Why discuss Miscellaneous countries

Wacha1

JF-Expert Member
Dec 21, 2009
16,682
8,233
Kwa nini members wengi wanajadili sana maswala ya Rwanda, Burundi, Kenya, Somalia kuliko mambo yanayowahusu hususan yanayotokea ndani ya Tanzania?

Pamoja na kuwa member wa hii forum kwa muda mrefu nimegundua kwamba Watanzania wachangiaji wengi wa hii Forum wanapenda sana kuongelea yale yanayotokea kwa majirani wachilia, Somalia et al. Hawa ndio tunasema ni wasomi ambao huenda wakawa na mawazo ya kuiondoa Tanzania kwenye dimbwi la umasikini na kuwavusha wengi ambao hata hawafahamu JF. Je ni ukweli usiopingika kwamba wengi wao maendeleo wanayoyaongelea ni yale ambayo wameyaona kwenye luninga tu? Kwenye vitabu na sinema et al. Wengi wao hawajasafiri kwenye nchi ambazo kweli ni ishara ya maendeleo. Wengi wanajaribu kulinganisha jinsi nchi yetu inavyotakiwa kufanya shughuli zake lakini wanashindwa kuona kwamba hivi viinchi vya Kenya, Rwanda, Burundi, Congo, Somalia et al ni failed states.

Tujivunie kufuata mifano ya nchi kama Sweden, Norway, UK, USA, Singapore, Japan, Canada etc. Demokrasi ya Uingereza au USA ni Zaidi ya miaka 400. Huko ndiko tunaweza kuona vipi and how we can develop na kututoa hapa tulipo. Kuangalia nchi ambazo ni changa ambazo wao wanauana kama kima au tumbili ni mapungufu kwa wale ambao wanafahamu Tanzania inahitaji chachu ya aina gani ili iendelee. JF kama kweli tunataka tuwe sauti inayosikika tuache ufinyu wa fikra na tuwe wachambuzi kweli sio mambo ya fitina ya kujadili kanga au vitenge. Hayo tuyaache kwenye sports na burudani. Tunapoingia kwenye mambo ya msingi ya kizazi kijacho cha Tanzania tuwe more than serious kuonyesha kwamba tunafahamu nini tunachokiongelea. Tumekuwa taifa kubwa na ni lazima tuwaenzi wale waliolipigania taifa hili kwa udi na uvumba kutoka kwenye minyororo ya wakoloni. Tulikuwa na kina Mkwawa, Kinjekitile, Mirambo, Chabruma, Seuta, Nyerere, Sokoine et al. Tutakuwa hatuwatendei haki watoto wetu na kizazi kijacho kwa urithi tulioachiwa na kuacha mafisi machache ya ndani na nje kuja kujineemesha kwa jasho la walipa kodi wa Tanzania. Nafahamu wengi wamesoma kwenye nchi hizo za magharibi/mashariki na wana michango mikubwa tu lakini wanajificha hawataki kuonekana humu na kutoa duku duku zao. Tanzania ni kwa ajili ya kizazi kijacho bring in your good ideas.
 
Last edited:
Je ni ukweli usiopingika kwamba wengi wao maendeleo wanayoyaongelea ni yale ambayo wameyaona kwenye luninga tu? Kwenye vitabu na sinema et al.

Wacha1,

Unaweza mtoa Mtanzania nje, lakini Utanzania kamwe hata akishinda bingo hata uacha!

kuna vitu vyepesi sana ambavyo ni chachu ya maendeleo binafsi na hata ya jumla ambayo tunayapuuzia sana: quality, time management, dependability, reliability, efficiency na accountability.

Tuna ubingwa wa : procrastination, no planing, time wastage, whiners, content with inferiority, text book cramming and lack real life exposure ambazo zina embrace completely culture na ways of living za watu.

Nimeona watu wamekwenda hizo nchi zenye maendeleo na kwa kukosa ujasiri, walikaa kwa kujifungia kama kondoo kwenye zizi, na kondoo wenzao. Sana sana wakiona ngombe au mbuzi (wakenya na waafrika wenzao), watafunguka kidogo.

TUna umahiri wa kwenda kutembea kutumbua, lakini hatujifunzi kwa kuona, kuangalia au tunapokaa na kuishi tukisoma, hatujifunzi kingine zaidi ya kile cha darasani na mbinu za kubuni jinsi ya kuishi tukiwazia tutakachorudi kukifanya nyumbani kwa utaalamu na mazingira ya nyumbani badala ya huku ugenini.

Nikupe mfano: Ujenzi wa nyumba hasa Dar. Mtu kakaa nchi ambazo ceiling ni futi 9-10, mgawanyo wa vyumba vya ndani ni tofali nyembamba na zenye matundu ya hewa. Lakini akirudi Bongo, kwanza atakwenda na design zile zile za nyumbani ambazo si open space (urefu futi 8), lay out ni msongamano na kuta za ndani kalaza tofali na milango ya thamani kubwa sana. Aidha, badala ya kutumia ufundi sanifu wa kutumia vifaa mbora na vyenye kutunza mazingira au recyclables, ataendelea na vifaa duni na vyeney kukosa viwango.

Sasa jiulize, huyu miaka 6 majuu, hakujifunza kwa kuangalia au kudadisi? ni mfano mdogo tuu kama huo. Bado akija kujenga maliwato na mfereji wa maji machafu, ataonelea hakuna shida kuweka dimbwi au mchuruziko wa maji machafu.

Anachofurahia yeye ni hadhi ya kusoma na kuishi nje, fedha zaidi na umombo.

Nenda kazini anakofanya kazi, ukiondoa vijembe na majungu, hatuwezi kuleta mabadiliko chanya au kufundisha wenzetu kutumia exposure yetu ili kuleta ubora na ufanisi katika utendaji kazi.

Ukataji tamaa ni haraka sana, ilhali alipokuwa mbeba boksi, uchacharikaji kuhakikisha ana kibarua na fedha za mahitaji alifanya.

Sasa naelezea haya ambayo wazi ni hasi, kuonyesha ni vipi tabia zisizoendelevu zinashindwa kutufanya tuwe bora.

Ujanja wa kwenda kula Kampiski, pamba za nguvu na umaridadi, hata punda wa Sembe wanavyo ambao wao ni kutua, kujisaidia na kuondoka na bulungutu.

Sasa tunajiweka karibu si na wakenya tuu, bali hata kule vijijini hatuoni umuhimu kuwapa maendeleo walao kama ya Dar es Salaam kwa kutumia mali ghafi na utaalamu kuboresha maisha.

Lakini tusisahau, pia tuna tabia mbaya ya kudhulumiana maendeleo tukitaka wengi wawe watwana huku sisi ni mabwana nyapara.

Leo hii kuna Watanzania zaidi ya 15,000 ambao wamewahi kuishi nje ya Afrika zaidi ya mwaka mmoja, iwe ni Latin America, Asia, North Amerika, Ulaya hata Australia.

We could influence jirani na mtaani kwa vitu vidogo vidogo kuhamasisha usafi wa mazingira, kuweka kifusi kwenye barabara, kuweka mfereji, kujitolea kufundisha watoto masomo kwa bure, na hata gengeni kufundisha muuza nyanya namna ya kufanya bidhaa ziwe bora, safi na kuweka akiba.

Tuking'ang'ania vyeti vyetu na kuhangaika na simu 5, kupiga soga zisizo na mshiko wa kichwa wala miguu kuitana wakuu na big ups nyingi huku hatuelewi jambo bali ni ushabiki, unaanza jiuliza kama upeo wetu kwa kuitwa wasomi ulikuwa ni kukariri tuu bila kuwa na tafakari?

Kule kwenye Kurumbizi (Twitter) najionea hoja na maswali yasiyo na umakini wala kuelewa kinachoendelea. Zaidi ni kushindwa kwentu kutumia character 140 kufikisha ujumbe mfupi wenye maana.

Labda tuanze kutoa twisheni za jinsi gani smartphone inaweza kutuvusha kwenye lindi la usingizi hata kutumia Twitter, Whatsapp au hata simple search kwenye Google.

Utaniwiwa radhi kwa lugha kali kidogo.

Ntakuchekesha la mwisho: Kwa wiki takribani 5. nimekuwa nauliza watu randomly walioko Tanzania tena wasomi: Je ni shughuli gani ya uzalishaji mali au biashara ya kujitegemea inaweza kunipatia daily net (after expenses) ya dola $150-250?

Ni wawili au watatu walidiriki kuja na majibu, na nikawaambia mtaji wangu ni $1000 tu. Bado somo halijaeleweka!
 
Rev. Kishoka

Sifikirii kuna mtu anapuuza haya uliyosema bali wengi wanakariri tu kama kasuku na hawafahamu jinsi ya ku-manage time na kuwa reliable kwa yale wanayofanya, wachilia mbali quality na efficiency of that delivery licha ya kuchukua responsibility kwa yale wanayofanya. Mfano mzuri ni JK, Mkapa pamoja na Mwinyi madudu waliyofanya hawajachukua responsibility yoyote na wanaendelea kuchota pesa za walipa kodi. Hakuna adhabu yoyote ambayo wanapata kutokana na madudu waliyofanya. Kama wangekuwa makini wangetubu kwa uovu waliowafanyia walipa kodi na kuacha kuchota pesa za walipa kodi.

Tatizo sio kujifunza, tatizo ni kuishi kwa kubahatisha na kuogopa status quo. Ukiangalia wengi waliokwenda nje kwa kulipiwa na serikali hawajitumi kwa sababu wanafahamu kwamba wamesoma lakini wakirudi nyumbani watapata vyeo hata kama wamefeli. Culture ya kubebana. Angalia Sumaye alikwenda kusoma Havard ili aje apate cheo tena na kuwakamua zaidi walipa kodi wakati alikuwa failure mkubwa.

Wapo Watanzania ambao walikwenda nje na kujiendeleza wao wenyewe sio kutegemea serikali kimaisha wapo mbali sana. Hiyo figure ya 15000 naona ndogo sana, kuna Watanzania wengi sana nje.

