Muda mfupi uliopita nimepita karibu na viwanja vya shule ya sekondari ya kinyerezi iliyopo manispaa ya ilala jijini dar.
Nimeona watu waume kwa wake vijana wazee na watoto wote kwa ujumla wao wakiwa wamevalia mavazi mazuri ninayoyapenda ya kiislam(mimi ni mkristo).
Kwa kuwa nafahamu kuwa shule ya sekondari ya kinyerezi ni ya serikali, nikalazimika kumwuliza mwenyeji wangu(yeye ni muislam) kulikoni?
Amenijibu kwa masikitiko makubwa kwamba siku hizi baadhi ya shule zinafanya mahafali mbili tofauti. Moja kwa ajili ya wakristo na nyingine kwa ajili ya waislam. Na hao watoto wamekuwa wakisoma pamoja kwa miaka kadhaa. Mwenyekiti ameendelea kuonyesha masikito makubwa juu ya mbegu hii mbaya ya ubaguzi inayopandwa kwenye udongo mzuri wa watoto wetu.
Nimebaki najiuliza maswali mengi bila majibu.
1. Haya yameanza lini?
2. Je serikali yetu(inayajua haya na imeyaruhusu)
3. Aliyeanzisha haya anajua madhara yake?
4. Vipi kwa watoto ambao ni waumini wadini zingine tofauti na ukristo na uislam au wapagani, je hawana haki ya kushiriki mahafali?
Naomba kutoa hoja. Nadhani hili ni jambo la kukemewa.
Niko tayari kusahihishwa au kupata maelezo sahihi pale ambapo maelezo yangu yataonekana kuwa yana mapungufu.
Mungu ibariki Tanzania.
Nimeona watu waume kwa wake vijana wazee na watoto wote kwa ujumla wao wakiwa wamevalia mavazi mazuri ninayoyapenda ya kiislam(mimi ni mkristo).
Kwa kuwa nafahamu kuwa shule ya sekondari ya kinyerezi ni ya serikali, nikalazimika kumwuliza mwenyeji wangu(yeye ni muislam) kulikoni?
Amenijibu kwa masikitiko makubwa kwamba siku hizi baadhi ya shule zinafanya mahafali mbili tofauti. Moja kwa ajili ya wakristo na nyingine kwa ajili ya waislam. Na hao watoto wamekuwa wakisoma pamoja kwa miaka kadhaa. Mwenyekiti ameendelea kuonyesha masikito makubwa juu ya mbegu hii mbaya ya ubaguzi inayopandwa kwenye udongo mzuri wa watoto wetu.
Nimebaki najiuliza maswali mengi bila majibu.
1. Haya yameanza lini?
2. Je serikali yetu(inayajua haya na imeyaruhusu)
3. Aliyeanzisha haya anajua madhara yake?
4. Vipi kwa watoto ambao ni waumini wadini zingine tofauti na ukristo na uislam au wapagani, je hawana haki ya kushiriki mahafali?
Naomba kutoa hoja. Nadhani hili ni jambo la kukemewa.
Niko tayari kusahihishwa au kupata maelezo sahihi pale ambapo maelezo yangu yataonekana kuwa yana mapungufu.
Mungu ibariki Tanzania.