who is this muccadam?????????

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,360
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amemjia juu mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach kwa kumtaka aende mahakamani haraka na kwamba haogopi vitisho.
Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka alisema hayupo tayari kumuomba radhi na kwamba, fedha alizotaka alipwe kama fidia ya kuchafuliwa, hatazilipa.
Alisema yupo tayari kupelekwa mahakamani na kwamba, haogopi vitisho kwani anachokijua ni kwamba, sheria itafuata mkondo wake na si vinginevyo.
Profesa Tibaijuka alisema maamuzi ya mmiliki huyo anayaheshimu kwani ana haki kwenda kumshtaki mahakamani.
Alisema taarifa iliyotolewa na Muccadam kwenye vyombo vya habari inayodai kuwa tayari amemuandikia barua, haina ukweli kwani hadi sasa hajaipata.
“Unajua huu mkasa haupo kwake peke yake. Ni watu wengi umewakuta. Ila yeye anataka kujifanya kama ni mtu special (maalum). Jambo hilo haliwezekani. Sheria itachukua mkondo wake,” alisema Profesa Tibaijuka.
Alisema kiwanja hicho namba 1006, kina miaka zaidi ya 30 na kwamba, viongozi waliomaliza muda wao waliwahi kusema kuwa ni cha umma ila yeye anataka kutumia nguvu.
Alisisitiza kuwa maeneo yote, ambayo ni mali ya umma yaliyonunuliwa na watu binafsi, lazima serikali itayarudisha.
Alisema upangaji wa miji unatakiwa nidhamu na kusisitiza kuwa kesi ya kiwanja hicho ni rahisi sana.
Profesa Tibaijuka alisema atafanya kazi kwa mujibu wa ramani iliyopangwa kwani hiyo ni moja ya kazi zake.
Mwanzoni mwa wiki hii, Profesa Tibaijuka alifanya ziara kuzungukia maeneo ya umma na kubaini viwanja vya Ocean Road na Palm Beach vikiwa vimejengwa na kuagiza vibomolewe haraka kutokana na kuwa mali ya umma.
Hata hivyo, mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach, alikaidi agizo hilo, badala yake alimpa waziri huyo siku saba kumuomba radhi kwa madai ya kumchafulia jina kwa kuambiwa amenunua kiwanja cha umma kwa njia za kinyemela.
Pia alimtaka waziri huyo kumlipa Sh. bilioni 2 na kutishia kwamba, atampeleka mahakamani asipotekeleza mambo hayo.



CHANZO: NIPASHE

Mucadam ni nani, kwa nini atake special treatment?
 
Ni muhindi mmoja ambaye anayejua haki hupatikana mahakamani.
Tatizo la mawaziri wetu wanapenda maigizo sana,sikuona haja ya waziri kutembelea maeneo ya wazi ili kutoa tamko la serikali,anataka kuonekana mkali?hajui kuna watu ni wabishi by nature.huyo muhindi alishatambua kile kinachoitwa "worst case cenario"hivyo anafurahia jazba za Tibaijuka.
Ushauri wa bure kwa mawaziri;wajitahidi kuwa execative zaidi mfano Tibaijuka angeweza kuwaita (mara moja) watu waliochukua maeneo ya wazi na kuwaamuru kuyarejesha tuseme ndani ya siku 7(kumbuka enzi za mrema)
huu ndo ubaya wa kuchakachua serikali haitaheshimiwa kamwe!
 
Hawa watu wamezoea kutumia mahakama kuvunja taratibu kwa sababu ya pesa zao, dawa ya watu hawa ni 'dark justice' tu!
 
Ni muhindi mmoja ambaye anayejua haki hupatikana mahakamani.
Tatizo la mawaziri wetu wanapenda maigizo sana,sikuona haja ya waziri kutembelea maeneo ya wazi ili kutoa tamko la serikali,anataka kuonekana mkali?hajui kuna watu ni wabishi by nature.huyo muhindi alishatambua kile kinachoitwa "worst case cenario"hivyo anafurahia jazba za Tibaijuka.
Ushauri wa bure kwa mawaziri;wajitahidi kuwa execative zaidi mfano Tibaijuka angeweza kuwaita (mara moja) watu waliochukua maeneo ya wazi na kuwaamuru kuyarejesha tuseme ndani ya siku 7(kumbuka enzi za mrema)
huu ndo ubaya wa kuchakachua serikali haitaheshimiwa kamwe!

