Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,360
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amemjia juu mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach kwa kumtaka aende mahakamani haraka na kwamba haogopi vitisho.
Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka alisema hayupo tayari kumuomba radhi na kwamba, fedha alizotaka alipwe kama fidia ya kuchafuliwa, hatazilipa.
Alisema yupo tayari kupelekwa mahakamani na kwamba, haogopi vitisho kwani anachokijua ni kwamba, sheria itafuata mkondo wake na si vinginevyo.
Profesa Tibaijuka alisema maamuzi ya mmiliki huyo anayaheshimu kwani ana haki kwenda kumshtaki mahakamani.
Alisema taarifa iliyotolewa na Muccadam kwenye vyombo vya habari inayodai kuwa tayari amemuandikia barua, haina ukweli kwani hadi sasa hajaipata.
Unajua huu mkasa haupo kwake peke yake. Ni watu wengi umewakuta. Ila yeye anataka kujifanya kama ni mtu special (maalum). Jambo hilo haliwezekani. Sheria itachukua mkondo wake, alisema Profesa Tibaijuka.
Alisema kiwanja hicho namba 1006, kina miaka zaidi ya 30 na kwamba, viongozi waliomaliza muda wao waliwahi kusema kuwa ni cha umma ila yeye anataka kutumia nguvu.
Alisisitiza kuwa maeneo yote, ambayo ni mali ya umma yaliyonunuliwa na watu binafsi, lazima serikali itayarudisha.
Alisema upangaji wa miji unatakiwa nidhamu na kusisitiza kuwa kesi ya kiwanja hicho ni rahisi sana.
Profesa Tibaijuka alisema atafanya kazi kwa mujibu wa ramani iliyopangwa kwani hiyo ni moja ya kazi zake.
Mwanzoni mwa wiki hii, Profesa Tibaijuka alifanya ziara kuzungukia maeneo ya umma na kubaini viwanja vya Ocean Road na Palm Beach vikiwa vimejengwa na kuagiza vibomolewe haraka kutokana na kuwa mali ya umma.
Hata hivyo, mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach, alikaidi agizo hilo, badala yake alimpa waziri huyo siku saba kumuomba radhi kwa madai ya kumchafulia jina kwa kuambiwa amenunua kiwanja cha umma kwa njia za kinyemela.
Pia alimtaka waziri huyo kumlipa Sh. bilioni 2 na kutishia kwamba, atampeleka mahakamani asipotekeleza mambo hayo.
CHANZO: NIPASHE
Mucadam ni nani, kwa nini atake special treatment?
Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka alisema hayupo tayari kumuomba radhi na kwamba, fedha alizotaka alipwe kama fidia ya kuchafuliwa, hatazilipa.
Alisema yupo tayari kupelekwa mahakamani na kwamba, haogopi vitisho kwani anachokijua ni kwamba, sheria itafuata mkondo wake na si vinginevyo.
Profesa Tibaijuka alisema maamuzi ya mmiliki huyo anayaheshimu kwani ana haki kwenda kumshtaki mahakamani.
Alisema taarifa iliyotolewa na Muccadam kwenye vyombo vya habari inayodai kuwa tayari amemuandikia barua, haina ukweli kwani hadi sasa hajaipata.
Unajua huu mkasa haupo kwake peke yake. Ni watu wengi umewakuta. Ila yeye anataka kujifanya kama ni mtu special (maalum). Jambo hilo haliwezekani. Sheria itachukua mkondo wake, alisema Profesa Tibaijuka.
Alisema kiwanja hicho namba 1006, kina miaka zaidi ya 30 na kwamba, viongozi waliomaliza muda wao waliwahi kusema kuwa ni cha umma ila yeye anataka kutumia nguvu.
Alisisitiza kuwa maeneo yote, ambayo ni mali ya umma yaliyonunuliwa na watu binafsi, lazima serikali itayarudisha.
Alisema upangaji wa miji unatakiwa nidhamu na kusisitiza kuwa kesi ya kiwanja hicho ni rahisi sana.
Profesa Tibaijuka alisema atafanya kazi kwa mujibu wa ramani iliyopangwa kwani hiyo ni moja ya kazi zake.
Mwanzoni mwa wiki hii, Profesa Tibaijuka alifanya ziara kuzungukia maeneo ya umma na kubaini viwanja vya Ocean Road na Palm Beach vikiwa vimejengwa na kuagiza vibomolewe haraka kutokana na kuwa mali ya umma.
Hata hivyo, mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach, alikaidi agizo hilo, badala yake alimpa waziri huyo siku saba kumuomba radhi kwa madai ya kumchafulia jina kwa kuambiwa amenunua kiwanja cha umma kwa njia za kinyemela.
Pia alimtaka waziri huyo kumlipa Sh. bilioni 2 na kutishia kwamba, atampeleka mahakamani asipotekeleza mambo hayo.
CHANZO: NIPASHE
Mucadam ni nani, kwa nini atake special treatment?