Swala la msingi sifikirii kama Kenyans au Burundians ni mfano kwa sababu wengi wao nawafahamu ni wabinafsi sana na wana chuki kubwa sana kwa Watanzania. Kuna nchi ambazo tunaweza kujifunza kwa mfano UK, Canada, Singapore etc. Nitakupa mfano hivi leo kama ningekuwa na uwezo ningewasomesha Watanzania kwenye nchi zilizoendelea kila mwaka wanafunzi 1000 tu (a year) kwa kuwapeleka Vyuo vikuu mahiri UK, USA, Sweden, Japan na Ujerumani pamoja na Urusi. Kila nchi wanafunzi 200 kwa mwaka kwa muda wa miaka 20. Nafahamu wapo ambao hawatarudi lakini wengi watarudi. Baada ya hapo ungeona mambo yanabadilika.

Tumekaa kuwategemea wale wanaofanya kwenye balozi zetu nje ati ndio wawe viongozi wetu mfano Mkapa. Alichofanya ni kuuza mashirika ya uma bila kufanya tathmini yoyote. Hasara yake hailipiki. Mabalozi wetu wengi hawafahamu kwa nini wamechaguliwa kwenda huko waliko. Hawafahamu nini wanatakiwa kufanya ni kubebana tu kwa kwenda mbele ni aibu.

Mkuu Kishoka mtoto umleavyo ndivyo anavyokua, tumekuwa washabiki zaidi wa kupeleka watoto kwenda kusoma Kenya ati kwa sababu watoto watazungumza kimombo, mbona Kenya kwenyewe sio wazungumzaji wa kimombo kizuri? Kama ni hivyo si basi tungewapeleka kusoma Zimbabwe wanaongea kiingereza kizuri kuliko Kenyans na kama kimombo ndio issue kwa nini basi tusifanye mpango kabambe wa kuwapata walimu wa kimombo kutoka Wingereza? Tusitake maendeleo kwa njia ya mkato hayatatokea. Swala ni mipango na hilo JPM kaanza na kubomoabomoa watu wanataharuki. Tuangalie nchi zilizoendelea walifanyaje kufika huko waliko? Tujifunze kutoka kwa magwiji sio walalahoi kutuzidi sisi. Hatuwezi kuendelea kamwe kama tutaendelea kuangalia pua zetu yaani Kenya, Rwanda, Burundi, Rwanda na Uganda. Tutaendelea kwa kuangalia UK, USA, Singapore, Sweden, Japan etc. How did they do it? Je, UK wamebadilishaje utaratibu wao wa kufanya kazi kuanzia serikali kuu hadi serikali za mitaa, wilaya etc.

Swala jingine ni jinsi viongozi wetu wanavyochujwa, tunatumia misingi gani? Je, wanafuata principals za Project Management? Leadershpi qualities? Au ndio basi ule msemo wa kuongoza kutokana na jinsi unavyofikiri. Je, wanayoyafanya ni value for money? Au ndio basi ni kutumia pesa za walipa kodi kama wanavyotaka kwa sababu kuna kisima cha kukusanya.

BTW sikugusia swala la nyumba etc kwa sababu nafahamu tukiweza kwenye issues nilizododosa huko mambo yatanyooka tu. Pamoja na miundo mbinu etc. Nitafarijika tukiweka fast trains kuunganisha miji yetu yaani naondoka na treni Mwanza saa mbili asubuhi saa tano asubuhi niko Dar Es Salaam. Yes I said that can be done.
 
Rev. Kishoka

Sifikirii kuna mtu anapuuza haya uliyosema bali wengi wanakariri tu kama kasuku na hawafahamu jinsi ya ku-manage time na kuwa reliable kwa yale wanayofanya, wachilia mbali quality na efficiency of that delivery licha ya kuchukua responsibility kwa yale wanayofanya. Mfano mzuri ni JK, Mkapa pamoja na Mwinyi madudu waliyofanya hawajachukua responsibility yoyote na wanaendelea kuchota pesa za walipa kodi. Hakuna adhabu yoyote ambayo wanapata kutokana na madudu waliyofanya. Kama wangekuwa makini wangetubu kwa uovu waliowafanyia walipa kodi na kuacha kuchota pesa za walipa kodi.

Tatizo sio kujifunza, tatizo ni kuishi kwa kubahatisha na kuogopa status quo. Ukiangalia wengi waliokwenda nje kwa kulipiwa na serikali hawajitumi kwa sababu wanafahamu kwamba wamesoma lakini wakirudi nyumbani watapata vyeo hata kama wamefeli. Culture ya kubebana. Angalia Sumaye alikwenda kusoma Havard ili aje apate cheo tena na kuwakamua zaidi walipa kodi wakati alikuwa failure mkubwa.

Wapo Watanzania ambao walikwenda nje na kujiendeleza wao wenyewe sio kutegemea serikali kimaisha wapo mbali sana. Hiyo figure ya 15000 naona ndogo sana, kuna Watanzania wengi sana nje.

Swala la msingi sifikirii kama Kenyans au Burundians ni mfano kwa sababu wengi wao nawafahamu ni wabinafsi sana na wana chuki kubwa sana kwa Watanzania. Kuna nchi ambazo tunaweza kujifunza kwa mfano UK, Canada, Singapore etc. Nitakupa mfano hivi leo kama ningekuwa na uwezo ningewasomesha Watanzania kwenye nchi zilizoendelea kila mwaka wanafunzi 1000 tu (a year) kwa kuwapeleka Vyuo vikuu mahiri UK, USA, Sweden, Japan na Ujerumani pamoja na Urusi. Kila nchi wanafunzi 200 kwa mwaka kwa muda wa miaka 20. Nafahamu wapo ambao hawatarudi lakini wengi watarudi. Baada ya hapo ungeona mambo yanabadilika.

Tumekaa kuwategemea wale wanaofanya kwenye balozi zetu nje ati ndio wawe viongozi wetu mfano Mkapa. Alichofanya ni kuuza mashirika ya uma bila kufanya tathmini yoyote. Hasara yake hailipiki. Mabalozi wetu wengi hawafahamu kwa nini wamechaguliwa kwenda huko waliko. Hawafahamu nini wanatakiwa kufanya ni kubebana tu kwa kwenda mbele ni aibu.

Mkuu Kishoka mtoto umleavyo ndivyo anavyokua, tumekuwa washabiki zaidi wa kupeleka watoto kwenda kusoma Kenya ati kwa sababu watoto watazungumza kimombo, mbona Kenya kwenyewe sio wazungumzaji wa kimombo kizuri? Kama ni hivyo si basi tungewapeleka kusoma Zimbabwe wanaongea kiingereza kizuri kuliko Kenyans na kama kimombo ndio issue kwa nini basi tusifanye mpango kabambe wa kuwapata walimu wa kimombo kutoka Wingereza? Tusitake maendeleo kwa njia ya mkato hayatatokea. Swala ni mipango na hilo JPM kaanza na kubomoabomoa watu wanataharuki. Tuangalie nchi zilizoendelea walifanyaje kufika huko waliko? Tujifunze kutoka kwa magwiji sio walalahoi kutuzidi sisi. Hatuwezi kuendelea kamwe kama tutaendelea kuangalia pua zetu yaani Kenya, Rwanda, Burundi, Rwanda na Uganda. Tutaendelea kwa kuangalia UK, USA, Singapore, Sweden, Japan etc. How did they do it? Je, UK wamebadilishaje utaratibu wao wa kufanya kazi kuanzia serikali kuu hadi serikali za mitaa, wilaya etc.

Swala jingine ni jinsi viongozi wetu wanavyochujwa, tunatumia misingi gani? Je, wanafuata principals za Project Management? Leadershpi qualities? Au ndio basi ule msemo wa kuongoza kutokana na jinsi unavyofikiri. Je, wanayoyafanya ni value for money? Au ndio basi ni kutumia pesa za walipa kodi kama wanavyotaka kwa sababu kuna kisima cha kukusanya.

BTW sikugusia swala la nyumba etc kwa sababu nafahamu tukiweza kwenye issues nilizododosa huko mambo yatanyooka tu. Pamoja na miundo mbinu etc. Nitafarijika tukiweka fast trains kuunganisha miji yetu yaani naondoka na treni Mwanza saa mbili asubuhi saa tano asubuhi niko Dar Es Salaam. Yes I said that can be done.

Mambo anayofanya JPM tuliyasema na kujadili 2016.
 
1593101351537.png
Tanzanian small-scale miner Saniniu Kuryan Laizer, 52, poses with two of the biggest of the country's precious gemstones, Tanzanite, as a millionaire during the ceremony for his historical discovery in Manyara, northern Tanzania, on June 24, 2020. Filbert Rweyemamu, AFP via Getty Images

1593101449093.png
Tanzanian small-scale miner Saniniu Kuryan Laizer, 52, poses with the enlarged check copy from the government after selling two of the biggest of the country's precious gemstones, Tanzanite, during the ceremony for his historical discovery in Manyara, northern Tanzania, on June 24, 2020. - Laizer found the stones weighing 9.27 and 5.1 kilograms respectively in the northern Mirerani hills, an area which President John Magufuli had fenced off in 2018 to stop smuggling of the gem. He sold them to the government for 7.7 billion Tanzanian shillings (nearly $3.3 million). The broken biggest record of Tanzanite was 3.5 kilograms.
Filbert Rweyemamu, AFP via Getty Images


A small-scale miner in Tanzania became a millionaire after finding and selling the two largest tanzanite stones ever unearthed in the country. The government gave Saniniu Laizer a giant check worth 7.74 billion Tanzanian shillings ($3.35 million) for the two dark violet-blue gemstones which weigh 9.27 kilograms (20.43 pounds) and 5.108 kilograms (11.26 pounds), according to the Ministry of Minerals. President John Magufuli called to congratulate Laizer live on television.

Laizer, 52, told the BBC he plans to invest in the community and slaughter one of his cows to celebrate.

"There will be a big party tomorrow," Laizer told the outlet. "I want to build a shopping mall and a school. I want to build this school near my home. There are many poor people around here who can't afford to take their children to school."

He added that he plans to continue looking after his 2,000 cows.

Tanzanite can only be found in a small northern region of the East African country. The gems were discovered in a mine surrounded by a wall built by the government to prevent illegal mining. ''The government set up trading centers around the country to all small-scale miners, who typically mine by hand, to sell their gems and gold to the government, Reuters reported.

“This is a confirmation that Tanzania is rich,” Magufuli told minerals minister Doto Biteko, per Reuters.''

Wasiopenda wajinyonge, hatuwezi kuendelea kuwa makuwadi wa wazungu. We can do it, everybody should play his part.
 
JPM kwa mara nyingine tena anaweka rekodi mpya Tanzania kwa kuweza kutumia pesa za ndani kufanya uchaguzi wa mwaka huu. Nchi za magharibi ambazo walifikiri atakwenda kukinga bakuli hawaamini wamebaki kushangaa. Bado siku watakapokuja kutembea kama wakipenda watashangaa wenyewe.

Thank you very much Rais wetu JPM, hapa ni kazi tu.
 
JPM kwa mara nyingine tena anaweka rekodi mpya Tanzania kwa kuweza kutumia pesa za ndani kufanya uchaguzi wa mwaka huu. Nchi za magharibi ambazo walifikiri atakwenda kukinga bakuli hawaamini wamebaki kushangaa. Bado siku watakapokuja kutembea kama wakipenda watashangaa wenyewe.

Thank you very much rais wetu JPM, hapa ni kazi tu.
Deni la Taifa lipo katika hali gani?
 
Deni la Taifa lipo katika hali gani?
Sina figures right now lakini mara ya mwisho nilipoangalia ukuaji wake umeendelea kuwa constant kwa miaka kadhaa. Miradi mingi ya kimkakati ndio itawezesha Tanzania ijiimarishe financially. Unless kama unasoma habari za udaku ie fake news kwamba uchumi wetu ni mbaya sana.

JPM ni mtetea wa maslahi ya nchi yetu, madini sasa yanafaidisha Tanzania; Reli ndio itakuwa Mwarobaini wachilia mbali Umeme wa Bwawa la Mlm Nyerere Bomba la mafuta ni icing the cake. Tuombe uzima tu!

Media reports Tanzania’s economy is awful: Is this gospel truth,
 
Wabongo mlio na mpunga nunueni shares DSE uchumi wa Tanzania unakua na wakati ni huu msije kulalamika hamkuona hii habari. Shares za makampuni ya cement, sigara pamoja na Tanzania breweries pamoja na Banks mbalimbali CRDB, Akiba pamoja na kampuni za simu hasa Airtel ambayo ni mbia wa Tanzania Government. Wakati ni huu. Unaweza kuanza na kiasi kidogo hata millioni moja.
 
Sina figures right now lakini mara ya mwisho nilipoangalia ukuaji wake umeendelea kuwa constant kwa miaka kadhaa. Miradi mingi ya kimkakati ndio itawezesha Tanzania ijiimarishe financially. Unless kama unasoma habari za udaku ie fake news kwamba uchumi wetu ni mbaya sana.
JPM ni mtetea wa maslahi ya nchi yetu, madini sasa yanafaidisha Tanzania; Reli ndio itakuwa Mwarobaini wachilia mbali Umeme wa Bwawa la Mlm Nyerere Bomba la mafuta ni icing the cake. Tuombe uzima tu!

Media reports Tanzania’s economy is awful: Is this gospel truth,
Kwahiyo kama huna figure ujnapata wapi ujasiri wa kusema '' kaweka rekodi ya kutumia pesa za ndani''
Kwa taarifa tu wakati unatafuta data ni kwamba, deni la Taifa limeongeza kiasi kwamba kuna shaka ya kukopesheka.

Pili, madini yameiinufaishaje Tanzania? tofauti na siku za nyuma.

Tatu, reli itakuwa mwarobaini kwa kwa kupanua wigo gani wa uchumi?
 
Kwahiyo kama huna figure ujnapata wapi ujasiri wa kusema '' kaweka rekodi ya kutumia pesa za ndani''
Kwa taarifa tu wakati unatafuta data ni kwamba, deni la Taifa limeongeza kiasi kwamba kuna shaka ya kukopesheka.
Pili, madini yameiinufaishaje Tanzania? tofauti na siku za nyuma.
Tatu, reli itakuwa mwarobaini kwa kwa kupanua wigo gani wa uchumi?
Huo ujasiri naupata kutoka vyanzo vya habari za kuaminika, mwezi uliopita BOT walitoa figures hizo nilizisoma ndio base yangu vile vile JPM mara kadhaa kwenye mikutano yake amesema hivyo. Mimi namwamini kwa sababu yeye ndio Rais na kuwa rais kuna jukumu la responsibility. Wewe Nguruvi3 hata unapoongopa hapa huna responsibility yoyote, ni hoe hae tu na hata unavyodanganya hivi hakuna pimbi yoyote anayekusikiliza.

Swala la madini hakuna mtu yoyote ulimwenguni anayefuatilia maswala ya madini kwenye stock exchanges nk hafahamu kwamba Tanzania ya sasa sio ile ya zamani. Tunafahamu Serikali imepata pesa kiasi gani kwenye Tanzanite, gold etc. kama hilo hulifahamu pole sana. Kama upo Tanzania tembelea Merelani pamoja na masoko ya madini uone jinsi Watanzania wachimba madini wazawa walivyo na nyuso za furaha.

Reli ni kufanya usafiri wa haraka popote Tanzania na kupunguza mrundikano/msongamano wa malori barabarani na kuharibu njia zetu. Kama hulifahamu hilo sifahamu unahitaji msaada gani. Mfano tafiti zilizofanywa pale Ubungo wananchi kuchelewa kulikuwa kunaondoa muda mwingi wa Watanzania kufanya shughuli nyingine muhimu pamoja na kupunguza ajali nk kama hilo hulifahamu unahitaji msaada gani?
 
"Wacha1, post: 36707451, member: 20496"]
Huo ujasiri naupata kutoka vyanzo vya habari za kuaminika, mwezi uliopita BOT walitoa figures hizo nilizisoma ndio base yangu vile vile JPM mara kadhaa kwenye mikutano yake amesema hivyo.
OK, no problem Sir. Tulitaka kujua vyanzo vyako na muhimu zaidi takwimu.
Mimi namwamini kwa sababu yeye ndio Rais na kuwa rais kuna jukumu la responsibility. Wewe Nguruvi3 hata unapoongopa hapa huna responsibility yoyote, ni hoe hae tu na hata unavyodanganya hivi hakuna pimbi yoyote anayekusikiliza.
Haa! mbona unajishuku! nani kaukuuliza haya yote.
Nani kakuuliza kama unamwini JPM au la. Inaonekana unashaka fulani na nafsi yako inakueleza hivyo.

Ndugu yangu kuna ukweli na kuamini.Ukweli unasimama wenyewe lakini kuamini ni suala la mtu.
Hakuna tatizo kama unaamini chochote, lolote na yoyote.
Kuna tatizo pale unapodhani kile unachoamini ni ukweli na kwamba kila mtu anatakiwa aamini kama wewe.
Kuhusu uhohe hahe mbona ninao siku nyingi! kitu kimoja nina uhakiki, ninapoandika kuna watu wanasoma na mmoja wapo ni wewe. Kwahiyo kama kuna pimbi ninayemjua, wakwanza ni wewe mheshimiwa
Swala la madini hakuna mtu yoyote ulimwenguni anayefuatilia maswala ya madini kwenye stock exchanges nk hafahamu kwamba Tanzania ya sasa sio ile ya zamani.
Alaa! sikujua bwana. Kwani Tanzania ya sasa inaongozwa na akina nani?

Si hawa hawa waliokuwa makatibu wakuu, manaibu mawaziri na mawaziri! Hebu nitajie katika uongozi uliopo, kiongozi mmoja tu aliyetokea miaka 5 iliyopita na ambaye hakuwahi kuwa sehemu ya mfumo.
Tatizo la hii hoja yako ni kuwa waliokaa kimya Tanzani ikitopolewa ndiyo mashujaa leo, real!
Tunafahamu Serikali imepata pesa kiasi gani kwenye Tanzanite, gold etc. kama hilo hulifahamu pole sana.
Wewe unafahamu, sisi tusiofahamu hatufahamu kwasababu wewe umesema tu unafahamu.
Tutafahamu ukiweka tawkimu. Huna! hata hivyo porojo zako zinapendeza
Kama upo Tanzania tembelea Merelani pamoja na masoko ya madini uone jinsi Watanzania wachimba madini wazawa walivyo na nyuso za furaha.
Lini wachimbaji walikuwa na huzuni? Iliyokuwa na huzuni ni serikali. Madini yanachimbwa Mererani , muuzaji mkubwa ni Kenya, msafishaji ni India. Guess what, walikuwepo, waliona uozo huo hawakusema.
Reli ni kufanya usafiri wa haraka popote Tanzania na kupunguza mrundikano/msongamano wa malori barabarani na kuharibu njia zetu. Kama hulifahamu hilo sifahamu unahitaji msaada gani.
Wakati Wahindi wanang'oa mataruma, hawa hawa walikuwepo. Walikaa kimya!
Mfano tafiti zilizofanywa pale Ubungo wananchi kuchelewa kulikuwa kunaondoa muda mwingi wa Watanzania kufanya shughuli nyingine muhimu pamoja na kupunguza ajali nk kama hilo hulifahamu unahitaji msaada gani?
Tafiti hizo umeziona leo. Sisi tulizungumzia hili hapa Jamii forum miongo mingi tu.
Wazo la Treni ya Mwakyembe chimbuko lake ni hapa Jamii forum.

Stigler imeongelewa hapa miaka dahari. Wazo la SGR lipo hapa miaka dahari, tena lionyeshwa kwa ushahidi jinsi wenye malori walivyohujumu Treni.

Wazo la barabara ya Bagamoyo Tanga limetoka hapa. Hayo ni kwa uchache sana.

Sisi hatusbiri kusimama ubungo kuhesabu magari.
Tena overpass ya Ubungo ni sehemu tu wala suluhisho. Tulishauri feeder road

Utashangaa ring road Dodoma, wazo limetoka hapa. sasa unataka uje na kitu gani ?
MATAGA teh teh teh! mbavu zangu Mataga! kwi kw kwi jamani Mataga tuacheni tupumue!
 
Mawazo/wazo hubaki kuwa hivyo. Swala ni utendaji kama huwezi kutenda endelea kuwa na mawazo pengine mawazo huwa yanatatua matatizo bila vitendo. JF wengi huwa tunaandika kwa sababu hatuna uwezo wa kutenda, kama wazo lako limetendeka basi shukrani kwako kwa sababu umechangia maendeleo ya Watanzania kwa namna moja au nyingine. Wala usifikiri yanayotendeka hayakuwa mawazo ya wengine vile vile unaposhangaa wewe wenzako hawashangai.

Kuhusu kuwa hapa unasema mlijadili miaka ya nyuma, hayo ni mawazo na kwa mujibu wa JF data mimi ni senior kuliko wewe sasa unapojishaua kama bibi sijui maana yake ni nini? MATAGA tafsiri yake as far as I know ni ''Make Tanzania Great Again'' pengine wewe una tafsiri ingine, au la pengine unaweza share na members.
 
MATAGA tafsiri yake as far as I know ni ''Make Tanzania Great Again'' pengine wewe una tafsiri ingine, au la pengine unaweza share na members.
Serikali iliwahi kemea uagizaji wa mitumba, sijui kama katazo lipo au la!

Lengo la kuimarisha viwanda vya nyumbani hasa nguo lakini pia kuzuia udhalilishaji ikizingatiwa kuwa; Mitumba ilikuwa ya chupi, suruali, T-shirt, Viatu , hadi 'wigi ''

Mitumba si ya nguo tu kwa waafrika, hata majina ya watu nayo pia tunaagiza kutoka nje ya nchi.

tumekwenda mbele zaidi na kuagiza misemo ya watu (mantra) au kauli mbiu.
MAGA ni Make America great again, kauli mbiu ya Rais Trump. Marekani bado wanahoji mantiki ya kauli hiyo.

Miaka 60 ya Uhuru watu wameshindwa kubuni hata kauli mbiu na sasa ni MATAGA.
Mataga ni kielelezo cha kuvia kwa fikra kwa washiriki wa kundi au ''organization' hiyo.

Make Tanzania great again ina maana gani?
Lini Tanzania ilikuwa great ikiwa tupo katika kundi la nchi masikini sana duniani?

Lakini pia kama kuna eneo Tanzania ''ilikuwa great! '' ni medani za kimataifa ambapo wengine wamekaririwa wakisema ''Dar es Salaam ilikuwa kama Mecca au Vatican'' kwa aliyetaka Diplomasia za kimataifa.

Kwasasa ni historia, tumefutika na kupoteza ushawishi wetu kabisa , silaha yetu tuliyokuwa nayo.
Mataga hawaoni! wanajivunia mantra za mitumba.

Mataga wanazungumzia '' dhana ya kuletewa maendeleo''. Kwamba fulani atawaletea maendeleo.
Maendeleo ni hatua na mchakato shirikishi. Maendeleo si gunia au kontena la bidhaa linaloletwa na kubwagwa . Ninapowasikia Mataga ninaondokewa na shaka na uwezo wao wa kufikiri achilia mbali elimu.

Mataga hawaelezi wananchi, hali ye deni letu la ndani ipoje? deni la nje ipoje!
Anayelipa deni si Mataga au CCM ni Wananchi wa Tanzania, kujua ukubwa wa deni lao ni haki si fadhila.

Mataga wanazungumzia elimu bure! wasichozungumzia ni ubora wa elimu, kama unawasaidia wahitimu.

Mataga watakwambia ujenzi wa SGR! Wasichoweza kukueleza ni kuhusu bahari.
Kwanini samaki aliyevuliwa bahari ya Hindi na meli za China awe na bei nafuu ?

Kwanini tusitumie bahari na maziwa katika kuongeza wigo wa pato la Taifa?
Kwanini tusiwe ''exporter' wakubwa wa samaki katika nchi za maziwa makuu?

Mataga watakwambia tumeongeza bei za korosho kwa wakulima.
Wasichokueleza ni kwamba kwa arable land, kwanini Tanzania iagize mchele kutoka nje?
Nini kilitokea lower Moshi irrigation ? Mbarali na Dakawa?Nini kimetokea kwa 'the big five''?

Kwa kumalizia , Mataga ni kielelezo cha kuvia kwa akili za Watanzania.
Ni kundi lisilojua linazungumzia nini na kwanini, tatizo kubwa sana nchini, na Mheshimiwa kama ni mshiriki na wale wengine wenye ID nyingi hapa, habari za Mataga zina nafasi kwingine, si hapa.

Fikirieni kama mnalisaidia taifa ukiachilia mbali matumbo yenu.
Kama hamuwezi kubuni kauli mbiu, mnaweza nini?
 
Nguruvi3

Numbers do not lie:


''ECONOMISTS have said Tanzanians are now highly enjoying 'bigger national cake,' following robust reforms made by the government, which have seen the country's Gross Domestic Product (GDP) more than double.

The country's GDP has more than doubled to 124tri/- in the past five years in comparison to 52.9tri/- in 2015, thanks to major economic reforms, including the consistent plans and bold decisions made by the fifth phase government under President John Magufuli.

According to the National Bureau of Statistics (NBS) Statistical Report on the success of the fifth phase government on economic growth and improvement of livelihood of Tanzanians, the high GDP performance is equal to an average of 6.9 per cent growth in the past five years in comparisons to 6.3 per cent registered in 2015.

In the same period, the average per capita income earned per person in dollar terms rose to 1,063.3 US dollars equivalent to 2.38m/- in comparison to 622 US dollars (979,513/-) in 2015.

Orbit Securities Head of Research and Analytics Imani Muhingo said GDP growth means total national expansionof economic activities thus "a bigger national cake" for everyone.

"As long as GDP growth is faster than population growth, everyone's share in the economy rises by the balance," Mr Muhingo told the 'Daily News'.

He, however, caution that not everyone shall gain equally because of income inequality, but Tanzania has one of the lowest Gni coefficients globally.

Mr Muhingo also said "this shows the government's focus on infrastructure development that is paying off, because most of the construction sector growth is spearheaded by the government."


NBS report showed that the construction sector became the major contributor to the robust GDP growth by 25.6 per cent as the government is executing major flagship projects, including the Standard Gauge Railway (SGR), flyovers, bridges, roads, ports and airport expansions.

Generally, rising GDP will translates to a higher standard of living, because diminishing national income causes the standard of living to decline.

An economist-cum-banker, Dr Hildebrand Shayo, said an increase in real GDP, ceteris paribus, will cause an increase in average interest rates in an economy.

"An increase in GDP will raise the demand for money because people will need more cash to make the transactions necessary for purchase. In other words, real money demand rises due to the transactions demand effect," Dr Shayo said.

Tanzania enters into that bracket of middle-income countries with Gross National Income (GNI) per capita between 1,026 US dollars and 3,995 US dollars.

This new income status for Tanzania implies improved living standards by way of higher quantity and quality of goods and services consumed.

Others are better quantity and quality of social services like health, education and water, lower mortality and morbidity rates, higher literacy rates, lower poverty levels as well as more quantity and quality of economic infrastructure.

The other sectors that made huge contribution to GDP growth are namely agriculture (19.4 per cent), industries (9.8 per cent) as well as works and communication (8.8 per cent).

However, analysts said agriculture's contribution was still low and also show how the agriculture sector is underutilized and how there's so much opportunity in the sector.

"This raises the need for further investment in agriculture which would mostly mechanize the sector and raise a new challenge of unemployment. "And this is why we need more factories, especially agricultural processing factories that would absorb unemployed personnel from a mechanized agricultural sector," Mr Muhingo said.

However, other urged that in the country the development of this sector has been measured via multiple primary measures like income, employment, sales, value added and economic multipliers.

"Infrastructure that could present true picture of this sector contribution is inadequate and there is a need to do more, because this sector hold potential that could contribute more to our economy," Dr Shayo said.''

Tanzania: Economists - Tanzanians Enjoy Bigger National Cake
 
Hofu, hofu, hofu.
Tangu 2016 wachangiaji wengi au waandishi wa makala kwenye magazeti au kwenye tv waliacha kufanya hivyo.
Kwa mfano hapa jamii forum, utakumbuka uchaguzi wa 2015 kulikuwa na mijadala mirefu moja uliongozwa na Nguruvi, lakini hii 2020 hakuna tena mijadala kama ile. Kwa sasa ni rahisi sana kujadili uchumi au siasa au jamii ya nje kuliko hapa Tz. Kujadili ya hapa unaweza teleza
 
Hofu, hofu, hofu.
Tangu 2016 wachangiaji wengi au waandishi wa makala kwenye magazeti au kwenye tv waliacha kufanya hivyo.
Kwa mfano hapa jamii forum, utakumbuka uchaguzi wa 2015 kulikuwa na mijadala mirefu moja uliongozwa na Nguruvi, lakini hii 2020 hakuna tena mijadala kama ile. Kwa sasa ni rahisi sana kujadili uchumi au siasa au jamii ya nje kuliko hapa Tz. Kujadili ya hapa unaweza teleza
Sidhani kama ni swala la kuteleza au hofu, nionavyo mimi wengi wanajadili kwa kuvutia kamba kwenye manufaa yao na sio manufaa mapana ya nchi. Wengi wanaweka ushabiki wa maslahi yao kwanza kabla ya utaifa. Ni aibu kwa sababu Watanzania tuna uwezo mkubwa sana wa kufanya mambo makubwa. Lets not lose hope and try to convince others that it can be done.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom