Who Recruited Kikwete and what did they see in him and when?

MM you are very right, ukizisoma hizi cables vizuri utagundua JK yupo kutimiza matwaka ya watu fulani fulani (Nchi za magharibi? mfano ni cable inayohusu JK, Waitara na Kapuya)....je, ni yapi ambayo hatuyajui kuhusu JK na "ushosti" wake na Marekani?
 
Kikwete "aliandaliwa" kushika position ya juu kwenye Uongozi wa nchi mara tu Mzee Mwinyi alipopata nafasi ya kuwa Rais. Utakumbuka namna alivyopandishwa vyeo haraka na kuwa Waziri kamili (tena wa Wizara nyeti) baada ya muda mfupi. Kikwete hakuwahi kuwa chaguo la Mwl. Nyerere (kama ilivyokuwa kwa Mzee Mwinyi), na ni wazi alionekana mtu "sahihi" na "rahisi" "kumtumia" kubadili mfumo na kulegeza misimamo ya kizalendo ya awamu ya kwanza.

Mzee Mkapa "alisaidia" kum-expose Kikwete kwenye "siasa" na "fitna" za kimataifa wakati alipomteua kuwa Waziri wa Mambo ya Nje (huko bila shaka waliokuwa wanamwandaa walipata fursa ya kumwahidi misaada yao na kupata ahadi ya "kutimiziwa" mahitaji yao baada ya kupata U-Rais).

Mambo yanafunguka sasa na wa kulaumiwa ni sisi kwa kutokuwa "wasikivu", na bahati mbaya kuwa na utaratibu usiokidhi haja wa kuwapata viongozi wakuu.
Mkuu tukiangalia hapo kwenye RED , ina maana JK naye anamwandaa Ngeleja kushika uongozi maana alimpandisha haraka haraka hadi kuwa waziri kamili kwenye wizara nyeti ????
 
Nimesoma hizi Wikileak diplomatic cables na kuona JK anavyoingizwa sehemu mbalimbali na kujikuta ninajiuliza hilo swali. Sijui wengine mmeona pattern fulani au mmejiuliza swali au kupata majibu ya swali hilo?

Nothing in him,Nguvu za giza zilitufunika macho ya rohoni na kuvutiwa na macho ya nje yaliyoona upole,tabasamu na utanashati.wachache walioona macho ya rohoni walituonya juu ya hili.
 
Inashangaza zaidi kwamba huyu mkulu alikuwa minister wa foreign affairs for 10 years of which hata kama alikuwa mzembe mzembe before, basi angejifunza mambo mengi kuhusu diplomacy!!!!!!!

Lakini mkuu mm wala sishangai na mbaya zaidi the guy has role-modelled plenty. Kwa hiyo huko mbele tutegemee even some worse reckless leaders kuliko hata yeye!!!! The trend and pattern that I see kuhusu taifa letu ni kuporomoka kwa maadili, kukosekana uwajibikaji, kukumbatia ujanja ujanja etc. Imagine juhudi kubwa mno zimefanyika kupindisha ukweli, to lower the leadership bar, and to convince the masses that what we have and what we are is the best. Na watu aina ya JK eti ndiyo tunaambiwa wanafaa kuongoza taifa hili. Cry my beloved country.

CCM itabeba dhambi ya taifa hili kwani ilipewa opportunity na majority kulinda interest zetu public wakazi personalize ole yao ni kubwa!
 
Kikwete was recruited by CCM na zile kamati zao sijui CC mara NEC hatiamae watz tukalazimika kumchagua kama raisi kwa kuwa anatokea CCM bila kujari kuwa nafaa kuwa raisi au lah
CCM waliona kuwa Kikwete anafaa kwa sababu ilikuwa zamu ya waislamu,handsome etc
Na CCM waliliona ilo hasa katika uongozi wake katika nyazifa mbalimbali walizompa wakaona anazimudu ivyo wakaona na uraisi atauweza
Nadhani MM nimejibu maswali yako,so CCM ndo waliotuletea ili janga wakijua fika watz huwa wanachagua chama na si mtu kama mtu!
Ndo maana kipindi kile waliposimama Mrema na Mkapa ,Ben akapeta na tukampiga chini Mrema ambaye tulikuwa tunamjua with proven experience ya utendaji ila kwa sababu ya chama alikuwako hatukumpa kura za kumfanya awe raisi.
Ni hayo tuu kwa leo
 
Kwa upande wangu hao jamaa hawahusiki na huyu jamaa kuingia madalakani kwake,huyu mkuu aliingia madalakani kwa mfumo wetu na jamii yetu ilivyojipanga na kwa msaada wa Rais wa awamu ya PILI kumjenga na kwa kuwa na bashasha la kupendwa [Charismatic=A person attracts, influences, and inspires people by their personal qualities.-].

Kidogo historia ya kule alikopita na malezi pia ni athari ambazo zinachangia kutoa zana mpya [Thsesis],na pia upenzi binafsi juu ya aina fulani ya life style.Mfano ukiweka aina mbili ya life sytle kati kuchagua uchina au umarekani hakika kwa mhusika atachagua umarekani kwa sababu ya haiba yake [personality].

Hivyo Tangu alipopata ufahamu na kwa kuwa mwanzoni enzi ya ujana wake,alipenda sana style ya uchina yaani ukomledi,lakini kadri alivyokuwa anakuwa na kukutana na changamoto nyingi za mabadiliko ya jamii na tabia za wakuu wake zikiwemo kuathiliwa kisaikolojia kama kweli lille tendo la Monduli lilikuwepo [ambalo kwa zama zile ilikuwa ni aina ya uzalendo kisha uzalendo wake unawekwa wazi kwa wahusika,na kwa kuwa yeye ni kijana mdogo wakati ule, pata picha alivyopona kwenye mtafaruku ule na wazee wale hakika,kwa kijana yoyote angejenga hasira za ndani kwa ndani na mfumo huo,

Kwa hiyo hawa wadau kawajua na kujihusha nao sana na kuvutiwa na style yao ya maisha,baada ya kuwa waziri wa mambo ya Nchi za Nje,lakini si vinginevyo.

Huyo mkuu ni mpenzi wa kinamama. Wanamuita "handsome" tabasamu lake endelevu linawamaliza wakinamama. Sasa kwa kuwa wengi wa wapiga kura ni wakina mama hayo ndiyo matokeo kwamba ameweza kupeta katika kipindi cha kwanza na hata cha pili ingawa ukweli ni kwamba utendaji wake katika kipindi cha kwanza tu ungeweza kumnyima kuendelea na kipindi cha pili lakini kwa kuwa wapiga kura wengi ni wakinadada na wao hawajui juu ya utendaji ingawa ndiyo wanaobeba mandoo ya maji mabarabarani kusaka maji, ndiyo wanaopika kwenye giza na balaa zingine zote bado wakati wa kura wanaangalia u-handsome na bahati mbaya hata kwa "population" ndiyo wengi kwa hiyo kama jamaa angekuwa na kipindi cha tatu bado angepita kwa sababu akitabasamu tu wakinadada wote taabani wanatoa kura bila kujijua. Inabidi somo la nguvu lipite kwa wanaume ili uchaguzi ujao wajitokeze kwa wingi katika kupiga kura na pia wawaelimishe madada juu ya hatari ya kuvutiwa na tabasamu na u-handsome pasipo kuangalia uwezo wa mtu.
 
Huyo mkuu ni mpenzi wa kinamama. Wanamuita "handsome" tabasamu lake endelevu linawamaliza wakinamama. Sasa kwa kuwa wengi wa wapiga kura ni wakina mama hayo ndiyo matokeo kwamba ameweza kupeta katika kipindi cha kwanza na hata cha pili ingawa ukweli ni kwamba utendaji wake katika kipindi cha kwanza tu ungeweza kumnyima kuendelea na kipindi cha pili lakini kwa kuwa wapiga kura wengi ni wakinadada na wao hawajui juu ya utendaji ingawa ndiyo wanaobeba mandoo ya maji mabarabarani kusaka maji, ndiyo wanaopika kwenye giza na balaa zingine zote bado wakati wa kura wanaangalia u-handsome na bahati mbaya hata kwa "population" ndiyo wengi kwa hiyo kama jamaa angekuwa na kipindi cha tatu bado angepita kwa sababu akitabasamu tu wakinadada wote taabani wanatoa kura bila kujijua. Inabidi somo la nguvu lipite kwa wanaume ili uchaguzi ujao wajitokeze kwa wingi katika kupiga kura na pia wawaelimishe madada juu ya hatari ya kuvutiwa na tabasamu na u-handsome pasipo kuangalia uwezo wa mtu.

