Who influenced Nyerere: His Ujamaa Philosophy and Azimio Principles?

WildCard said:
Someni yote aliyoyaandika Mwalimu; sikilizeni hotuba zake zinazoendelea kurushwa na redio yetu ya Taifa; mtagundua kwamba akili na mawazo ya Mwalimu vilikuwa vya kwake mwenyewe na aliweza kuyasimamia vizuri yale yote aliyoyaona ni sahihi na ya MSINGI kwa TAIFA letu.Angalieni mifano hapa kwa majirani zetu tu. Mtu anakuwa maarufu kwa sababu ya KABILA yake, DINI yake, UTAJIRI wake,... Rais anahutubia watu wake kupitia wakalimani...

WildCard,

..tumeishi wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere. we have first hand experience ya matokeo ya utekelezaji wa mawazo yake.

..halafu wakati wa harakati za kupigania Uhuru, Mwalimu alilazimika kutumia mkalimani ktk mikutano ya hadhara mara mbili. ilitokea ktk maeneo ya mwanza na mbulu.

..sasa utaona kwamba hata wakati wa mkoloni Mwingereza Kiswahili kilikuwa kimesambaa maeneo mengi mno. ukweli huo unapingana na ile dhana kwamba Mwalimu Nyerere ndiye aliyekikuza kiswahili Tanzania.
 
WildCard,

..tumeishi wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere. we have first hand experience ya matokeo ya utekelezaji wa mawazo yake.

..halafu wakati wa harakati za kupigania Uhuru, Mwalimu alilazimika kutumia mkalimani ktk mikutano ya hadhara mara mbili. ilitokea ktk maeneo ya mwanza na mbulu.

..sasa utaona kwamba hata wakati wa mkoloni Mwingereza Kiswahili kilikuwa kimesambaa maeneo mengi mno. ukweli huo unapingana na ile dhana kwamba Mwalimu Nyerere ndiye aliyekikuza kiswahili Tanzania.

jokaKuu,
Serikali ya Nyerere isingechukua uamuzi wa kukifanya Kiswahili lugha ya taifa yale maeneo unayoyataja yangeendelea kuhitaji wakalimani kwa sababu kusingekuwepo juhudi zozote za kukiendeleza Kiswahili. Waulize Wakenya.
 
Jasusi said:
Serikali ya Nyerere isingechukua uamuzi wa kukifanya Kiswahili lugha ya taifa yale maeneo unayoyataja yangeendelea kuhitaji wakalimani kwa sababu kusingekuwepo juhudi zozote za kukiendeleza Kiswahili. Waulize Wakenya.

Jasusi,

..kwanza kuna ile dhana kwamba, Mwalimu kwa juhudi zake binafsi ndiye aliyewezesha kiswahili kuenea Tanzania nzima. hilo siyo kweli.

..Kiswahili kilikuwa lugha ya uchumi na biashara. yeyote yule aliyehitaji ku-interact na jamii nyingine za Tanganyika alilazimika kujifunza kiswahili. kilisambaa Tanganyika yote bila kuundiwa sheria ya kukifanya kuwa lugha ya taifa.

..Mwalimu anaweza kupewa sifa kwa kukitambua kiswahili, na kukipa hadhi lugha ya taifa. lakini hilo la kumkweza, na kudai kwamba yeye ndiye aliyekisambaza, na kukipa umaarufu Kiswahili, ni dhana ya kutiliwa mashaka kidogo.

NB:

..kama Kiingereza kingekuwa kinazungumzwa na wa-Tanganyika wengi kuliko Kiswahili, basi naamini kabisa kingeendelea kuwa "lugha ya taifa."
 
Fortunately you do not have monopoly on the truth, do you? Hii dhana ya kuita maoni ya wengine uwongo ni dhana muflisi.

Hakuna nilichodai hapo ambacho hakina uthibitisho.

Nimeweka vielelezo vya wanaojua kuliko mimi, wasomi wanaonizidi, maandishi ya waliofanyiwa huo unduli wa mawazo (kama sio unduli period) na J.K. Nyerere, na watafiti waliompenda J.K. Nyerere.

Sasa wewe ukija hapa kutuambia eti Mzee Bomani kakwambia J.K. Nyerere alikuwa anasikia ya watu isipokuwa tatizo ni kwamba Watanzania wenzake walikuwa hawawezi kujenga hoja huko ni kupumbazika (hoodwinked).

Utanambiaje Nyerere alikuwa haogopi hoja za wengine wakati Mwanasheria Mkuu mstaafu katika kongamano la Tanganyika Law Society anatoa hotuba kujadili kuboreshwa kwa Katiba, kutoka hapo Mwanasheria Mkuu J.S. Warioba anaagiza awekwe kizuizini, na J.K. Nyerere kweli nae anatia saini preventive detention order ? (2)

Mbunge Eli Anangisye, anaongea bungeni kuhusu fiscal policy ya Nchi, anatoka hapo anakamatwa ! Ndugu zangu, umesikia hilo, kuchangia kikao cha bajeti Bungeni! (3)

Hebu imagine! Sekunde mbili, u pose u imagine. Mbunge! Sisemi waliotuhumiwa na uhani, sijui Bibi Titi, sisemi Otini Kambona, na McGhee na Mattaka na Banyikwa. No, wabunge wanaochangia bajeti!

