The Finest
JF-Expert Member
- Jul 14, 2010
- 21,607
- 6,071
Hiki ni kisa cha kweli cha rafiki yangu ila jina la muhusika ndio nimelibadilisha. Naandika kwa masikitiko sana kwa jinsi hali aliyonayo sasa hivi inasikitisha sana nafikiria ila kichwani mwangu maswali ndio mengi kuliko majibu, najiuliza ni kwanini lakini??
Ukimuona Angela sio yeye ile hali ya uanamke haipo tena, nguo anazovaa yeye ni zile zinazofunika mwili kuanzia juu hadi chini. Angela is not confident anymore anaonekana kama vile ana miaka 40. Angela amekuwa kwenye abusive relationship kwa muda mrefu amekuwa akipigwa na mumewe mara kwa mara na kumfukuza nje ya nyumba kwa kuwa ana watoto na huyu mume Angela ilikuwa inambidi arudi kwa mumewe kumuomba msamaha hii yote alikuwa anafanya kwa ajili ya watoto wake, alikuwa anataka watoto wake wamalize shule kabla hajachukua uamuzi mwingine.
Mumewe alikuwa ameishajua udhaifu wake uko wapi na ndio akaamua kuwa anatumia nafasi hiyo kumdhalilisha, Angela naye aliendelea kuishi na hali hiyo akitegemea iko siku labda mambo yatabadilika, ila siku mambo yalipokuwa magumu ndipo aliamua kuchukua uamuzi wa kuondoka hii ni baada ya mumewe kumjeruhi kwa kisu na mpaka sasa Angela ana makovu ya visu mwilini, natamani laiti kama mngeweza kumuona jinsi alivyo sasa hivi inasikitisha sana swali nililomuuliza ni kuwa pamoja na haya yote kwanini aliendelea kukaa kwenye ndoa ya namna hiyo akanijibu ni kwasababu ya watoto.
Nashindwa kueleza mambo mengine zaidi sababu ni ya aibu na ya kusikitisha sana mwanaume ambaye umezaa naye watoto leo hii anakuuliza "Kama wewe ni mwanamke kweli basi nionyeshe huo uanamke wako uko sehemu gani"? hivi sielewi.
NB: Mume wake ameishafikishwa kwenye vyombo vya kisheria kwa kosa la kumjeruhi
Najua ni wengi sana wako katika hali kama hii lakini hawasemi kwa kuhofia wakiacha ndoa zao jamii itawaelewa vibaya, ni kitu gani kinachokufanya uendelee kukaa kwenye ndoa ya namna hiyo????