Kama Faizafox kwa jamaa humwambii kitu kaisha babisa
 
Nimesoma hizi Wikileak diplomatic cables na kuona JK anavyoingizwa sehemu mbalimbali na kujikuta ninajiuliza hilo swali. Sijui wengine mmeona pattern fulani au mmejiuliza swali au kupata majibu ya swali hilo?

MM, I think you are trying to say "why has the guy been singled out." Of course we have had other presidents before him, not only that, but we also have had American diplomats in the country before Retzer... Out of them all, why the hell then this guy is being singled out going back to his foreign ministerial engagements??!!

I think the following congratulatory message is weighty enough to answer some if not all of your questions:

Obama_statement.jpg

Source: https://www.jamiiforums.com/tanzani...-people-shein-but-skip-congratulating-jk.html
 
Mkuu tukiangalia hapo kwenye RED , ina maana JK naye anamwandaa Ngeleja kushika uongozi maana alimpandisha haraka haraka hadi kuwa waziri kamili kwenye wizara nyeti ????

Mkuu nimeuona mtego wako, wala "anachi ntu!".......Pamoja na Ngeleja, yupo pia Membe, Dr. Mwinyi, Dr. Migiro...na huwezi jua hata Malima anaweza kuwemo katika wanaoandaliwa.

Tumefika hapa tulipo kutokana na mapungufu kwenye utaratibu wa upatikanaji wa Viongozi wakuu, tujiulize kwa dhati: Je, tuendelee kuwa wajinga na vibaraka wa nchi za Magharibi? Au, kama sivyo, Tunatokaje kwenye mtego huo?
 
Jamani, kuhusu mkuu wa dola kupitishwa kuwa mgombea, habari nilizowahi kusikia ni kwamba wakati majina matatu yalipouwa yakijadiliwa, JK, Salim na Mwandosya, kulikuwa na dalili kwamba walitaka kumtupa JK kwa madai kadhaa, kutia ndani fedha nyingi zilizotumika wakati wa kampeni yake kuwania kuteuliwa kugombea uraisi kwa tiketi ya CCM, ambazo nyiki ya fedha hizo zilitoka mataifa ya Kiarabu kupitia kwa Rostam. JK aliposikia walitaka kumtosa aliweka wazi kwamba kama CCM wasingempitisha kuwa mgombea basi angejiunga na upinzani na akawahakikishia kwamba Salim au Prof Mwandosya wasingefua dafu kwake kama angekuwa mgombea wa upinzani na mmoja wao akawekwa kama mgombea wa CCM. Kuona hivyo ikawa Mkapa hana jinsi bali kuamua kumpitisha, japo hakulifurahia. Ila Mkapa inasemakana alifanya makubaliano pia na JK kwamba angempigia debe apitishwe kwa kujenga kwenye uteuzi wa mwisho wa CCM, ikiwa na yeye JK amlinde Mkapa atakapokuwa raisi. Inaonekana Mkapa alikuwa na wasiwasi juu ya baadhi ya mambo aliyofanya akiwa raisi. Inasemekana hili liiwatia hasira vigogo wengi wa CCM kwa sababu waliona kama walikuwa "blackmailed" na hivyo wakawa hawampi JK ushirikiano alipokuwa raisi. Na JK aliwatibua zaidi kwa kumteua Lowasa kuwa PM kinyume na kile walichodhani walikuwa na makubaliano naye kwamba angalau asimpe Lowasa u-PM.

