Why dr slaa

Jolebatawi

JF-Expert Member
Dec 10, 2011
549
230
Watanzania tuwe makini sana na nchi yetu.
Mjadala wa kumjadili Dr Slaa nahisi sasa umepamba moto kila kona ya nchi hii ikiongozwa na wanaCCM.
Swali langu ni kwanini nchi hii maskini tusijadili masuala mazito kwa mustakabali wa kizazi hiki na kijacho??soko la ajira limekuwa gumu,,wakazi hifadhi ya ngorongoro wameanza kufa kwa njaa huku mfutakamba naibu waziri anasema hakuna atakayekufa kwa njaa,,huku gharama ya kesi ya dowans yafikia bilioni 54 na zaidi,,maambukizi ya ukimwi yanazidi kupaa sababu ya umaskini na mengine mengi yanayohitaji mjadala wa kitaifa.
Ndugu zangu kueni makini sana na CCM,wanapozidiwa na wapinzani wanavunja uongoz na kuweka wapya klisha wanaanza kuzunguka na kupiga kelele zisizo na tija,nakwakuwa watz ni wasahaulifu nao wanajikuta kwenye mkumbo wa ushabiki wasijue wanatuangamiza taratibu.
Mfano Nape anasema dr slaa ana kadi ya ccm,lakini katiba ya ccm inasema mtu akihamia chama kingine tayari amejiondoa ndani ya ccm ila anapotosha umma makusudi ili watu wasijadili masuala ya msingi waelekeze mijadala ya kipuuzi kwakuwa wananufaika na ujinga wetu watz.
Mtu anahama chadema leo na kwenda ccm na kusema chadema ina wenyewe,hizo ni za muishiwa hivi nani asiyejua ccm ndiyo vinara wa siasa za kujuana??eti chadema ya kikanda,hizo ni propaganda zilizopigwa siku nyingi sana je huyo mtu wakati anaingia chadema hakuzisikia hizo tetesi??iweje leo atuaminishe kuwa chama ni cha kikanda???kwani hilo ni jambo jipya kusikika ndani ya tanzania hii.
MWISHO:1.Wanaoikosoa chadema waje na hoja mpya tena zinazothibitika na zenye ushaidi wa kisayansi
** * * * * * * * 2.WATANZANIA KUWENI MACHO SANA NA WANAOJALI MATUMBO YAO KAMA AKINA NAPE
** * * * * * * * *KARIBUNI TUJADILI KWA HOJA
 
CCM wanafeli, adui wao sio Chadema wala Slaa.<br>Hivi zile nguvu nyingi zinazotumiwa na Polisi dhidi ya raia zinamuathiri nani?<br>JK amechelewa sana kusema CCM iache kulitegemea jeshi la polisi kwenye kudhibiti upinzani
 
Bila polisi CCM kwisha!!!. Mwenyekiati hakuwa anamaanisha, bali utani wa siasa. Kama alimaanisha, na kwa vile ndiye amiri jeshi mkuu atangaze tena!
 
Dr Slaa na chama chake ndio madereva wa siasa ya Tanzania kwa sasa kama sio yeye basi ni Mbowe au Mnyika mdee au msigwa,nasari nakadhalika ndio mwendo mdundo
 
CCM wote ni narrow minded ndio maana wanamjadili mtu badala ya masuala ( issues ). Tuwapeleke kuzimu 2015
 
Lazima watunge uwongo na kujifunza siasa uchwara ili kuichafua cdm! Hata hivyo wamechelewa sana kwani watanzania wa leo sio wa mwaka 2000 election ya 2015 wajiweke tiyari kurejesha vyote walivyotuibia kwa kutumia mlango wa amani.
 
Nyambaff mlitaka wenyewe tuwe tuna discuss watu, msipige kelele sasa.
 
Ndugu yangu Nduka hivi historia ya siasa tz huijui,,eti chadema ndio walioanzisha kudiscuss m2 na si facts,nahisi unaendeleza mkakati wenu wa kudanganya wadanganyika.Nilikuwa na matumaini sana na ccm mwaka 2005 na kauli mbiu *
yenu ya ari mpya,nguvu mpya na kasi mpya tena rais akiwa mwenye sura ya ubichi,kumbe mkatupeleka kuzimu,baadaye mkasema chama kimepoteza mvuto kwa sababu ya makamba mkamtimua,wakaja mavuvuzera wakina nape ooh tunawavua magamba mapacha watatu,sera ikafeli mkaamua kumvua gamba mukama,sasa hivi eti tumepata muarobaini wa kukikomboa chama naye ni mangula na kinana.NI SUALA LA MUDA TU KWA HAWA WAPYA COZ HAWANA JIPYA NA KWA SASA WATANZANIA HATUDANGANYIKI KIPUMBAVU (SASA DUNIA NI KAMA KIJIJI)
 
Thanx pakawapakawa "bila polisi na tume ya uchaguzi ccm kwisha".Tusipige mayowe CHADEMA inakua taratibu na ccm inakufa taratibu hata kama mtashinda 2015 ila mtavujishwa jasho sawasawa kutoka kwa CHADEMA,watawakimbiza mchakamchaka sawasawa na maximum ya utawala wenu hautazidi mwaka 2020.ILA 2015 KUKIWA NA KATIBA MPYA ISIYOCHAKACHULIWA PAMOJA NA TUME HURU YA UCHAGUZI MAGAMBA MJIANDAE KUAGA IKULU.NAMHURUMIA NAPE SIJUI ATAKULA WAPI COZ SASA ANAKULA KWA KUPIGA KELELE NA KURUSHIWA MAKOMBO YA IKULU.
 
nachojua ccm kwa sasa wanahaha kutafuta nini cha ku counter mandaifu yao na cha ajabu wanaangalia without badala ya within ...ila nachoshukuru cdm ni chama makini sana wamekaa kimya siku wakiamka utasikia mziki wake aisee
 
Nape ana uhakika wa kukaa kibanda cha uani kwa mzee Pale Msoga ndo maana hapangilii maneno, anaongea kama mlevi tu.
 
njaa mbaya yaani mtu mzima unasema uongo bila haibu usichezee njaa hasa hhawa wanaotembea kwa migongo ya posho za walala hoi bila uongo hawazipati hapo walishakutana wakasifiana umeona nimemchana Dr. si uliona yule jamaa alietupa bajeti ya wapinzani walimtunza pesa mafisadi wenzao. posho zingine zina laana unakula pesa ya wananchi wamechoka lazima ikutokee puani. kiama kinakuja subilini
 
Mbona hamsemi Shibuda maana wakati mwingine nasikia anaendaga kwenye vikao vya ccm.
 
Back
Top Bottom