Waterbender
JF-Expert Member
- Oct 2, 2018
- 6,697
- 8,499
Nashukuru mmkubwaSUV ni gari ya abiria na siyo mizigo yenye 4WD na umbo linaloiruhusu kwenda off road.
SUV huwa na nafasi kubwa kutoka aridhini mpaka body linapoanzia ukilinganisha na magari mengine. Huwa na muundo ambao mbele kabisa kuna bonet ambalo ndani yake hukaa injini kisha hufuatiwa na sehemu yenye nafasi kubwa ya kukaa abiria. Body lake hujengwa juu ya chasis japo kuna baadhi ya category body haina chasis.
Hizi gari hazina mkia kama zilivyo sedan kwahivyo siti za nyuma hukunjwa kwa ajili ya vijimizigo mfano cruiser hardtop na zingine huwa na kijinafasi kidogo kwa ajili ya tumizigo twa kawaida.
Kuna category kibao za SUV ila nakutajia mifano yake kwa ujumla tu, mifano hiyo ni
-land cruiser (gx, vx, prado )
- Nissan (patrol, safari, xtrail )
-Range rover (defender, discovery, velar )
-GMC (yukon denali )
-Lincoln navigation
-cadillac escalade
-chevrolet (trail blazer, tahoe, suburban )
-dodge (calliber, nitro )
Just to mention few mkuu, hope umepata mwanga