Zaidi ya yote, taarifa zinasema JK alifanya pact na Lowasa kwamba baada ya uraisi wa JK kwisha Lowasa ndiye angekuwa raisi na JK alipasa kulisimamia hili.

Wenye taarifa zaidi watueleze.
 
TZ hatujawahi kua karibu na Marekani kama hivi sasa, kwa kweli ukifatilia Wikileak, Safari za JK US nk, naishia na jibu moja tu!! JK ini kibaraka wa wamerikani. Maswali ni mengi, kwanini umekua kibaraka? Ni wapi tunakokwenda ?
 
Sio lazima uwe na degree kujua huyu JK anauza nchi...msaliti wa nchi na wananchi wake. Kiongozi mbovu mbovuuuuuuuuuuuuuu. Tusikae kimpya..hili sio swala la CCM au Chadema, hili ni swala la Taifa zima,nchi yetu. Tusiangalie vyama vyetu, huyu siyo CCM/CUF/CHADEMA, huyu ni msaliti wa watu wake....Yes I said it !
 
Nimesoma hizi Wikileak diplomatic cables na kuona JK anavyoingizwa sehemu mbalimbali na kujikuta ninajiuliza hilo swali. Sijui wengine mmeona pattern fulani au mmejiuliza swali au kupata majibu ya swali hilo?
Afadhali umeuliza wewe maanake wengine tukisema itaonekana tuna wivu, Wajamaa na wasiopenda maendeleo.
 
Msamehe bure FaizaFoxi, hili swala huenda analitazama kiimani zaidi na inamfanya apuuze na kucheka, hukumbuki Kiongozi wa dini aliyesema Kikwete anaandamwa kwasababu ya dini yake tuu na si kwamba ni kiongozi mbovu?

Sasa nimeelewa mkuu.Kwake hii ni issue mtambuka.
 
Wamarekani walianza hii effort kwetu in fifties.... it will take us 100 years kureverse walichofanya

FYI, hata rais ajaye atatoka kwenye "pot" yao tu... tutake tusitake

MTM

Mkuu I partially agree. However, ukiangalia Egypt; Mubarack alikuwa anashinda kila wakati kwasababu ya shinikizo la Wamarekani/kipenzi cha wamarekani. Pale wananchi waliposema hapana; ilibidi damu imwagike. Rais wa Syria naye nikipenzi cha wamarekani. Wananchi tukiamua tunaweza kabisa kukataa huu ukoloni, However; your statement will remain to be true mpaka watanzania tutakapoona umuhimu wakujitoa kwaajili ya nchi.
 
Mie nadhani Jk kajijenga mwenyewe na baadae alipopata umaarufu miaka ya mwanzoni ya 90 watu wengine wakatumia umaarufu wake kuongeza nguvu yake hawani pamoja na Lowasa, Rostam, AH Mwinyi (aliyepotezwa na Mkapa) na waandishi wa habari (ama kwa kujua au bila kujua) wote kwa pamoja wakaanza kuchafua washindani wengine na kumpamba yeye. Akakubalika sana 2005, lkn alishindwa kutimiza matamanio ya watu na hvyo kupoteza umaarufu hadi kupata kura chini ya 50% miaka mitano baadaye.
 
Unapenda sana kuchekacheka FF sijui kwa nini? issue sensitive kama hii wewe unacheka,umezisoma hizo cables MM anazozisema?Inasikitisha sana dada'etu,kama haujazisoma tafuta muda uzisome(hata kama zinakukera), utafakari....Utaelewa kwa nini MM kaanzisha huu uzi
<br />
<br />
kichwa chake kidogo ndo sabab
 
Ni Mkapa! Alikuwa na rais & mwenyekiti wa chama na angeweza kumpiga chini kama angeamua. Kwanza alimpa wizara rahisi (mambo ya nje kwa miaka 10). Angepewa wizara ngumu kwa muda wa kutosha udhaifu wake ungeonekana mapema

Hayo niliyopigia mstari yana ukweli asilimia 99.9.
Mkuu, umeweka ukweli wazi..
 
Back
Top Bottom