"At a meeting of the National Executive Committee held in Tanga last October, nine TANU members were expelled. They included ...the former TANU Youth League Secretary and MP, Mr. E. Anangisye , who was in detention and apparently was closely connected with Kambona. The other seven who were expelled were all Members of Parliament who had been outspoken on various issues. Two had objected to the way that Ujamaa villages were being set up in their region, West Lake; another had complained about lack of freedom within the party and had objected to the failure of Zanzibar to carry out elections. The MPs who were expelled lost their seats in the National Assembly. They were not accused of specific violations of the Arusha provisos on economic accumulation but were said by party newspaper to have "grossly violated the Party creed both in their actions and attitudes, all of which sum up to a very clear opposition to the Party and its policies."( 1 )

Nimesema siwezi kufunga kamba za viatu vya Nyerere, lakini, tusiongopeane kuhusu yaliyojiri. Tusishtuke tukisikia mtu anasema hero fulani sio hero, au hakupata sifa fulani tulizodhani kapata. Ndio nchi nyingine zilivyoendelea hivyo, kutoogopa kuchambuana na kukosoana na kuambiana ukweli. Ndiko tunakokwenda huko, na watu watazidi kuongezeka Tanzania wanaosema kuwa mambo sio kama, na hayakuwahi kuwa kama, tulivyoimbishwa toka utotoni. Msiogope ukweli!

( 1 ) Foreign Affairs; April 1969 Edition; pg. 545-

(2) Chris Maina Peter; Incarcerating the Innocent: Preventive Detention in Tanzania; 1997 The Johns Hopkins University Press, Human Rights Quarterly 19.1 (1997) 113-135

(3 )Raymond F. Hopkins, The role of an MP in Tanzania, Swarthmore College; Ludovick S Mwijage, The dark side of Nyerere's Legacy;
 
Kuhani,Kishoka,Jasusi,Mwanakijiji,

..naona Jenereli Ulimwengu naye anatoa mawazo yake hapa kuhusu Azimio na mazingira ya kisiasa wakati wa serikali ya awamu ya kwanza.

Jenerali Ulimwengu said:
..Azimio la Arusha lenyewe lilikuwa kwa kiwango kikubwa ni azimio la Nyerere, ingawaje lilipitishwa na Halmashauri Kuu ya TANU, na kwa kuungwa mkono na maelfu ya Watanzania, likawa azimio la Watanzania wote.

..Ukweli ni kwamba hakukuwa na mjadala uliowahusisha wananchi (au hata wana-TANU) katika utungaji wa azimio lenyewe wala katika mbinu za utekelezaji wake.

..Mwaka 1968, tutakumbuka, walichomoza wabunge kadhaa waliotaka kufurukuta na kuihoji TANU ndani ya Bunge la chama kimoja. Alichofanya Nyerere ni ‘kuwashitaki' wabunge hao (Kaneno, Bakampenja, Choga, Masha, Anangisye, Mwakitwange) ndani ya vikao vya chama. Wakanyang'anywa uwanachama wa TANU, na hivyo wakapoteza ubunge.

..Huo ukawa ndio mwisho wa kutaka kuhoji cho chote ndani au nje ya TANU. Wengi wa wabunge hao machachari wa wakati huo wamekwisha kufariki (lakini walikuwa wamekwisha kufa kisiasa muda mrefu kabla ya kuaga dunia), ukimwacha Masha, ambaye sasa ni mbunge wa Afrika Mashariki baada ya miaka mingi ya kuishi uhamishoni-laini katika Umoja wa Mataifa.

Hakika ilianza kusadikika kwamba ukipata laana ya Kambarage ujue umemalizika kisiasa, imani ambayo imezidi kujengeka katika miaka ya karibuni.

Utamaduni ulioanzishwa wakati wa Nyerere umeendelea ndani ya chama-tawala kiasi kwamba majadiliano ni nadra sana, na mara nyingi mijadala huzuka ili kumshughulikia mtu fulani, na wala si kusaili hoja wala falsafa. Athari mojawapo ya utamaduni huo ni kwamba hivi sasa, Nyerere akiwa hayupo, hakuna kiongozi hata mmoja, hata wale waliokuwa safu ya mbele kabisa katika kuhubiri Ujamaa leo hii huwezi kuwatambua.

Hali hii ilianza kujitokeza hata wakati Mwalimu akiwa madarakani. Kadri umri ulivyoongezeka na nguvu za mwili kupungua ndivyo kasi ya kusimamia sera na utekelezaji wake ilivyoendelea kupungua, kiasi kwamba chama na sera zake vilianza kuonyesha uzee kadri nywele za Mwalimu zilizvyozidi kuwa nyeupe.

