Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Dr. Steven Chu, mwanasayansi aliyeshinda nishani ya Nobeli katika fani ya Fizikia ameteuliwa na Rais mtarajiwa wa Marekani Bw. Barack Obama kuwa waziri wa Nishati.
Nanukuu majukumu yake na wasifu wake kama yalivyoandikwa kwenye gazeti la New York Times;
Tukija kwenye wizara ya Fedha, aliyeteuliwa kuwa waziri wa fedha ni mchumi aliyebobea ambaye alikuwa ni Rais(Gavana) wa Benki Kuu ya Marekani-New York Bw. Tim Geithner, Ulinzi yupo aliyekuwa mkuu wa shirika la kijasusi CIA, Robert Gates, National Security yuko Generali mstaafu James Jones, Mambo ya nje yuko Hillary Clinton, bado tuje Kilimo, Elimu, Biashara, Usalama, Sheria kote huko wameteuliwa watu waliobobea katika fani hizi na hivyo kuashiria kuwa wataingia kufanya kazi kwa umahiri, wakitumia juhudi, maarifa na ujuzi walio nao katika hizi fani.
Najiuliza je Tanzania ya 2010 tutapata kina Dr. Cho wetu?
Nikiangalia wizara kama ya Nishati na madini, sidhani kama tumewahi kuwa na Waziri ambaye ni mtaalamu wa sekta ya Nishati au madini. Yona, Kikwete walikuwa wachumi, Msabaha ni mtu wa mambo ya Kimataifa, Karamagi ni biashara na sasa Ngeleja ni mwanasheria.
Ni lini wizara nyeti kama hii ya Nishati na Madini ikapata mtu bingwa kama Dr. Cho? Bingwa ambaye ataweza kututatulia tatizo sugu la umeme na kusambaa kwa umeme nchi nzima, atakayelipigania taifa lake kulinda madini yetu, atakayesimama kidete kuhakikisha kuwa Tanzania inaelekea kwenye mwendo wa kutumia nishati safi kwa uzalishaji mali na matumizi ya nyumbani, atakayehakikisha kuwa mafuta yetu na hata ile gesi ya Songosongo na makaa ya mawe Kiwira yanalizindua taifa letu kiuchumi?
Hata nikija kwenye suala la wizara ya fedha, mipango na uchumi, ni lini tutarusi kwenye zile enzi za kuwa na Waziri mwelewa mwenye utaalamu wa Uchumi, Fedha, Uhasibu na Mipango na si kuwekewa vilaza kama Mramba na Mkullo ambao si kwamba hawakuonekana hawajui kitu, bali wana kaharufu ka uzembe, kukosa uwajibikaji na kuvunda kama vile ufisadi?
Tatizo liko wapi? ni ile sheria au kifungu cha katiba kinachosema Waziri lazima awe mbunge? Mbona Mwandosya ni mwanasayansi bingwa hatukumpeleka Nishati na Madini?
Je Kilimo, Mifugo na Utalii tumewapeleka kina nani?
Je kama tatizo si Katiba kwa maana ya kuwa makatibu wakuu wa wizara hizi watakuwa ni wataalamu au watu bingwa wa fani, je ni tunaweza kukiri kuwa ni sera za chama au ilani ya chama ndiyo mbaya maana inashurtisha mgombea wa uraisi na mizengwe ya ndani ya chama kuwa na Serikali ya kishkaji iliyo na sera za kishkaji?
Au tatizo ni sisi wananchi kuwa hatujitumi katika fani zetu bila kutegemea kuona tuna Waziri bingwa au wanasiasa bingwa? Je kuna uwezekano wa Mkinga kulima chai kwa ziada bila kusubiri Waziri wa Kilimo awe ni Phd. wa mavi ya kuku na samadi?
Na elimu kwani jukumu la kumwelimisha mtoto ni shurti tuwe na Prof. Mmari au hata gwiji mwenzetu humu Mwalimu Augustine Moshi kama waziri wa Elimu ndipo watoto wetu waelimike?
Je ni lini tutaachana na mazoea ya kutoa Uwaziri eti kuleta mgawanyiko wa majimbo, jinsia, makabila na dini na si kutumia uzoefu wa mtu katika nyanja kama Dr. Anna Tibaijuka?
Where are our freakin Dr. Cho and others?
Nanukuu majukumu yake na wasifu wake kama yalivyoandikwa kwenye gazeti la New York Times;
Dr. Chu will be taking on one of the most challenging jobs in government at the Department of Energy. He will be responsible for the maintenance and development of the nations nuclear weapons stockpile, as well as for modernizing the nations electrical power delivery system.
He will also play a central role in directing the research and development of alternative energy sources needed to replace fossil fuels in a era of constrained carbon emissions. Mr. Chu shared a Nobel Prize in physics in 1997 for work on supercooled atoms.
At the Lawrence Berkeley laboratory, he has sponsored research into biofuels and solar energy and has been a strong advocate of controlling greenhouse gas emissions.
Scott Segal, director of the Electric Reliability Coordinating Council, an industry group, said he was pleased that Dr. Chu had the technical expertise to realistically assess future energy technologies.
His experience seems to dovetail perfectly with the president-elects commitment to bringing new energy technology to market in a timely fashion, Mr. Segal said. An understanding of the art of the possible in energy technology will be critical to the development of a cost-effective climate change policy.
Tukija kwenye wizara ya Fedha, aliyeteuliwa kuwa waziri wa fedha ni mchumi aliyebobea ambaye alikuwa ni Rais(Gavana) wa Benki Kuu ya Marekani-New York Bw. Tim Geithner, Ulinzi yupo aliyekuwa mkuu wa shirika la kijasusi CIA, Robert Gates, National Security yuko Generali mstaafu James Jones, Mambo ya nje yuko Hillary Clinton, bado tuje Kilimo, Elimu, Biashara, Usalama, Sheria kote huko wameteuliwa watu waliobobea katika fani hizi na hivyo kuashiria kuwa wataingia kufanya kazi kwa umahiri, wakitumia juhudi, maarifa na ujuzi walio nao katika hizi fani.
Najiuliza je Tanzania ya 2010 tutapata kina Dr. Cho wetu?
Nikiangalia wizara kama ya Nishati na madini, sidhani kama tumewahi kuwa na Waziri ambaye ni mtaalamu wa sekta ya Nishati au madini. Yona, Kikwete walikuwa wachumi, Msabaha ni mtu wa mambo ya Kimataifa, Karamagi ni biashara na sasa Ngeleja ni mwanasheria.
Ni lini wizara nyeti kama hii ya Nishati na Madini ikapata mtu bingwa kama Dr. Cho? Bingwa ambaye ataweza kututatulia tatizo sugu la umeme na kusambaa kwa umeme nchi nzima, atakayelipigania taifa lake kulinda madini yetu, atakayesimama kidete kuhakikisha kuwa Tanzania inaelekea kwenye mwendo wa kutumia nishati safi kwa uzalishaji mali na matumizi ya nyumbani, atakayehakikisha kuwa mafuta yetu na hata ile gesi ya Songosongo na makaa ya mawe Kiwira yanalizindua taifa letu kiuchumi?
Hata nikija kwenye suala la wizara ya fedha, mipango na uchumi, ni lini tutarusi kwenye zile enzi za kuwa na Waziri mwelewa mwenye utaalamu wa Uchumi, Fedha, Uhasibu na Mipango na si kuwekewa vilaza kama Mramba na Mkullo ambao si kwamba hawakuonekana hawajui kitu, bali wana kaharufu ka uzembe, kukosa uwajibikaji na kuvunda kama vile ufisadi?
Tatizo liko wapi? ni ile sheria au kifungu cha katiba kinachosema Waziri lazima awe mbunge? Mbona Mwandosya ni mwanasayansi bingwa hatukumpeleka Nishati na Madini?
Je Kilimo, Mifugo na Utalii tumewapeleka kina nani?
Je kama tatizo si Katiba kwa maana ya kuwa makatibu wakuu wa wizara hizi watakuwa ni wataalamu au watu bingwa wa fani, je ni tunaweza kukiri kuwa ni sera za chama au ilani ya chama ndiyo mbaya maana inashurtisha mgombea wa uraisi na mizengwe ya ndani ya chama kuwa na Serikali ya kishkaji iliyo na sera za kishkaji?
Au tatizo ni sisi wananchi kuwa hatujitumi katika fani zetu bila kutegemea kuona tuna Waziri bingwa au wanasiasa bingwa? Je kuna uwezekano wa Mkinga kulima chai kwa ziada bila kusubiri Waziri wa Kilimo awe ni Phd. wa mavi ya kuku na samadi?
Na elimu kwani jukumu la kumwelimisha mtoto ni shurti tuwe na Prof. Mmari au hata gwiji mwenzetu humu Mwalimu Augustine Moshi kama waziri wa Elimu ndipo watoto wetu waelimike?
Je ni lini tutaachana na mazoea ya kutoa Uwaziri eti kuleta mgawanyiko wa majimbo, jinsia, makabila na dini na si kutumia uzoefu wa mtu katika nyanja kama Dr. Anna Tibaijuka?
Where are our freakin Dr. Cho and others?