SASATELE
Senior Member
- Sep 12, 2011
- 167
- 89
Watanzania tuna tatizo sugu la lack of maintenance!! Ukiangalia barabara zetu unakuta mitaro ya maji taka imeziba na wahusika hawazibui, ukiangalia nyumba, kuta zimechakaa hazipakwi rangi miaka nenda miaka rudi. Ukimpangisha mtu nyumba yako hafanyi simple maintenance hata ya kunyonya maji taka anataka mwenye nyumba umfanyie kila kitu. Nyavu za mbu zimetoboka na wanawe wanapata shida eti ofisa wa benki na tai anasubiri hadi baba mwenye nyumba aje. Ukiangalia watu wanavyoteseka na vitambi utachoka, mtu kupanda ngazi anahema ulimi nje, ukiwaambia fanya mazoezi upunguze uzito na uwe fit uishi zaidi ya miaka 50 anakwambia ya nini tabu kukimbia/kujog kama kichaa? Nenda Gym basi, aah sina hela lakini bar hakosi!!. Yaani hakuna maintenance kuanzia public utilties hadi miili yetu watz. Jamani hili nalo ni sababu ya umaskini au culture? Tufanyeje tutoke hapo nasi tuyaendee maendeleo kama ya wenzetu?