wife anapokulalamikia rafiki yako anamtaka....

Kama umekuta msg ya kumtukana nafikiri anaonesha msimamo ila na wewe endelea kudeal na mkeo
Haya mambo ya kuambiwa na mpenzi wako kua fulani anamtaka si ya kuamini sana, mara nyingi utakuta yeye mwenyewe mkeo ndie anaemtaka jamaa ila hiyo inakua ni njia ya kuondoa kile kilichomjaa moyoni mwake kwa kusema eti jamaa anamtaka.
Nakutakia kila la heri "ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO"

poa kiongozi kwa ushauri mzuri
 
Mbona hujajibu swali langu mkuu... number ya wife kaitoa wapi na yeye ni mgeni hapo mtaani?
 
Pole sn,nakushauri utumie busara zaidi kuliko hacra na km utaamua kukomalia hiyo ishu uwe umeshajipanga kupokea matokeo ya maamuzi yako,japo nina mashaka kidg je ni mara yake ya kwanza kutongozwa mpaka ashindwe kuonyesha mcmamo wake mpaka aje kushtaki kwako?ongea vizuri na mkeo.
 
Pole sn,nakushauri utumie busara zaidi kuliko hacra na km utaamua kukomalia hiyo ishu uwe umeshajipanga kupokea matokeo ya maamuzi yako,japo nina mashaka kidg je ni mara yake ya kwanza kutongozwa mpaka ashindwe kuonyesha mcmamo wake mpaka aje kushtaki kwako?ongea vizuri na mkeo.

ahsante kiongozi kwa ushauri
 
hiyo namba alipataje? alimjuaje kama ni jirani?
Muite huyo jamaa umuulize kama ni kweli then umpe onyo. angalia asikuvunjie ndoa. usitumie hasira. mia
 
kuna ka mtihani kananiumiza kichwa kidogo...
kuna jamaa amehamia hapa mtaani kama mwezi mmoja hivi.
baada ya wiki wife akaniambia huyu jamaa anamsumbua kwa kumpigia simu za kumtaka...
nikamwambia aachane nae.
sasa jana nimeshika simu ya wife nimekuta kuna sms za kumtukana jamaa. sasa nipo sielewi nimuadhibu wife kwa kuendelea kuwasiliana na jamaa au nimuadhibu jamaa kwa kutaka kuharibu nyumba yangu.
NIPO NJIA PANDA
Nimejaribu kupitia ushauri wa wadau mbalimbali waliochangia kukupa ushauri wanapendekeza uanze kuchukua hatua kuanzia nyumbani yaani kwa mkeo . kwa mimi nionavyo mke wako hakuwa na kosa kukueleza yale yanayo msibu kuhusu jirani yenu aliyekuwa anamtongoza akimini wewe ndio mlinzi wake na mmewe. Amini mkeo alikuwa anahitaji msaaada kutoka kwako na ndiyo maana akaja kukueleza. wapo wanaume hata akiambiwa hapana na mwanamke aliye mtongoza na analazimisha utadhani anataka kufufua wafu. wanaume fataki wapenda wake za watu dawa yao ni ndogo sana, ungepanga na mkeo mkamtengenezea mtego huyo bwana halafu akategenezewa utaratibu. baada ya hapo ingekuwa fundisho na mji angehama tu. Tusiwahukumu wake zetu kwa kila wanacho twambia kuhusiana na maswaibu yanayo wapata. wanahitaji upendo , ushirikiano na kuaminiwa
 
Kwa hiyo usingekuwepo kusumbuliwa ingekuwa sawa? Mkeo anauza tigo-rusha, ama jamaa kapataje namba? Ongea na mai waifu wako akuambie uzuri
anamwambia asimsumbue yupo na mume wake, lakini si nilimwambia aachane nae?!
 
Mie nakuomba uwe mpole tena ujifanye kama hauna habari na hilo jambo, alafu fanya uchunguzi wa kimya kimya kama mkeo anakupiga changa la macho ana uhusiano wa kisiri utamgundua tu, Kuliko kumvaa jamaa front au kumkomalia wife akueleze ukweli.

Unaweza kukuta mkeo hana inshu yoyote na jamaa lakini kwa kumkomalia jambo ambalo hakulifanya anaweza kwenda kumpa jamaa bure "liwalo na liwe"
 
kuna ka mtihani kananiumiza kichwa kidogo...
kuna jamaa amehamia hapa mtaani kama mwezi mmoja hivi.
baada ya wiki wife akaniambia huyu jamaa anamsumbua kwa kumpigia simu za kumtaka...
nikamwambia aachane nae.
sasa jana nimeshika simu ya wife nimekuta kuna sms za kumtukana jamaa. sasa nipo sielewi nimuadhibu wife kwa kuendelea kuwasiliana na jamaa au nimuadhibu jamaa kwa kutaka kuharibu nyumba yangu.
NIPO NJIA PANDA

Kinga ni bora kuliko tiba lakini pia mkeo yuko sahihi kabisa kukueleza na wewe kama mwanaume wala usipanic, lingekuwa taizo kama hakukueleza ila big up kwa mkeo anastahili pongezi.Ningekupa ushauri mzito kidogo kama ungekuwa umeeleza vema suala zima kwani hatujui kama huyo rafikiyo naye ana mke ama la, ila all in all usiangalie ulikoangukia angalia ulipojikwaa ambapo ni kwa rafiki yako mwite friendly mzungumze unaweza jua mambo mengi na ambayo hukuwa unayajua pia, ila usimwite kwa kuja kumfanyia ugomvi wala fujo. Hatujui wewe pia una miaka mingapi kwenye ndoa yako ila kukupa mbini za nini cha kufanya.Ila kwa kuwa umeeleza kwa ufupi basi zungumza na rafikiyo kiutu uzima.
 
Kinga ni bora kuliko tiba lakini pia mkeo yuko sahihi kabisa kukueleza na wewe kama mwanaume wala usipanic, lingekuwa taizo kama hakukueleza ila big up kwa mkeo anastahili pongezi.Ningekupa ushauri mzito kidogo kama ungekuwa umeeleza vema suala zima kwani hatujui kama huyo rafikiyo naye ana mke ama la, ila all in all usiangalie ulikoangukia angalia ulipojikwaa ambapo ni kwa rafiki yako mwite friendly mzungumze unaweza jua mambo mengi na ambayo hukuwa unayajua pia, ila usimwite kwa kuja kumfanyia ugomvi wala fujo. Hatujui wewe pia una miaka mingapi kwenye ndoa yako ila kukupa mbini za nini cha kufanya.Ila kwa kuwa umeeleza kwa ufupi basi zungumza na rafikiyo kiutu uzima.

ahsante mkuu kwa ushauri mzuri, nitaufanyia kazi
 
Pole sana, kwanza huyo mkeo aliitoa wapi number ya cm ya huyo jamaa alohamia mtaani mwezi mmoja tuu? walikua na mazungumzo gani mpaka wakapeana number za cm? inamaana huyo ndio wa kwanza kumtongoza tangu umuowe? au wote wanao mtongoza wote anakwambia? tumia busara ya kiume fikiri kabla hujafanya maamuzi......
 
Back
Top Bottom