Why Magufuli administration misses the point on Government splurge

Status
Not open for further replies.
I believe
1614313389868.jpg
 
PALE MAITI INAPOKUWA NI BORA KULIKO MGONJWA

Mazungumzo baina ya Marafiki wawili Wa Huko Mbinga.
Bwana Ndunguru &
Bwana Komba.

Ndunguru: Naumwa sana rafiki yangu Komba nimelazwa wiki ya pili sasa sina pesa kabisa.

Komba: Unaumwa nini Kaka?

Ndunguru: Homa imenibana kweli aisee na naona pesa za kugharimia matibabu zinaniishia kabisa.

Komba: Ningekusaidia Bro bahati mbaya kuna kiwanja tulipatana na muuzaji majuzi ndo nataka kesho nikanunue.

Ndunguru: Sawa Kaka, ila siko vizuri kabisa kipesa. Nisaidie walau kidogo Ndugu yangu.

Komba: Iko hivi, bajeti zote tunazopanga Mimi na Mke wangu, huwa hazivunjwi Ndugu yangu. Nimebakiwa na hiyo Milioni 5 tu ya kiwanja.

Ndunguru : Ukinisaidia hata laki mbili tu inatosha Rafiki yangu. Nikipona tu nitakulipa, nitazirudisha.

Komba: Hapo itakuwa ngumu kidogo, na vipi umejaribu kuupigia Uongozi wa Chama chetu cha Wafanyabiashara?

Ndunguru : Ndio, wamenichangia 30,000 tu.

Komba: Anzia hata hiyo Bro. Get well soon.

BAADA YA NDUNGURU KUFARIKI

Komba : Bw. Ndunguru alikuwa rafiki yangu mkubwa tulioshibana, tuliyeshirikiana katika mambo mengi sana, hivyo Mimi kama Rafiki aliyekuwa zaidi ya Ndugu natoa mchango Milioni moja cash.

Chama cha Wafanyabiashara: Tumehuzunishwa sana na taarifa hii, kwani Bw. Ndunguru alikuwa Mtu muhimu sana katika Chama chetu, ameacha pengo kubwa, halitazibika.

Sisi tutagharamia gharama zote za hapa msibani, kuanzia chakula, usafiri hadi mazishi yote yaishe.

UJUMBE WANGU KWENU

Naomba ifikie kipindi tubadilike kwa kuanza kumthamini Mgonjwa kuliko Maiti. Yaani Mtu akishafariki, Marehemu ndio tunamuenzi sana kuliko alipokuwa Mgonjwa!!?

Maana kuthamini Maiti, Marehemu kuliko Mgonjwa ni unafiki uliopitiliza sana.

Huenda huyo Mtu angesaidiwa kwa nguvu kubwa kama inayoonekana kwenye mazishi asingefikia hadi kufa.

Kibaya zaidi ni pale ambapo Mtu hakuwahi kwenda hospitali kumjulia hali Mgonjwa makusudi kabisa, lakini anajifanya yeye ndo Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi na kutayarisha risala ndefu ya wasifu wa Marehemu.

MUNGU atuhurumie. Tujitafakari saana na Tubadilike jamani!!
 


The scripture says a man who interjects before he hears in full there's more hope in a fool than in him....

The real complaint is not long calls but short calls which are frequent and costs more....so deducing long calls was an issue missed a point...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom