What's the story: Ulipataje kazi unayofanya au uliyowahi kufanya?

Mimi haikua rahisi hata kidogo. Namaliza chuo sina referee wala godfather.Nilihastle mbaya eeh Mungu nisamehe. Loga sana saa nyingine nakalia kiti ya ofisi natafakari nakumbuka afu nabakia kucheka tu.Life is not with heartless people. Risk it all to achieve your goal.If succession is your goal then winning is not your option.Sorry usifuate kama imani yako hair unusu.
Mkuu unamoyo wa kishujaa sana. bado sijapata kazi, ila hio njia huwa inaniogopesha kipindi na soma (o level) kuna mwalimu nilisikiaga story zake. Huwa zinaniogopesha mpaka leo.
 
  • Thanks
Reactions: vvm
Wadau vipi kazi hampati tena ? Natamani kujua story zenu mlipataje kazi ili nawengine tujifunze mawili matatu, ya kuapply tuyatumie yakuepuka tuyaepuke vile vile!
Bado tunatafuta ushahidi
 
  • Thanks
Reactions: vvm
Kamwe usidharau mtu yoyote..

Kazi yangu ya kwanza ya kueleweka niliipata kupitia mlinzi niliyekuwa nimepanga nae jirani, alikuwa ana mazoea ya kuniomba pasi kila siku jioni....siku moja akanambia kuwa Mkurugenzi wa kampuni anayolinda anataka mtu kitengo fulani pale ofisini kwao, akaniuliza kama nafasi hiyo inanifaa? nikamjibu kuwa nimesomea hiyo fani. Basi kesho yake akiwa anatoka shift asubuhi akanipigia simu niende hapo, nikaenda na vyeti vyangu, akanishika mkono mpaka ofisini kwa Mkurugenzi, sikuamini kilichotokea maana sikufanyiwa interview wala lolote lile nikaambiwa nijiandae kusaini mkataba nianze kazi kesho yake, nikakabidhiwa ofisi siku hiyo hiyo pamoja na kutambulishwa kwa management na my team. Mpaka leo sijajua yule mlinzi alimuambia nini yule mkurugenzi, nilijifunza kuheshimu watu zaidi kuanzia siku ile mpaka na kesho daima
 
Kama kuna wadau ambaye alisomea Mechanical ICT Environmental na electrical engineering degree ya kwanza wanapenda kupata uzoefu Naomba wanicheki inbox kuna taasisi moja ipo tu vizuri Ila naona hawapeleki cv

Nina mdogo wangu amesoma bioprocessing Engineering itamfaa ? wanalipa ??
 
Kamwe usidharau mtu yoyote..
Kazi yangu ya kwanza ya kueleweka niliipata kupitia mlinzi niliyekuwa nimepanga nae jirani, alikuwa ana mazoea ya kuniomba pasi kila siku jioni....siku moja akanambia kuwa Mkurugenzi wa kampuni anayolinda anataka mtu kitengo fulani pale ofisini kwao, akaniuliza kama nafasi hiyo inanifaa? nikamjibu kuwa nimesomea hiyo fani. Basi kesho yake akiwa anatoka shift asubuhi akanipigia simu niende hapo, nikaenda na vyeti vyangu, akanishika mkono mpaka ofisini kwa Mkurugenzi, sikuamini kilichotokea maana sikufanyiwa interview wala lolote lile nikaambiwa nijiandae kusaini mkataba nianze kazi kesho yake, nikakabidhiwa ofisi siku hiyo hiyo pamoja na kutambulishwa kwa management na my team. Mpaka leo sijajua yule mlinzi alimuambia nini yule mkurugenzi, nilijifunza kuheshimu watu zaidi kuanzia siku ile mpaka na kesho daima
Duuuh hongera sana jamaa
 
  • Thanks
Reactions: vvm
Hadi sasa hivi nimeshafanya kazi sehemu nne.
1.Dar es Salaam.
Nilikua nimemaliza internship,nafasi za serikali hazijatoka wala nini, niko tu kitaani napiga daywaka za vijiweni za kuunga unga hapa na pale, ali mradi nisile wali mkavu. Kuna chuo fulani hivi wakawa wametoa tangazo wanataka Tutorial Assistants,nikatupia application yangu, mimi na mshikaji wangu wa karibu sana, tukaitwa interview wote wawili. Siku ya interview tumeenda pale chuoni,tunacheki majengo ya chuo yamechakaa kinyama,tunaulizana na mshikaji wangu,hawa wataweza kweli kutulipa mpunga wa kutosha? Tulifika pale mida ya saa tatu asubuhi, ila kuja kuingia kwenye interview mimi niliingia kama saa kumi na moja hivi jioni!! Nimechoka mbaya, na interview kiukweli haikwenda poa, nilimbwela mbwela Sanaaa!! (kumbuka hii ndio ilikua interview yangu ya kwanza kabisa tangu nimalize intern). Baada kama ya wiki moja hivi,nikapigiwa simu kwamba nimefaulu interview, niripoti hapo chuoni kwa ajili ya kusaini mkataba na kuanza kazi!! Mimi na mshikaji wangu wote tulipata;Ila sasa mshikaji wangu yeye akawa amepata nafasi pia Bugando Hospitali (yuko hapo hadi sasa), so akapiga chini kule, kwa vile mimi nilikua sina option,nikatimba, nikasaini mkataba (permanent and pensionable), nikaanza kazi rasmi. Salary haikua mbaya sana (ukizingatia ndio ilikua my first salary apart from zile posho za internship).
Tatizo la pale bwana:kwanza ilikua unakuja asubuhi, unakaa tuu ofisini hamna lolote unalofanya, hamna cha kufundisha, au kuelekezwa au chochote, unakaa tuu unacheza na laptop hadi mda wa kazi ukiisha unarudi home (chuo kilikua kimepata matatizo kidogo,so walizuiliwa kudahili na NACTE wanafunzi wa first year,ambao mimi ndo kuna somo ilibidi niwe nawafundisha). Tatizo lingine ikawa wanachelewesha mishahara balaa. Miezi mingine hadi tarehe 10 ndo kitu kinasoma!! Nilikaa pale miezi mitatu tuu, nikaona hapa nimeingia cha kike!! Nikasepa.
2.Arusha.
A small NGO fulani hivi ya Waingereza ambao wanajihusisha na projects mbalimbali za afya,elimu,biashara. Kama kawaida, niliona tu nafasi kwenye zoom, nikatupia application, nikaitwa interview nikaenda, after a week nikapigiwa simu nikaripoti kazini.
Hapa nilianza kazi kwa salary ambayo ni ndogo kuliko hata kazi ya kufundisha niliyoacha. Sema huku apart from salary,kulikua na viallowance vya hapa na pale vingi, pamoja na pesa za dili za hapa na pale.
Tatizo la hapa likawa country director wa Tanzania alikua na matatizo matatizo sana...!! Alikua anaendesha ile NGO kama kampuni ya kwake binafsi. Kelele nyingiiii, micro-management kwa sanaaa!!! I stayed with this organization for 5 months tuu, nikasepa.
3.Mbeya
Hii ilikua ni kliniki kwa ajili ya watoto, ambayo iko funded na International NGO moja ya Wamarekani. Na yenyewe niliona tangazo kwa gazeti, nika apply, nikaitwa interview, nikapanda basi from Arusha hadi Mbeya (the longest journey by bus i have ever experienced), tuliingia mbeya saa saba na nusu usiku, saa mbili asubuhi nikagonga interview, ilienda vizuri sana (i was very very confidence by this time nilikua nimezoea interviews tayari, na nimejiandaa kweli kweli, na nikaulizwa maswali yale yale kama bahati ya mtende). After two weeks, nikapigiwa simu nimefaulu interview niende Mbeya kuanza kazi. Hii kazi kwa kweli benefits zake zilikua nzuri mno compared na kazi zangu zilizopita. I stayed at this organization for 1yr and 4months, then I left. Sababu zilikua mbili tatu; Kwanza, kulikua hakuna uhakika wa funds za kuendeleza mradi kutoka kwa wamarekani kwa mwaka unaofuata (though walikuja kupata wakaendelea), lakini pia management ya hii organization ya hapa bongo walikua very discouraging kwa wafanyakazi, na wanadharau wafanyakazi.
4.Mbeya
Mradi mkubwa dealing with HIV/AIDS in the Southern Highlands zone. Na yenyewe niliona tangazo, nika apply, nikaitwa kwa interview, nikatusua. (sio kirahisi hivyo,hii ilikua mara ya pili kuitwa interview hii organization,na mara ya kwanza nilidunda). It has been 1 yr 9 months now, and still counting, and i can confidently say that this has been my dream job!!
N.B.
1.Hapa nimeandika kirahisi sana kwa kujumuisha zile interviews nilizofanikiwa tuu, but safari hii haijawahi kuwa rahisi kwangu, nitafungua uzi wa kuelezea my failures katika interviews kadhaa ambazo nimewahi kufanya na nikadunda, ili kuwatia moyo vijana wanaotafuta ajira sasa hivi wakomae na wasikate tamaa!!!
2.Katika kazi zote ambazo nimewahi kuzifanya kama nilivyoeleza hapo juu, Sijawahi hata mara moja kupata kazi kwa sababu ya kufahamiana na mtu fulani kwenye hiyo organization, au kupewa 'memo'. I was purely depending on applying for the jobs, na kuitwa kwenye interview panapo majaliwa, na kuonyesha uwezo wangu wakati wa interview!! Kwa hiyo pia vijana mnaotafuta, msikate tamaa kwamba hujuani na watu kwenye hayo ma organization, pambana kweli kweliz ipo siku utafanikiwa!!

Itapenza sana ukiweka uzi wa hizo down falls.
 
Kama kuna wadau ambaye alisomea Mechanical ICT Environmental na electrical engineering degree ya kwanza wanapenda kupata uzoefu Naomba wanicheki inbox kuna taasisi moja ipo tu vizuri Ila naona hawapeleki cv
Wanatoa nauli
 
  • Thanks
Reactions: vvm
Nilitumiwa message na recruitment agency kupitia linked in, nikafanya interview ya kwanza kwao, ya pili nikafanya kwa client wao na namshukuru niliipata ingawa baadae nilikuja kuacha kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu.
Siku ya interview ya pili mwishoni niliambiwa " of all the candidates we have interviewed, you have shown a great character and being very honest Thank you...! Hii statement ilinifanya nihisi nimekosa kazi ila mungu si athumani niliipata japo haikuwa riziki.
Baada ya kuacha kazi ya hapo juu nilienda mkoani kwa muda ili kumuuguza mzazi wangu mpaka pale mungu alivyomchukua nikaamua kurudi mjini Dsm.
Nikaanzia kwa dada yangu mmoja hivi wa hiari ambaye nilijuana naye kipindi nipo ofisi A kwani kampuni yetu ilikuwa ni mteja wao.

Nikamueleza masahibu niliyopitia na kumuomba anisaidie connection niweze kurudi tena kwenye ajira. Kwa kuwa alikuwa anatambua uchapakazi wangu na ananifahamu kwa kiasi chake, akanifanyia favor kwa kunirecommend kwa meneja wa kampuni moja kubwa tu na kumuomba anipe nafasi maana nina uwezo mzuri kiutendaji.

Mwenyezi mungu akanijaalia nikaitwa kwenye interview zote 2 nikapita na sasa nipo kazini. May allah bless her and her family always.
 
Sentensi ya mwisho sio kweli
Nakumbuka baada ya kumaliza chuo nimerusha tu application tuwili tutatu nikaona chenga.....

Ndugu yangu mmoja akaniambia unahangaika na nini kwenye kuomba kazi relax pale ofisini kuna kazi itatangazwa lakni hakuna namna tena ya kutangaza as long as wewe upo consider yourself successful ....

Aisee haikuchukua hata mwezi mwanaume nimevutiwa waya nikaenda kula kozi maalaum kujifua zaidi baada ya miezi kadhaa nikabidhiwa ofisi sasa hivi nakula tumilioni twangu kadhaa na maisha yanasonga.....

Tanzania ya sasa bila kuwa na referee ni kazi bure huwezi amini utaishia kufungia maandazi vyeti aisee....
 
Kamwe usidharau mtu yoyote..

Kazi yangu ya kwanza ya kueleweka niliipata kupitia mlinzi niliyekuwa nimepanga nae jirani, alikuwa ana mazoea ya kuniomba pasi kila siku jioni....siku moja akanambia kuwa Mkurugenzi wa kampuni anayolinda anataka mtu kitengo fulani pale ofisini kwao, akaniuliza kama nafasi hiyo inanifaa? nikamjibu kuwa nimesomea hiyo fani. Basi kesho yake akiwa anatoka shift asubuhi akanipigia simu niende hapo, nikaenda na vyeti vyangu, akanishika mkono mpaka ofisini kwa Mkurugenzi, sikuamini kilichotokea maana sikufanyiwa interview wala lolote lile nikaambiwa nijiandae kusaini mkataba nianze kazi kesho yake, nikakabidhiwa ofisi siku hiyo hiyo pamoja na kutambulishwa kwa management na my team. Mpaka leo sijajua yule mlinzi alimuambia nini yule mkurugenzi, nilijifunza kuheshimu watu zaidi kuanzia siku ile mpaka na kesho daima
Aisee noma sana mkuu...!!
 
Back
Top Bottom