Who is superpower in EAC? TZ or Kenya?

RUTAJUMBUKIRWA

Senior Member
May 3, 2009
185
89
Wanajamii,
Kila ukanda una nchi ambayo inachuliwa kama super power. Mfano S.Africa ni top kwa ukanda wa southern, Egypt north, nigeria West Africa na Angola Central Africa.

Sasa ndani ya jumuiya ya Africa Mashariki nani zaid? Wanansema Kenya je ni kweli? na tutumie vigezo gani ku-grade nchi.
 
Suala la pembe za ndovu ndio litaamua nani ni superpower kwa nguvu ya hoja. Maana hapa nguvu ya hoja ni kutetea maslahi yote y a kiuchumi ya nchi husika.

Hivyo nchi itakayokuwa kila mara ina tetea maslahi yake ya kiuchumi kwa 'nguvu ya hoja' maana kila wakati kutaibuka masuala ya 'kutetea uchumi wa nchi husika' inabidi Tanzania ione mbali na kuwa na 'mangi-meza' (bureaucrats) wengi ambao ni pro-active ktk kutetea masuala ya ardhi, ajira,utalii, viwanda, biashara, madini, mashirika/kampuni za kitanzania, maliasili n.k
 
Sijui swali lako linalenga wapi. Kama unazungumzia muktadha wa EAC suala muhimu si nani economic powe house. Suala muhimu ni kwamba kila nchi itafaidika vipi na mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi (economic integration) uliopo. Kwa uelewa wangu ambao kila nchi ina fursa ya kufaidika na EAC. Mjadala wa nani mkubwa, nani wa kati na nani mdogo hauwezi kutusaidia. Na kwa kuwa ushirikiano huu ni private-sector driven, wewe kama unaweza kuuza karanga, njugu, etc, kwa nchi nyingine, uza. Kila mmoja akifanya hivyo sote kama wantanzania tutafidika. Binafsi namfahamu kijana mmoja kutoaka Mwanza ambaye ana kiwanda mwaka 2005 alikuwa na kiwanda kidogo cha kutengeneza pipi. Mwaka huo huo alithubutu kuingia soko la Kenya, soko ambalo wabongo wengi wanaliogopa. Huyu kijana alifanikiwa sana na sasa si mwenzetu tena. Ameisha move to next level. Tuache mijadala tufanye kazi.
 
Kwa mifano hiyo aliyoitaja anamaanisha kiuchumi, hakuna sababu za kuhit arround the bush Kenya wapo mbali saana ni EASTAFRICA
 
bila kupoteza muda na kufinyangafinyanga maneno wala kujipendelea, Kenya wapo juu mkuu
 
Naona ni kichekesho kidogo kuita nchi kama Tanzania, Kenya au Angola "superpower". Zote ni nchi hafifu zilizopo mbele katika ufisadi, mashimo barabarani na utendaji hovyo serikalini.

Hata Nigeria ni superpower namna gani? Wana mafuta hivyo kuna pesa kiasi lakini ufisadi tele na vita za wenyewe kieneo. "Super" walikuwa matapeli wa Nigeria walipoanza kufanya mambo yao kwa njia ya Email na kuwakamua watu kote duniani ila tu siku hizi kuna wengine pia. ("mimi mjane wa rais marehemu nataka kupeleka pesa za siri nje unisaidie kwa kunipa akaunti yako utapata nusu ya bilioni...)

Naona mchangiaji alisema vema akiandika swali la pekee ni je nchi gani ina nguvu zaidi kiuchumi katika Afrika Mashariki maana hii muhimu kwa maendeleo si verma kuwa na tofauti kubwa mno katika ushirikiano.
 
Here we go again.
Maneno mengi hayavunji mfupa, let's all get to work, tufikishe nchi zetu tunapotaka ziwe, it begins with YOU.
 
south africa ni super power
africa nzima.
asilimia 48 ya uchumi wa africa ni wao.

tanzani itakuwa the largest economy in just three years
from now.

Huu ni utabiri au ni nini Mkuu? Yaani umeegemea kwenye Economic Analyisis yoyote au ni siasa siasa zaidi?

Kwanza naomba nikutahadharishe tu kuwa Kenya wameanza kuwekeza kwa wananchi wao kielimu, kitaaluma zaidi kwa miaka sasa na wanaendelea, wapo watu kule wanaothubutu wengi sana na wenye "skills" maradufu ya Tz. Sasa hii miaka mitatu ninayoona watoto wetu wanakimbia Hisabati, Kemia na Fizikia ndiyo indicator kweli? Ninawasiwasi kama itatokea tutakuwa tumedanganywa ili tulewe halafu wachukue wengine na ndiyo itakuwa mwisho wetu! Chunguza sana utagundua kuwa biashara nyingi hapo zinaendeshwa kwa "remote control" kutoka Kenya.
Bado hatujaamka Mkuu!
 
...Duh wabongo kwa porojo,kila mtu kapiga kona kutokujibu swali hakuna aliyejibu direct swali lilivyoulizwa...
....well sina uhakika na super power lakini nadhani Kenya wana nguvu sana kiuchumi lakini Tanzania wanatamba katika nyanja ya kimataifa kutokana na nguvu yake kisiasa.position ya Tz kisiasa nje ya mipaka yetu nadhani ina ushawishi mkubwa zaiidi kuliko nchi yeyote ya EA....
 
I think Kenya are the leading one,provided they have many industries thus they are exporting alot in EAC mkt,also many companies operating in Tz ar Kenyan oriented even though they are in Tz(means the owners),also there economy provides enough revenue to run there expenditures unlike other EA countries which are donor oriented to cover there deficit budget.
 
Uganda nao wanatupita soon,sisi tumebakia madharau tu na uchumi wa vitabuni!!wenzetu value for money,uchumi halisia wanasonga mbele!!
 
Wanajamii,
Kila ukanda una nchi ambayo inachuliwa kama super power. Mfano S.Africa ni top kwa ukanda wa southern, Egypt north, nigeria West Africa na Angola Central Africa.

Sasa ndani ya jumuiya ya Africa Mashariki nani zaid? Wanansema Kenya je ni kweli? na tutumie vigezo gani ku-grade nchi.

kweli niseme Angola iko southern sub-saharan not central na katika south African area SA ndio magwiji kule. huku ni kenya yaongoza, ethopia, halfu tanzania
 
ukweli ni kwamba, africa tuna matatizo yanayofanana sana. Lakini Kenya inakwenda vizuri, na ilianza zamani sana. Uganda na Rwanda wanafuata. Tz na Burundi tuko mwisho. Angalia kigezo kimoja tu cha elimu kwa watoto wa shule ya msingi utapata majibu. Kimsingi hatuwekezi katika elimu hapa tz kiasi kwamba leo necta hata hawajui cha kufanya. nchi moja inamifumo tofauti ktk mitaala yetu. hata miaka mia ijayo kama hali haibadirishwi hapa tz tutazidiwa na nchi zote.
 
1.SISI NI SUPER POWER KATIKA KUPIGA POROJO ZA KISIASA
2. SISI NI SUPER POWER KATIKA UCHAKACHUAJI WA KURA
3. SISI NI SUPER POWER KATIKA KUOMBA OMBA MIASAADA NJE WAKATI (sisi si super power kwa mali asili)
4. SISI NI SUPERPOWER KWA ELIMU DUNI
5. SISI NI SUPER POWER KATIKA KUDAI KISWAHILI KITUMIKE MPAKA CHUO KIKUKUU WAKATI DUNIA INAKUWA KIJIJI
6. SISI NI SUPER POWER KATIKA KUDANGANYWA NA T-SHIRTS NA KANGA NA PILAU WAKATI WA UCHAGUZI AFU TUNACHAGUA MAKAPI NA MAFISADI KISHA TUNAGEUKA KUWA SUPERPOWER KATIKA KULALAMIKA HALI YA UCHUMI
 
nikisoma thread hii moyo unaniuma...ngoja niondoke zangu nipishe muendelee.
 
I like the mentality of the Boss, ambition is what spurs humanity on
 
Back
Top Bottom