Kama anajua sheria, mbona nasoma kuwa anatembea na barua za ikuluzinazohimiza apewe kiwanja badala ya hukumu za mahakama. Ikulu na viwanja wapi na wapi.
 
Kama anajua sheria, mbona nasoma kuwa anatembea na barua za ikuluzinazohimiza apewe kiwanja badala ya hukumu za mahakama. Ikulu na viwanja wapi na wapi.
Mkuu, hivi hujui kuwa nchi hii yeyote mwenye cheo kikubws ana uhuru wa kufanya lolote alitakalo? Ndio maana unaona hizo barua za ikulu za kugawa viwanja
 
Kama anajua sheria, mbona nasoma kuwa anatembea na barua za ikuluzinazohimiza apewe kiwanja badala ya hukumu za mahakama. Ikulu na viwanja wapi na wapi.

Usituambie kuwa Mkwere naye anaandika barua za kugawa viwanja! Makubwa haya! Ama kweli Tz mna Rahisi!!
 
Tibaijuka kaza buti usonge mbele. Tunataka tuone utendaji wa mahakama zetu na nguvu ya pesa.
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amemjia juu mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach kwa kumtaka aende mahakamani haraka na kwamba haogopi vitisho.
Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Profesa Tibaijuka alisema hayupo tayari kumuomba radhi na kwamba, fedha alizotaka alipwe kama fidia ya kuchafuliwa, hatazilipa.
Alisema yupo tayari kupelekwa mahakamani na kwamba, haogopi vitisho kwani anachokijua ni kwamba, sheria itafuata mkondo wake na si vinginevyo.
Profesa Tibaijuka alisema maamuzi ya mmiliki huyo anayaheshimu kwani ana haki kwenda kumshtaki mahakamani.
Alisema taarifa iliyotolewa na Muccadam kwenye vyombo vya habari inayodai kuwa tayari amemuandikia barua, haina ukweli kwani hadi sasa hajaipata.
“Unajua huu mkasa haupo kwake peke yake. Ni watu wengi umewakuta. Ila yeye anataka kujifanya kama ni mtu special (maalum). Jambo hilo haliwezekani. Sheria itachukua mkondo wake,” alisema Profesa Tibaijuka.
Alisema kiwanja hicho namba 1006, kina miaka zaidi ya 30 na kwamba, viongozi waliomaliza muda wao waliwahi kusema kuwa ni cha umma ila yeye anataka kutumia nguvu.
Alisisitiza kuwa maeneo yote, ambayo ni mali ya umma yaliyonunuliwa na watu binafsi, lazima serikali itayarudisha.
Alisema upangaji wa miji unatakiwa nidhamu na kusisitiza kuwa kesi ya kiwanja hicho ni rahisi sana.
Profesa Tibaijuka alisema atafanya kazi kwa mujibu wa ramani iliyopangwa kwani hiyo ni moja ya kazi zake.
Mwanzoni mwa wiki hii, Profesa Tibaijuka alifanya ziara kuzungukia maeneo ya umma na kubaini viwanja vya Ocean Road na Palm Beach vikiwa vimejengwa na kuagiza vibomolewe haraka kutokana na kuwa mali ya umma.
Hata hivyo, mmiliki wa kiwanja cha Palm Beach, alikaidi agizo hilo, badala yake alimpa waziri huyo siku saba kumuomba radhi kwa madai ya kumchafulia jina kwa kuambiwa amenunua kiwanja cha umma kwa njia za kinyemela.
Pia alimtaka waziri huyo kumlipa Sh. bilioni 2 na kutishia kwamba, atampeleka mahakamani asipotekeleza mambo hayo.



CHANZO: NIPASHE

Mucadam ni nani, kwa nini atake special treatment?

He is just a pain in the ass like Rostam Aziz
 
Back
Top Bottom