Expensive life
JF-Expert Member
- May 2, 2020
- 1,688
- 5,446
Miamba ya soka Tanzania Simba na Yanga jumapili hii zitamenyana katika kombe la FA hatua ya nusu fainali.
Ikumbukwe msimu huu yanga kapata matokeo mazuri dhidi ya mtani wake simba.
Jana katika pita pita zangu nilipita kwenye moja ya vijiwe vikubwa vya mashabiki wa timu hizi.
Kulikuwa na tambo nyingi ila mashabiki wa simba walienda mbali zaidi, pale walipo dai kuwa wao walisha acha zile tamaduni za kwenda kwa wataalamu yaani waganga.
Ila watani zao yanga tamaduni hizo bado wanazo. Ndipo mashabiki hao wa simba walipo apa kuwa, awamu hii matawi yao yote na vingozi wao wote, lazima waungane na kuwa kitu kimoja awamu hii lazima wazirudie zile tamaduni zao.
Kwa muono wangu mchezo huu utakuwa mkali na wa kusisimua. Licha ya simba kuwa na kikosi bora huku yanga wakiingia kama underdog kwenye mchezo huu.
Linapokuja suala la kujitoa basi wachezaji wa yanga huwa wanajitoa kweli kweli licha ya ubutu wa kikosi walichonacho.
Ila natoa tahadhari kwa vikosi vyote.
A. Yanga mnapaswa kusahau matokeo ya nyuma mliyoyapata dhidi ya simba.
Mnapaswa kukaa tena chini na kuja na mkakati mpya ni vipi tunaweza kupata matokeo mazuri tena dhidi ya simba.
Mkija na mentality ya kujiamini kuwa hawa tunawaweza huwa hawatusumbui hili linaweza likawagharimu. Ikumbukwe hii ni hatua ya mtoano ukifungwa huna chako.
B. Simba mpaka leo wanaamini kufungwa na watani zao ilikuwa ni bahati mbaya.
Ni kweli simba wanakikosi kizuri kuliko yanga, ila linapokuja suala la derby weka ubora wako pembeni.
Simba mnapaswa kuwaheshimu yanga kama mnavyo waheshimu Azam mnapokutana nao.
Mkakati wenu uwe tunakwenda kucheza na timu bora, tunapata vipi matokeo? Kaeni na wachezaji wenu muwaeleze wale ni bora kama sisi tunapaswa kujiandaa kweli kweli.
MWISHO
Marefarii tafadhali chezesheni vizuri msilete mapenzi yenu mkatuharibia mchezo.
Ikumbukwe msimu huu yanga kapata matokeo mazuri dhidi ya mtani wake simba.
Jana katika pita pita zangu nilipita kwenye moja ya vijiwe vikubwa vya mashabiki wa timu hizi.
Kulikuwa na tambo nyingi ila mashabiki wa simba walienda mbali zaidi, pale walipo dai kuwa wao walisha acha zile tamaduni za kwenda kwa wataalamu yaani waganga.
Ila watani zao yanga tamaduni hizo bado wanazo. Ndipo mashabiki hao wa simba walipo apa kuwa, awamu hii matawi yao yote na vingozi wao wote, lazima waungane na kuwa kitu kimoja awamu hii lazima wazirudie zile tamaduni zao.
Kwa muono wangu mchezo huu utakuwa mkali na wa kusisimua. Licha ya simba kuwa na kikosi bora huku yanga wakiingia kama underdog kwenye mchezo huu.
Linapokuja suala la kujitoa basi wachezaji wa yanga huwa wanajitoa kweli kweli licha ya ubutu wa kikosi walichonacho.
Ila natoa tahadhari kwa vikosi vyote.
A. Yanga mnapaswa kusahau matokeo ya nyuma mliyoyapata dhidi ya simba.
Mnapaswa kukaa tena chini na kuja na mkakati mpya ni vipi tunaweza kupata matokeo mazuri tena dhidi ya simba.
Mkija na mentality ya kujiamini kuwa hawa tunawaweza huwa hawatusumbui hili linaweza likawagharimu. Ikumbukwe hii ni hatua ya mtoano ukifungwa huna chako.
B. Simba mpaka leo wanaamini kufungwa na watani zao ilikuwa ni bahati mbaya.
Ni kweli simba wanakikosi kizuri kuliko yanga, ila linapokuja suala la derby weka ubora wako pembeni.
Simba mnapaswa kuwaheshimu yanga kama mnavyo waheshimu Azam mnapokutana nao.
Mkakati wenu uwe tunakwenda kucheza na timu bora, tunapata vipi matokeo? Kaeni na wachezaji wenu muwaeleze wale ni bora kama sisi tunapaswa kujiandaa kweli kweli.
MWISHO
Marefarii tafadhali chezesheni vizuri msilete mapenzi yenu mkatuharibia mchezo.