Wiki hii ilikuwaje kwako?

LINCOLINMTZA

JF-Expert Member
Mar 15, 2011
1,639
516
WanaJF nawasalimia wote!

"Siku hazifanani" ni msemo wa kiswahili uliozoeleka sana na ni waukweli.
Kwa sababu hiyo, wiki, miezi, miaka, milongo na karne nazo haifanani pia kwa sababu zinaundwa na siku.

Kwa upande wa wiki hii, nikiri kabisa kwamba haikuwa nzuri kwangu hasa katika mahusiano na baadhi ya Wanachama wezangu wa Jamii Forum. Kwa mfano, baadhi ya michango yangu iliwakera sana dada yangu mpendwa Natalia na kaka yangu chardams na wanachama wengine.

Kwa kuongezea, nimekuta "like" leo hii kwenye comment yangu ya tarehe 12/08/2011 saa 12.20 jioni kutoka Invisible nikiamini kwamba ananikumbusha kutembea kwenye komenti yangu.

Invisible liked post by LINCOLINMTZA On thread : Tanzania: The Legacy of President Jakaya Kikwete (2005-2015)

Liked On: Today, 08:48
Yote haya yanaonyesha kwamba wiki hii haikuwa nzuri kwenye mahusiano yangu na Watanzania wezangu, na wazalendo wezangu na wanachama wezangu wa JF hayakuwa mazuri kabisa.

Nachukua fursa hii kwa heshima na taadhima, kwa moyo mweupe kabisa, kuwaomba msamaha wanachama wote wa JF na hasa Natalia na chardams. Naamini hii ndo njia nzuriinayoweza kuuendeleza umoja wetu wa kitanzania.


Pamoja na hayo, ningependa "kushare experiences" yenu wanachama katika wiki hii inayoisha leo ijumaa. Je, ilikuwaje kwako katika mahusiano, mapenzi, kazi, uchumi, siasa, elimu, usafiri, familia, afya, na katika nyanja mbalimbali zinazofanana na hizo.

Asenteni sana wote na
nawatakia mapumziko mema ya mwisho wa wiki.

Wenu mwanachama mtiifu wa JF,

LINCOLINMTZA

Copy Natalia,
chardams na Invisible
 
duh... mie wiki hii ilikuwa mbaya sana kiuchumi kwani sikuingiza hata shilingi zaidi ya kutoa....
1. kazi ilikuwa poa sana
2. kielimu pia ilikuwa poa
3. kifamilia namshukuru Mwenyezi Mungu bado yu pamoja nasi
4. kiafya pia ilikuwa poa....
5. kiusafiri haikuwa poa cous mkoko wangu bado unadaiwa ushuru mkubwa kuliko hata bei niliyoagizia so bado upo bandarini
6. kiurafiki ni 50/50 cous kuna rafiki zangu wawili ni wagonjwa (get well soon my dear friends) na mwingine hapatikani hewani inabidi this weekend nimsake manually....
7. kimapenzi 50/50.....
 
ilivyokuwa kwangu

1.Kiafya ilikuwa njema sana
2.uhusiano na mungu nilijitahidi kutubu dhambi na nilijitokeza mbele ya madhabahu kwenda kumshukuru mungu
3.Kielemu nimeendelea kufanya vizuri
4.kiuchumi saving rate imeongezeka 75% of my income
5. kimapenzi single status imeniweka huru japo yule niliyemtoa bikira ameendelea kuongeza ukaribu
 
---Ki-Jeiefu ilikuwa mbaya sana tena sana, nilipigwa kibuti hadharani na FP..
---Kihalisia nashukuru Mungu ilikuwa mwemwele mwemwele...

FP ametulia sana kwenye michango yake, kwa hiyo kumtokea mtu kama huyu inabidi uaanzie mbali sana ili ashishutikie.
Hata hivyo kibuti kwa mara ya kwanza ni kawaida katika maisha ya namna hii, komaa naye tu mkubwa labda anataka kubembelezwa sana, Si unajua mabinti walivyo!
 
1. Kiafya mbayaa, nimeeng'oa jino jumanne hadi leo maumivu bado.
2. Kimapenzi doing well though distance with my hubby is killing me.
3. Ki JF JF shwari kabisa nimepata elimu, marafiki na burudani.
4. Kifinancially si mbaya vidili dii nilivyopiga last week malipo yamecheua si haba.
5. Kiimani na imani Mungu amenipigania wiko nzima na kunipa pumzi yake hadi leo. Mamshukuru kwa yote.
6. Kisocialization nashukuru wiki hii sijagombana na mtu nawala sijasutwa lool,

Ijumaa njema wana JF wote, mtangulizen Mungu kwa kila mfanyalo ambalo ni la kheri. Nawapenda sana but special salaam kwa wafuatao AshaDii mekumiss sana dada, KakaKiiza miss you, ila kule chit chat wasije wakanidunda lol, Babu DARKCITY busara zako zidumu, Mutta, LARA1, Erickb52 mtoto anakusalimu sana, Kongosho, @cacio, Mkirua Bishanga kaka u are not seen nowdays. Km mekusahau nsameheee
 
