Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
- Thread starter
- #101
Rev Kishoka:
Kwanza ningependa kukukosoa. Hakuna kitu cha bure. Vile vile misingi ya Ujamaa au usoshalisti haisemi kuwa
elimu au huduma za afya zitolewe bure.
Ujamaa na usoshalisti vyazo vyake ni umilikaji wa mitaji na mgawanyo wa mapato. Elimu iliyotolewa bure ilikuwa ni
sehemu ya mgawo wa mapato.
Lawama alizopata Nyerere ni sahihi kabisa. Kama elimu au huduma za afya ni sehemu ya mgawo wa mapato, je ni juhudi
gani watanzania walifanya kustahili mgao huo?
Vitabu vya Nyerere vinasema juhudi za kazi za watanzania zitumike katika kutoa elimu au kupata huduma za jamii. Lakini
hayo yaliishia vitabuni. Kwenye utendaji huduma zilitegemea mikopo na misaada kutoka kwa wahisani.
Mnaopiga kelele kutetea Nyerere kwa kutoa elimu ya bure naomba mtueleze ni vitu gani vilifanyika Tanzania kuweza kutoa elimu
ya bure. Watu hamna aibu kuona taifa mpaka leo linategemea misaada kutoka nje.
Zakumi,
Hakuna ambaye amesema kuwa Nyerere hakufanya makosa! Hata yeye mwenyewe alikiri hilo!
Sasa naomba niuulize, tukufanye wewe ni Rais wetu wa kwanza na ndio tumepata Uhuru, nchi ni changa, elimu na afya ni finyu na haba na hauna watu mahiri wa kutosha. Zaidi unabeba mzigo ulioachiwa na mtawala.
What would have Zakumi done? Tupe basi Manifesto yako ya ni jinsi gai ambavyo tungejenga Taifa letu na kuachana na utegemezi wa misaada.