What is your "Sweetest" Childhood Memory?? THAT It made you feel So Good and Speacial!

kutega visoda relini treni ikivikanyaga vinanyooka kisha tunatengeneza nakamba


Lazima umeishi Kiwalani Yombo...............mpk juzi nimekuta watoto wakifanya hii...........na nani alikuwa na uroho wa kula chakula cha mgonjwa kama mimi, mdogo wangu akiugua nautumia mwanya huo kumpiga mkwara aombe vitu vitamu vitamu.kama ujuavyo utotoni............ili akipona tucheze naye la sivyo nitakuwa namwacha home na asinifuate!...basi zitaombwa keki ama kukaangiwa mayai ambayo mwisho wa siku hawezi kuvila kutoka na kichefuchefu....ndipo napoitwa mimi "kumsaidia"................lakini haikudumu hii mbinu ilisitukiwa na mama yangu mdogo!
 

Do me a favour,ukipata muda shusha uzi maalum tujadili pros na cons za malezi haya ya bakora vs non bakora ( I for one i treat it as domestic violence)
Si vyema suala la kutandika watoto viboko kulifanya kuwa ni la kurithisha toka kizazi hadi kizazi, lakini kusema kweli ni vigumu kwa wengi kuwa na saikolojia ya watoto kiasi cha kuweza kujua njia mbadala ya malezi. Hata baadhi ya nchi ambazo sasa zimeacha malezi kwa viboko zamani zilikuwa zinafanya hivyo na kuna misemo yao (mfano Spare the rod spoil the child) ambayo mpaka leo wahafidhina wanaikumbuka na wengine wanajuta kwa nini wameondosha bakora katika malezi.

Lakini binafsi naamini malezi bila bakora inawezekana kabisa, hasa katika vizazi hivi ambavyo utandawazi unasaidia sana kupanua watu akili na kujielimisha katika malezi. Mafunzo na maelekeza kwa maneno na vitendo vitumike kama njia mbadala.

Nakumbuka miaka ya 90 tulikuwa na kampeni hii na kaulimbiu yetu ilikuwa:
ACHA TABIA MBAYA - PIGA NGOMA USIPIGE MTOTO.
 
Genuinely.... nashindwa hata pa kuanzia.... Niliishi page two ku qoute...:A S embarassed:
 
ADI, afu nilipokua kua ka teen, ndo enzi hizo mabreka(b reak dance) yamapamba moto.
Usipoalikwa kwenye sherehe kuwa stage show unaenda kunywa sumu hapo late 80's.

I wish nikuone the way you break dance...lol... Raha saana kuwaona, hasa kama wajua mioindoko... Na miaka ya 80 ndio zao hizi.... kipindi hicho Michael Jackson Moto wa kuotea mbali...lol (as much as moves zake hazikua break dance kivile)

I do remember the times I had my report form at hand (mind you I was a bright kid) the feeling that came in my mums eyes when she opened it and later the whole house went happy because of me, tunapikiwa chips and promises of going out. I think those are the very best moments when I think of my childhood.

That was so good.... Another adoring mom.... Yaani Mungu wa ajabu imagine you were young but you could still be able to read furaha ya mamako ndani ya macho yake... I hope you are still doing that and that some lady has not made you forget the sweet memory of your mom. Thank you for sharing, and regards to your mom with Love.... hoping she is still around....

I will never forget mchezo wa baba na mama, mi nlikua baba wakat mwingine mtoto yaani nikikumbuka nataman kurudi utoton ila basi umri umekwenda.

hahahaha..... wewe unatamani kurudi utoto sabb tu ya kucheza baba? lol.... vipi upendi hii ya ubaba ya utu uzima? lol

Yaani AD we acha tu! nikikumbuka utoto najidharau kwa kweli namshangaa huyu hapa chini anautaka ubaba wa utotoni, naona huu ubaba wa ukubwani mgumu!

Nawee umeona eeh? lol

Hahhaahha hahahaha,nitakupm unambie style ya kupanga mito unapolala na uwepo wa big shem lol!

Asa kuna kituko kingine bana hiki mpaka kesho huwa nikikumbuka nacheka sana,
Kwanza nilikuwa napenda sana kuvaa vitu vya mama,km viatu na nguo,
Siku ya siku nakumbuka padri wetu alikuja hm,
Mie nikuwa nimelala na baba chumban asa mama akaja kumwamsha baba padri kaja baba alipotoka tu na mie nikashuka kitandan kulikuwa na tenga flan la kuwekea ngu chafu nikazana na kuibuka na brazia ya mama nikajitupia na kutoka seblen nikaenda kusimama katikati ya sebule watu walichanganyikiwa nakumbuka mama alikurupuka na kuja kuninyakua km mwewe anavonyakuwa kifaranga yani nilisabababisha b onge la aibu aisee!!!

Wewe ni kiboko!! Naona Mtambuzi kakulandaisha eeh? lol

I can not imagine.... I just hope hio sidiria haikua nyeupe na chafu! lol..... Naona mamako alipata :shock:
 

- Siku niliyokula pilipili kwa makusudi na kuenda kliniki nikidai nina homa. Dokta kunipima, nilikuwa na sijui madigrii mangapi. Hadithi ndefu lakini uongo ule ulinilazimu kulazwa hospitali wiki moja.

- Siku hizo vitabu na vifaa vyote tulipewa bure, tukimaliza mwaka tunarejesha na kupewa vyengine. Kumbe katika kitabu kimoja kulikuwa na barua aliyonijibu "mchumba wangu". Mwalimu aloikamata akatishia kumwambia baba yake ambaye alikuwa daktari wa meno. Siku ya pili daktari alikuja shule (kumbe kwa ukaguzi wa kawaida wa afya zetu) lakini mimi nilidhani ndio amekuja kunishikisha adabu. Sikuwa na raha muda wote mpaka alipoondoka. Badae mwalimu aliniita na kunionya nisizowee, kusoma kwanza mademu baadae.

- Pamoja na yote hayo walimu waikuwa wananipenda kwani nilikuwa hodari. Sikusoma darasa la 2 nikapelekwa la 3, sikusoma la 4 nikapelekwa la 5 na sikusoma la 6 nikapelekwa la
saba. Nilikuwa ninafurahia zawadi za mwanafunzi bora.


Mamammia.... Nimechekaje.... nimefurahije? Hizi nilizoacha ndizo hasa zimenichekesha.... Inaonesha you were that kind of kind ambae as much as ni mtundu, jamii inampenda na kumkubali saana. I wish I knew you right now ili nirelate story ulotoa na what you are, what you do, na what you portray...

Na I think walimu wako understood you, ndio maana walikua nakupenda... Kwa kweli naomba nitoe pongezi... kuruka madarasa hivo, ulimaliza primary upo darasa la ngapi? Na have you got any kid ambae amefuata intelligence zako ki hivo? Jibu if only you don't mind... Thank you for sharing....

Hehehehe.......... Mwalimu mkuu, usiniulize jinsia yake tafazali.....


hahahaha.... I just hope kama alikua mwanamke hukua na kioo close, maana kwa watoto na wakubwa ni tofauti....lol
 
Jamani.... another post on a wonderful Mom.... inanifanya nitafakari if I am doing the same thing for my son.... Kwamba na yeye siku moja somewhere ambako hamna anae nifahamu atasimulia haya mnayo simulia hapa. I guarantee you huko your mom would be very proud if she reads this post..... Thank you for sharing Gamba chovu..... be good to all the women basi in courtesy of your mama.... Pamoja saana.

Thanks ADI...
GeeCee is a very close friend of mine.. I will let him know of the sweet words you wrote to him..

Thanks once again..
 
Utotoni,nilikuwa napenda sana maharage kuliko mboga zinginezo. Mam wakati mwingine alinibadilishia mboga na kunipikia njegere. Nilipomuhoji wapi maharage ? Alikuwa akiniambia kuwa leo nimekupikia maharage ya kizungu,naridhika na kufurahi. Ikawa mboga yangu ya pili. ...Wonderfull enough hadi leo nilapo wali huwa sihitaji mboga nyingine zaidi ya maharage.
> On other side naujali sana upendo wa mama yangu,biashara yake ya vitumbua na mshahara wake mdogo wa ualimu wa primary umenifikisha hapa nilipo.
...I love u mam!
 
