi ya AI, AI ndiko dunia inakoelekea. Unapozungumzia mapinduzi ya nne ya viwanda unazungumzia AI. Atakaye tawala AI ataishika dunia. Kwenye hii sekta US ndiyo alikuwa pioneer lakini China amecatch up na kuna uwezekano mkubwa wa kumpita US. Ili AI ifanye kazi inahitaji mabilioni ya data wanasema China kwa idadi yake ya watu na sheria zake kuhusu usiri wa data hiki ni kitu rahisi sana kwake. Kwa hiyo AI ya china ndiyo iko kwenye mazingira bora ya kustawi.

Hiki kitabu kingine (China disruptors)kinazungumzia makampuni ya China. Makampuni binafsi ndiyo huendesha uchumi wa nchi zilizoendelea. Ukiulizwa leo kati ya China na Marekani ni wapi makampuni yanapata ushindani mkubwa wa kibiashara kutoka makampuni mengine ya ndani unaweza sema US. Haiko hivyo, China kwa kila kampuni moja linalosimama kuna makampuni maelfu kadhaa yanakuwa yamekufa. China hakuna copyrights law au tuseme hazisimamiwi kihiivyo, sasa ukigundua kitu leo kesho mwenzako ameiga. Mara kakampuni kameanzishwa kameiga. Makampuni yamebuni mbinu mbalimbali, app kama we chat imebidi iwe app ya kila kitu ili kusurvive. Hizi biashara za mitandaoni, Makampuni ya China yanawekeza mtandaoni na yanajenga store(duka), yanafanya kila mbinu. Ni mazingira magumu sana kusurvive. Hilo linamaanisha nini? Linamaanisha kampuni inayoweza survive China ikitoka huku duniani hakuna wa kusimama nayo. Pia Kampuni zao zina njaa balaa, zinanunua kampuni za Marekani kama zina kichaa vile. Kitu kingine ni quality ya bidhaa, wamejifunza sana kwenye hii sekta.

Military, kwanza wanasema China hana tabia ya ubeberu(emperialism) hivyo hana haja ya kuweka mabase ya mbali na kushika sehemu za mbali. Changamoto kubwa ya kijeshi kwa China ni South China Sea na Taiwan. Hii south China Sea anagombania na mataifa mengi sana lakini wanasema kwa jinsi nchi hizi na hata Taiwan yenyewe zinavyoitegemea China kwa uchumi wao hakuna atakayethubutu kupigana au kuleta fyokofyoko japo wananunua mandege, manyambizi na kubluff. China anahakikisha wanamtegemea zaidi kiuchumi(Sun tzu anasema kumpiga adui bila kupigana ndiyo hekima kuu)

China imeendelea mpaka hapo kwa sababu ya kubadili sera zake na kuruhusu zaidi sekta binafsi kuingia kwenye uchumi. Lakini mageuzi hayo hayatoshi bado na kila siku yanafanyika ili kufanya shughuli fulani za kiuchumi zifanyike. Waandishi wanasema China bado inahitaji kufanya mapinduzi makubwa zaidi ili izidi kusonga mbele vinginevyo maajabu ya kiuchumi iliyoyapata miaka ya karibuni hayataweza kusogea mbele tena. Isipofanya mabadiliko makubwa kwenye sera zake na namna inavyoendesha mambo isahau kuipita US.

Mi nimeona nizungumzie upande wa China, ila mambo ya kuifanya Marekani ishinde au ishindwe siyaelewi vizuri, imekuwa nchi isiyotabirika, si ajabu ikatumia advantage yake(jeshi).
Kwa muono wangu, ni ukweli usiopingika kwamba China imekuwa exporter mkubwa wa mechandise duniani hivi karibuni.

Na hicho ndicho kitu kilichochangia kukuza sana uchumi wa China.

Na sababu kubwa ni cheap labor iliyopo China.

Sasa cheap labor ain't an everlasting solution, Kwasababu siku wachina wakiwa middle class tu usitegemee tena wataanza kuwa cheap kwa kiasi hicho.

Hebu pitia hapo www.yourstory.com uone namna makampuni ya US yameanza kuwekeza kwa fujo nchini India.

Kwahiyo you can see how they are shifting their manufacturing business to India.

Ukiangalia uchumi wa China utaona kuna COPY CATS, MTAJI kutoka US hasa NASDAQ, NYSE na Cheap labor.
 
Kwenye hoja ya pili, service market ndio ukomavu wa biashara na uzalishaji. Ndio maana kina Apple wanauza devices ila bado wanawekeza kwenye huduma kama Apple Tv na iOS za kuendeshea hizo products. China bado inazalisha tu ila kwa kasi sana inakuja. Marekani ina patents nyingi sana zinazotumika duniani na inaendelea kusajiri nyingine. Uzalishaji wa China hata Vietnam na India wanaweza jaribu kuweka mazingira rafiki wakavuta kiasi kidogo cha uwekezaji, US ana biashara ambazo huzikuti kwingineko kirahisi. Hatujaona China ikija na conglomerates kama CocaCola, Pepsi, Microsoft, McDonald's, Nike, Ford au Boeing.
Mkuu umeongelea mambo mengi sana, lakini mimi ntajikita kwenye Uchumi tu.

China is the greatest exporter of merchandise in the world, and some of the merchandise are American owned. This is the single biggest advantage China has over America. Marekani anauza Uchina bidhaa za kiasi cha dola za kimarekani Billion 110, huku Uchina anauza Marekani bidhaa za kiasi cha dola za Kimarekani Billion 396.6 Billion. Nadhani hili litoshe tu kukuonesha kwamba Uchina yuko mbele ya Marekani.

Kwenye International Trade kuna kitu kinatwa The Corporate Inversion ambapo makampuni huamua kubadilisha urai wake na kwenda nchi nyingine ili kupata mazingira marahisi ya uwekezaji kama kodi na soko la ajira. Hayo makampuni ya Kimarekani uliyoyataja kama Nike, CocaCola, Boeing na Conglomorates nyingi ambazo ziko Patented America yamewekeza sana Uchina kwasababu nilizokutajia hapo awali. Unajua kwanini wanafanya hivi ?? The basic feature of Modern Capitalist Economy is the Export of Capital.

Chanzo kikubwa cha Trade War ya Donald Trump ilikuwa ni kuhakikisha kwamba anazuia Corporate Inversion ili ajira na nguvu ya uzalishaji virudi Marekani. Mwaka 2017 Ford Motors walitaka kuhamia Mexico wakapigwa mkwara kwamba bidhaa zao zitatozwa Tarrif kubwa pindi zinapoingia Marekani wakaogopa: Alichofanya ni kukimbilia kurekebisha mkataba wa NAFTA.
 
Kwenye hoja ya pili, service market ndio ukomavu wa biashara na uzalishaji. Ndio maana kina Apple wanauza devices ila bado wanawekeza kwenye huduma kama Apple Tv na iOS za kuendeshea hizo products. China bado inazalisha tu ila kwa kasi sana inakuja. Marekani ina patents nyingi sana zinazotumika duniani na inaendelea kusajiri nyingine. Uzalishaji wa China hata Vietnam na India wanaweza jaribu kuweka mazingira rafiki wakavuta kiasi kidogo cha uwekezaji, US ana biashara ambazo huzikuti kwingineko kirahisi. Hatujaona China ikija na conglomerates kama CocaCola, Pepsi, Microsoft, McDonald's, Nike, Ford au Boeing.

Hatuoni dunia ikikimbilia kuwekeza kwenye soko la hisa la China, Wachina wenyewe makampuni yao makubwa wanayasajiri kwenye soko la Kimarekani. Hatuoni cream za dunia zikikimbilia China, Wachina wanaenda kusoma na kufanya kazi Marekani na sio kinyume chake.

Hatuoni fedha ya China ikifanya manunuzi, hata China yenyewe haijiamini ina-devaluate Yuan yao ili kuzuia matumizi yake kwenye exchange duniani. USD inazunguka dunia nzima bila kuathiri uchumi wa US.

Hapo namba tatu kwenye jeshi. Marekani ina jeshi kubwa mno na lenye nguvu. Dunia haijalishuhudia jeshi la US likiitetea mipaka yake, huwa tunaona vita za kujitakia ambazo wakishindwa simply wanaondoka. China haina silaha za aina yoyote kutishia Marekani, ukiachana na makombora kama DF-41 vita ya China vs US hakuna Mchina atakanyaga kwenye shores za mainland US. China doctrine zake ni kuizuia US isifike Southern China sea, hata ikitaka kufikisha majeshi yake eneo kama Maryland itaanzaje? Tangu WW2 tunajua madhara ya kupigia vita kwako yalivyo, US kaingia vita zote za karne ya 20 na 21 bila kupigana nyumbani.

Hizi Norinco na Shenyang haziwezi tengeneza silaha za kuzishinda Raytheon, General Dynamics, Boeing, Lockheed Martin, Huntington Ingalls, Northrop Grumman na nyingine nyingi za US.

China hakuna derivative ya DARPA yenye miradi mikubwa ya kimapinduzi kwenye ulinzi. Elimu ya China nayo sio supportive sana kwenye ulinzi kama US. Hata uuzaji wa silaha US anaongoza kuwauzia superpowers ila China bado ananunua silaha muhimu kwa Russia. China anauza silaha kwa kina Nigeria, Pakistan, Sri Lanka ambao wanakwepa masharti na kutafuta bei nafuu ila hawana budget ya kuchukua kwa wingi.

Bila hata allies US vs China lazima China isiishinde US kimapigano. US inaweza shinda au kutoka suruhu ila sio kushindwa. Kwanza experience aliyonayo US ni kubwa mno na yuko kila mahala duniani.

Kwenye ujasusi, cyber warfare na cyber security bado US anamzidi China. Hapa China hajaifikia Israel au Russia.

Tukiachana na ulinzi ambao ni muhimu kuhakikisha usalama wa biashara zote za nchi na ustawi wa sera zake. Maendeleo yajayo tumekubaliana yanatokana na nani anafanya nini na anamiliki nini kwa sasa katika teknolojia.

China ina kina Huawei, ZTE na CSMC ambao hawajazishinda Intel, AMD au Apple.

Kampuni kubwa za magari duniani haziko China. Hata kampuni za EV zinazoibuka US inaongoza ila China iko karibu sana.
5G China anaongoza ila wapo kina Ericsson na Nokia walikuwa wanakuja (hawana fedha). Ikumbukwe Nokia na Ericsson waliitoa 4G, Japan walishatoa 3G kupitia Docomo. Leo hii wako wapi?
Tutakuja kupata 6G wakitokea watu ambitious kama Elon Musk.

Artificial Intelligence na robotics wapo US, Japan na Russia wanakuja vizuri. Tumeona baadhi ya demo za robots kutoka US na Russia ila hatujaona demo za China. AI iko integrated sana kwenye teknolojia za magari kama Tesla na kwenye smartphone. Kwenye AI kompyuta na robots zitafidia watu na uzalishaji utapungua gharama uku kasi ikiwa ileils hakuna likizo wala kuchoka. China sioni kama anaongoza hapa, atategemea idadi yake ya watu na gharama zake ndogo za uzalishaji.

Nilitazama production site ya F-35, wanatumia laser beam kuelekeza mfanyakazi wapi pa kufunga nati, wapi pa kuchomeka hiki. China hana precision hii kwenye uzalishaji na hivo faults kwenye systems muhimu kama kompyuta hazikwepeki wakati huo speed ya kuzalisha hana ila atategemea wingi wa watu.

Teknolojia nyingine za zamani kidogo kwa US bado China hajazifikia. China hana true stealth technology ambayo US anayo tangu 1980s, hana uwezo wa kutengeneza injini za ndege kama P&W pale US, aircraft carrier ndio anayo moja ya kwake ikiwa diesel powered wakati US anazo zaidi ya kumi nuclear powered, nuclear submarines bado sana. Yani nuclear technology bado hajafikia US, mpaka majuzi hapa China ilikuwa inatumia coal wakati wenzake walishahama muda sana uko.

Katika ustaarabu na kutegemeana kwa mifumo na taasisi China haijaongoza. Benki, mashirika ya bima, mifuko ya uwekezaji popote duniani na taasisi zinazojitegemea viko zaidi wazi na endelevu kwa US. Utasikia FDA imezuia Monsanto kuuza dawa flani, FAA imezi-ground Boeing Max mpaka izichunguze, FBI imechunguza Russiagate na kukuta rais Trump hana hatia. Ingekuwa China ungesikia CPP wamefanya hivi, serikali imefanya kile, serikali ime...
Nchi haina hata mgawanyo wa mamlaka itaanzaje kuongoza ulimwengu.