Katika hali ya kutokuwapo na mjadala, sera zilizolenga kumkomboa Mtanzania zikaishia kumletea matatizo ambayo yaliupa Ujamaa jina baya. Serikali ikajiingiza katika biashara isiyokuwa yake – kuuza nyama na chumvi; vyama vya ushirika vikavunjwa; serikali za mitaa zikafutwa, na kadhalika.
 
Kuhani,Kishoka,Jasusi,Mwanakijiji,

..naona Jenereli Ulimwengu naye anatoa mawazo yake hapa kuhusu Azimio na mazingira ya kisiasa wakati wa serikali ya awamu ya kwanza.

The Serpent Generale,

Unaweza kuiweka linki tuisome habari nzima?

Tukirudi kwenye hoja ya Jenerali Ulimwengu, swali linakuja, je kama Nyerere alicheza faulo, ni kwa nini basi walioadhirika au wenine ambao walikuwa kwenye kamati kuu au halmashauri kuu walikaa kimya na kuburuzwa na Nyerere?

Ni woga gani ambao watu wa TANU walikuwa nao kuwa walimwogopa mtu mmoja na huko wala si kumpa heshima?

Nyerere alikuwa na uwezo wa kushawishi watu, kwa hoja na si vitisho.

Something is wrong with the so called Politicians of Tanzania. No one is ready to stand up and get counted, always wishy washy and the Yes Sir mentatility is not Nyerere's fault.
 
Jasusi,

..kwanza kuna ile dhana kwamba, Mwalimu kwa juhudi zake binafsi ndiye aliyewezesha kiswahili kuenea Tanzania nzima. hilo siyo kweli.

..Kiswahili kilikuwa lugha ya uchumi na biashara. yeyote yule aliyehitaji ku-interact na jamii nyingine za Tanganyika alilazimika kujifunza kiswahili. kilisambaa Tanganyika yote bila kuundiwa sheria ya kukifanya kuwa lugha ya taifa.

..Mwalimu anaweza kupewa sifa kwa kukitambua kiswahili, na kukipa hadhi lugha ya taifa. lakini hilo la kumkweza, na kudai kwamba yeye ndiye aliyekisambaza, na kukipa umaarufu Kiswahili, ni dhana ya kutiliwa mashaka kidogo.

NB:

..kama Kiingereza kingekuwa kinazungumzwa na wa-Tanganyika wengi kuliko Kiswahili, basi naamini kabisa kingeendelea kuwa "lugha ya taifa."

jokaKuu,
Hapo nakubaliana na wewe. Mwalimu alitambua umuhimu wa Kiswahili kama lugha ya kuleta mshikamano Tanzania. Sidhani kuna mtu aliyesema kuwa Mwalimu ndiye aliyesambaza Kiswahili. Lakini serikali yake ilitambua umuhimu wa kuwepo lugha moja katika taifa lenye makabila zaidi ya 120. Kwa hiyo ikawa policy ya makusudi kuwa Kiswahili kiwe ndiyo lugha ya taifa. Tuendelee.
 
The Serpent Generale,

Unaweza kuiweka linki tuisome habari nzima?

Tukirudi kwenye hoja ya Jenerali Ulimwengu, swali linakuja, je kama Nyerere alicheza faulo, ni kwa nini basi walioadhirika au wenine ambao walikuwa kwenye kamati kuu au halmashauri kuu walikaa kimya na kuburuzwa na Nyerere?

Ni woga gani ambao watu wa TANU walikuwa nao kuwa walimwogopa mtu mmoja na huko wala si kumpa heshima?

Nyerere alikuwa na uwezo wa kushawishi watu, kwa hoja na si vitisho.
Something is wrong with the so called Politicians of Tanzania. No one is ready to stand up and get counted, always wishy washy and the Yes Sir mentatility is not Nyerere's fault.

Nadhani ni ile nidhamu yetu ya woga ndio iliofanya wengi wasithubutu kuzichallenge hoja za Nyerere hence kuaminika kuwa hoja zake ni kali. Pia sidhani katika nchi ya watu millioni 30 kusiwe na watu hata kumi wanaoweza kwenda toe to toe na Nyerere. Angalia jinsi watu wanavyojadiliana kwa uhuru hapa...enzi za Nyerere kulikuwa na uhuru kama huu kweli?
 
Joka, Jasusi,

Je hii inferiority complex ambayo tunaiona kutoka kwa Wanasiasa wetu na hata jamii kwa ujumla tuliitoa wapi? ni kutokana na Ukoloni au ni kitu ambacho hata kabla ya Ukoloni na utumwa tulikuwa nacho wakati wa machifu, watemi na watawala wa kale?

There is a need to weed out this serious and damaging complexity problem that has dwell amongst Tanzanians and so are Blacks in general!

Ninaposikia lawama kuwa Nyerere aliburuza najiuliza ni hivi, how did Mwalimu manage to manipulate all those brains, if we claim that he bullyied his way?
 
Hakuna nilichodai hapo ambacho hakina uthibitisho.

Nimeweka vielelezo vya wanaojua kuliko mimi, wasomi wanaonizidi, maandishi ya waliofanyiwa huo unduli wa mawazo (kama sio unduli period) na J.K. Nyerere, na watafiti waliompenda J.K. Nyerere.

Sasa wewe ukija hapa kutuambia eti Mzee Bomani kakwambia J.K. Nyerere alikuwa anasikia ya watu isipokuwa tatizo ni kwamba Watanzania wenzake walikuwa hawawezi kujenga hoja huko ni kupumbazika (hoodwinked).

Utanambiaje Nyerere alikuwa haogopi hoja za wengine wakati Mwanasheria Mkuu mstaafu katika kongamano la Tanganyika Law Society anatoa hotuba kujadili kuboreshwa kwa Katiba, kutoka hapo Mwanasheria Mkuu J.S. Warioba anaagiza awekwe kizuizini, na J.K. Nyerere kweli nae anatia saini preventive detention order ? (2)

Mbunge Eli Anangisye, anaongea bungeni kuhusu fiscal policy ya Nchi, anatoka hapo anakamatwa ! Ndugu zangu, umesikia hilo, kuchangia kikao cha bajeti Bungeni! (3)

Hebu imagine! Sekunde mbili, u pose u imagine. Mbunge! Sisemi waliotuhumiwa na uhani, sijui Bibi Titi, sisemi Otini Kambona, na McGhee na Mattaka na Banyikwa. No, wabunge wanaochangia bajeti!

At a meeting of the National Executive Committee held in Tanga last October, nine TANU members were expelled. They included ...the former TANU Youth League Secretary and MP, Mr. E. Anangisye , who was in detention and apparently was closely connected with Kambona. The other seven who were expelled were all Members of Parliament who had been outspoken on various issues. Two had objected to the way that Ujamaa villages were being set up in their region, West Lake; another had complained about lack of freedom within the party and had objected to the failure of Zanzibar to carry out elections. The MPs who were expelled lost their seats in the National Assembly. They were not accused of specific violations of the Arusha provisos on economic accumulation but were said by party newspaper to have "grossly violated the Party creed both in their actions and attitudes, all of which sum up to a very clear opposition to the Party and its policies."( 1 )

Nimesema siwezi kufunga kamba za viatu vya Nyerere, lakini, tusiongopeane kuhusu yaliyojiri. Tusishtuke tukisikia mtu anasema hero fulani sio hero, au hakupata sifa fulani tulizodhani kapata. Ndio nchi nyingine zilivyoendelea hivyo, kutoogopa kuchambuana na kukosoana na kuambiana ukweli. Ndiko tunakokwenda huko, na watu watazidi kuongezeka Tanzania wanaosema kuwa mambo sio kama, na hayakuwahi kuwa kama, tulivyoimbishwa toka utotoni. Msiogope ukweli!

( 1 ) Foreign Affairs; April 1969 Edition; pg. 545-

(2) Chris Maina Peter; Incarcerating the Innocent: Preventive Detention in Tanzania; 1997 The Johns Hopkins University Press, Human Rights Quarterly 19.1 (1997) 113-135

(3 )Raymond F. Hopkins, The role of an MP in Tanzania, Swarthmore College; Ludovick S Mwijage, The dark side of Nyerere's Legacy;

Sawasawa, na mimi nimeweka kumbukumbu zangu za mazungumzo na Mzee Bomani, lakini sijaita hoja zako uwongo. Huyu alifanya kazi na Mwalimu tangu enzi za TANU na alikuwa waziri mpaka kwenye utawala wa Mwinyi. Unaweza kudharau maoni yake kwa sababu zako mwenyewe lakini si kuita maoni ya wengine, hasa wale waliofanya kazi za karibu na Mwalimu kuwa waongo. Nitawasikiliza wasomi hoja zao na pia nitasikiliza hoja za wale waliofanya kazi kwa ukaribu na Mwalimu akiwemo Mkapa na Butiku, ambao wote nimezungumza nao sana. That is my point.
 
Nadhani ni ile nidhamu yetu ya woga ndio iliofanya wengi wasithubutu kuzichallenge hoja za Nyerere hence kuaminika kuwa hoja zake ni kali. Pia sidhani katika nchi ya watu millioni 30 kusiwe na watu hata kumi wanaoweza kwenda toe to toe na Nyerere. Angalia jinsi watu wanavyojadiliana kwa uhuru hapa...enzi za Nyerere kulikuwa na uhuru kama huu kweli?

Nyani,

I will be honest on this from a leadership perspective and my analysis of Tanzania history and what went through between 1962-1972.

Mwaka 1964 jeshi la Tanzania lilfanya maasi. Mwaka huo huo, Zanzibar kulitokea Mapinduzi.

