Habari zenu wana jf. Mwenzenu wifi yangu ananishangaza na nashindwa kumsaidia. Ana msichana wa kazi ana miaka 20, huyo msichana sio kwamba katulia kivile anapenda umbea na akisikia jambo lolote anasema bila kufikiri. Wifi yangu yuko masomoni cha kushangaza karudi likizo na kumsimulia house girl kwamba ana wasiwasi mume wake(kaka yangu) anatembea na mwanamke ambaye ni jirani kwa sababu huyo mwanamke anampigia kaka yangu simu na kumtumia sms, mara anamsimulia hamwamini mumewe maana wanakaa bila kuonana mda mrefu. Mara ooh mume wangu ana mpango jambo fulani nimemkataza, mara ndugu wanaomba fedha tumekataa. Yani anamwambia siri zote za ndani. Na mimi nkifika hourse girl ananhmwagha kila kitu akisahau wale ni ndugu zangu. Na kama ananiambha mi bila woga majirani. Alafu anavyoongea naona anawadharau wifi na kaka zaidi. Naogopa kumwambia wifi awe makini na hg asijeniona namfatilia. Siwezi ongea na kaka nisijekuwa mchonganishi.Cha ajabu huyo hg anayemwamini nshamfurumua mara nyingh akimwandalia kaka chakula huku kavaa kanga na chupi tu. Mi sielewi