Naamini ili nchi iipite Marekani lazima kwanza iifikie, hata Britain kabla haijapitwa na Marekani kwanza zililingana kisha Marekani akaipita. Sasa China hajaweza kulingana na Marekani, hayuko mzimamzima kuna vitu yuko mbele vingine nyuma kabisa uko
Mbona covid 19 imemhenyesha hvyo Licha ya hizo decoration ulizozielezea hivyo unless Chinese ambao kwa mda mfupitu wameweza kuuzibiti ugonjwa
 
Kwa muono wangu, ni ukweli usiopingika kwamba China imekuwa exporter mkubwa wa mechandise duniani hivi karibuni.

Na hicho ndicho kitu kilichochangia kukuza sana uchumi wa China.

Na sababu kubwa ni cheap labor iliyopo China.

Sada cheap labor ain't an everlasting solution, Kwasababu siku wachina wakiwa middle class tu usitegemee tena wataanza kuwa cheap kwa kiasi hicho.

Hebu pitia hapo www.yourstory.com uone namna makampuni ya US yameanza kuwekeza kwa fujo nchini India.

Kwahiyo you can see how they are shifting their manufacturing business to India.

Ukiangalia uchumi wa China utaona kuna COPY CATS, MTAJI kutoka US hasa NASDAQ, NYSE na Cheap labor.
There you're talking Mr Mkaruka,
Sababu ambazo zilisababisha wazalishaji wa kimarekani na Ulaya wakimbilie Uchina miaka ya 80's: Ndizo zitawafanya wakimbilie sehemu nyingine duniani kwasababu ya Growth of the Middle Class in China. Lakini pili, ni kwamba Chinese Population is aging, dependency ratio is unhealthy compared to India and Afrika.

India dependency ratio yao kati ya wazee na vijana ni 40/60: Ikimaanisha kwamba wazee ni wachache kuliko vijana ambao ni asilimia 60 ya watu wote nchini India. Uchina atakuwa na mzigo mzito sana hasa pale ambapo atatakiwa atoe pensheni kwa idadi kubwa ya wazee ambao nchini kwake sasa. Tatizo kubwa ambalo wachumi wengi wanalisema kuhusu India ni kwamba hiyo asilimia 60 ya vijana, wengi ni wanawake ambao bado hawajaelimika na kuingizwa kwenye soko la ajira kama ambavyo Uchina ilifanya miaka ya 70's na Marekani miaka ya 30's kipindi cha vita ya dunia.

Sasa katika sehemu ambazo zitafanikiwa kupata uwekezaji mkubwa kuliko hata India ni Afrika kama itakaa vizuri,
The Economist wanasema The World Cheapest and Skilled Labor is found in China lakini ukija Afrika kwa nchi kama Kenya na Ethiopia mazingira ni bora zaidi. Mfanyakazi wa Uchina mwenye utaalamu (Technician) huohuo mshahara wake ni mara kumi ya mtaalamu (Technician) kutoka Kenya na Ethiopia. This is the cheapest labor ever....

Ukiangalia na uwepo mkubwa wa rasilimali ambao Afrika inao, basi tusishangae karne zijazo Afrika inaweza ikawa Industrial Power House of the World. Sema tatizo kubwa Afrika ni moja tu, na wewe unalifahamu, hivyo sitalizungumzia kabisa maana mada nzima inaweza haribika.
 
Mbona covid 19 imemhenyesha hvyo Licha ya hizo decoration ulizozielezea hivyo unless Chinese ambao kwa mda mfupitu wameweza kuuzibiti ugonjwa
Unakoelekea utasema Tanzania hakuna CORONAVIRUS. Kinacho kufanya unaona Coronavirus ni kubwa sana US ni uwazi wa taarifa zao.

China mpaka ulivyoona wameamua kuweka wazi 2019 ujue hali ilikuwa ishakuwa tete. Zimwi halifichiki tena.
 
ukweli ni kwamba nguvu za kiuchumi zinahamia asia, marekani anajitahidi kuzuia hilo kwa kushirikiana na mataifa ya asia kama vile japan south korea! Hoa jamaa ni wajinga sana! Elon musk alishasema uchumu wa china utakua mara mbili au tatu zaidi ya wa marekani! kwa mara ya kwanza box office ya china ndo imeongoza kwa mauzo ya filamu mwaka huu kuipita marekani!
 
Back
Top Bottom