#COVID19 WHO: Maambukizi na vifo vya Corona vyapungua

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Shirika la Afya Duniani, WHO limesema idadi ya wagonjwa na vifo vitokanavyo na COVID-19 vimeendelea kupungua ulimwenguni katika wiki iliyopita.

WHO imesema leo kuwa zaidi ya visa milioni 3.6 na chini ya vifo 60,000 vimeripotiwa kati ya Septemba 13 na 19. Kupungua kwa kiasi kikubwa cha visa hivyo kumeripotiwa kwenye nchi za Mashariki mwa Mediterania na Kusini Mashariki mwa Asia.

WHO imesema idadi kubwa ya vifo vipya imeripotiwa Marekani, Urusi, Brazil na Mexico. Wakati huo huo, India imesema itaanza kutoa chanjo ya virusi vya corona kwa watoto wenye umri wa miaka 12 au zaidi kuanzia mwezi ujao.

Urusi kwa upande wake imetangaza kuwa takriban watu milioni 40 nchini humo wamepata chanjo kamili ya COVID-19.

Chanzo: DW Swahili
 
But we still have a long way to go in order to eliminate this PANDEMIC and go back to our normal life. Hopefully 🙏🏾 2022 will be much better when it comes to this PANDEMIC as compared to 2020 and 2021.
 
Tu dalili tumeanza kuja tena yani ni kama ka upepo kuna miezi itakandamiza tena
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Naam Mkuu sasa hivi nchi nyingi za MABEBERU zinaelekea kipindi cha baridi na wataalamu wa magonjwa kama haya wametabiri kwamba idadi ya maambukizi na vifo kutokana na COVID-19 wakati wa msimu wa baridi itaongezeka sana.

Tu dalili tumeanza kuja tena yani ni kama ka upepo kuna miezi itakandamiza tena
 
Shirika la Afya Duniani, WHO limesema idadi ya wagonjwa na vifo vitokanavyo na COVID-19 vimeendelea kupungua ulimwenguni katika wiki iliyopita.

WHO imesema leo kuwa zaidi ya visa milioni 3.6 na chini ya vifo 60,000 vimeripotiwa kati ya Septemba 13 na 19. Kupungua kwa kiasi kikubwa cha visa hivyo kumeripotiwa kwenye nchi za Mashariki mwa Mediterania na Kusini Mashariki mwa Asia.

WHO imesema idadi kubwa ya vifo vipya imeripotiwa Marekani, Urusi, Brazil na Mexico. Wakati huo huo, India imesema itaanza kutoa chanjo ya virusi vya corona kwa watoto wenye umri wa miaka 12 au zaidi kuanzia mwezi ujao.

Urusi kwa upande wake imetangaza kuwa takriban watu milioni 40 nchini humo wamepata chanjo kamili ya COVID-19.

Chanzo: DW Swahili

Habari mbaya sana kwa wapinga chanjo wanaposikia msisitizo kuwa kwenye chanjo.
 
Back
Top Bottom