What's the story: Ulipataje kazi unayofanya au uliyowahi kufanya?

Kwenye Ishu ya ajira kila mtu na Bahati yake na Mungu wake..Ila MaHR wawe waaminifu mbele zao na mbele za Mungu..Unaimwita mtu kutoka mkoani tayari kumbe unamtu wako wa hiyo nafasi kwanini umsumbue aingie gharama zisizokuwa za lazima..si bora uachane naye kwenye interview au usitangaze hiyo nafasi.
HR unatangaza nafasi ya kazi tayari kuna watu wako wako kwenye ajira hii naikumbuka nilikuwa nikifanya kazi taasisi fulani ya fedha..nafasi zikatangazwa mwezi 5 kwenye gazeti huku watu walikwisha ingizwa kwenye ajira toka mwezi 3. vijana wakaomba nafasi za kazi hakuna hata mmoja aliyeitwa kwenye interview maana HR alikwisha jaza watu wake na hawakuwa na interview.
 
Hahaa niko passion na rural issues tu.Aise mimi sio mdau wa kusafisha rungu naamua kuacha maana wenyeji walinitisha appetite ikakata
Ahahahahah majamaa walikupa warning mapema.........na mademu Wa bush kwa kubabaikia wageni hasa walotoka town.....bila mkwara wake zao na mademu zao wangekuwa hatarini. BTW hvi huko rushwa,ruhita, ngenge,kishuro n.k, kuna Mizigo kweli???
 
Nilitumiwa message na recruitment agency kupitia linked in, nikafanya interview ya kwanza kwao, ya pili nikafanya kwa client wao na namshukuru niliipata ingawa baadae nilikuja kuacha kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu.
Siku ya interview ya pili mwishoni niliambiwa " of all the candidates we have interviewed, you have shown a great character and being very honest Thank you...! Hii statement ilinifanya nihisi nimekosa kazi ila mungu si athumani niliipata japo haikuwa riziki.
 
Mimi baada ya kumaliza chuo harakati za kusaka ajira zikaanza nilisota kitaa kwa mwaka mmoja. Kipindi wakati bado nipo kitaa nikakutana mwanamke ambaye kwasasa ni mke wangu tukaanzisha uhusiano kipindi hicho, Maisha yakaendelea kusonga bila kutarajia nikampa ujauzito alipoulizwa akanitaja nikaitwa kwao kuulizwa nikakubali. Kwakuwa tulikuwa tunaishi mtaa mmoja na wazazi wangu na wake wanajuana wakakaa chini kuyajenga ikabidi nimuoe . Baada ya miezi mitatu nikiwa naishi na mke wangu tunalea mimba dada yake akaja kuniambia niende kwenye interview na copy za vyet ktk idara moja ya serikali nilipofika nilijitambulisha basi wakachukua copy wakaniambia nitoke nje baada wiki NNE nikapigiwa simu nilipoti kazini. Mpaka Leo nipo na kazi hiyo hiyo.
Siku ukimsaliti ndo utakuwa mwisho wa hiyo kazi. Pole, nakupa pole kwasababu maisha yako yote utakuwa mtumwa wa ndoa yako
 
Hio part time Ilikua RWERU APD kibeta wakati huo Kuna zile evaluations na baselines katika ADPs mbali mbali nyingi nilikua sikosi asee zile hela za burebure kabisa... sema kazi Ilikua kubebelea vile vifaa tu na madodoso

nishafanya evaluation za mbuka ADP, rweru, katerero, misenyi,, izigo, ruhita n.k


cc Smart911
Mkuu kwan kwa sasa hauwezi nisaidia angalau nipate pa kutulizia akili huko maana nimemalza chuo cna pa kushika samahan lakini
 
Hadi sasa hivi nimeshafanya kazi sehemu nne.
1.Dar es Salaam.
Nilikua nimemaliza internship,nafasi za serikali hazijatoka wala nini, niko tu kitaani napiga daywaka za vijiweni za kuunga unga hapa na pale, ali mradi nisile wali mkavu. Kuna chuo fulani hivi wakawa wametoa tangazo wanataka Tutorial Assistants,nikatupia application yangu, mimi na mshikaji wangu wa karibu sana, tukaitwa interview wote wawili. Siku ya interview tumeenda pale chuoni,tunacheki majengo ya chuo yamechakaa kinyama,tunaulizana na mshikaji wangu,hawa wataweza kweli kutulipa mpunga wa kutosha? Tulifika pale mida ya saa tatu asubuhi, ila kuja kuingia kwenye interview mimi niliingia kama saa kumi na moja hivi jioni!! Nimechoka mbaya, na interview kiukweli haikwenda poa, nilimbwela mbwela Sanaaa!! (kumbuka hii ndio ilikua interview yangu ya kwanza kabisa tangu nimalize intern). Baada kama ya wiki moja hivi,nikapigiwa simu kwamba nimefaulu interview, niripoti hapo chuoni kwa ajili ya kusaini mkataba na kuanza kazi!! Mimi na mshikaji wangu wote tulipata;Ila sasa mshikaji wangu yeye akawa amepata nafasi pia Bugando Hospitali (yuko hapo hadi sasa), so akapiga chini kule, kwa vile mimi nilikua sina option,nikatimba, nikasaini mkataba (permanent and pensionable), nikaanza kazi rasmi. Salary haikua mbaya sana (ukizingatia ndio ilikua my first salary apart from zile posho za internship).
Tatizo la pale bwana:kwanza ilikua unakuja asubuhi, unakaa tuu ofisini hamna lolote unalofanya, hamna cha kufundisha, au kuelekezwa au chochote, unakaa tuu unacheza na laptop hadi mda wa kazi ukiisha unarudi home (chuo kilikua kimepata matatizo kidogo,so walizuiliwa kudahili na NACTE wanafunzi wa first year,ambao mimi ndo kuna somo ilibidi niwe nawafundisha). Tatizo lingine ikawa wanachelewesha mishahara balaa. Miezi mingine hadi tarehe 10 ndo kitu kinasoma!! Nilikaa pale miezi mitatu tuu, nikaona hapa nimeingia cha kike!! Nikasepa.
2.Arusha.
A small NGO fulani hivi ya Waingereza ambao wanajihusisha na projects mbalimbali za afya,elimu,biashara. Kama kawaida, niliona tu nafasi kwenye zoom, nikatupia application, nikaitwa interview nikaenda, after a week nikapigiwa simu nikaripoti kazini.
Hapa nilianza kazi kwa salary ambayo ni ndogo kuliko hata kazi ya kufundisha niliyoacha. Sema huku apart from salary,kulikua na viallowance vya hapa na pale vingi, pamoja na pesa za dili za hapa na pale.
Tatizo la hapa likawa country director wa Tanzania alikua na matatizo matatizo sana...!! Alikua anaendesha ile NGO kama kampuni ya kwake binafsi. Kelele nyingiiii, micro-management kwa sanaaa!!! I stayed with this organization for 5 months tuu, nikasepa.
3.Mbeya
Hii ilikua ni kliniki kwa ajili ya watoto, ambayo iko funded na International NGO moja ya Wamarekani. Na yenyewe niliona tangazo kwa gazeti, nika apply, nikaitwa interview, nikapanda basi from Arusha hadi Mbeya (the longest journey by bus i have ever experienced), tuliingia mbeya saa saba na nusu usiku, saa mbili asubuhi nikagonga interview, ilienda vizuri sana (i was very very confidence by this time nilikua nimezoea interviews tayari, na nimejiandaa kweli kweli, na nikaulizwa maswali yale yale kama bahati ya mtende). After two weeks, nikapigiwa simu nimefaulu interview niende Mbeya kuanza kazi. Hii kazi kwa kweli benefits zake zilikua nzuri mno compared na kazi zangu zilizopita. I stayed at this organization for 1yr and 4months, then I left. Sababu zilikua mbili tatu; Kwanza, kulikua hakuna uhakika wa funds za kuendeleza mradi kutoka kwa wamarekani kwa mwaka unaofuata (though walikuja kupata wakaendelea), lakini pia management ya hii organization ya hapa bongo walikua very discouraging kwa wafanyakazi, na wanadharau wafanyakazi.
4.Mbeya
Mradi mkubwa dealing with HIV/AIDS in the Southern Highlands zone. Na yenyewe niliona tangazo, nika apply, nikaitwa kwa interview, nikatusua. (sio kirahisi hivyo,hii ilikua mara ya pili kuitwa interview hii organization,na mara ya kwanza nilidunda). It has been 1 yr 9 months now, and still counting, and i can confidently say that this has been my dream job!!
N.B.
1.Hapa nimeandika kirahisi sana kwa kujumuisha zile interviews nilizofanikiwa tuu, but safari hii haijawahi kuwa rahisi kwangu, nitafungua uzi wa kuelezea my failures katika interviews kadhaa ambazo nimewahi kufanya na nikadunda, ili kuwatia moyo vijana wanaotafuta ajira sasa hivi wakomae na wasikate tamaa!!!
2.Katika kazi zote ambazo nimewahi kuzifanya kama nilivyoeleza hapo juu, Sijawahi hata mara moja kupata kazi kwa sababu ya kufahamiana na mtu fulani kwenye hiyo organization, au kupewa 'memo'. I was purely depending on applying for the jobs, na kuitwa kwenye interview panapo majaliwa, na kuonyesha uwezo wangu wakati wa interview!! Kwa hiyo pia vijana mnaotafuta, msikate tamaa kwamba hujuani na watu kwenye hayo ma organization, pambana kweli kweliz ipo siku utafanikiwa!!
Very interested with this. Thank u mkuu
 