Last edited by a moderator:
1. Kiafya mbayaa, nimeeng'oa jino jumanne hadi leo maumivu bado.
2. Kimapenzi doing well though distance with my hubby is killing me.
3. Ki JF JF shwari kabisa nimepata elimu, marafiki na burudani.
4. Kifinancially si mbaya vidili dii nilivyopiga last week malipo yamecheua si haba.
5. Kiimani na imani Mungu amenipigania wiko nzima na kunipa pumzi yake hadi leo. Mamshukuru kwa yote.
6. Kisocialization nashukuru wiki hii sijagombana na mtu nawala sijasutwa lool,

Ijumaa njema wana JF wote, mtangulizen Mungu kwa kila mfanyalo ambalo ni la kheri. Nawapenda sana but special salaam kwa wafuatao AshaDii mekumiss sana dada, KakaKiiza miss you, ila kule chit chat wasije wakanidunda lol, Babu DARKCITY busara zako zidumu, Mutta, LARA1, Erickb52 mtoto anakusalimu sana, Kongosho, @cacio, Mkirua Bishanga kaka u are not seen nowdays. Km mekusahau nsameheee
KOKUTONA nshakwambia mbona husikii? Kongosho kaniweka ndani kinyumba sifurukuti ati! amapile 'shuntama' yashuba yatamu na 'tanaka' upo hapo?
 
Last edited by a moderator:
bishanga mkopo wangu wa dola milioni mbili citibank umpata approval leo,kitaa watanikomaje? kwanza nampeleka secretary BAHAMAS TUKASUUZE ROHO TUPIGE TEKE UMASKINI NDO MENGINE YAJE BAADAE,WERA WERAAAAAAAA
 
Last edited by a moderator:
Ndio nini hii?

Nakunatisha na TS

bishanga mkopo wangu wa dola milioni mbili citibank umpata approval leo,kitaa watanikomaje? kwanza nampeleka secretary BAHAMAS TUKASUUZE ROHO TUPIGE TEKE UMASKINI NDO MENGINE YAJE BAADAE,WERA WERAAAAAAAA
 
Aggggrhhh:
yaani mnavo ongelea weekend mna niumiza sanaaaa.
maana mie nlikua off work toka juma4,naingia kazini usiku,na kesho tena usiku.
Damn.
Namisi harusi hivi hivi kesho.
 
Aggggrhhh:
yaani mnavo ongelea weekend mna niumiza sanaaaa.
maana mie nlikua off work toka juma4,naingia kazini usiku,na kesho tena usiku.
Damn.
Namisi harusi hivi hivi kesho.

Mkuu Speaker za masiku? Kumbe wewe ulikuwa na good time toka J'4? Vipi uchumi umepanda?
 
Mkuu Speaker za masiku? Kumbe wewe ulikuwa na good time toka J'4? Vipi uchumi umepanda?

Ha ha ha,kiasi flani mkuu.
Habari njema sana,ila nina pishana sana na JF,nikiwa off nakua nimechoka mbaya
au nahitaji ku-update kichwa changu ili nihamie kwenye green pastures very soon kwa
hiyo naimiss sana JF.
 
kikazi ilikuwa bomba bosi kasafiri no pressure, no tightdeadline but sad cause no overtimekiuchumi ilikuwa mbaya vimeo kibao wanikopakiroho kesho sabato naenda kusali(karibuni jf member wote)kijamii niko poa sijagombana na mtu whole week, demu aliyekuwa anajipendekeza kwangu nimemshitukia kimeokisiasa sio mkereketwa miekiafya naendelea vizuri
 
Pia kwa upande wangu wiki imeenda poa kwa baadhi ya masuala,
kubwa kuliko lote ni fundi kuniletea furniture zangu baada ya mbilinge ya mda mrefu!

Kimahusiano ni pasu kwa pasu, majuzi ilikuwa mizinguo ila jana nikapata dinner moja matata na leo nazama kuchek movie mapema then ntamalizia kwenye harusi ya jamaa angu.

Kifamilia, Malaika ameamka na kihoma kidogo ila nmewahi hospital wamemchek wamempa dawa saiv anacheza na wenzake.

Kiroho, dah bado nmekuwa mdeni wa Mungu, nina kadi ya mchango wa ujenzi wa kanisa afu bado sijamaliza deni ila nashukuru kwenye bajeti yangu ya wiki hii nmetenga kabisa ili kesho nkamalize.

Ki-jf jf ni poa (japo kukosekana kwa mtu flani kunakaribia kunitoa roho)
labda kama kuna mwenye tatizo na mimi ila mi nina amani na wajumbe wote humu.

Namuomba Mungu kwa wiki nyingine, iwe nzuri zaidi kuliko ile ingine.

JG!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom