ELNIN0
JF-Expert Member
- Nov 26, 2009
- 4,161
- 1,460
Wana ndugu
Jana nimesoma walimu wamepigwa miaka 14 jela, Viboko na kazi ngumu kwa ajili ya wizi wa pesa za shule ya msingi shilling za Kitanzania 800,000.
Waliotiwa hatiani ni walimu 3 yule wa nne aponea chupuchupu.
Swala la Msingi.
Hivi huu wizi unatofautiana? mwizi si ni mwizi tu jamani? sasa kwa nini anayeiba kidogo anahukumiwa mapema na adhabu yake ni kali - huyu mwizi mwingine anayeiba mamillioni yeye kwanza kesi yake inachukua muda, then inafikia hatua mahakama inakosa kifungu cha kumtika hatiani kulikoni?
Inaniuma sana kuona wezi hadi wanadiriki kurudisha pesa walizoiba serikalini na wanapewa risti ya Received by Goverment of Tanzania - lakini hadi leo tunao mitaani na suala la wao kufungwa hilo kwa yeyote hapa JF atakubalina na mimi kwamba hafungwi hata mmoja wa hao jamaa.
Sheria iwe msumeno kama mwizi ni mwizi tu hata kama Umeiba bata au mamilioni ya shilling. Sheria ya wizi isibakie kuwahukumu walalahoi tu.
Hili ni tatizo na lipo katika mfumo mzima wa utoaji haki hapa nchini kwetu. kuna mkongomani mmoja aliniambia - "In Tanzania if you have money you will never go to jail" Nimeamini
Jana nimesoma walimu wamepigwa miaka 14 jela, Viboko na kazi ngumu kwa ajili ya wizi wa pesa za shule ya msingi shilling za Kitanzania 800,000.
Waliotiwa hatiani ni walimu 3 yule wa nne aponea chupuchupu.
Swala la Msingi.
Hivi huu wizi unatofautiana? mwizi si ni mwizi tu jamani? sasa kwa nini anayeiba kidogo anahukumiwa mapema na adhabu yake ni kali - huyu mwizi mwingine anayeiba mamillioni yeye kwanza kesi yake inachukua muda, then inafikia hatua mahakama inakosa kifungu cha kumtika hatiani kulikoni?
Inaniuma sana kuona wezi hadi wanadiriki kurudisha pesa walizoiba serikalini na wanapewa risti ya Received by Goverment of Tanzania - lakini hadi leo tunao mitaani na suala la wao kufungwa hilo kwa yeyote hapa JF atakubalina na mimi kwamba hafungwi hata mmoja wa hao jamaa.
Sheria iwe msumeno kama mwizi ni mwizi tu hata kama Umeiba bata au mamilioni ya shilling. Sheria ya wizi isibakie kuwahukumu walalahoi tu.
Hili ni tatizo na lipo katika mfumo mzima wa utoaji haki hapa nchini kwetu. kuna mkongomani mmoja aliniambia - "In Tanzania if you have money you will never go to jail" Nimeamini