  • Thanks
Reactions: vvm
Kazi ninayoifanya sasa ni kazi ya tatu.
Ni kazi ambayo niliipata kupitia rafiki mfanyakazi mwenzangu ambaye tulikuwa tunafanya naye kazi kwenye kazi yangu ya 2.Alinipigia simu akaniambia kuna sehemu wanataka mtu peleka cv basi baada nikaenda Mungu akajalia.
-Kazi yangu ya pili niliipata humu Jamiiforum nilijitambulisha mimi ni nani,sifa zangu na nini naweza fanya basi Mungu akajalia 1person akanipick soon.sitasahau nilipata kazi sehemu nzuri kupitia JF.That why I respect jf mpaka kesho,coz sikutarajia kwa %kubwa kwamba kupitia jf ningeweza kupata kazi.
-Kazi ya kwanza niliipata kupitia class met wangu wa chuo.alikuwa anafanya kazi sehemu akaulizwa kama kuna mtu anamfahamu anayeweza fanya kazi fulani basi akanipoint tu nikapeleka cv Mungu akajalia.

:Nilichojifunza
Yeyote unayekutana nae maishani,sehemu yeyote ile anaweza kuwa sababu ya wewe kupiga hatua na kufikia ndoto zako.Mungu atusaidie kuweze kuhusiana na watu vizuri.Hata kwenye hii mitandao ya kijamii ambayo hatujuani,trust me unaweza kula bingo la kiuhalali kabisa kama mimi nilivyopata kazi.
 
Kazi ninayoifanya sasa ni kazi ya tatu.
Ni kazi ambayo niliipata kupitia rafiki mfanyakazi mwenzangu ambaye tulikuwa tunafanya naye kazi kwenye kazi yangu ya 2.Alinipigia simu akaniambia kuna sehemu wanataka mtu peleka cv basi baada nikaenda Mungu akajalia.
-Kazi yangu ya pili niliipata humu Jamiiforum nilijitambulisha mimi ni nani,sifa zangu na nini naweza fanya basi Mungu akajalia 1person akanipick soon.sitasahau nilipata kazi sehemu nzuri kupitia JF.That why I respect jf mpaka kesho,coz sikutarajia kwa %kubwa kwamba kupitia jf ningeweza kupata kazi.
-Kazi ya kwanza niliipata kupitia class met wangu wa chuo.alikuwa anafanya kazi sehemu akaulizwa kama kuna mtu anamfahamu anayeweza fanya kazi fulani basi akanipoint tu nikapeleka cv Mungu akajalia.

:Nilichojifunza
Yeyote unayekutana nae maishani,sehemu yeyote ile anaweza kuwa sababu ya wewe kupiga hatua na kufikia ndoto zako.Mungu atusaidie kuweze kuhusiana na watu vizuri.Hata kwenye hii mitandao ya kijamii ambayo hatujuani,trust me unaweza kula bingo la kiuhalali kabisa kama mimi nilivyopata kazi.
Kweli kabisa mkuu
 

Similar Discussions

29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom