Gottee
R I P
- Sep 7, 2008
- 174
- 1
Wana JF,
Taarifa nilizonazo ni kuwa CCM imetwaa Majimbo mawili ambayo CHADEMA ilikuwa ikitegemea kuyatwaa. La kwanza ni lile la Mbeya Vijijini ambalo lilikuwa linagombwa na Shitambala (CHADEMA) na Mchungaji Mwanjali (CCM) Mchungaji Mwanjali amefanikiwa kutetea kiti chake. Lingine ni lile lililokuwa likigombwa na Siame, inasemekana nalo CCM (Siame) wametwaa.
Kinachowashangaza wengi hapa ni ujio wa Kingunge Ngombale Mwiru wa ghafla hapa Mbeya. Habari zingine zinasemwa Shitambala ameuza Jimbo hilo kama alivyofanya kwenye ule uchaguzi mdogo. Habari zinaendelea kusema 'Wazito' wa CCM pia walikutanishwa na Mr Sugu na kuahidi kumfungia donge nono, Mr Sugu aidha kwa kusoma alama za nyakati au kwa uzalendo wake aliwatolea nje. Jana tumeshuhudia Mabomu ya Machozi zaidi ya 50 yakivurumishwa na mengine yameendelea kusikika hata leo asubuhi.
Ninachojiuliza kuna haja ya kusema Kikwete atapoteza Urais wake au ni kutaka kujua Asilimia atakazoshinda? 45 au 60 au 80 au 100 kabisa?
Yale niliyokuwa nayafikiria ndiyo haya. Watanzania tujiandae kukaa bila Utawala kwa miaka mingine mitano.
Nyerere uko wapi? Machozi ya samaki yamekwenda na maji!
Taarifa nilizonazo ni kuwa CCM imetwaa Majimbo mawili ambayo CHADEMA ilikuwa ikitegemea kuyatwaa. La kwanza ni lile la Mbeya Vijijini ambalo lilikuwa linagombwa na Shitambala (CHADEMA) na Mchungaji Mwanjali (CCM) Mchungaji Mwanjali amefanikiwa kutetea kiti chake. Lingine ni lile lililokuwa likigombwa na Siame, inasemekana nalo CCM (Siame) wametwaa.
Kinachowashangaza wengi hapa ni ujio wa Kingunge Ngombale Mwiru wa ghafla hapa Mbeya. Habari zingine zinasemwa Shitambala ameuza Jimbo hilo kama alivyofanya kwenye ule uchaguzi mdogo. Habari zinaendelea kusema 'Wazito' wa CCM pia walikutanishwa na Mr Sugu na kuahidi kumfungia donge nono, Mr Sugu aidha kwa kusoma alama za nyakati au kwa uzalendo wake aliwatolea nje. Jana tumeshuhudia Mabomu ya Machozi zaidi ya 50 yakivurumishwa na mengine yameendelea kusikika hata leo asubuhi.
Ninachojiuliza kuna haja ya kusema Kikwete atapoteza Urais wake au ni kutaka kujua Asilimia atakazoshinda? 45 au 60 au 80 au 100 kabisa?
Yale niliyokuwa nayafikiria ndiyo haya. Watanzania tujiandae kukaa bila Utawala kwa miaka mingine mitano.
Nyerere uko wapi? Machozi ya samaki yamekwenda na maji!