WikiLeaks:Kenya yaifokea Marekani

Saint Ivuga

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
54,363
58,386
WikiLeaks:Kenya yaifokea Marekani.


101129100845_raila_odinga_226x170_getty.jpg
Raila Odinga


Serikali ya Kenya imepuuzilia mbali taarifa zilizofichuliwa na tovuti ya Wikileaks ambazo zinamnukuu balozi wa Marekani nchini humo, Micheal Rannenberger, akisema kwamba Rais Mwai Kibaki na waziri mkuu Raila Odinga ndio kikwazo kikuu katika kuleta mageuzi nchini Kenya.
Balozi huyo pia alinukuliwa akisema serikali ya Marekani haitasita kuendesha kampeni kupitia makundi ya kiraia ili kuhakikisha mabadiliko yanafanyika.
101206120945_wikileaks_ch_afp_106.jpg
Tovuti ya WikiLeaks


Akizungumza na BBC akiwa jijini London, Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga amemshutumu bwana Rannenberger kwa kuwa mnafiki. ''Taarifa zinazotolewa na WikiLeaks ni uvumi mtupu. Yale yote yaliyomo ni masengenyo. Ni watu wanaokusengenya, wanayozungumza kukuhusu hadharani ni tofauti na yale wanayozungumza kisiri,'' akasema bwana Raila.
Kuhusu madai kuwa yeye na rais Kibaki hawakuchukuwa hatua zozote kwa kutekeleza mageuzi yanayohitajika, ili kuhakikisha kuwa machafuko ya baada ya uchaguzi kama yale yaliyoshuhudiwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 yatokee tena bw Raila amesema, '' Bwana Ranneberger anaishi nchini Kenya kama mgeni. Iwapo anataka kutushauri ana haki ya kufanya hivyo. Lakini vile vile wageni ni sharti watuheshimu''.
Nayo taarifa kutoka ikulu ya rais ya Nairobi imepuuzilia mbali madai hayo ya balozi wa Marekani kwa kusisitiza kuwa rais Mwai Kibaki ana historia nzuri ya kutekeleza mageuzi kwa kufanikisha kuidhinisha kwa katiba mpya ya taifa hilo.
Taarifa hizo za kisiri, ni miongoni mwa stakabadhi ambazo zimefichuliwa na tovuti ya Wikileaks , kuhusiana na nchi ya Kenya na viongozi wake
SOURCE:BBC
 
Wikileaks ni noma! Ituvujishie basi na ma-news ya hapa bongo ya kina rowasa na mafisadi wenzake.nadhani sasa hivi wanatetemeka huko waliko.
 
Hii mbona ipo wazi ila hili balozi aliripoti wakti ule jamaa wansusua kutengeneza katiba mpya!
Ila bado kuna mwansheria mkuu na mzee wa tume ya rushwa wamerekani wanasema ni vikwazo kwa kurushwa, ha wawataki pia!
 
The niggling question for Kenya and the rest of Africa has always been how deep can we bite the very hand that presumably is feeding us?
 
Wikileaks ni noma! Ituvujishie basi na ma-news ya hapa bongo ya kina rowasa na mafisadi wenzake.nadhani sasa hivi wanatetemeka huko waliko.

Yaani naona kama wanachelewa vilee kutuvujishia za bongo..nazisubiri kwa hamu kweli
 
WikiLeaks:Kenya yaifokea Marekani.


101129100845_raila_odinga_226x170_getty.jpg
Raila Odinga


Serikali ya Kenya imepuuzilia mbali taarifa zilizofichuliwa na tovuti ya Wikileaks ambazo zinamnukuu balozi wa Marekani nchini humo, Micheal Rannenberger, akisema kwamba Rais Mwai Kibaki na waziri mkuu Raila Odinga ndio kikwazo kikuu katika kuleta mageuzi nchini Kenya.
Balozi huyo pia alinukuliwa akisema serikali ya Marekani haitasita kuendesha kampeni kupitia makundi ya kiraia ili kuhakikisha mabadiliko yanafanyika.
101206120945_wikileaks_ch_afp_106.jpg
Tovuti ya WikiLeaks


Akizungumza na BBC akiwa jijini London, Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga amemshutumu bwana Rannenberger kwa kuwa mnafiki. ''Taarifa zinazotolewa na WikiLeaks ni uvumi mtupu. Yale yote yaliyomo ni masengenyo. Ni watu wanaokusengenya, wanayozungumza kukuhusu hadharani ni tofauti na yale wanayozungumza kisiri,'' akasema bwana Raila.
Kuhusu madai kuwa yeye na rais Kibaki hawakuchukuwa hatua zozote kwa kutekeleza mageuzi yanayohitajika, ili kuhakikisha kuwa machafuko ya baada ya uchaguzi kama yale yaliyoshuhudiwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 yatokee tena bw Raila amesema, '' Bwana Ranneberger anaishi nchini Kenya kama mgeni. Iwapo anataka kutushauri ana haki ya kufanya hivyo. Lakini vile vile wageni ni sharti watuheshimu''.
Nayo taarifa kutoka ikulu ya rais ya Nairobi imepuuzilia mbali madai hayo ya balozi wa Marekani kwa kusisitiza kuwa rais Mwai Kibaki ana historia nzuri ya kutekeleza mageuzi kwa kufanikisha kuidhinisha kwa katiba mpya ya taifa hilo.
Taarifa hizo za kisiri, ni miongoni mwa stakabadhi ambazo zimefichuliwa na tovuti ya Wikileaks , kuhusiana na nchi ya Kenya na viongozi wake
SOURCE:BBC

WikiLeaks inawapumbaza walimwengu, sijaona point yoyote ya maana katika WikiLeaks zaidi ya kuelezea umbea wa wanadiplomasia wa Marekani. Hakuna habari yoyote ambayo ni ya maana na Ulimwengu wa wakati huu. Watu watatumia muda mwingi kusoma WikiLeaks wakati wamarekani wanaendelea kujitanua duniani, isije ikawa WikiLeaks ni wakala wa Marekani na mashirika yake ili kuwapumbaza watu.
 
Back
Top Bottom