Ukiangalia mazingira ya Afrika, tayari kulishaanza kutokea matatizo ya kisiasa na kuingiliwa na nchi za kigeni kama Marekani (Lumumba, Mashoeshoe nk.), mapinduzi na hata jitihada kujitenga.

Vitu kama hivi ni rahisi sana kuleta na kubadilisha sura ya nchi na hata kujenga hofu kwa walioko madarakani.

Sasa kama wale waliokuwa wanampinga Nyerere hawakuweza kujenga hoja zao kusimama kidete kuwa wanapinga hoja au sera kwa sababu kadhaa, kwa nini tusitegemee kwa mazingira ya nyakati zile Nyerere na wasaidizi wake wasiwe reactionary na kamatakamata mshikemshike isifanyike?

Yes on eye level, Nyerere was wrong to allow his surbodinates to victimize everyone who was opposing him. Was it out of fear follow up to the uprising and instability in other parts of Africa? Possibly yes!

Leo huwezi kuona Mkapa, Kikwete hata Lowassa wakituhofia kuwa tutaleta mapinduzi, au jeshi kuwapindua. Wanatuhofia kuwa tutaleta mapinduzi kwenye sanduku la kura na hoja zetu kubadilisha fikra na mawazo ya Watanzania kupitia demokrasia huku wao wakiwa na wasiwasi kuhusu Ubinafsi wao!

Wakati wa Nyerere hata baada ya Karume kuuwawa na mapinduzi kila kona ya Afrika na kubainika kuwa chimbuko wala si tofauti ya fikra bali ni ukuwadi wa ama Marekani au Urusi!
 
..naona Jenereli Ulimwengu naye anatoa mawazo yake hapa kuhusu Azimio na mazingira ya kisiasa wakati wa serikali ya awamu ya kwanza.

Jokakuu,

Sasa huyo ni Jenerali Ulimwengu, mmoja wa protege wa Nyerere, pamoja na kina Mkapa. Amesema yale yale tunayoyasema. Na yeye "ana chuki na J.K. Nyerere" kama Kuhani alivyo? Eeeh ?

Ni kwamba Jenerali Ulimwengu anaweka rekodi straight. Sio kwamba ana kikorosho na J.K. Nyerere. Huyu Nyerere alikuwa original thinker, aliyependa nchi yake, na kila alilofanya alifanya kwa manufaa ya Nchi. Naamini hilo kabisa, 100%. J.K. Nyerere sio kina Chenge hawa wanaofanya kazi kwa manufaa ya akaunti zao. Natambua hilo sawia.

Lakini, kwa sababu tu unafanya kitu kwa manufaa ya Nchi haina maana ulichofanya ni sahihi/busara. Katika jamii ninayoishi sasa hivi, Magharibi, Mama anaweza kutenda jinai kwa kumkanya mtoto wake kwa makofi. Mama mwenye nia nzuri kabisa, anaetaka mtoto wake asije kuwa na tabia ya "chuki" na "juha" kama Kuhani. Lakini, jamii hii inaona, na nadhani kuna la kujifunza hapa, kwamba, nia njema haihalalishi kila kitu. Ok? Kuna cha kujifunza hapo. Kwamba, kusema J.K. Nyerere alikuwa na nia nzuri tumuache apumzike ni such glib analysis of incredible proportions.

Mada hapa ni chanzo cha mawazo ya J.K. Nyerere. Wengine wakasema mawazo yake J.K. Nyerere Watanzania wenzake walikuwa hawana uwezo wa kujenga hoja kupingana nae. Wengine tukasema hiyo si kweli! Sasa, kama naharibu thread yenu ninyongeni, nifungieni. Haki yangu, hata hivyo, nipeni. Kuna wabunge walifungwa jela (nimeweka vielelezo matundiko ya juu), makamu wa Rais akauawa baada ya Nyerere kuombwa asimrudishe Zanzibar akakataa ili tu kumfurahisha Karume (niwemeka vielelezo matundiko ya juu). Mimi nitakuwa wussy nikiogopa kupinga bunk za kupotosha hapa, vitu ambazo hata wakina Jenerali Ulimwengu wanavisema -mtu anaeandika kila kukicha miaka enda miaka rudi, yuko exposed kwa kila aina ya wasomaji na hajaambiwa anakosea hiyo historia. Itakuwa hao kina Mzee Bomani, kina "ndio-Mzee" wa J.K. Nyerere ? Tafadhali! Tafadhali! For the sake our children, history and truth, tafadhali!

Jokakuu, ahsante kwa kupenda ukweli.
 
Kishoka,

..of course, Mwalimu alikuwa na ushawishi mkubwa sana. hilo lazima tukiri.

..mazingira ya chama kimoja nayo yali-discourage watu wasihoji, na zaidi kuminya nafasi ya ku-dissent peacefully.

..Zuberi Mtemvu alipotofautiana na Mwalimu, aliamua kuanzisha chama chake. sheria ilimruhusu.