I wish I knew you right now ili nirelate story ulotoa na what you are, what you do, na what you portray...

Na I think walimu wako understood you, ndio maana walikua nakupenda... Kwa kweli naomba nitoe pongezi... kuruka madarasa hivo, ulimaliza primary upo darasa la ngapi? Na have you got any kid ambae amefuata intelligence zako ki hivo? Jibu if only you don't mind... Thank you for sharing....
Hiyo red ya juu maelezo yake yako "faraghani".
Nilimaliza primary darasa la 7 lakini nilisoma kwa miaka minne badala ya miaka saba. Baada ya kumaliza sekondari na kusomea ualimu miaka miwili, niliajiriwa kazi ya ualimu sekondari nikiwa na umri wa miaka 20, nikiwa na umri sawa na wanafunzi wangu na wengine kunizidi umri (saikolojia niliyojifunza chuoni ilinisaidia ku"cop" na mazingira).

Ndio, ninao mabinti wawili ambao uelewa wao unanishangaza, kunifurahisha na kunipa moyo, lakini nisingependa waruke madarasa kama mimi kwani wanaweza kumaliza shule wakiwa wadogo sana.
BADO TUNASUBIRI KUSIKIA TOKA KWAKO
 
Zipo nyingi ila hii inaniumiza hadi leo. Tulikua kampan ya watoto sita na mimi nlkua fundi mzuri sana wa kutengeneza magari ya mabati ya kuvuta na kamba, sasa tukawa tunaua mijusi tukawa tunaitengenezea majeneza ya gamba la mgomba tunapakia kwenye hayo magar nlyokua natengeneza tunasafirisha hadi shambani kwa mmoja wetu tunazika na tulkua tunafanya kama msiba wakweli na tukafanya hvyo mara nyingi na hatukuwah kuzika shamba tofauti na hilo mara zote, kilichokuja kutokea kwenye hiyo familia ndo kinanfanya nkumbuke kwa uchungu tukio hili hadi leo japo ilkua utoto, familia karibu yote imetetekea akiwapo tuliekua tunachezanae wa hiyo familia tulikua tunaenda kuzika mijusi kwao naye akishiriki bila kujua tunaichulia familia yao, ilikua miaka kati ya 92 na 95. INANIUMA SANA JAPO SINA UHAKIKA UHUSIANO WA MISIBA YA KWAO NA UTUNDU WETU.
 
Aisee! Hii imenigusa? Kwa nini mliwaza biashara ya maziko? Mlikuwa mnapima majeneza ama mnakunja marehemu mijusi mikia? Hautetemeki mikono? Coz nikiwa kiddo niliambiwa ukiua mijusi mikono itakuwa kitetemeshi!
Zipo nyingi ila hii inaniumiza hadi leo. Tulikua kampan ya watoto sita na mimi nlkua fundi mzuri sana wa kutengeneza magari ya mabati ya kuvuta na kamba, sasa tukawa tunaua mijusi tukawa tunaitengenezea majeneza ya gamba la mgomba tunapakia kwenye hayo magar nlyokua natengeneza tunasafirisha hadi shambani kwa mmoja wetu tunazika na tulkua tunafanya kama msiba wakweli na tukafanya hvyo mara nyingi na hatukuwah kuzika shamba tofauti na hilo mara zote, kilichokuja kutokea kwenye hiyo familia ndo kinanfanya nkumbuke kwa uchungu tukio hili hadi leo japo ilkua utoto, familia karibu yote imetetekea akiwapo tuliekua tunachezanae wa hiyo familia tulikua tunaenda kuzika mijusi kwao naye akishiriki bila kujua tunaichulia familia yao, ilikua miaka kati ya 92 na 95. INANIUMA SANA JAPO SINA UHAKIKA UHUSIANO WA MISIBA YA KWAO NA UTUNDU WETU.
 
Back
Top Bottom