GT,
Nadhani kuna mahali Companero kasema kaiandika mwenyewe. Kama ni hivyo basi kama kaiandika mwenyewe accademically akishakupa source utajua who he is, au?
hivi hawa viongozi wa leo mawazo yao yanatoka wapi?
bevic@rocketmail.comNaam, nimeiandika mwenyewe. Sina tatizo na wasifu wangu kujulikana. Kama kuna mtu anataka nakala ya hiyo mada anipe anuani ya barua pepe yake nami nitamtumia mara moja. Katiba yetu, katika Ibara ya 18, inasema kila mtu ana haki ya kupata taarifa muhimu kama hizi zinazohusu maendeleo ya jamii yetu.
Kwa tafsiri ya haraka tulitakiwa tumtafute Kambona na kumpigia magoti. Na sio kumuita haini. Kama ilivyokuwa miaka hiyo ya kawawa mfuata upepo. Yote kwa yote ni muda muafaka sasa kufanya mapinduzi ya kifikra kisha tutambue kuwa Tanzania ni yetu sote na sio ya wanabagamoyo kama ilivyo sasa.
Mimi siko UK wala USA, nipo hapa URT. Karibu sana tujenge nchi ya watu ambao Mwalimu Nyerere aliwatabarukia vitabu vyake vya Ujamaa. Sasa tunaanza upya baada ya SAPs na PRSP kushindwa kazi kwa miaka 28 ambayo ni miaka mingi zaidi ya miaka 10 tuliyotekeleza Azimio la Arusha la Ujamaa na Kujitegemea. Tunaanza kwa kurudisha Mwongozo. Hii itasaidia watumishi wa umma wasichanganye utumishi na biashara binafsi kama walivyochanganya kina Richmonduli. Hivi jiulize inakuwaje waziri awe na biashara ya ndege alafu akipoteza tu uwaziri eti hiyo biashara inafilisikia!Mwongozo utahakikisha kuwa kamwe kodi zetu hazibeiliauti mafisadi!Kwa jasho lao watakula!Ujamaa, kama ulivyo Uhuru, ni kazi!Na hata misahafu inasema asiyefanya kazi na asile!Haisemi liwa ule!
Nyerere alikuwa akifuatilia mrengo wa Labor akiwa Uingereza lakini aliye mu influence UJAMAA ni AbdulRahman Babu.Waungwana,
Ni nani na ni misingi gani ya utashi iliyojijenga kwenye akili za Julius Kambarage wa Nyerere kutuletea Ujamaa na Kujitegemea na hata Azimio la Arusha?
Wengi tunadhania kuwa ni safari yake ya China 1966. Wengine wanadai ni wale ma-Labor na Socialist wa Uingereza.
Tunajua kuwa tumeangalia sana Ujamaa wetu na Azimio kwa mkao wa Great Leap Forward na Cultural Revolution za China ya Mao na Leninism/Stalinism ya Command Economy, New Economic Policy, Collective farming, na hata matunda ya Bolshevik revolution na sera kama Prodrazvyorstka!
Tukija huku kwetu Afrika tunadai kuna Ujamaa wa Kiafrika, Pan Africanism na mengine mengi.
Lakini bado nafikiri ni kitendawili kwetu kuwa ni ushawishi gani na kwa maono gani Nyerere alikaa chini na kutuletea Ujamaa na Kujitegemea na Azimio la Arusha?
Nikirudia Historia na kuangalia kinachotokea Marekani kiuchumi mwaka huu na nyakati hizi, narudi kujiuliza, falsafa za kiuchumi na kujenga jamii za Marekani zilimkosha Mwalimu Nyerere hasa kuangalia Historia ya great depression?
Je FDR (Franklin Delano Roosevelt) na New Deal yake, Fransiscans/Jesuit philosophy na hata Keynesian Policies zilimbadilisha vipi huyu Mkulu wetu? Planned Economy za National Recovery Administration wakati wa Great Depression ya Marekani na hata Public Works ya Nazi German vilikuwa na nafasi gani?Je alichungulia Front Populaire ya Leon Blum wa Ufaransa na kudonoa mambo kadhaa?
Je kujinasua kwa Marekani baada ya Uhuru wake kutoka Uingereza na kujijenga kama taifa linalojitegemea na si kutegemea falme ya Uingereza na kiburi cha Kimarekani pia kilichangia kumjenga Nyerere kuwa na kiburi cha masikini jeuri?
Twajua Julius Nyerere alikuwa mwana historia mzuri hata ukiangalia na kumpima kutafsiri kwake kwa Julius Kaisari na Mfanyabiashara wa Venisi kazi za William Shakespear zinaonyesha ni influence gani ya fasihi, historia na falsafa alikuwa nayo.
Je Keynes alikuwa na infuence gani kwa Nyerere ambaye alisoma fasihi, historia , uchumi na falsafa alipokuwa Makerere na hata Edinburgh?
What about Wealth of nations, je Nyerere alifanya modification ya principles za Adam Smith akipewa baraka na Labor Party ya Uingereza chini ya ushawishi wa Mama Joy Wickens? Maana ukiangalia Azimio la Arusha, pamoja na kuuzwa kuwa linapiga vita Ubepari, in fact linaruhusu ubepari na mfumo wa Kibepari kwa kiasi fulani hasa linaposema kuwa Viongozi wasiwe na zaidi ya hisa katika makampuni mawili!
Je Plato, Aristotle, Socrates, Ghandi na hata Yesu au Mtume Mohamed wali-play part gani kum-influence Nyerere?
Je alisoma sana Das Kapital na Communist Manifesto ya Karl Marx, akamchanganya Trosky na Friederich Engels?
Je sisi kama Taifa kwa kumfuata Kiongozi wetu tulikuwa ni majaribio (experiment) ambayo mataifa makubwa yalikaa kando kuangalia huyu mwanafalsafa na mwanamapinduzi wa Afrika akikoroga na kuunganisha mifumo ya kiuchumi ya Ubepari, Ukabaila, Ukomunisti na Ujamaa na kuunda Ujamaa wa Kiafrika ambao ulilenga kwenye kujitegema na hata kuzaa Azimio la Arusha kubana tabaka la viongozi na kuhamasisha umiliki wa mali kwa umma na si watu binafsi?
Tumeegemea sana kusema tumeunda Ujamaa wetu kutokana na ziara yake ya China na kuharibika kwa uhusiano wetu na Uingereza kulikotokea kipindi hicho hicho.
Je inawezekana kuwa kiwango kikubwa cha falsafa zake za Ujamaa na Azimio ni mgawanyiko sawa wa influence za magharibi wakati wa depression na mashariki wakati wa uprising na mapinduzi?
Nyerere alikuwa akifuatilia mrengo wa Labor akiwa Uingereza lakini aliye mu influence UJAMAA ni AbdulRahman Babu.
hakuwatelekeza mkuu ila hakuwa na jinsi na ndio maana alisema ule ujumbe kama angekuwa na uwezo angekisukuma kisiwa kizima cha Zanzibar mbali huko katika kati ya bahari kwa sababu Km70 ni ndani ya Uzio wetu wa kiusalama (200 Km) huwezi kuwakimbia. Ujue ilikuwa kazi kubwa kuwapatanisha ASP na watu wenye Ukomunist ama asili ya Kiasia Unguja.Lakini akamtelekeza sana Babu na Hanga. Na kuruhusu wapotezwe na Manyang'au.Inaniudhi sana historia hii