..wanasiasa wengi wanadai wanajiunga huko ili kutumikia wananchi, lakini ukweli unabaki kwamba siasa pia ndiyo ajira yao inayowawezesha kuhudumia familia zao.

..utaona basi kunakuwa na kuoga fulani ktk kusimamia yale mtu anayoamini, kwa kuogopa kukosa mkate wa watoto.

..nadhani badala ya kuhoji, na ku-entervene kabla mambo hayajaharibu, wasaidizi wa Mwalimu walimuacha ajionee mwenyewe matokeo ya utekelezaji wa nadharia zake.


Kuhani,

..binafsi naamini bila kuchambua pale alipokosea Mwalimu basi nchi hii haiwezi kusonga mbele.

..nilisikitika sana Kishoka alivyoanzisha ile thread nyingine. tena nilijiapiza kuendelea kuchangia hapa hapa, labda wanifungie.

..binafsi sitofautiani sana na mawazo mengi ya Mwalimu, kinachonikwaza ni utekelezaji wa mawazo hayo.

..sasa kama kusema hayo tu watu wanataka kututenga kana kwamba ni wakoma na kutuanzishia thread yetu ili tukasemee huko ilinikera kidogo. inakuwa kama kupelekwa na kuishi kijiji cha wakoma.

..any way, naamini Kishoka ni mtu mzima huyu, mwenye busara zake. ndiyo maana unaona tunaendelea na mjadala.
 
Jokakuu,

Sasa huyo ni Jenerali Ulimwengu, mmoja wa protege wa Nyerere, pamoja na kina Mkapa. Na yeye "ana chuki na J.K. Nyerere" kama Kuhani alivyo? Eeeh ?

Ni kwamba Jenerali Ulimwengu anaweka rekodi straight. Sio kwamba ana kikorosho na J.K. Nyerere. Huyu Nyerere alikuwa original thinker, aliyependa nchi yake, na kila alilofanya alifanya kwa manufaa ya Nchi. Naamini hilo kabisa, 100%. J.K. Nyerere sio kina Chenge hawa wanaofanya kazi kwa manufaa ya akaunti zao. Natambua hilo sawia.

Lakini, kwa sababu tu unafanya kitu kwa manufaa ya Nchi haina maana ulichofanya ni sahihi/busara. Katika jamii ninayoishi sasa hivi, Magharibi, Mama anaweza kutenda jinai kwa kumkanya mtoto wake kwa makofi. Mama mwenye nia nzuri kabisa, anaetaka mtoto wake asije kuwa na tabia ya "chuki" na "juha" kama Kuhani. Lakini, jamii hii inaona, na nadhani kuna la kujifunza hapa, kwamba, nia njema haihalalishi kila kitu. Ok? Kuna cha kujifunza hapo. Kwamba, kusema J.K. Nyerere alikuwa na nia nzuri tumuache apumzike ni such glib analysis of incredible proportions.

Mada hapa ni chanzo cha mawazo ya J.K. Nyerere. Wengine wakasema mawazo yake J.K. Nyerere Watanzania wenzake walikuwa hawana uwezo wa kujenga hoja kupingana nae. Wengine tukasema hiyo si kweli! Sasa, kama naharibu thread yenu ninyongeni, nifungieni. Haki yangu, hata hivyo, nipeni. Kuna wabunge walifungwa jela (nimeweka vielelezo matundiko ya juu), makamu wa Rais akauawa baada ya Nyerere kuombwa asimrudishe Zanzibar akakataa ili tu kumfurahisha Karume (niwemeka vielelezo matundiko ya juu). Mimi nitakuwa wussy nikiogopa kupinga bunk za kupotosha hapa, vitu ambazo hata wakina Jenerali Ulimwengu wanavisema -mtu anaeandika kila kukicha miaka enda miaka rudi, yuko exposed kwa kila aina ya wasomaji na hajaambiwa anakosea hiyo historia. Itakuwa hao kina Mzee Bomani, kina "ndio-Mzee" wa J.K. Nyerere ? Tafadhali! Tafadhali! For the sake our children, history and truth, tafadhali!

Jokakuu, ahsante kwa kupenda ukweli.

You are dumb as rock! Where is your investigation findings, Mr. Dumbo?
 
Kuhani,
Shida yako una tabia ya "to give a dog a bad name in order to kill it. Kubali kuwa hukumjua Mzee Bomani. Huna haki hata kidogo kumwita "ndio mzee." Bomani was a capitalist per excellence. Hata kwenye Azimio la Arusha hakukubaliana na kila kitu, lakini he was a nationalist, na aliipenda nchi yake kama alivyokipenda chama chake cha TANU/CCM. He had his disagreements with Nyerere lakini alimheshimu na kuheshimu uongozi wake. He was not a "yes sir" man. Like I said, you do not have monopoly on the truth.
 
..binafsi naamini bila kuchambua pale alipokosea Mwalimu basi nchi hii haiwezi kusonga mbele.

