Wilaya ya Handeni ina waganga wa jadi 6600, Kwamsisi inasifika zaidi

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,005
9,872
Wilaya ya Handeni imejipanga kuhamasisha jamii kuondokana na imani za kishirikina, badala yake ijikite kwenye shughuli za maendeleo kwenye ngazi za kaya na vijiji.

Wakati yakielezwa hayo wilaya hiyo inatajwa kuwa na jumla ya waganga wa jadi 6,600.

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Toba Nguvila alibainisha hayo baada ya kushtushwa na idadi hiyo na baadhi ya vijiji vyake, kikiwamo cha Kwamsisi kuwa na sifa iliyoenea ndani na nje ya nchi kwa kubobea kwa uchawi. Nguvila kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba.

“Mahala popote nchini, mtu akitishia kwamba nitaenda Kwamsisi basi ataogopwa. Hatupaswi kuiendekeza sifa hii kwa sababu uchawi hauleti maendeleo,” alisema Nguvila na kuwataka kuondokana na sifa hiyo na wawe na sifa ya maendeleo.

Nguvila alitoa kauli hiyo alipozungumza na wakazi wa Kata ya Kwamsisi, baada ya kupokea mradi wa maji wa Kijiji cha Mkaramo uliojengwa kwa Sh143.3 milioni na Shirika la World Vision, akitaka waondokane na sifa ya waganga wengi na wachawi.

Nguvila alisema Wilaya ya Handeni ina fursa nyingi katika sekta ya Kilimo, mazingira, mifugo na madini ambazo zimekuwa zikiwafaidisha wageni na kuwaacha wenyeji katika lindi la umaskini, akisema hali hiyo lazima ibadilike.

Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Kwamsisi waliozungumza na Mwananchi walisema imani ya kishirikina imetawala eneo lao na husababisha baadhi yao kushindwa kujenga nyumba za kisasa kwa kuhofia kulogwa na wanaojihusisha na uchawi.
 
Wilaya ya Handeni imejipanga kuhamasisha jamii kuondokana na imani za kishirikina, badala yake ijikite kwenye shughuli za maendeleo kwenye ngazi za kaya na vijiji.

Wakati yakielezwa hayo wilaya hiyo inatajwa kuwa na jumla ya waganga wa jadi 6,600.

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Toba Nguvila alibainisha hayo baada ya kushtushwa na idadi hiyo na baadhi ya vijiji vyake, kikiwamo cha Kwamsisi kuwa na sifa iliyoenea ndani na nje ya nchi kwa kubobea kwa uchawi. Nguvila kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba.

“Mahala popote nchini, mtu akitishia kwamba nitaenda Kwamsisi basi ataogopwa. Hatupaswi kuiendekeza sifa hii kwa sababu uchawi hauleti maendeleo,” alisema Nguvila na kuwataka kuondokana na sifa hiyo na wawe na sifa ya maendeleo.

Nguvila alitoa kauli hiyo alipozungumza na wakazi wa Kata ya Kwamsisi, baada ya kupokea mradi wa maji wa Kijiji cha Mkaramo uliojengwa kwa Sh143.3 milioni na Shirika la World Vision, akitaka waondokane na sifa ya waganga wengi na wachawi.

Nguvila alisema Wilaya ya Handeni ina fursa nyingi katika sekta ya Kilimo, mazingira, mifugo na madini ambazo zimekuwa zikiwafaidisha wageni na kuwaacha wenyeji katika lindi la umaskini, akisema hali hiyo lazima ibadilike.

Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Kwamsisi waliozungumza na Mwananchi walisema imani ya kishirikina imetawala eneo lao na husababisha baadhi yao kushindwa kujenga nyumba za kisasa kwa kuhofia kulogwa na wanaojihusisha na uchawi.

Umeme wa REA umefika huko?
 
Wilaya ya Handeni imejipanga kuhamasisha jamii kuondokana na imani za kishirikina, badala yake ijikite kwenye shughuli za maendeleo kwenye ngazi za kaya na vijiji.

Wakati yakielezwa hayo wilaya hiyo inatajwa kuwa na jumla ya waganga wa jadi 6,600.

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Toba Nguvila alibainisha hayo baada ya kushtushwa na idadi hiyo na baadhi ya vijiji vyake, kikiwamo cha Kwamsisi kuwa na sifa iliyoenea ndani na nje ya nchi kwa kubobea kwa uchawi. Nguvila kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba.

“Mahala popote nchini, mtu akitishia kwamba nitaenda Kwamsisi basi ataogopwa. Hatupaswi kuiendekeza sifa hii kwa sababu uchawi hauleti maendeleo,” alisema Nguvila na kuwataka kuondokana na sifa hiyo na wawe na sifa ya maendeleo.

Nguvila alitoa kauli hiyo alipozungumza na wakazi wa Kata ya Kwamsisi, baada ya kupokea mradi wa maji wa Kijiji cha Mkaramo uliojengwa kwa Sh143.3 milioni na Shirika la World Vision, akitaka waondokane na sifa ya waganga wengi na wachawi.

Nguvila alisema Wilaya ya Handeni ina fursa nyingi katika sekta ya Kilimo, mazingira, mifugo na madini ambazo zimekuwa zikiwafaidisha wageni na kuwaacha wenyeji katika lindi la umaskini, akisema hali hiyo lazima ibadilike.

Baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Kwamsisi waliozungumza na Mwananchi walisema imani ya kishirikina imetawala eneo lao na husababisha baadhi yao kushindwa kujenga nyumba za kisasa kwa kuhofia kulogwa na wanaojihusisha na uchawi.
6,600 ni orodha ya waganga wakienyeji na wachawi, hapo inaelekea wote wameorodheshwa ila hajaelezea kama waganga na wachawi wote wanahudumu wilaya ya Handeni, na nivofahamu HANDENI ina uhaba wa Madaktari na maji lakini suali linakuja: je serikali inatambua uchawi na wachawi?
Kama imewasajili na kutoa idadi yao hao wachawi(pamoja na serikali kutotambua uchawi)kwanini isiwachukulie hatua kwa kosa la ulozi pia na kukwamisha maedeleo ya HANDENI?.
huyo mkuu wa wilaya anatafuta kiki na sidhani kama anauzoefu wa nyanja ya utumishi wa umma, bora apate ushauri kwa walomtangulia akina Godwin Gondwe
 
Back
Top Bottom