Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,555
- 217,837
Alikamatwa siku chache kabla ya uchaguzi mkuu wa 2020 na kupewa kesi ya uongo ya kutakatisha pesa na Uhujumu uchumi kwa amri ya CCM na DPP Biswalo Mganga, ambaye jana ameapishwa kuwa jaji wa Mahakama kuu.
Leo ameachiwa huru baada ya Mahakama kuona kwamba Mashitaka yake yalikuwa ya uongo , ya kughushi na yaliletwa Maalum ili kumkomoa kwa vile alikuwa kiongozi wa Chadema.
Nachukua nafasi hii kumuomba Mwenyezi Mungu atoe hukumu ya Haki kwa DPP Mhusika na wale wote waliohusika na uovu huu uliojaa unyama ambao haujawahi kuwepo kwenye nchi hii tangu kuumbwa kwa mbingu na ardhi , kama wapo waliokufa lakini wakati wa uhai wao walishiriki uovu huu basi moto wao wa Jehanamu uongezwe mara 100.