..nilisikitika sana Kishoka alivyoanzisha ile thread nyingine. tena nilijiapiza kuendelea kuchangia hapa hapa, labda wanifungie.

..binafsi sitofautiani sana na mawazo mengi ya Mwalimu, kinachonikwaza ni utekelezaji wa mawazo hayo.

..sasa kama kusema hayo tu watu wanataka kututenga kana kwamba ni wakoma na kutuanzishia thread yetu ili tukasemee huko ilinikera kidogo. inakuwa kama kupelekwa na kuishi kijiji cha wakoma.

..any way, naamini Kishoka ni mtu mzima huyu, mwenye busara zake. ndiyo maana unaona tunaendelea na mjadala.

JokaKuu,

Not everything is merry and rosey about Nyerere, that I agree and I will be on top of the mountain declaring that.

Lakini kwenye hili, nilichokuwa naepusha ni ile tabia ya kuburuzana kuharibu mada midhali mtu anataka kuharibu kwa kuwa ana lake jambo.

Ndio maana nikaenda kufungua thread nyingine, kuwa huko basi tukae tukichanguya mapungufu ya Nyerere kwa kuwa hapa nilikuwa najaribu tufanye tathmini ya kuwa ni vipi alipata influence ya kuwa mjamaa na hata kutuletea Azimio.

NI kweli mjadala umeshapoteza njia na mantiki na badala ya kuchangua ni nini Mwaliki alijifunza hata kuona Ujamaa ni bora na kuoanisha na maisha yetu, mjadala umegeuka kama ile mingine kujadili kufeli kwa ujamaa na mapungufu ya Nyerere!
 
..binafsi naamini bila kuchambua pale alipokosea Mwalimu basi nchi hii haiwezi kusonga mbele.

Tatizo ni kwamba adherents wa J.K. Nyerere wanadhani kwamba tukisema huyu hero wetu alikosea pale na hapa basi ghafla ataanguka kwenye pedestal tuliyomuweka. Ataacha kuwa Baba wa Taifa. Wanahofia hilo. Mimi naamini J.K. Nyerere ni mnara na muasisi wa nchi yetu. Tena, let me break it to you, binafsi nadhani makosa ya kiuchumi tunayombambika J.K. Nyerere inawezekana ni yetu wote - Ujamaa ulishindwa, wataalam wanasema, moja ya sababu ni wananchi hawakuwa na mwamko/nia/motivation. Hili nadhani ni la wote, japo ni J.K. Nyerere ndie alichora mchoro. Tunapokosoa era ya J.K. Nyerere kwa namna fulani tunajiangalia wote, tukiongozwa na J.K. Nyerere, tulikosea wapi? Ili tusibugistepu tena. Sio vibaya tukaangalia tulipojikwaa, nakubaliana na wewe kabisa.

..nilisikitika sana Kishoka alivyoanzisha ile thread nyingine. tena nilijiapiza kuendelea kuchangia hapa hapa, labda wanifungie.

Japo alichofanya kufungulia watu thread nyingine amefanya ki-kejeli kejeli (angalia aliyoandika mle ) bado namuelewa, thread lazima iwe na muelekeo. Tatizo ni kwamba anasema hapa sio pa kueleza mapungufu ya Nyerere lakini anaona ni poa topic zisizohusika kabisa za kumpamba pamba J.K. Nyerere kupitia vipaza sauti vyake kama Mzee Bomani. Kwa hiyo, unaweza kuleta lolote hapa, mada yoyote hapa ya Nyerere, al muradi umuimbie imbie mapambio J.K. Nyerere. Hata ya kupotosha! Rev. Kishoka anaonyesha double standard.

...binafsi sitofautiani sana na mawazo mengi ya Mwalimu, kinachonikwaza ni utekelezaji wa mawazo hayo.
Mimi kinachonikwaza zaidi ni kwamba Watanzania wengi hawajapewa taarifa zote za kilichojiri kuhusu era ya J.K. Nyerere. Bado wanalishwa taarifa za kina Mzee Bomani (tena hapa na assume kwamba ni kweli Mzee Bomani kamwambia Jasusi haya mambo). Simlaumu sana J.K. Nyerere kuhusu idea zake za Uchumi, ila napenda dunia ijue ukweli wa kilichojiri.

...sasa kama kusema hayo tu watu wanataka kututenga kana kwamba ni wakoma na kutuanzishia thread yetu ili tukasemee huko ilinikera kidogo. inakuwa kama kupelekwa na kuishi kijiji cha wakoma.
Inakera, lakini ukikumbuka kwamba wakati wa J.K. Nyerere wewe Jokakuu ungepandishwa kwenye Land Rover na kitambaa cheusi usoni na pingu ukapelekwa kwenye chumba cha giza kwa mateso, au kijijini kwenu, basi adhabu za kina Painkiller na Ole ni cha mtoto.

...any way, nadhani Kishoka ni mtu mzima huyu, mwenye busara zake. ndiyo maana unaona tunaendelea na mjadala.

Swadakta. Hamna mtu level-headed hapa na menye civility kama Rev. Kishoka. Lakini kwenye mijadala inayogusa hisia zake kama huu, anashindwa kuwa consistently even-tempered. Inasikitisha.

Sawasawa, na mimi nimeweka kumbukumbu zangu za mazungumzo na Mzee Bomani, lakini sijaita hoja zako uwongo. Huyu alifanya kazi na Mwalimu tangu enzi za TANU na alikuwa waziri mpaka kwenye utawala wa Mwinyi. Unaweza kudharau maoni yake kwa sababu zako mwenyewe lakini si kuita maoni ya wengine, hasa wale waliofanya kazi za karibu na Mwalimu kuwa waongo. Nitawasikiliza wasomi hoja zao na pia nitasikiliza hoja za wale waliofanya kazi kwa ukaribu na Mwalimu akiwemo Mkapa na Butiku, ambao wote nimezungumza nao sana. That is my point.

Bu who?

Jamani, jamani, jamani, angalia unavyo vurunda hapa?

Unaenda kumuuliza Mzee Butiku kesi za Mzee Nyerere?

Butiku ?

Jasusi, Butiku kweli ? Surrogate wa Nyerere ?
 
Zakumi,

Nyerere alikuwa mjamaa na alisema kuwa Ujamaa ni Imani na ni watu. Alileta mfumo wa ujamaa akiamini ni njia ya kujenga taifa linalojitegemea.

Wamarekani walisema ubepari ndio njia pekee ya mafanikio na maendeleo, wakaruhusu soko huria na watu kujifanyia wanavyotaka.

Sasa common denominator hapa ni hizo unazosema, chakula, paa na afya, sisi Tanzania tulipokuwa na sera za kutoa afya na elimu bure, tulikoromewa kwa ni makosa makubwa.

Kweli ilikuwa makosa makubwa kwa kuwa hatukuwa na mtaji wa kutosha, lakini ili kuwa ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kuwa kila mtu anapata furs ya kusoma na kuwa na afya njema.

Marekani, elimu ya msingi na sekondari ni bure, afya pamoja na kuwa kila mtu anahitaji bima, bado kama huna bima unaweza kwenda tibiwa hospitali bure.

Swali ni kwa nini iwe sawa kwa Marekani kuwa na elimu bure na hata huduma za afya bure lakini iwe ni sumu kwa Tanzania? tutang'ang'ania kuwa Tanzania haikuwa na mtaji wa kutosha? je kujenga nchi na taifa tukiwa na watu wenye siha bora na elimu tungefanikiwa vipi kama tungesema kila mtu alipie ili kunusuru viwanda na kujijenge utajiri?

Rev Kishoka:

Kwanza ningependa kukukosoa. Hakuna kitu cha bure. Vile vile misingi ya Ujamaa au usoshalisti haisemi kuwa
elimu au huduma za afya zitolewe bure.

Ujamaa na usoshalisti vyazo vyake ni umilikaji wa mitaji na mgawanyo wa mapato. Elimu iliyotolewa bure ilikuwa ni
sehemu ya mgawo wa mapato.

Lawama alizopata Nyerere ni sahihi kabisa. Kama elimu au huduma za afya ni sehemu ya mgawo wa mapato, je ni juhudi
gani watanzania walifanya kustahili mgao huo?

Vitabu vya Nyerere vinasema juhudi za kazi za watanzania zitumike katika kutoa elimu au kupata huduma za jamii. Lakini
hayo yaliishia vitabuni. Kwenye utendaji huduma zilitegemea mikopo na misaada kutoka kwa wahisani.

Mnaopiga kelele kutetea Nyerere kwa kutoa elimu ya bure naomba mtueleze ni vitu gani vilifanyika Tanzania kuweza kutoa elimu
ya bure. Watu hamna aibu kuona taifa mpaka leo linategemea misaada kutoka nje.
 
I could do it, but I won't. I wish some one could dare to show me where Nyerere broke a law duly promulgated by the August House. Mkinionesha hapo tutaanza mjadala kuhusu Prevention and Detention.
 
Bu who?

Jamani, jamani, jamani, angalia unavyo vurunda hapa?

Unaenda kumuuliza Mzee Butiku kesi za Mzee Nyerere?

Butiku ?

Jasusi, Butiku kweli ? Surrogate wa Nyerere ?

Kuhani,
Hiyo ndiyo shida yako. Yaani yeyote aliyefanya kazi karibu na Mwalimu ni surrogate. Akina Bomani, ambao walikuwa independent minded umeshawapachika "u-yes sir." Unawafanya watu kama wasio na akili vile. Inaonekana unataka sources za upande mmoja tu--the anti-Mwalimu. Kwako Butiku, Bomani and Mkapa may not be reliable sources, lakini hao unaowaaminia walimjuaje Mwalimu kama hawakuzungumza na watu waliofanya naye kazi kwa ukaribu?
 
Back
Top Bottom