Wakuu katika akili ya kawaida isiyohitaji shahada wezi wa EPA, wahujumu uchumi na hawa Viongozi wa Chadema kina J. Nassary, Dr. Slaa, G. Lema na wengine wanaowaelimisha raia wasiendelee kunyanyaswa, kudhulumiwa haki zao, kuibiwa rasilimali zao na kutendewa maovu mengine mengi, nani alipaswa kuhojiwa na polisi wetu, na ikiwezekana kufunguliwa mashitaka? Je kwa hiki wanachofanya polisi chini ya ccm kuna tofauti gani na majambazi walioteka basi la abiria na kuwaamuru watu wote kuinamisha vichwa au kulala chini na kila anayetaka kunyanyuka au kuamka anashughulikiwa ili wengine wasithubutu, tukisema ccm na polisi ni sawa na majambazi wa aina hiyo sina hakika kama ni makosa. Sijawahi kusikia polisi wakiwahoji wezi wa mali za Umma na viongozi wabadhirifu hata siku moja ni mpaka Rais aseme, Polisi kuweni wazalendo hii nchi ni yetu sote hata ninyi inawahusu, siyo ya viongozi wa ccm peke yao? Nawasilisha.